Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 24 April 2015

RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI APENDEZESHA SHEREHE YA CHAUKIDU SILVER SPRING, MARYLAND NCHINI MAREKANI


Meza kuu toka kushoto ni Rais wa CHAUKIDU Prof.Lioba Moshi, Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula na Mama Sitti Mwinyi wakuhudhuria sherehe ya Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani. Mhe. Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiwa mgeni rasmi sherehe iliyofanyika Silver Spring, Maryland nchini Marekani siku ya Alhamisi April 23, 2015 na kuhudhuriwa na wadau wa Kiswahili kutoka mataifa mbalimbali wakiwemo Wamarekani wanaozungumuza lugha ya Kiswahili.
Dr. Hamza Mwamoyo mkuu wa idhaa ya Kiswahili Voice of Amerika (VOA) akimsabahi Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi huku wakipata picha ya kumbukumbu wenginine kwenye picha ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula na Mama Sitti Mwinyi.
Farida(kulia) wa Farida Catering akiwaelekeza Rais msataafu Ali Hassan Mwinyi, Mama Sitti Mwinyi na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula aina ya vyakula alivyopika katika kuhitimisha sherehe ya CHAUKIDU siku ya Alhamisi April 23, 2015 Silver Spring, Maryland nchini Marekani. Hii ni mara ya pili kwa Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuonja mapishi ya Farida Catering mara ya kwanza ilikua katika shere ya miaka 3 ya Vijimambo iliyofanyika mwaka 2013 Capitol Heights.
Farida akiwaonyesha ustadi wa ukutaji matunda Rais mstaafu Mhe. Ali Hassan Mwinyi, Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula na Mama Sitti Mwinyi.
Prof. Lioba Moshi akiongea machache ya kumshukuru Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuhudhuria sherehe ya CHAUKIDU tangia mchana na usiku bila kuchoka pia alimshukuru Balozi wa Tanzania nchini Marekani kwa kuwezesha kuja nchini kwa Rais Msataafu aliyependezesha na kunogesha sherehe ya chama chao na baadae alimkaribisha Balozi Liberata Mulamula kuongea machache.
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akitoa shukurani zake kwa CHAUKIDU kwa kufanikisha sherehe yao na baadae aliwatambulisha maafisa na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani akiwemo Balozi wa heshima Ahmed Issa na wadau mbalimbali wakiwembo waandishi wa vitabu Kapuya kutoka California na Mzee Safari kutoka Maryland na baadae kumkaribisha Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuongea na wadau wa Kiswahili nchini Marekani.
Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiongea na wadau wa Kiswahili katika kuhitimisha sherehe ya CHAUKIDU iliyofanyika siku ya Alhamisi April 23, 2015 Silver Spring, Maryland. Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi mbali na kuwashukuru CHAUKIDU pia alitumia fulsa hiyo kuweka sawa baadhi ya maneno la lugha ya Kiswahili ambayo hukosewa kutamkwa ipasavyo kwa kutoa mfano alisema katika kiswahili kahuta tarehe 1 au tarehe 2 usahihi ni tarehe mosi na tarehe pili huku akitolea mfano kwa lugha ya kiingereza kwamba hata nao hutamka 1st na 2nd mfano mwingine alisema unaposema nawaahidini ni ahadi unayotoa kwa watu wasiokuwepo mbele yako lakini unaposema ninakuahidini ndio sahihi kwa ahadi unayotoa kwa watu waliopo mbele yako na mengine mengi.
Kamati nzima ya CHAUKIDU ikipata picha ya kumbukumbu 

No comments: