Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 1 November 2015

IBADA YA KUMBUKUMBU YA MAREHEMU GODFREY MNGODO, COLUMBUS, OHIO


Pr. Mwakabonga akiongoza ibada ya kumbukumbu ya marehemu Godfrey Mbiu
Mngodo iliyofanyika siku ya Jumamosi Octoba 31, 2015 Columbus, Ohio nchini
Marekani na kuhudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki wakiwemo wafanyakazi wa
kituo cha utangazaji Sauti ya Amerika idhaa ya Kiswahili (VOA). Marehemu
Godfrey Mbiu Mngodo aliaga Dunia Tarehe 11 Septemba, 2015 Dar es Salaam na
kuzikwa Tanga. Godfrey Mbiu Mngodo amefanya kazi katika sehemu
mbalimbali kama Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD), Voice of America,
wizarani na kituo cha Channel Ten ameacha watoto 10 na wajukuu 14. PICHA NA
KWANZA PRODUCTION/VIJIMAMBO
Mmoja ya mtoto wa marehemu Michael Mngodo akiwa na mwanae Alvin
wakifuatilia ibada ya kumbukumbu ya mpendwa baba yake marehemu Godfrey Mbiu
Mngodo iliyofanyika siku ya Jumamosi Octoba 31, 2015 Columbus, Ohio nchini
Marekani.
Familia ya Mngodo ikifuatilia Ibada.
Pr. Mwakaboma akifanya maombi kwa wanafamilia.
Michael Mngodo akisoma wasifu wa mpendwa baba yake. Kulia ni mtoto wake
Alvin.
Ndugu, jamaa na marafiki wakifuatilia ibada. Kwa Picha zaidi bofya HAPA

No comments: