Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 19 August 2014

[VIDEO]: Mazungumzo na Liberatus Mwang'ombe na Solomon Chris baada ya Uchaguzi DMV‏


Mubelwa Bandio kati akiwa na aliyekuwa mgombea wa nafasi za Mwenyekiti wa Jumuiya DMV Liberatus Mwang'ombe (L) na mgombea nafasi ya Katibu Msaidizi Solomon Chris (R0 wakati wa mahojiano

Agosti 9, 2014, Jumuiya waTanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia nchini Marekani ilifanya uchaguzi wake mkuu.

Matokeo yake yamekuwa yakipingwa na waliokuwa wagombea wa uchaguzi huo kutokana na sababu mbalimbali.

Wamaketi na Vijimambo Blog na Kwanza Production kueleza sababu hasa za kupinga matokeo hayo siku ya Jumatano ya Agosti 13, 2014.

Karibu uungane nasi kusikia wanachopinga

Mazungumzo na Salma Moshi kuhusu uchaguzi DMV‏




 Salma Moshi akizungumza na Mubelwa Bandio kwenye mahojiano haya


Agosti 9, 2014, Jumuiya waTanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia nchini Marekani ilifanya uchaguzi wake mkuu.

Matokeo yake yamekuwa yakipingwa na waliokuwa wagombea wa uchaguzi huo kutokana na sababu mbalimbali.

Mmoja wa wagombea hao, Salma Moshi amaketi nasi kueleza sababu hasa za kupinga matokeo hayo siku ya Jumatano ya Agosti 13, 2014 chini ya utayarishaji wa Vijimambo Blog


Karibu uungane nasi kusikia anachopinga

 
 

Wednesday 13 August 2014

Mahojiano ya Kwanza Production na Jhiko Manyika a.k.a JhikoMan‏



JhikoMan akitumbuiza kwenye Tamasha la Majahazi 2013
Karibu katika mahojiano kati ya Kwanza Production na Jhiko Manyika a.k.a
JhikoMan aliyejiunga nasi moja kwa moja kutoka Helsinki Finland mwishoni mwa mwezi Julai

Amezungumza
mengi kuhusu ziara yake ya Ulaya iliyoanza mwezi wa nne, maonyesho
aliyofanya, kazi alizorekodi na pia watu aliowashirikisha kwenye albamu
yake mpya ijayo.

Amezungumzia IMANI ya RASTA na pia MUZIKI WA TANZANIA kwa ujumla

Ameongea mengi mema

KARIBU UJIUNGE NASI


Tuesday 12 August 2014

Pitapita ya Mswahili mitaani;Mtu Kwao.!!!!!!!



Tulikutana na hili bango mitaani hapa UK,kuona Bendera ya Kwetu,"Tanzania" Tukavutiwa..
Nyumbani Kwetu ni Kuzuri,Watu wa Kwetu ni Wakarimu..Karibuni Tanzania Karibuni Mtwara. Mambo Ipo Huko!!!!!!!
"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima

Hotuba fupi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Azania Bank kwa DIASPORA‏


Mkurugenzi Mtendaji wa Azania Bank Charles Singili alipokuwa akizungumzia huduma za benki yake kwa waTanzania jijini Washington DC
PICHA ZOTE KWA HISANI YA IKULU
Hotuba fupi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Azania Bank Charles Singili alipokutana na waTanzania waishio nchini Marekani usiku wa Agosti 2, 2014.

Hotuba hii ilitolewa kwenye mkutano kati ya waTanzania wa Marekani na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk Jakaya Kikwete

Karibu umsikilize




Monday 11 August 2014

CITE SUMMER CONFERENCE 2014 COVENTRY WEST MIDLANDS UK WITH MWL.MWAKASEGE.[Tujikumbushe Picha za Mkutano na Mchungaji Daniel Kulola,Uliofanyika Coventry]



Picha hizi za chini ni mkutano wa zamani kidogo na Mchungaji Daniel Kulola,Ulifanyika Coventry UK.
Si vibaya tukijikumbusha.....



























Picha kutoka Maktaba ya Swahili Na Waswahili

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 10 August 2014

Muendelee na JumaPili hii kwa Amani na Upendo;Burudani-Franck Mulaja,Alleluya,Nzambe malamu..!!!!!!

Wapendwa;Nimatumaini yangu Jumapili inaendelea vyema;Iwe yenye Imani,Kuomba pasipo kukoma,Uponyaji,Shukrani na kujitoa kwa wenye kuhitaji.

14.Hata walipowafikia wanafunzi, waliona mkutano mkuu wakiwazunguka, na waandishi wakijadiliana nao,15. Mara mkutano wote walipomuona walishangaa, Wakamwendea mbio,wakamsalimu.16.Akawauliza, Mnajadiliana nini nao?

Neno La Leo;Marko Mtakatifu:9:1-50

17.Mtu mmoja katika mkutano akaijibu,Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako,ana pepo bubu;18. Na kila  ampagaapo,humbwaga chini, naye hutoka povu na kusaga meno na kukonda;Nikasema na wanafunzi wako wamtoe pepo, wasiweze.19.Akawajibu,akasema,Enyi kizazi kisichoamini,nikae nanyi hata lini?Nichukuliane nanyi hata lini?Mleteni kwangu.20.Wakamleta kwake;hata alipomwona,mara yule pepo alimtia kifafa;naye akaanguka chini,akagaagaa,akitokwa na povu.

21.Akamuuliza babaye,Amepatwa na haya tangu lini?Akasema tangu utoto.22.Na mara nyingi amemtupa katika moto,na katika maji,amwangamize;Lakini ukiweza neno lolote, utuhurumie, na kutusaidia.

23.Yesu akamwambia, Ukiweza!Yote yawezekana kwake aaminie.







"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.