Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 11 December 2016

Niwatakie Jumapili hii iwe Njema kwenu;Kwaya ya Mamajusi (Mamajusi Choir) - Tunalindwa na Nyingine..


Wapendwa/Waungwana;Ni matumaini yangu Mungu anawalinda na amewaamsha salama,
Wenye shida/Tabu Mungu akawaguse na kuwaponya katika yote...
Yeye ni kila kitu,Tumaini,Upendo,Uponyaji,Utukufu,Baraka,Amani,Furaha vipo kwakwe Muumba
Mbingu na nchi...yeye Atoshaa!!!!















Neno La Leo;Wakolosai:3;5-17 Na Yakobo:3;1-18



Wakolosai:3:5-17

Maisha ya kale na maisha mapya
5Basi, ueni chochote kilicho ndani yenu ambacho ni cha kidunia: Uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu). 6Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi. 7Wakati mmoja nyinyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo. 8Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: Hasira, tamaa na uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu. 9Msiambiane uongo, kwani nyinyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote, 10mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu. 11Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
12Nyinyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo, basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu. 13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe nyinyi. 14Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo, kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili. 15Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo nyinyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani! 16Ujumbe wa Kristo na ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani. 17Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.






Yakobo:3;1-18

Ulimi
1Ndugu zangu, wengi wenu msiwe waalimu. Kama mjuavyo, sisi waalimu tutapata hukumu kubwa zaidi kuliko wengine. 2Lakini kama mtu hakosi katika usemi wake, basi, huyo ni mkamilifu, na anaweza kutawala nafsi yake yote. 3Sisi huwatia farasi lijamu kinywani mwao ili watutii; na kwa njia hiyo twaweza kuwaongoza kokote tunakotaka. 4Meli nazo pia, ingawa ni kubwa sana, na husukumwa na upepo mkali, huweza kugeuzwa kwa usukani mdogo sana, zikaelekea kokote nahodha anakotaka. 5Vivyo hivyo, ulimi, ingawa ni kiungo kidogo cha mwili, hujisifia makuu sana.
Moto mdogo waweza kuteketeza msitu mkubwa. 6Hali kadhalika ulimi ni kama moto. Umejaa maovu chungu nzima, unayo nafasi yake katika miili yetu na hueneza ubaya katika nafsi zetu zote. Huteketeza maisha yetu yote kwa moto utokao Jehanamu kwenyewe. 7Binadamu anaweza kuwafuga wanyama, na amefaulu kufuga viumbe vyote – wanyama wa mwituni, ndege, nyoka na viumbe vya baharini. 8Lakini hakuna mtu aliyefaulu kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kiovu, hakitawaliki, na kimejaa sumu inayoua. 9Kwa ulimi sisi twamshukuru Bwana na Baba yetu. Kwa ulimi huhuo twawalaani watu, watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu. 10Maneno ya kubariki na ya kulaani hutoka katika kinywa kimoja. Ndugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa hivyo. 11Je, chemchemi moja yaweza kutoa maji matamu na maji machungu pamoja? 12Ndugu zangu, je, mtini waweza kuzaa zeituni? Au, mzabibu waweza kuzaa tini? Chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.
Hekima itokayo juu mbinguni
13Je, ni nani mwenye hekima na akili miongoni mwenu? Basi, aoneshe jambo hilo kwa mwenendo wake mzuri na kwa matendo yake mema yanayofanyika kwa unyenyekevu na hekima. 14Lakini ikiwa mioyo yenu imejaa wivu, chuki na ubinafsi, basi, msijisifu na kusema uongo dhidi ya ukweli. 15Hekima ya namna hiyo haitoki juu mbinguni; hekima hiyo ni ya ulimwengu, na ya kidunia, tena ni ya kishetani. 16Maana popote palipo na wivu na ubinafsi, hapo pana fujo na kila aina ya uovu. 17Lakini hekima itokayo juu mbinguni, kwanza ni safi; inapenda amani, upole na huwajali watu; imejaa huruma na huzaa matunda ya matendo mema; haina ubaguzi wala unafiki. 18Uadilifu ni mazao ya mbegu ambazo wapenda amani hupanda katika amani.
Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe sana.

Saturday 10 December 2016

Jikoni Leo; Na da'Fathiya (Aroma of Zanzibar)UNGA WA PUFF PASTRY - KISWAHILI





Mahitaji 1

Siagi vikombe 3
Unga wa ngano kikombe 1

Mahitaji 2

Unga wa ngano vikombe 4
Chumvi vijiko 2 vidogo
Maji ya ndimu kijiko 1 kidogo
Maji ya baridi kikombe 1
Siagi 1/2 kikombe


Shukrani;
Aroma of Zanzibar

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Tuesday 6 December 2016

TANZIA: MAREHEMU FELIX KAPINGA ATAZIKWA LEO TAREHE 06/12/2016 MKOANI NJOMBE


Marehemu Felix Kapinga enzi za uhai wake. 

Wanajumuia ya wanafunzi waliosoma Tumaini University - Iringa, Songea Boys High School na Lugalo Secondary School wanasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa mwanafunzi mwenzao Marehemu Felix Kapinga kilichotokea Usiku wa Tarehe 3/12/2016 katika Hospitali ya Ikonda Mission Mkoa wa Njombe baada ya kuugua kwa muda mfupi. 
Tunachukua fursa hii kutoa pole kwa Mke wa marehemu, Mtoto wa marehemu, Mama mzazi wa marehemu, wafanyakazi wenzake kutoka Njombe community Bank, Ndugu, jamaa, Marafiki na wana familia kiujumla kwa msiba huu walioupata, tunaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi. 

Mazishi yanatarajiwa kufanyika leo tarehe 06/12/2016 huko huko Njombe katika eneo la kijiji kinachotambulika kwa jina la Ramadhani  ambako Mama mzazi wa marehemu ndiko anakoishi, shighuli za Mazishi zinategemewa kufanyika kuanzia saa 6.00 Mchana. Kwa taarifa zaidi unaweza ukawasiliana kwa namba 
+255 713 254553

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE
AMIN.