Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Kheri na Baraka. Show all posts
Showing posts with label Kheri na Baraka. Show all posts

Wednesday 1 January 2020

Heri Ya Mwaka Mpya [Happy New Year] 2020....

Shalom,Habari,Hamjambo Wapendwa/Waungwana?
Heri Ya Mwaka Mpya...!!
Ni matumaini yangu wewe unayesoma hapa umevuka salama kutoka
mwaka 2019-2020.....
Tumshukuru Mungu katika yote yaliyopita mwaka jana..
Pia Tumshukuru Mungu kwa Neema aliyotupa ya kuingia mwaka huu 2020..

MUNGU  akatuongoze kwa kila jambo,Kama itakavyompendeza yeye...

Tukajifunze zaidi,pale tulipo jikwaa ikawe somo
Pale tulipo kosea tuka sahihishe
Pale tulipo koseana/kwazana tukasameheane na tuwe makini tusije rudia kosa..
Tukawe na kiasi...


Tukaongeze juhudi na maarifa pale tulipoishia tukaendeleze zaidi..
Na Mungu akatusadie tuweze kufanikisha kazi tuliyotumwa hapa Duniani
[Kusudi la Mungu likatimie sawasawa na mapenzi yake..]



Salaam kwa wasomaji wangu wote,wanablogu[blogger]familia..
Ndugu wa Mimi#,Msuya#[Diary yangu]
Dada wa mimi,Yasinta#[Maisha Na Mafanikio]
Dadake,#Mija[mwanamke wa Shoka]
Kakake,#Simon Kitururu
#Matondo na wengine wooote tulikuwa pamoja enzi hizo....

Nawapenda sana na nawatakia kila lililojema..
Ngoja niendelee kupika...[Jikoni Leo...?]


"Swahili Na Waswahili"2020...

Thursday 1 August 2019

Leo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwangu,Burudani-Pokea Sifa,Huniachi,Mkono wa Bwana,Zawadi gani mimi nitamtolea Bwana?..


Sifa na utukufu Namrudishia Mungu...
(mimi nitoe nini ambacho cha thamani kwako Mungu?)
Asante kwa Wazazi,Familia,Ndugu,Jamaa,Marafiki,Ninaofanya nao kazi
na wengine wote kwa sala/maombi na mengine yote...
Nawapenda kwa kumaanisha.



Mungu mlinzi wetu
1Anayekaa chini ya ulinzi wa Mungu Mkuu,
anayeishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,
2ataweza kumwambia Mwenyezi-Mungu:
“Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu;
Mungu wangu, ninayekutumainia!”
3Hakika Mungu atakuokoa katika mtego;
atakukinga na maradhi mabaya.
4Atakufunika kwa mabawa yake,
utapata usalama kwake;
mkono wake91:4 mkono: Au uaminifu. utakulinda na kukukinga.
5Huna haja ya kuogopa vitisho vya usiku,
wala shambulio la ghafla mchana;
6huna haja ya kuogopa baa lizukalo usiku,
wala maafa yanayotokea mchana.
7Hata watu elfu wakianguka karibu nawe,
naam, elfu kumi kuliani mwako,
lakini wewe baa halitakukaribia.
8Kwa macho yako mwenyewe utaangalia,
na kuona jinsi watu waovu wanavyoadhibiwa.
9Wewe umemfanya Mwenyezi-Mungu kuwa kimbilio lako;
naam, Mungu aliye juu kuwa kinga yako.
10Kwa hiyo, hutapatwa na maafa yoyote;
nyumba yako haitakaribiwa na baa lolote.
11 Taz Mat 4:6; Luka 4:10 Maana Mungu atawaamuru malaika zake,
wakulinde popote uendapo.
12 Taz Mat 4:6; Luka 4:11 Watakuchukua mikononi mwao,
usije ukajikwaa kwenye jiwe.
13 Taz Luka 10:19 Utakanyaga simba na nyoka,
utawaponda wana simba na majoka.
14Mungu asema: “Nitamwokoa yule anipendaye;
nitamlinda anayenitambua!
15Akiniita, mimi nitamwitikia;
akiwa taabuni nitakuwa naye;
nitamwokoa na kumpa heshima.
16Nitamridhisha kwa maisha marefu,
nitamjalia wokovu wangu.”

Zaburi 91








Mafundisho kuhusu sala
1Kwanza kabisa, nawasihi muombe dua, msali na kumshukuru Mungu kwa ajili ya watu wote, 2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema. 3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu, 4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli. 5Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu, 6ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia, kwamba Mungu anataka kuwaokoa watu wote. 7Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi. 9Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa, 10bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu. 11Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza. 12Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya. 13Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa. 14Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu. 15Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.

1 Timotheo 2








Shukrani;

POKEA SIFA - The Light Bearers


MKONO WA BWANA by Zabron singers


Apostle John Komanya - Zawadi gani

Huniachi (Album Usifadhaike) - by Reuben Kigame and Sifa Voices Featuring Gloria Muliro


"Swahili Na Waswahili" Mungu yu mwema

Sunday 2 September 2018

Natumaini Jumapili ni njema/inaendelea vyema;Burudani-No Longer Slaves - Jonathan David & Melissa Helser ,Who You Say I Am - Hillsong Worship,Passion - Let It Be Jesus ft. Christy Nockels




Wapendwa/Waungwana;Nawatakia kila la heri,baraka na amani....





+


















Neno La Leo;Wafilipi 2;12-18

Mwanga kwa ulimwengu

12Wapenzi wangu, nilipokuwa nanyi mlinitii daima, na hata sasa niwapo mbali nanyi endeleeni kutii. Fanyeni kazi kwa hofu na tetemeko kwa ajili ya ukombozi wenu, 13kwani Mungu ndiye afanyaye kazi daima ndani yenu, na kuwapeni uwezo wa kutaka na kutekeleza mambo yanayopatana na mpango wake mwenyewe.
14Fanyeni kila kitu bila kunungunika na bila ubishi, 15ili mpate kuwa watu safi, wasio na lawama, kama watoto wanyofu wa Mungu wanaoishi katika ulimwengu mbaya na uliopotoka. Mtangara kati yao kama nyota zinavyoliangaza anga, 16mkishika imara ujumbe wa uhai. Na hapo ndipo nami nitakapokuwa na sababu ya kujivunia katika siku ile ya Kristo, kwani itaonekana dhahiri kwamba bidii yangu na kazi yangu havikupotea bure.
17Hata ikiwa nitatolewa mhanga pamoja na imani yenu iliyo tambiko kwa Mungu, basi, nafurahi sana na kuwashirikisha nyinyi nyote furaha hiyo. 18Hali kadhalika nanyi mnapaswa kufurahi na kunishirikisha mimi furaha yenu.











"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 3 August 2018

Shukrani zangu kwenu kwa maombi,sala/dua kwenye kumbumkumbu ya kuzaliwa kwangu..

Hamjambo Wapendwa/Waungwana?
Mimi na Familia yangu hatujambo Mungu yu mwema..!!
Tarehe 1/8  ni siku ya kumbukumbu yangu ya kuzaliwa...
Namshukuru sana Mungu kwakunipa  kibali cha kuuona mwaka mwingine....

Maombi yangu  ikimpendeza Mungu anipe miaka mingi yenye
Amani,Busara,Hekima,Shukrani,Furaha  na kumtegemea yeye Mungu zaidi katika safari yangu ya maisha.....

Shukrani kwa  Familia yangu,Ndugu,Jamaa na Marafiki kwa Maombi,sala/duwa zetu na katika yote..
Mungu aendelee kuwabariki na kuwaongezea  zaidi ya pale mlipojitoa...
Nawapenda.

Ombi langu kwako wewe unayesoma hapa
ikikupendeza naomba upitie
Neno La Mungu;Luka1;1-80
na ukipata kibali/ukiguswa unaweza kushiriki nasi
kwa njia ya Email;rasca@hotmail.co.uk
Sms/WhatsApp;+44 750 44 100 40
au comment...wewe umejifunza nini kupitia Neno hili
au umelielewaje?
Nitafurahi sana.....



1Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu. 2Waliyaandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona mambo hayo kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo. 3Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango, 4ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
Ahadi ya kuzaliwa kwa Yohane
5Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha ukuhani cha Abiya. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni. 6Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama. 7Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8Siku moja, ilipokuwa zamu yake kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu, 9Zakaria alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani. 10Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani. 11Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani. 12Zakaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia. 13Lakini malaika akamwambia, “Zakaria, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane. 14Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake. 15Atakuwa mkubwa mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake. 16Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao. 17Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama ya Elia. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
18Zakaria akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.” 19Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu; nimetumwa niseme nawe, nikuletee hizi habari njema. 20Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
21Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakaria huku wakishangaa juu ya kukawia kwake hekaluni. 22Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani. 24Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema: 25“Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
Ahadi ya kuzaliwa kwa Yesu
26Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, 27kwa msichana mmoja bikira aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. 28Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu, ewe uliyejaliwa neema na Mungu! Bwana yuko nawe!”
29Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: Maneno hayo yanamaanisha nini? 30Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. 31Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu. 32Yeye atakuwa mkubwa na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake. 33Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”
34Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?” 35Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu. 36Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa. 37Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.” 38Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
Maria anamtembelea Elisabeti
39Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yudea. 40Huko, aliingia katika nyumba ya Zakaria, akamsalimu Elisabeti. 41Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu, 42akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa. 43Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu? 44Nakuambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha. 45Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokuambia.”
Utenzi wa Maria
46Naye Maria akasema,
“Moyo wangu wamtukuza Bwana,
47roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu.
Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49Kwa kuwa Mungu Mwenye Nguvu amenifanyia makuu,
jina lake ni takatifu.
50Huruma yake kwa watu wanaomcha
hudumu kizazi hata kizazi.
51Amefanya mambo makuu kwa mkono wake:
Amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52amewashusha wenye nguvu kutoka viti vyao vya enzi,
akawakweza wanyenyekevu.
53Wenye njaa amewashibisha mema,
matajiri amewaondoa mikono mitupu.
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake,
akikumbuka huruma yake,
55kama alivyowaahidia wazee wetu,
Abrahamu na wazawa wake hata milele.”
56Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
Kuzaliwa kwa Yohane Mbatizaji
57Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume. 58Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakaria. 60Lakini mama yake akasema, “Sivyo, bali ataitwa Yohane.” 61Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?” 62Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani. 63Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu. 64Papo hapo, midomo na ulimi wake Zakaria vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu. 65Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea. 66Wote waliosikia mambo hayo, waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
Utenzi wa Zakaria
67Zakaria, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka unabii huu:
68“Atukuzwe Bwana Mungu wa Israeli,
kwani amewajia na kuwakomboa watu wake.
69Ametupatia Mwokozi shujaa,
mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70Aliahidi hapo kale
kwa njia ya manabii wake watakatifu,
71kwamba atatuokoa mikononi mwa maadui zetu
na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72Alisema atawahurumia wazee wetu,
na kukumbuka agano lake takatifu.
73Alimwapia Abrahamu babu yetu,
kwamba atatujalia sisi
74tukombolewe mikononi mwa maadui zetu,
tupate kumtumikia bila hofu,
75tuwe wanyofu na waadilifu mbele yake,
siku zote za maisha yetu.
76Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu,
utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77kuwatangazia watu kwamba wataokolewa
kwa kuondolewa dhambi zao.
78Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma.
Atatuchomozea mwanga kutoka juu,
79na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo,
aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
80Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionesha rasmi kwa watu wa Israeli.

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Sunday 15 July 2018

Natumaini Jumapili ni Nejma;Burudani-MKONO WA BWANA by Zabron singers kahama ,WALTER CHILAMBO - ONLY YOU..








Hamjambo Juma pili yako ilikuwaje/inaendeleaje?
Hapa kwetu ni salama kabisa Mungu yu mwema..
hali ya hewa ni joto kijua kinawaka ni shangwe tuu....!!
Niwatakie kila lililojema na mapumziko mema tayari kwa kujiandaa na 
pilika za juma tatu.....

Neno La Leo Methali 30;1-14



Mawaidha ya Aguri

1Maneno ya Aguri, mwana wa Yake. Mawaidha ambayo mtu huyu alimwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.30:1 Ithieli, Ukali: Majina hayo yaweza kumaanisha Nimechoka ee Mungu; nimechoka na sina nguvu.
2Mimi ni mpumbavu mno, wala si mtu;
nayo akili ya binadamu sina.
3Sijajifunza hekima,
wala sijui kitu juu ya Mungu Mtakatifu.
4Ni nani aliyepanda juu mbinguni akashuka chini?
Ni nani aliyekamata upepo mkononi?
Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa?
Ni nani aliyeiweka mipaka yote ya dunia?
Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe?
Niambie kama wajua!
5Maneno yote ya Mungu ni ya kuaminika;
yeye ni ngao yao wote wanaomkimbilia.
6Usiongeze neno katika maneno yake,
asije akakukemea, nawe ukaonekana mwongo.
7Mambo haya mawili nakuomba ee Mungu,
wala usinikatalie kabla sijafa:
8Uniondolee uongo na udanganyifu;
usinipe umaskini wala utajiri;
unipatie chakula ninachohitaji,
9nisije nikashiba nikakukana;
nikasema, “Mwenyezi-Mungu ni nani?”
Au nisije nikawa maskini nikaiba,
na kulikufuru jina lako ee Mungu wangu.
10Usimchongee mtumwa kwa bwana wake,
asije akakulaani, ukaonekana una hatia.
11Kuna watu ambao huwalaani baba zao,
wala hawana shukrani kwa mama zao.
12Kuna watu ambao hujiona kuwa wema,
kumbe bado hawajatakaswa uchafu wao.
13Kuna na wengine – kiburi ajabu!
Hudharau kila kitu wanachokiona.
14Kuna watu ambao meno yao ni kama upanga,
na magego yao ni kama visu.
Wako tayari kuwatafuna maskini wa nchi,
na wanyonge walio miongoni mwa watu!







"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe sana.

Sunday 3 June 2018

Jumapili Njema;Burudani-at the cross,Lion And The Lamb




Natumaini hamjambo,Jumapili yako ilikuwaje/inaendeleaje?
Hapa kwetu ni salama kabisa Mungu yu mwema ametupa kibali cha  kuungana na wapendwa wengine katika ibada ya Jumapili na ilikuwa njema....
Niwatakie kila lililo jema Na wale wanaorudi shuleni kesho Mungu akawaongoze,
Wafanyakazi/waliojiajili Mungu akabariki kazi za mikono yenu....

Neno la Leo;1Wafalme17;1-24









1Basi Elia wa kijiji cha Tishbe huko Gileadi, akamwambia mfalme Ahabu, “Ninaapa kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli aliye hai ambaye mimi ninamtumikia: Hakutakuwa na umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.” 2Kisha, neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Elia: 3“Ondoka hapa uelekee mashariki, ukajifiche penye kijito cha Kerithi kilichoko mashariki ya mto Yordani. 4Huko, utapata maji ya kunywa katika kijito hicho tena nimewaamuru kunguru wakuletee chakula.” 5Basi, Elia akatii agizo la Mwenyezi-Mungu, akaenda kukaa kwenye kijito cha Kerithi kilichoko mashariki ya mto Yordani. 6Kunguru wakawa wanamletea mkate na nyama, asubuhi na jioni; akapata na maji ya kunywa katika kijito hicho. 7Lakini, baada ya siku chache kijito kikakauka kwa sababu hapakunyesha mvua nchini.
Elia na mama mjane wa Sarefathi
8Hapo, neno la Mwenyezi-Mungu, lilimjia Elia: 9“Ondoka uende mjini Sarefathi, karibu na Sidoni, ukae huko. Nimemwamuru mwanamke mmoja mjane akupatie chakula huko.” 10Basi, Elia akaondoka, akaenda Sarefathi. Alipofika penye lango la mji, alimkuta mwanamke mmoja mjane anaokota kuni. Elia akamwita mwanamke huyo na kumwambia “Niletee maji ninywe.” 11Yule mwanamke alipokuwa anaondoka, Elia akamwita tena na kumwambia, “Niletee na kipande cha mkate pia.” 12Huyo mwanamke akamwambia, “Nakuapia kwa jina la Mwenyezi-Mungu, Mungu wako aliye hai, sina mkate hata kidogo. Nilicho nacho ni konzi ya unga katika chungu na mafuta kidogo katika chupa. Nimefika hapa kuokota kuni, kisha niende nyumbani kupika chakula hicho, mwanangu na mimi tule, kisha tufe.” 13Elia akamwambia, “Usiogope. Nenda ukafanye kama ulivyosema. Lakini nitengenezee mimi kwanza na kuniletea andazi dogo, kisha jitengenezee wewe na mwanao chakula. 14Maana, Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, asema hivi: ‘Unga ulioko chunguni mwako hautapungua wala mafuta yaliomo ndani ya chupa hayataisha, mpaka hapo mimi Mwenyezi-Mungu nitakaponyesha mvua nchini.’” 15Basi, huyo mwanamke mjane akaenda akafanya kama alivyoambiwa na Elia hata mama huyo, jamaa yake na Elia wakapata chakula kwa siku nyingi. 16Unga chunguni haukupunguka, wala mafuta katika chupa hayakwisha sawa kabisa na neno la Mwenyezi-Mungu alilomwambia Elia aseme.
Elia anamfufua mtoto wa mama mjane
17Baada ya hayo, mwana wa mwanamke huyo mwenye nyumba akaugua, na hali yake ikazidi kuwa mbaya, hata mwishowe akafariki. 18Huyo mwanamke akamwambia Elia, “Ewe mtu wa Mungu, una kisa gani nami? Kumbe ulikuja kwangu kuzifichua dhambi zangu na kusababisha kifo cha mwanangu?” 19Elia akamwambia, “Nipe mwanao.” Basi, Elia akamtwaa mtoto kifuani pa mama yake, akamchukua juu chumbani mwake, akamlaza juu ya kitanda chake. 20Kisha akamsihi Mwenyezi-Mungu akisema, “Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, je, hata mwanamke huyu mjane ambaye ninakaa kwake, naye ananitunza, unamletea balaa kwa kumwua mwanawe?” 21Kisha Elia akajinyosha juu ya mtoto huyo mara tatu na kumwomba Mwenyezi-Mungu, “Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, mrudishie mtoto huyu roho yake!” 22Mwenyezi-Mungu akasikiliza ombi la Elia; mtoto akaanza kupumua tena. 23Elia akamrudisha mtoto chini kwa mama yake, akamwambia, “Tazama! Mwanao yu hai.” 24Huyo mwanamke mjane akamwambia Elia, “Sasa najua kwa hakika kwamba wewe ni mtu wa Mungu, na maneno aliyokupa Mwenyezi-Mungu uyaseme ni ya kweli.”










"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Sunday 27 May 2018

Natumai Jumapili ilikuwa/inaendelea Vyema;Burudani-NAKUSHUKURU MUNGU,AUNGURUMAPO SIMBA,KWA NEEMA - UKOMBOZI KKKT MSASANI






Wapendwa/waungwana  Nimatumaini yangu mmekuwa na jumapili njema
Hapa kwetu ni salama kabisa na Mungu ametupa kibali cha kushiriki ibada na wapendwa 
wengine kanisani...
Basi muendelee luwa na wakati mwema na Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea
sawasawa na mapenzi yake.....


Neno La leo;Yakobo 4;1-17


Mapigano na ugomvi wote kati yenu vinatoka wapi? Hutoka katika tamaa zenu mbaya ambazo hupigana daima ndani yenu. Mnatamani vitu na kwa vile hamvipati mko tayari kuua; mwatamani sana kupata vitu, lakini hamvipati; hivyo mnagombana na kupigana. Hampati kile mnachotaka kwa sababu hamkiombi kwa Mungu. Tena, mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya; mnaomba ili mpate kutosheleza tamaa zenu. Nyinyi ni watu msio na uaminifu kama wazinzi. Je, hamjui kwamba kuwa rafiki wa ulimwengu ni kuwa adui wa Mungu? Yeyote anayetaka kuwa rafiki wa ulimwengu anajifanya adui wa Mungu. Msifikiri kwamba Maandiko Matakatifu yamesema maneno ya bure, yanaposema: “Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu ana wivu mkubwa.” Lakini, neema tunayopewa na Mungu ina nguvu zaidi; kama yasemavyo Maandiko: “Mungu huwapinga wenye majivuno lakini huwapa neema wanyenyekevu.” Basi, jiwekeni chini ya Mungu; mpingeni Ibilisi naye atawakimbieni. Mkaribieni Mungu, naye atakuja karibu nanyi. Osheni mikono yenu enyi wakosefu! Safisheni mioyo yenu enyi wanafiki! Oneni huzuni, lieni na kuomboleza; kicheko chenu na kiwe kilio; na furaha yenu iwe huzuni kubwa. Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni. Ndugu, msilaumiane nyinyi kwa nyinyi. Anayemlaumu ndugu yake na kumhukumu, huyo huilaumu na kuihukumu sheria. Kama ukiihukumu sheria, basi, wewe huitii sheria, bali waihukumu. Mungu peke yake ndiye mwenye kuweka sheria na kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi, wewe ni nani hata umhukumu binadamu mwenzako? Basi, sasa sikilizeni nyinyi mnaosema: “Leo au kesho tutakwenda katika mji fulani na kukaa huko mwaka mzima tukifanya biashara na kupata faida.” Nyinyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Nyinyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena. Mngalipaswa kusema: “Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile.” Lakini sasa mwajivuna na kujigamba; majivuno ya namna hiyo ni mabaya. Basi, mtu ambaye hafanyi lile jambo jema analojua kwamba anapaswa kulifanya, anatenda dhambi.














"Sawahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

Sunday 18 February 2018

Nawatakia Jumapili yenye Amani;Mungu akawafariji waliopoteza wapendwa wao Tanzania,Burudani-Kinondoni Revival Choir Nafsi Yangu Yakutamani,Twalilia Tanzania,Ukifa utakwenda wapi?...



Shalom Wapendwa/Waungwana,Nimatumaini yangu Jumapili ilikuwa njema/inaendelea vyema
Upande huu ni njema kabisa tunaungana na wapendwa wetu huko Nyumbani Tanzania
Familia/ndugu,jamaa waliopoteza wapendwa wao sababu ya siasa na mengineyo
Mungu akawafariji,akawape nguvu,uvumilivu,imani 
Mungu akaiongoze na kuwaongoza wa Tanzania wakawe salama moyoni,Amani ikatawale,huruma,upendo ukadumu kati yetu..
Mungu wetu  ukawe dereva wa hii gari Tanzania ,ukatupitishe njia zilizo zako  maana njia zako ni salama,hizi njia zetu hazita tufikisha tuendako siko kabisa....
Neno lal leo;2 Timotheo 3:1-17


Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. Watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu; watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema; watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo. Baadhi yao huenda katika nyumba za watu na huwateka wanawake dhaifu waliolemewa mizigo ya dhambi na ambao wanaongozwa na tamaa za kila aina; wanawake ambao wanajaribu daima kujifunza lakini hawawezi kuufikia ujuzi wa huo ukweli. Watu hao huupinga ukweli kama vile Yane na Yambre walivyompinga Mose. Hao ni watu wa akili potovu na imani ya uongo. Lakini hawataweza kuendelea zaidi kwa maana upumbavu wao utaonekana wazi kwa wote. Ndivyo ilivyokuwa kwa akina Yane na Yambre. Wewe, lakini, umeyafuata mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudi yangu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, subira yangu, udhalimu na mateso. Unayajua mambo yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Lustra. Nilivumilia udhalimu mkubwa mno! Lakini Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote. Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya kumcha Mungu katika kuungana na Kristo Yesu lazima adhulumiwe. Watu waovu na wadanganyifu wataendelea kuwa wabaya, wakidanganya wengine, na wao wenyewe wakidanganywa. Lakini wewe dumu katika ukweli ule uliofundishwa ukaukubali kabisa. Wawajua wale waliokuwa waalimu wako, wakumbuka kwamba tangu utoto wako umejua Maandiko Matakatifu ambayo yaweza kukupatia hekima iletayo wokovu kwa njia ya imani kwa Kristo Yesu. Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, kuonya, kusahihisha makosa, na kuwaongoza watu waishi maisha adili, ili mtu wa Mungu awe mkamilifu, na tayari kabisa kufanya kila kazi njema.

2 Timotheo 3:1-17








"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

Sunday 11 February 2018

Natumaini Jumapili imekuwa njema/inaendelea vyema;Burudani-Mungu Hawezi kukusahau,Siku Ya Furaha ni Leo,Umenifanya Ibada,Kwa Viwango Vingine...

Shalom..!!Hamjambo wapendwa/Waungwana?
Ni Jumapili nyingine tena Mungu ametupa kibali cha kuiona na kuabudu..
Mungu wetu yu mwema sana upande huu..
Ni matumaini yangu nawe unayesoma hapa/uliyepita hapa umekuwa na wakati mzuri..
Kama ndiyo sema Ameeeen..!!
Kama siyo Mungu hajakuacha wala hajakusahau endelea kumtumainia yeye tuu
ni swala la muda/wakati yeye hutenda kwa wakati unaofaa na atakutendea sawasawa na mapenzi yake..
Niwatakie kila lililo jema,furaha,mkawe salama moyoni,amani ya Kristo Yesu ikawe nanyi,Upendo ukadumu kati yetu..




Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii, lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu, akamteua avimiliki vitu vyote. Yeye ni mngao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwatakasa binadamu dhambi zao, ameketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.

Neno La Leo;Waebrania 1:1-14




Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii, lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu, akamteua avimiliki vitu vyote. Yeye ni mngao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwatakasa binadamu dhambi zao, ameketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu. Mwana ni mkuu kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu kuliko jina lao. Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Wewe ni Mwanangu; mimi leo nimekuwa Baba yako.” Wala hakusema juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu.” Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae, mzaliwa wa kwanza, ulimwenguni alisema: “Malaika wote wa Mungu na wamwabudu.” Lakini kuhusu malaika, alisema: “Amewafanya malaika wake kuwa upepo, na wahudumu wake ndimi za moto.” Lakini kuhusu Mwana, Mungu alisema: “Kiti chako cha enzi, ee Mungu, chadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki. Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako, amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa kuliko wenzako.” Na tena: “Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako. Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi. Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma.” Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.” Malaika ni nini ila roho wanaomtumikia Mungu na ambao hutumwa kuwasaidia wale watakaopokea wokovu?









"Swahili Na Waswahili"Mungu awabariki.

Thursday 4 January 2018

SALAAM ZA MWAKA MPYA;BURUDANI-SLIGHT BEARERS- INUA MACHO,POKEA SIFA,SIFA KWA BWANA..




Salaam Wapendwa/Waungwana;Heri ya Mwaka Mpya..!
Ni matumaini yangu wote mpo salama na Mungu anaendelea kuwapigania..
Tunamshukuru Mungu kwa nafasi hii tena ya kuuona mwaka huu..
Mwaka uliyopita pia natumai ulikuwa na Baraka nyingi hata kama kulikuwa na mapito/Mjaribu yoyote ni changamoto katika maisha..
Mungu wetu atabaki kuwa Mungu..
Mimi namshukuru Mungu kwa yote aliyonitendea,kuna mengi mazuri na yaliyo mema,
Baraka na palipo kuwa na ugumu/mapito ilikuwa njia ya kujifunza zaidi na kujiweka sawa
kwa yanayokuja..
Mwaka huu ukawe mwaka wenye Amani,Upendo,Furaha,Ushidi,Afya njema,Mafanikio,
Mungu akatupe neema ya kufuata njia zake,Tukasimamie Neno lake amri na sheria zake
siku zote za maisha yetu..
Mungu wetu akatubariki nasi tukapate Neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Tukapande katika wema,fadhili,Hekima,Busara na yote yanayompendeza Mungu wetu na tukavune yaliyo yake Mungu wetu..
Uwe Mwaka wa Shukrani,Shuhuda na kujitoa kwa wengine..
Tukawe salama moyoni na Mungu wetu akatuongoze katika yote..
Asanteni sana na Mungu akawatendee sawasawa na Mapenzi yake..
Nawapenda.














"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Sunday 6 August 2017

Natumaini Jumapili ilikuwa/inaendelea Vyema;[Shukrani zangu kwenu]..Burudani-Mercy Masika & Angel Benard - Huyu Yesu,SINACH - I KNOW WHO I AM,EBEN-VICTORY...

Wapendwa/Waungwana nimatumaini yangu wote hamjambo na Mungu anawatendea sawasawa na mapenzi yake..
Hapa tulipo Jumapili inaendelea vyemakabisa na Bwana ametupa kibali cha kuungana na wengine katika Ibada..
Natumaini nawe unayesoma hapa umepata neema/kibali cha kushiriki na wenzio..
na kama ulikosa Mungu akakupe neema ya kuweza kushiriki wakati mwingine..


Shukrani zangu kwa wote mlioniombea na kunitakia heri kwa Anniversary yetu mimi na Isaac..
Pia kwa Birthday yangu..Asanteni sana na Mungu aendelee kuwabariki na kuongezea zaidi ya mlipojiatoa..
Tulikuwa na wakati mzuri sana na Tunamshukuru Mungu kwa neema na kibali alichotupa cha kuendelea kufikia hapa tulipo..
Shukrani kwa wazazi wangu,Mume wangu na watoto wetu,Ndugu,Jamaa na marafiki wote..
Nawapenda...!

Neno La Shukrani;

Nakushukuru, ee Mwenyezi-Mungu, kwa moyo wangu wote, naimba sifa zako mbele ya miungu. Ninasujudu kuelekea hekalu lako takatifu; nalisifu jina lako, kwa sababu ya fadhili zako na uaminifu wako; kwa sababu umeweka jina lako na neno lako juu ya kila kitu. Nilipokulilia, wewe ulinijibu; umeniongezea nguvu zangu. Wafalme wote duniani watakusifu, ee Mwenyezi-Mungu, kwa sababu wameyasikia maneno yako. Wataimba sifa za matendo yako, ee Mwenyezi-Mungu, kwa maana utukufu wako ni mkuu. Ingawa wewe ee Mwenyezi-Mungu, uko juu ya wote, unawaangalia kwa wema walio wanyonge; nao wenye kiburi huwaona kutoka mbali. Hata nikikumbana na taabu, wewe wanilinda; waunyosha mkono wako dhidi ya hasira ya maadui zangu wakali; kwa nguvu yako kuu wanisalimisha. Ee Mwenyezi-Mungu, utatimiza yote uliyoniahidi. Fadhili zako, ee Mwenyezi-Mungu, zadumu milele. Usisahau kazi ya mkono wako mwenyewe.
Zaburi 138:1-8


Ee Mwenyezi-Mungu, wewe umenichunguza; wewe wanijua mpaka ndani. Nikiketi au nikisimama, wewe wajua; wajua kutoka mbali kila kitu ninachofikiria. Watambua nikienda au nikipumzika; wewe wazijua shughuli zangu zote. Kabla sijasema neno lolote, wewe, ee Mwenyezi-Mungu, walijua kabisa. Uko kila upande wangu, mbele na nyuma; waniwekea mkono wako kunilinda. Maarifa yako yapita akili yangu; ni makuu mno, siwezi kuyaelewa. Nikimbilie wapi ambako roho yako haiko? Niende wapi ambako wewe huko? Nikipanda juu mbinguni, wewe upo; nikijilaza chini kuzimu, wewe upo. Nikiruka hadi mawio ya jua, au hata mipakani mwa bahari, hata huko upo kuniongoza; mkono wako wa kulia utanitegemeza. Kama ningeliomba giza linifunike, giza linizunguke badala ya mwanga, kwako giza si giza hata kidogo, na usiku wangaa kama mchana; kwako giza na mwanga ni mamoja. Wewe umeniumba, mwili wangu wote; ulinitengeneza tumboni mwa mama yangu. Nakusifu maana nimefanywa kwa namna ya ajabu, matendo yako ni ya ajabu; wewe wanijua kabisakabisa. Umbo langu halikufichika kwako nilipotungwa kwa siri na ustadi ndani ya dunia. Wewe uliniona hata kabla sijazaliwa, uliandika kila kitu kitabuni mwako; siku zangu zote ulizipanga, hata kabla ya kuweko ile ya kwanza. Ee Mungu, mawazo yako ni makuu mno; hayawezi kabisa kuhesabika. Ningeyahesabu yangekuwa mengi kuliko mchanga. Niamkapo, bado nipo pamoja nawe.


                                                Amina...!!!


 Neno La Leo;

Maadamu Kristo aliteseka kimwili, nanyi pia mnapaswa kujiimarisha kwa nia hiyo yake; maana mtu akisha teseka kimwili hahusiki tena na dhambi. Tangu sasa, basi, maisha yaliyowabakia kuishi hapa duniani yanapaswa kuongozwa na matakwa ya Mungu, sio na tamaa za kibinadamu. Wakati uliopita mlikuwa na muda mrefu wa kufanya mambo wanayofanya watu wasiomjua Mungu. Mliishi maisha ya anasa, ubinafsi, ulevi, ugomvi, kunywa mno na ya ibada haramu za sanamu. Sasa, watu hao wasiomjua Mungu wanashangaa wanapoona kwamba hamwandamani nao tena katika hali ya kuishi vibaya, na hivyo wanawatukaneni. Lakini watapaswa kutoa hoja juu ya jambo hilo mbele yake Mungu aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa! Ndiyo maana Habari Njema ilihubiriwa hata kwa hao waliokufa, ili baada ya kuhukumiwa katika maisha yao ya kimwili kama wengine, waishi kwa ajili ya Mungu kwa njia ya Roho. Mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na kukesha ili muweze kusali. Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi. Muwe na ukarimu nyinyi kwa nyinyi bila kunung'unika. Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine kama wakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu. Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumikia anapaswa kutumikia kwa nguv
u anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina. Wapenzi wangu, msishangae kuhusu majaribio makali mnayopata kana kwamba mnapatwa na kitu kisicho cha kawaida. Ila furahini kwamba mnashiriki mateso ya Kristo ili muweze kuwa na furaha tele wakati utukufu wake utakapofunuliwa. Heri yenu ikiwa mnatukanwa kwa sababu ya jina la Kristo; jambo hilo lamaanisha kwamba Roho mtukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa nanyi. Asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu ambaye anapaswa kuteseka kwa sababu ni mwuaji, mwizi, mhalifu au mwovu. Lakini kama mtu akiteseka kwa sababu ni Mkristo, basi, asione aibu, bali amtukuze Mungu, kwa sababu mtu huyo anaitwa kwa jina la Kristo. Wakati wa hukumu umefika, na hukumu hiyo inaanza na watu wake Mungu mwenyewe. Ikiwa hukumu hiyo inaanzia kwetu sisi, basi, mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasioamini Habari Njema ya Mungu? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Ni vigumu kwa watu waadilifu kuokolewa; itakuwaje basi, kwa wasiomcha Mungu na wenye dhambi?” Kwa hiyo, wale wanaoteseka kufuatana na matakwa ya Mungu, wanapaswa, kwa matendo yao mema, kujiweka chini ya Muumba wao ambaye ni wa kuaminika kabisa.

1 Petro 4:1-19
Mungu aendelee kuwabariki na kuwalinda wakati wote..
Wenu Rachel-siwa na kwaniaba ya familia yangu
tunasena Asanteni Sana.



















"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.