Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 9 December 2013

Mheshimiwa January Makamba akihutubia waTanzania DMV‏


Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mhe. January Makamba alipohutubia waTanzania na jamii zao waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara zilizofanyika Laurel Maryland Desemba 7, 2013 kwa uratibu wa blog ya VIJIMAMBO


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 8 December 2013

Tumalizie J'Pili kwa Upendo na Amani;Burudani-Bonni Mwaitege,Fungua Moyo Wako na Nyingine!!!!

Wapendwa;Tumalizie J'Pili hii kwa Wema,Busara,Hekima,Amani,Unyenyekevu na Upendo..

Malaika wa BWANA hufanya kituo,Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.


Neno La Leo;Zaburi 34:1-12.
Onjeni mwone ya kuwa BWANA yu mwema;
Heri mtu yule anayemtumaini
.





"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Friday 6 December 2013

RIP Nelson Mandela Dead at 95 - Hanson Baliruno New Ugandan



Dunia yaomboleza kifo cha Mandela;Tanzania imetangaza siku tatu za maombolezo.

Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela
Tanzania imetangaza siku tatu za maombolezo kuanzia tarehe 6 hadi 8 Desemba, 2013, kufuatia kifo cha rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.
Rais Jakaya Kikwete wa nchi hiyo pia ameagiza kuwa katika kipindi hicho cha siku tatu bendera zote zitapepea nusu mlingoti.
Kufuatia kifo hicho Rais Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini na kupitia kwake kwa mkewe Bi Graca Machel, wanafamilia wote na wananchi wote wa Afrika ya Kusini kufuatia kifo cha Mzee Nelson Mandela kilichotokea tarehe 5 Desemba, 2013 baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Rais ameuelezea msiba huu kuwa ni msiba mkubwa kwetu sote.
"Afrika ya Kusini, Afrika na dunia kwa ujumla imepoteza mtu mashuhuri na shujaa mkubwa wa Karne ya 20 na 21.Tunaelewa machungu waliyonayo wananchi wa Afrika ya Kusini kwa kupoteza kiongozi shupavu, jasiri, mwana mapinduzi , mvumilivu na mstahimilivu". Ameongeza Rais Kikwete.
Rais amemuelezea Mzee Mandela kuwa ni kielelezo cha aina yake kwa wanadamu kwa moyo wake wa kusamehe, huruma na upendo uliomwezesha kuwaunganisha wananchi wa Afrika ya Kusini kuwa taifa moja baada ya kipindi kirefu cha mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi.
"Mandela ni mfano bora kwa wanadamu wa jinsi binadamu muungwana anavyopaswa kuwa . Ni wajibu wa wana Afrika Kusini, Afrika na dunia kuiga mfano wake hasa moyo wake wa uzalendo, kujitolea hata maisha yake kwa ajili yake na wananchi wenzake". Rais ameongeza kusema, "Tuzidi kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Mzee Mandela mahali pema peponi".
Mandela amefariki huko Johannesburg akiwa na umri wa miaka 95 na yeye ndiye aliyeiongoza Afrika Kusini kutoka mikononi mwa watawala wa ubaguzi wa rangi baada ya kufungwa jela kwa miaka 27.
Mandela alikuwa anatibiwa homa ya mapafu nyumbani kwake baada ya kulazwa hospitalini kwa miezi mitatu.
Katika taarifa yake kwa watu wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, alisema kuwa Mandela amewaaga lakini yuko mahali salama.
Rais Zuma amesema kuwa taifa limepoteza mtu waliyemjua kama mtoto wa taifa hilo.
Mandela aliwahi kushinda tuzo ya amani ya Nobel, na kutambulika kama rais aliyeheshimika sana hasa kwa kupatanisha watu wa Afrika Kusini baada ya kutoka gerezani.

Habari Na;http://www.bbc.co.uk/swahili/

Thursday 5 December 2013

Jikoni Leo;How to Make Mabuyu na Vingine vingi Kutoka kwa-Sheikha Agil

Waungwana ni Jikoni Leo; Tuangalie Mapishi mbalimbali kutoka kwa da'Sheikha..
Mmmhh hakika sikuhizi kama wewe ni mpikaji na unataka kujifunza mapishi tofauti hakuna linaloshindikana.
Usitafute visingizio, Oohh mama nanihii nipikie oohhh sijafundishwa na mama/shangazi/dada,Nyumbani...


Pia kama unakinyaa,Hupendi kula chakula cha mtu usiyemjua/sehemu usiyoiamini usafi wake.Ingia Mitandaoni tuu kila kitu utapata  maelekezo yoote na upike mwenyewe...
Haya TEAM[Timu] Mapishi kazi kwenu............


Shukrani;Sheikha Agil

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Wednesday 4 December 2013

HUYU NA YULE: Mahojiano na waTanzania Evans Mhando na Fatuma Matulanga wakiwa CHINA‏


WaTanzania Evans Mhando (L) na Fatuma Matulanga (M) walipokutana jijini Beijing nchini China. Wiki hii walikuwa wageni katika kipindi cha HUYU NA YULE kinachotayarishwa na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production

Katika huyu na yule wiki hii, nimepata nafasi ya kuzungumza na vijawa
wawili wa kiTanzania wanaosoma nchini China. Nao ni Fatuma Matulanga
aliyeko Beijing na Evans Mhando aliyeko Nanchang ambao kwa pamoja
tumejadili mambo kadhaa na zaidi kuhusu vijana

Wameeleza mengi wakioanisha kijana na maisha ya China na Tanzania ikiwemo

1: TOFAUTI KATI YA KIJANA WA CHINA NA TANZANIA

2:TOFAUTI
KATI YA ELIMU YA CHINA NA KWINGINE. Ni kweli kuwa China haifunzi
ubunifu na ndio maana wanasifika kwa kuendeleza kuliko kubuni?

3: MALALAMIKO KUWA BIDHAA ZA CHINA HAZINA UBORA, YANATAZAMWA VIPI HUKO CHINA?

4: NI KIPI WANACHOJUA SASA KUHUSU CHINA AMBACHO HAWAKUJUA KABLA HAWAKWENDA CHINA?

5: MABADILIKO YA SERA YA MTOTO MMOJA MNAONA IMEPOKELEWA VIPI HAPO?

6: NI KIPI WANACHOTAMANI KINGETOKA CHINA KWENDA TANZANIA (HASA KATIKA TASNIA YA HABARI?)

Na mengine mengi

Ni
huyu na Yule ya Mubelwa Bandio wa Jamii Production akihojiana na Fatuma
Matulanga na Evans Mhando, wanahabari wa shirika la utangazaji la
Tanzania (TBC) wanaojiendeleza kielimu nchini China


Kwa maoni ama ushauri, usisite kutuandikia kupitia jamiiproduction@gmail.com
--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Tuesday 3 December 2013

Kipindi cha familia kutoka Jamii Productuion...Majukumu ya Baba katika Familia‏


Karibu katika kipindi hiki cha FAMILIA kutoka Jamii Production.

Katika kipindi cha wiki hii, mjadala wa WAJIBU WA BABA KATIKA FAMILIA umefungua mfululizo wetu wa mijadala kuhusu wajibu wa mzazi kwa familia yake

Mbali na washiriki waliokuwemo studio, pia tumeshirikisha maoni toka kwa wasikilizaji wetu wapendwa waliyotoa kwenye ukurasa wa Facebook
Msimamizi wa kipindi Abou Shatry akifuatilia mjadala

Karibu uungane nasi



Mjadala ukiendelea
Mgeni wetu katika mjadala huu Isidory Lyamuya


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Kifuatacho Jamii Production...Fatuma Matulanga na Evans Mhando‏



Katika kipengele hiki cha HUYU NA YULE  wiki hii, nimepata nafasi ya kuzungumza na vijawa
wawili wa kiTanzania wanaosoma nchini China. Nao ni Fatuma Matulanga
aliyeko Beijing na Evans Mhando aliyeko Nanchang ambao kwa pamoja
tumejadili mambo kadhaa na zaidi kuhusu vijana

Wameeleza mengi wakioanisha kijana na maisha ya China na Tanzania ikiwemo

1: TOFAUTI KATI YA KIJANA WA CHINA NA TANZANIA

2:TOFAUTI KATI YA ELIMU YA CHINA NA KWINGINE. Ni kweli kuwa China haifunzi ubunifu na ndio maana wanasifika kwa kuendeleza kuliko kubuni?

3: MALALAMIKO KUWA BIDHAA ZA CHINA HAZINA UBORA, YANATAZAMWA VIPI HUKO CHINA?

4: NI KIPI WANACHOJUA SASA KUHUSU CHINA AMBACHO HAWAKUJUA KABLA HAWAKWENDA CHINA?

5: MABADILIKO YA SERA YA MTOTO MMOJA MNAONA IMEPOKELEWA VIPI HAPO?

6: NI KIPI WANACHOTAMANI KINGETOKA CHINA KWENDA TANZANIA (HASA KATIKA TASNIA YA HABARI?)

Na mengine mengi

Usikose kutembelea mtandao huu siku ya Jumatano ili kusikiliza mahojiano kamili

Ni huyu na Yule ya Mubelwa Bandio wa Jamii Production akihojiana na Fatuma
Matulanga na Evans Mhando, wanahabari wa shirika la utangazaji la
Tanzania (TBC) wanaojiendeleza kielimu nchini China

Monday 2 December 2013

[AUDIO]: Maandalizi ya matembezi ya hisani: NCHI YANGU, WAJIBU WANGU, TAIFA KWANZA‏


 Matukio Chuma, muandaaji wa matembezi ya hisani akizungumzia matembezi hayo yatakayofanyika Januari 11, 2014 yenye kauli mbiu Nchi yangu, wajibu wangu, taifa kwanza.

Katika mahojiano haya Chuma anazungumzia mambo mbalimbali kuhusu matembezi hayo, ikiwemo sababu ya kuyaandaa, sababu za kuyafanya katika njia waliyoamua kuyafanya (Dar-Moro), mambo ya kufanya kabla hujashiriki matembezi haya na mengine mengi.

Unaweza kuwasiliana nao kwa simu namba 0784 311-056, 0772 545-562 ama barua pepe ambayo ni kwetutanzania@yahoo.com

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 1 December 2013

Nawatakia J'Pili Njema yenye Baraka;Burudani-Bahati Bukuku,Naomba niulize na Nyingine!!!

Wapendwa muwe na J'Pili Njema yenye,Shukrani,Imani,Upendo na Furaha...
Ninyi ni chumvi ya dunia,lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee?
Neno La Leo;Mathayo Mtakatifu:5:11-16.
Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye Mbinguni.








"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.