Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 22 August 2017

Kikombe Cha Asubuhi;kitabu cha Hesabu..36-Mwisho wa kitabu cha Hesabu,Mungu wetu yu Mwema..




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Mungu wetu yu mwema sana..Tumshukuru Mungu katika yote..
Mtakatifu..Mtakatifu..Mtakatifu..!!
Baba wa Mbinguni,Mungu wetu na Muumba wetu..
Kimbilio letu na Mponyaji wetu,Mungu wa Wajane na Yatima..
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..!
Muweza wa yote,Baba wa Upendo,Baba wa Rehema..
Unastahili sifa Baba wa Mbinguni,Unastahili kuabudiwa Mungu wetu..
Hakuna kama wewe,wewe ni Alfa na Omega..

Jehovah..!Jehovah Nissi..!Jehovah Rapha..!Jehovah Shammah..!Jehovah Jireh..!Jehovah Shalom..!

Yahweh..!El Shaddai..!El Olam..!El him..!Adonai..!!!!!!!
Emanueli...Mungu pamoja nasi..!Unatosha Baba wa Mbinguni..!


Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu; yeye ni msaada wetu daima wakati wa taabu. Kwa hiyo hatutaogopa chochote, dunia ijapoyeyuka na milima kutikisika kutoka baharini; hata kama bahari ikichafuka na kutisha, na milima ikatetemeka kwa machafuko yake. Kuna mto ambao maji yake hufurahisha mji wa Mungu, makao matakatifu ya Mungu Mkuu. Mungu yumo mjini humo, nao hauwezi kutikiswa; Mungu ataupa msaada alfajiri na mapema. Mataifa yaghadhibika na tawala zatikisika; Mungu anguruma nayo dunia yayeyuka. Mwenyezi-Mungu wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu. Njoni mwone matendo ya Mwenyezi-Mungu; oneni maajabu aliyoyafanya duniani. Hukomesha vita popote duniani, huvunjavunja pinde na mikuki, nazo ngao huziteketeza. Asema: “Nyamazeni na kujua kuwa mimi ni Mungu! Mimi natukuka katika mataifa yote; mimi natukuzwa ulimwenguni kote!” Mwenyezi-Mungu wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..

Si kwa uwezo wetu wala si kwanguvu zetu Mungu wetu sisi kuwa hivi tulivyo..
Ni kwa Neema/rehema zako Jehovah..
Tunajishusha mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Baba wa Mbinguni..tunaomba utusamehe dhambi zetu zote ..
Tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mungu wetu tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea..
Mfalme wa Amani ukatamalaki na kutuatamia katika Nyumba zetu/Ndoa,watoto/familia,Ndugu/jamaa na wote wanaotuzunguka..
Baba wa Mbingu ukatuguse na mkono wako wenye nguvu..
Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu na ukatufunike kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Yahweh tunaomba utuepushe katika majaribu na utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..

Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu atautwaa upanga wake mkubwa, mkali na imara, na kuliadhibu dude Lewiyathani joka lirukalo na danganyifu; Mwenyezi-Mungu ataliua joka liishilo baharini. Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu atasema hivi: “Imbeni utenzi wa shamba langu zuri la mizabibu! Mimi, Mwenyezi-Mungu, ni mkulima wake; nalimwagilia maji kila wakati, ninalilinda usiku na mchana, lisije likaharibiwa na mtu yeyote. Silikasirikii tena shamba hili; kama miiba na mbigili ingelilivamia, mimi ningepambana nayo na kuichoma moto. Maadui za watu wangu wakitaka ulinzi wangu, basi, na wafanye amani nami; naam, wafanye amani nami.” Itakuja siku wazawa wa Yakobo watashika mizizi; naam, watu wa Israeli watachanua na kuchipua, na kuijaza dunia yote kwa matunda. Mungu hakuwaadhibu Waisraeli vikali kama alivyowaadhibu maadui wake; Waisraeli waliopotea vitani, ni wachache kuliko wale wa maadui zake. Aliwaadhibu watu wake kwa kuwapeleka uhamishoni. Wakati wa upepo mkali wa mashariki, aliwaondoa kwa kipigo kikali. Hivi ndivyo uovu wa wazawa wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo dhambi yake itakavyofutwa kabisa: Ataziharibu madhabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa; Ashera, wala madhabahu za kufukizia ubani hazitabaki. Mji ule wa ngome sasa umekuwa mtupu, umeachwa na kuhamwa kama jangwa, humo ndama wanalisha na kupumzika. Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; kina mama huyaokota wakawashia moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawafadhili. Siku hiyo, kutoka mto Eufrate hadi mpakani mwa Misri, Mwenyezi-Mungu ataipura nafaka yake, nanyi Waisraeli mtakusanywa mmojammoja. Siku hiyo, tarumbeta kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea nchini Ashuru au waliotawanywa nchini Misri watarudi na kumwabudu Mwenyezi-Mungu juu ya mlima mtakatifu huko Yerusalemu.


Roho Mtakatifu akatuongoze katika maisha yetu,tupate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..
Mungu wetu tunaomba Ukatubariki na ukabariki kazi za mikono yetu na vyote tunavyoenda kufanya/kutenda Baba wa Mbinguni tukatende sawasawa na mapezni yako..

Vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Mungu wetu ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe..
Ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo Yahweh nasi ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji....


Tazama wenye Shida/tabu,Mungu wetu na wote wanaopitia magumu/majaribu,walio katika vifungo mbalimbali Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu,wakapate kupona kimwili na kiroho pia..

wakaijue kweli yako na kusimamia Neno lako,Amri na sheria zako..nazo ziwaweke huru..



Hata hivyo, Mwenyezi-Mungu anangoja awafadhili, atainuka na kuwaonea huruma. Maana, Mwenyezi-Mungu ni Mungu atendaye haki. Heri wote wale wanaomtumainia. Enyi watu wa Siyoni, enyi watu wa Yerusalemu, hakika nyinyi hamtaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikeni. Ingawa Bwana atawalisha taabu na kuwanywesha dhiki, yeye ndiye Mwalimu wenu na hatajificha tena; nanyi mtamwona kwa macho yenu wenyewe. Mkienda kulia au kushoto, mtasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Njia ni hii; ifuateni.” Mtavifanya haramu vinyago vyenu vya miungu vilivyopakwa fedha na sanamu zenu zilizopakwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitu najisi, mkisema, “Poteleeni mbali!” Mtakapopanda mbegu zenu, Mwenyezi-Mungu atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakua na kuwapa mavuno mengi. Mifugo yenu nayo itapata malisho kwa wingi. Mafahali na punda wenu wa kulimia watapata malisho yaliyochambuliwa vizuri na kutiwa chumvi. Wakati utakapofika ambapo maadui watauawa na ngome zao kubomolewa, vijito vya maji vitatiririka kutoka kila mlima na kilima. Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwanga wa jua utakuwa mara saba ya mwanga wake wa kawaida, kana kwamba mwanga wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Mwenyezi-Mungu atakapoyafunga na kuyaponya majeraha aliyowaletea watu wake.


Mungu wetu ukaonekane popote tulipo,tupitapo,tunenapo Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako..
Ukatufanye chombo chema nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe..

Asante Mungu wetu kwa neema hii yakujifunza Neno lako..
Mungu wetu likakae nasi na likawe faida kwetu na kwa wengine..
Tukafuate na kiusimamia Neno lako na si maneno ya Dunia hii..
Ukatupe Neema ya kuendelea kujifunza zaidi..Tukawe na kiu na shauku ya kukujua zaidi..Ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia sauti yako Mungu wetu..



Tegeni sikio msikilize ninayowaambieni; sikilizeni kwa makini hotuba yangu. Je, alimaye ili kupanda hulima tu? Je, huendelea kulima na kusawazisha shamba lake? La! Akisha lisawazisha shamba lake, hupanda mbegu za bizari na jira, akapanda ngano na shayiri katika safu, na mipakani mwa shamba mimea mingineyo. Mtu huyo huwa anajua la kufanya, kwa sababu Mungu wake humfundisha. Bizari haipurwi kwa mtarimbo wala jira kwa gari la ng'ombe! Ila bizari hupurwa kwa kijiti na jira kwa fimbo. Mkulima apurapo ngano yake, haendelei kuipura mpaka kuvunja punje zake. Anajua jinsi ya kuipura kwa gurudumu, bila kuziharibu punje za ngano. Ujuzi huu nao watoka kwa Mwenyezi-Mungu wa majeshi. Mipango yake Mungu ni ya ajabu, hekima yake ni kamilifu kabisa.
Mungu wetu ukatuongoze vyema tunapoanza kitabu kingine..
Asante Mungu wetu kwa Neema ya kuweza kupitia/kusoma kitabu hiki tulichomaliza leo cha Hesabu Mungu wetu  na isiwe Mwisho utupe neema ya kukirudia mara nyingi na kuendelea kujifunza zaidi..


Baba wa Mbinguni ukawaguse na wengine wanaozongwa na kukosa muda wa kusoma Neno lako..Ukawape Neema ya kukutafuta na ukawape macho ya kuona na masikio ya kusikia..




Bado kidogo tu, msitu wa Lebanoni utageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba kuwa msitu. Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa kitabuni na kutoka gizani vipofu wataanza kuona. Wanyofu watapata furaha mpya kwa Mwenyezi-Mungu, na maskini wa watu watashangilia kwa furaha kwa sababu ya Mungu, Mtakatifu wa Israeli. Majitu makatili yataangamizwa, wenye kumdhihaki Mungu watakwisha, wote wanaootea kutenda maovu watatokomezwa. Watatoweka wale wanaopotosha kesi ya mtu mahakamani, watu wanaowafanyia hila mahakimu na wasemao uongo kuwanyima haki yao wasio na hatia. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu aliyemkomboa Abrahamu, asema hivi kuhusu wazawa wa Yakobo: “Wazawa wa Yakobo hawataaibishwa tena, hawatainamisha vichwa vyao tena kwa aibu. Watakapowaona watoto wao, watoto niliowajalia mimi mwenyewe, watalitukuza jina langu mimi Mtakatifu wa Yakobo; watakuwa na uchaji kwangu mimi Mungu wa Israeli. Waliopotoka rohoni watapata maarifa na wenye kununa watakubali kufunzwa.”


Si kwa nguvu zetu wala utashi wetu ni kwa neema zako Mungu  wetu..
Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe Mungu wetu..
Tunayaweka haya yote mikononi mwako Baba wa Mbinguni..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina...!

Asanteni sana wapendwa/waungwana kwakua pamoja..
Mungu wetu yu mwema sana ..!

Je wewe unayesoma hapa leo umefaidika/umejifunza chochote?
Kuna tulieanza naye Mwanzo mpaka sasa tunaenda pamoja?
kama siyo unaweza kutenga muda wako ukaanzia nyuma ili tuweze kwenda vyema..

ikikupendeza na Muombe Mungu akupe neema hiyo..

Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea katika maisha yenu
Msipungukiwe katika mahitaji yenu Baba wa Mbinguni akawape kama inavyompendeza yeye..
Nawapenda.

Urithi wa wanawake walioolewa

1Viongozi wa jamaa katika ukoo wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, mwana wa Yosefu, walikwenda kuzungumza na Mose na viongozi wengine wa koo za Waisraeli. 2Taz Hes 27:7 Wakasema, “Bwana wetu, Mwenyezi-Mungu alikuamuru kuwagawia watu wa Israeli nchi kwa kura, kuwa urithi wao; alikuamuru pia uwape binti za Selofehadi ndugu yetu urithi wa baba yao. 3Lakini wao wakiolewa na Waisraeli wa makabila mengine, urithi wao utatoka kwetu na kuwaendea watu wa kabila watakamoolewa; kwa hiyo urithi wetu sisi utapungua. 4Katika sikukuu ya ukumbusho urithi wao utahesabiwa pamoja na ule wa kabila watakamoolewa na hivyo kabila letu halitapata urithi huo tena.”
5Basi, Mose akawapa Waisraeli agizo lifuatalo kutoka kwa Mwenyezi-Mungu, akawaambia, “Watu wa ukoo wa kabila la Yosefu,36:5 kabila la Yosefu: Yaani ukoo wa Manase, Taz Hes 36:12. wamesema ukweli. 6Na hivi ndivyo anavyoamuru Mwenyezi-Mungu kuhusu binti za Selofehadi; wako huru kuolewa na mtu yeyote wampendaye, lakini waolewe katika kabila lao, 7ili urithi wa Waisraeli usihamishiwe kwa kabila lingine; kila Mwisraeli atazingatia urithi wa kabila lake. 8Mwanamke yeyote mwenye urithi katika kabila mojawapo la Israeli ni lazima aolewe na mtu wa kabila lake, ili kila Mwisraeli achukue urithi wa babu zake. 9Hivyo hapatakuwa na urithi wowote utakaohamishwa kutoka kabila moja hadi jingine. Kila kabila la Waisraeli litashikilia urithi wake.”
10Binti za Selofehadi walifanya kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Mose. 11Wote: Mala, Tirza, Hogla, Milka na Noa wakaolewa na binamu zao. 12Waliolewa katika jamaa za ukoo wa Manase mwana wa Yosefu, na urithi wao ukabaki katika kabila la baba yao.
13Hizo ndizo amri na maagizo ambayo Mwenyezi-Mungu aliwapa Waisraeli kwa njia ya Mose katika tambarare za Moabu, ngambo ya Mto Yordani karibu na mji wa Yeriko

Hesabu36;1-13


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: