Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 9 May 2012

Jikoni Leo;Kitabu cha Mapishi cha da'Miriam Rose.Mapishi ya vitumbua kutoka kwa da'Cecy!!!

Cookbook Sneak Peek – Kitabu cha mapishi

Muonekano wa kitabu cha mapishi cha"A Taste of Tanzania".

Cover ame-Design Mwenyewe na Picha amepiga mwenye.Kitabu kitatoka hivi karibuni.

Utakipataje;Ataweka wazi jinsi gani unaweza kupata Kitabu.Ukiingia pale kwake kunasehemu ya mawasiliano,Unaweza kuwasiliana nae Zaidi kupitia http://www.tasteoftanzania.com

Jee da'Miriam anajua KISWAHILI?JIBU;Ndiyo,anakichapa haswa, kama ulivyoona kwenye ile post iliyopita niliandika ni Mswahili.

Nafikiri nimewajibu nijuavyo Waungwana mlionitumia Email na mlionitumia Messages kwenye sim.Na nimeweka hapa kama kuna wengine waliokuwa na maswali kama haya nao Wamepata Jibu.

Haya Waungwana pata mapishi ya UJI na FUTARI kutoka kwa da'Miriam Rose.Hapo juu.

Hapo chini;Mapishi ya "VITUMBUA"Kutoka kwa da'Cecy anapatikana http://mapishinacecy.blogspot.co.uk.

Mswahili mimi kupika vikorombwezo saaaana siweziiiiii,Najua kupika kiasi cha Kula  MUBENA yangu na Watoto yangu na Wageni kidogo tuu,Si kila mtu anaweza kila kitu jamani, Watu na VIPAJI Vyao.MIMI nitakuwa nakurushia Matukio tuu hapa.Na nikipata Muda nitaweza Kuwatembelea Wapishi Nyumbani kwao na Kuwawekea MAZUNGUMZO na MAPISHI HAPA!!AU VIPI WAUNGWANA.SWAHILI NA WASWAHILI!!!PAMOJA SANA TUU.

5 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Ahsande, Uhongise we mlongo wangu maana tuko wangu ambao tunaweza kupika vya kula familia tu sasa hapa ni shule tu hakuna uvivu:-)

Anonymous said...

mwake mwake mutu yangu nakupendaje unapo nipeleka kwenye faniiiiiiiii itabidi tutafutane ili unipe moungozo wa kuendeleza faniiiiii hapa ushanitia hamu na tamani jiko sasa swahili na waswahili,ubarikiwe mpendwa sanaaaaaa

Mija Shija Sayi said...

Safi sana yaani, hongera kwa Kitabu Da Miriam Kinunda.. Mimi nasubiri pa kukipata...

emuthree said...

Shule muhimu, tupo pamoja ndugu wa mimi

Rachel Siwa said...

Pamoja waungwana,Mungu awe nanyi daima.@da'Yasinta mwenzangu ni mzuri/unaweza sana/Kipaji/unafanyavizuri NINI?

Anonymous;Ameen!!Karibu sana tuu,SWAHILI NA WASWAHILI.