Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Mahojiano. Show all posts
Showing posts with label Mahojiano. Show all posts

Friday 7 October 2016

Mahojiano na Mhe Peter Serukamba nchini Marekani


Karibu na asante kwa kujiunga nasi
Oktoba 6, 2016, tulipata fursa ya
kutembelewa studioni (Kilimanjaro Studio, Beltsville, Maryland) na
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini.
Tumejadili mengi tu kuhusu Tanzania yetu
KARIBU

Mahojiano na Rahima Shaaban. Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Ubunifu wa Beautiful Jamila




Kwanza Production

 Beautiful Jamila ilianzishwa mwaka 2013 na Rahima Shabani na makao makuu ni Atlanta Georgia.

Inajihusisha na harakati za kutangaza tamaduni za kiSwahili na kiAfrika.

Mwanzilishi wake aliungana nasi studio kuzungumza mengi kuhusu yeye, kampuni yake na tamasha lijalo




Wednesday 21 September 2016

Kipindi cha Reggae Time Pride Fm Sept 17 2016.....Mahojiano na Innocent Galinoma


Karibu katika kipindi cha REGGAE TIME ya Pride Fm Mtwara Tanzania.

Na leo, ni mazungumzo yangu na Innocent Galinoma ambaye alikuwa mkarimu sana kufika Kilimanjaro Studios kwa mahojiano.



Ni kuanzia saa tisa kamili alasiri kwa saa za Afrika Mashariki, mbili kamili kwa Marekani Mashariki

Jiunge nasi kupitia 87.8 Fm kwa mikoa ya kusini, ama www.878pridefm.com ama kupitia TuneIn, bofya tun.in/seTTx.

Thursday 4 August 2016

Wawakilishi wa Tanzania katika YALI 2016 wazungumza kuhusu kongamano lao Washington DC

Stanley Magesa (mjasiriamali) akifafanua jambo ndani ya studio kuhusu YALI 2016


Aug 3, 2016 tulipata fursa ya kutembelewa na kuhojiana na baadhi ya
Watanzania wanaowakilisha kwenye mkutano wa Mandela Washington
Fellowship - Young African Leaders Initiative (YALI) 2016 waliomaliza
mkutano wao hapa Washington DC

Walikuwa wakarimu sana kujiunga nasi Studio na kuzungumza nasi kuhusu mambo mbalimbali

Karibu uwasikilize



Heri Emmanuel (kati kutoka Mwanza) akieleza jambo huku Tusekile Mwakalundwa ( Mhadhiri na Mwanasheria kutoka Arusha) akisikiliza kwa makini. Kulia ni Mubelwa Bandio wa Kwanza Production na Vijimambo Radio
Baadhi ya wawakilishi wa YALI 2016 kutoka Tanzania, wajasiriamali Stanyey Magesa (Mwanza), Simon Malugu (Morogoro) na Lusajo Mwaisaka (Dar) wakiwa kwenye mahojiano Kilimanjaro Studio
Mshiriki wa YALI 2016 Heri Emmanuel (Mwanza) kulia akaifafanua jambo huku akisikilizwa na mshiriki mwenzake ambaye pia ni Mhadhiri na Mwanasheria Tusekile Mwakalundwa (Arusha) na mjasiriamali na Lusajo Mwaisaka (kutoka Dar)



Thursday 15 October 2015

Mahojiano na waasisi wa Jabali Afrika

Wawili kati ya waanzilishi wa JABALI AFRIKA, Justo Asikoye na Joseck Asikoye walipata fursa ya kutembelea Kilimanjaro Studio zilizopo Beltsville Maryland na kuzungumza na Mubelwa Bandio na Dj Luke Joe kuhusu kazi zao
Ilikuwa ni katika kipindi cha MISHUMAA YA KALE kinachosikika kila Ijumaa kuanzia saa 11 jioni kwa saa za Marekani ya Mashariki
KARIBU


Friday 13 February 2015

Mazungumzo na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi Pt II


Karibu sana na asante kwa kujiunga nasi katika kipindi hiki cha HUYU NA YULE

Tumepata fursa ya kuongea na Mhe. Balozi Mustafa Nyang'anyi

Tumefanya mazungumzo naye ya sehemu nne, kueleza safari yake kimaisha

Tunaendelea na sehemu ya pili ya mazungumzo yetu, ambapo Mhe Balozi Nyang'anyi anaanza kuelezea namna

1: Alivyoingia kwenye siasa (ubunge mwaka 1970)

2: Alivyopata taarifa za kwanza za uteuzi wake serikalini. Hapa napo pana mvuto wake kusikiliza.

3: Nafasi alizoshika kama naibu waziri na waziri kamili

4: Nafasi ya ukuu wa mkoa

5: Na hata harakati zake na pia alivyopata nafasi ya kuja kusoma Chuo Kikuu Havard

KARIBU

Kama ulikosa sehemu ya kwanza ya mazungumzo yetu, bonyeza READ MORE



Huyu na Yule ni kipindi kinachotayarishwa na Vijimambo Blog na kuzalishwa na Kwanza Production

Kwa mawasiliano, maoni ama ushauri, tafadhali wasiliana nasi kupitia kwanzaproduction at gmail.com

Monday 14 July 2014

Mahojiano na washiriki wa maonyesho ya Utamaduni wa Kenya hapa Washington DC


Kati ya Juni 25 na Julai 6, jiji la Washington DC lilikuwa mwenyeji wa maonyesho ya kila mwaka ya yanayohusu maisha a watu na jamii mbalimbali.

Mwaka huu, nchi ya Kenya ilishirikishwa, wakionyesha utamaduni wao na changamoto za kuzidumisha katika zama hizi za sayansi na teknolojia.

Kwanza Production ilipata fursa ya kutembelea maonyesho hayo na kuzungumza na baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo ambapo walieleza mengi ya kufurahisha.

KARIBU UUNGANE NASI


Zaidi ya washiriki 100 kutoka nchini Kenya waLIkuja hapa jijini kuonyesha mambo mbalimbali kama kutengeneza vyungu kwa ufinyanzi, uchongaji vinyago, mapambo ya shanga, useremala, nakshi za majengo, ujenzi wa majahazi, mapishi , muziki na mengine yanayotunza utamaduni wa nchi hiyo


Maelezo ya ujenzi na sehemu za JAHAZI (DHOW) toka kwa Ali Skanda aliyetoka Lamu Kenya
Na mtangazaji mkongwe abdushakur Aboud mbele ya Jahazi lililoletwa kwenye makumbusho ya hapa Washington DC kutoka Lamu nchini Kenya
Mtaalamu wa mapambo yatokanayo na shanga na usimamizi wa filamu nchini Kenya Emmah Irungu
Mwandishi wa habari kutoka Kenya BMJ Mureithi

Monday 16 June 2014

Mahojiano ya Kwanza Production na Fabian Lwamba wa Krystaal‏


Mubelwa Bandio wa Kwanza Production akimhoji Fabian Lwamba wa kundi la KRYSTAAL
Karibu kwenye mahojiano kati ya Kwanza Production na Fabian LwambaMmoja wa ndugu watatu wanaounda kundi la KRYSTAAL ambao walizaliwa kwenye familia iliyojiweza, lakini mgogoro wa kisiasa ukawafanya waikimbie Zaire na kutengana.
Lwamba Brothers


Walikuja kuungana Canada ambako kwa miaka 16 wamekuwa pamoja kama kundi la muziki wa injili.

Amezungumza pia mkanganyiko wa IMANI na TAMADUNI zetu.

Swali.... Ni upi muziki wa INJILI?

Na yeye ambaye ni Mchungaji katika kanisa lao, anasemaje kuhusu TOFAUTI YA KUABUDU KATI YA AFRIKA NA MAGHARIBI

Mpaka sasa, Krystaal wametoa albamu 6 na kupata tuzo 26
Karibu uungane nasi


Kwa maoni ama ushauri usisite kuwasiliana nasi kupitia kwanzaproduction at gmail.com

Wednesday 20 November 2013

Ana kwa Ana na Astronaut Dr Donald Thomas‏


Karibu katika mahojiano kamili na Dr Donald Thomas.

Mhandisi na mwanaanga wa Marekani

 Katika mahojiano haya, Dr Thomas anaeleza historia yake na namna ambavyo ALIHANGAIKA NA KUVUMILIA kabla hajapata nafasi ya kufanya kile alichokuwa akikipenda zaidi.

Ilimchukua miaka 9 tangu ajaribu kwa mara ya kwanza mpaka achaguliwe, na katika miaka hiyo, alituma maombi mara nne.

Ili kuongeza nafasi yake kufanikiwa akaamua kuchukua madarasa ya urubani, scuba diving, kufundisha, kuongeza elimu na mengine ili kufanikisha kile alichotaka kufanya japo hakukuwa na uhakika wa hilo.

Lakini aliamini katika atendalo.

Pia ameeleza maandalizi wanayofanya na mafunzo wanayopitia kuanzia wanapochaguliwa mpaka
wanapoenda kwenye mission hizo, hisia na uoga wake siku ya kwanza alipanda
space shuttle. Amezungumzia safari nzima na shughuli kuanzia
wanavyoondoka mpaka wanavyofika angani pamoja na changamoto za kuishi kwenye
orbit. Kuanzia kupika mpaka kutumia choo. Na pia, namna alivyopokea taarifa za
kulipuka kwa space shuttle Columbia. Shuttle aliyoitumia mara tatu kati ya nne
alizokwenda kwenye orbit.

Baada ya miaka 20 aliyofanya kazi kama mwanasayansi wa NASA, na safari nne kwenye Orbit, akastaafu na sasa ni Mkurugenzi wa Willard Hackerman Academy katika chuo kikuu cha Towson hapa Maryland ambapo anahimiza wanafunzi wa chekechea kujiunga na masomo ya Sayansi na Hesabu kwa manufaa ya kizazi kijacho

Nilipata fursa ya kuhojiana naye mwaka 2011




Kwa maoni, ushauri, nk usisite kutuandikia jamiiproduction@gmail.com


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Monday 18 November 2013

Dr Donald Thomas alipohojiwa na Jamii Production‏


Katika kipengele hiki cha HUYU NA YULE, wiki hii utasikia mahojiano niliyowahi kufanya na Dr Donald Thomas. Mhandisi na mwanaanga wa Marekani.

 Ilimchukua miaka 33 kutimiza ndoto zake za kuelekea kwenye Orbit. Na baada ya kwenda kwenye Orbit mara nne, akastaafu na sasa anahimiza wanafunzi wa chekechea kujiunga na masomo ya Sayansi na Hesabu kwa manufaa ya kizazi kijacho

Nilipata fursa ya kuhojiana naye ambapo alieleza mengi mema



Kwa maoni, ushauri, nk usisite kutuandikia jamiiproduction@gmail.com

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Tuesday 15 October 2013

Mahojiano ya Jamii Production na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Dr Charles Kimei‏

Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei (kulia) akizungumza na Jamii Production  ndani ya ofisi ya Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nchi za Marekani na Mexico uliopo Jijini Washington DC

Jumatano ya Oktoba 9, 2013, Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRBD Dr Charles Kimei akiambatana na Mkurugenzi wa Masoko wa (CRDB) Tully Mwambapa, Bw. Mkurugenzi wa Hazina (CRDB) Alex Ngusaru na Msaidizi wa Dk.Kimei , Kenneth Kasigila walikuwa jijini Washington DC (pamoja na mambo mengine) kueleza mipango ambayo CRDB inayo katika kuboresha huduma za akaunti ya Tanzanite pamoja na kutambulisha huduma mpya ya JIJENGE.

Jamii Production ilipata fursa ya kuhojiana na Dr Kimei ambaye amefafanua mengi kuhusu huduma hizo.

KARIBU UUNGANE NASI





Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei na akipata picha na mpiga picha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry baada ya mahojiano.

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 26 August 2012

Mario Van Peebles Exclusive Interview - Tanzania Films Critics Associati...!!!!!!


Mario Van Peebles interview with Tanzania Films Critics Association (TFCA 


The link above is about 15 Question and Answer of video Insightful interview with Film maker/Director/Producer, Actor Mario Van Peebles and Michael Cohen, talk about their new Movie "We the Party" and general view of Tanzania Film Industry in including Copyright aspects in combating piracy problems and their view of films activities here in Tanzania.
Tanzania Films Critics Association (TFCA)
----------------------------------------------

Saturday 7 April 2012

MAMA KANUMBA AONGEA;Mmmmmhh Pole sana Mama!!!!!!

Mama Mzazi wa Kanumba.
Mmmmhh,Pole sana Mama,Mungu akutie nguvu.
Picha na Video,kutoka ;http://bukobawadau.blogspot.co.uk   Ingia hapo kujua zaidi.Ahsanteni sana.

Sunday 9 October 2011

Mahojiano na Upendo Nkone, Upendo Kilahiro na Christina Shusho!!!




Habari kutoka kwa kaka Mubelwa[MB].Zaidi ingia;http:www.changamotoyetu.blogspot.com