Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 21 June 2016

Mahojiano na Makala Jasper kuhusu Tuzo ya National Geographic Society for Leadership



Makala Jasper ni Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika lisilo la kiserikali la Mpingo Conservation & Development Initiative (MCDI).

Juni 16, 2016, alitunukiwa tuzo ya National Geographic Society/Buffett Award for Leadership in African Conservation, akiwa ni mshindi miongoni ma washiriki 30 kutoka barani Afrika.

Tuzo hiyo imetokana na kazi anayofanya pamoja na wananchi katika Vijiji mbalimbali mkoani Lindi.
MCDI huwezesha wanakijiji kutumia rasilimali za misitu kujenga uchumi na kutunza mazingira.

Katika miradi inayofanyika chini ya MCDI, wananchi wameweza kujiendeleza na kujenga shule, hospitali, kununua chakula cha dharura na kutoa misaada kwa vijiji vingine.

Tuzo ya National Geographic Society/Buffet Award ni ya pili kupokelewa na Bw. Jasper.

Ya kwanza ilikuwa Whitley Fund for Nature Award aliyopokea nchini Uingiereza tarehe 27 Aprili, 2016.

Karibu umsikilize

Sunday 19 June 2016

Jumapili iendelee vyema Na Happy Father's Day;Burudani-Sarah K-Liseme,Nasema Asante Na Ambassadors Of Christ Choir - Moyoni Mwangu,Nimekupata Yesu,




Wapendwa/Waungwana;Natumaini Jumapi ilikuwa/inaendelea vyema,
Mungu azidi kuwalinda na kuwabariki kila iitwapo leo,msipungukiwe na Amani ya moyo,
Upendo,Furaha na Upendo....

"Happy Father's Day" kwa BABA yangu mpendwa Ulale kwa Amani[R.I.P]
Kwa BABA wa watoto wangu na wa BABA wote wanaojua makujukumu yao kama baba
Mungu azidi kuwapa Hekima,Busara,Upendo na utunzaji/Ulezi mwema...

Mungu akawabariki na kuwajaalia wananume wote wanaohitaji watoto
Mungu awape sawa sawa na amapenzi yake....
 Ameeen....










Neno La Leo;waefeso 3:14-21

Upendo wa Kristo
14Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba, 15aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni. 16Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu, 17naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo 18kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina. 19Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;21kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina.

Biblia Habari Njema














"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe wote.

Tuesday 14 June 2016

Msemaji wa serikali azungumza na Diaspora.......Jukwaa Langu Juni 13 2016


Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mindi Kasiga
Photo Credits: Wavuti.com
Katika kipindi hiki, tumezungumza na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mindi Kasiga ambaye ameeleza kuhusu nafasi na wajibu wa serikali kwa waTanzania waishio Diaspora.
Pia amegusia wajibu wa waTanzania hao kwa nchi yao na kujibu maswali mbalimbali
Karibu


Sunday 12 June 2016

Nawatakia Jumapili iliyo njema;Burudani-William Yilima-Yesu Nitie NguvuNimalize Salama,Ee MUNGU,Uko Wapi,Subiri Muujiza Wako,UmulunguMwinza....



Habari za Jumapili wapendwa/wangwana..
nawatakia jumapili yenye baraka tele...




Neno La Leo;Ufunuo 2:1-29
Ujumbe kwa Efeso







Ujumbe kwa Smurna






Ujumbe kwa Pergamumu








Ujumbe kwa Thuatira





































"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 7 June 2016

Mahojiano na Chef Issa Kapande toka Sweden


Chef Issa ma ma-Chef
 wa timu ya Stockholm, Sweden, waliposhiriki na kushika nafasi ya
kwanza katika kipengele cha timu za kanda kwenye mashindano ya Kombe la
Dunia la Mapishi  2014 yajulikanayo kama  
Villeroy & Boch Culinary World Cup 2014  yaliyofanyika nchini Luxemborg.
Chef Issa Kapande ni mpishi maarufu na mmiliki wa mgahawa mkubwa unaotoa
huduma za chakula cha Kitanzania nchini Sweden, unaojulikana kama
Tanzania Restaurant
Alikuwa mkarimu sana kujiunga na Mubelwa Bandio kuzungumzia safari yake katika fani ya upishi na mpaka alipofikia.
Karibu ujiunge nasi kusikiliza






Tuesday 31 May 2016

Kama umeguswa msaidie huyu bibi..






"Nimetumiwa na Rafiki"
~
Haya wapendwa  nataka ku share hii video na nyinyi na yoyote atakae pata imani please inbox Facebook[Nana O Al Wakuvuruga ]msaada wako. Miezi kadhaa nyuma niliwaho share hii video na baadhi ya groups ili atakae weza amsaidie huyu bibi kuna ambao wamejitolea alhamdulillah lakini kwa ufupi pesa itamtosha kwa miezi miwili mitatu kununulia kula yake halafu baada ya hapo atarudi to square one. Inawezekana mnajiuliza huyu bibi ni nani? Huyu bibi sihusiani nae na wala sijawahi kutana nae ila inshaAllah mwaka huu nitamtafuta nimjue kwa ukaribu. Mimi nilipewa video hii na mwenzangu ambae nae pia alipata kumjua mwaka jana alipoenda matembezi Tanzania. Akapewa habari ya bibi huyu ili kama anaweza amsaidie chochote. Kubwa alienipa hii taarifa kajua hawezi lifanya hili jambo peke yake ndio akanijulisha na mimi. Sasa kwa ufupi huyu bibi hakujaaliwa mtoto, amefadhiliwa na watu hicho chumba mnacho kiona kwenye video na picha nitawatumia mpate kuona vizuri mazingira anayo ishi. Hajui kula yake ataitolea wapi wala tiba, kabaki anapita akiomba ndio siku inaenda. Hicho chumba mnacho kiona kukinyesha mvua ya nguvu maji yanajaa huko chumbani kwake anashinda juu ya kitanda mpaka maji yakauke. Nahitaji watu wajitolee kwa hali na mali apate kukarabatiwa chumba chake na at least japo ajijue anapata japo mlo mmoja kwa siku. Wazee wetu kweli wana shida lakini naamini hawajafikia hali hii, kumbuka bibi huyu hakujaaliwa kuzaa kwahiyo hana matumaini zaid ya kuomba vijumbani. Please find it in your heart and inshaAllah donate whatever you can. I joke a lot this is not one of those jokes; its real for this elderly lady and ahe doesn't even know I'm doing this




"Swahili Na Waswahili"Kutoa ni Moyo.

Monday 30 May 2016

MISS TANZANIA USA PAGEANT AEESHA KAMARA TEMBELEA, KUONGEA NA KUTOA MSAADA KENTON HIGH SCHOOL


Miss Tanzania USA 2015-2016 Aeesha Kamara akiongea na wanafunzi wa Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam siku alipotembelea shuleni hapo katika moja ya majukumu yake ya kuhudumia jumuiya. Miss Kamara anadhamini wanafunzi wawili shuleni hapo
Miss Tanzania USA Pageant Aeesha Kamara akimkabidhi msaada mwalimu mipira siku alipotembela shule ya Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania USA Aesha Kamara akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wawili anaowadhamini kwa kuwasomesha shuleni hapo.
Picha ya pamoja