Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 13 March 2015

Pazi ReUnion USA. Mambo yazidi kupamba moto Houston Texas








 Watatu toka kushoto ni Richard Kasesela alipokua akiwasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa George  Bush Intercontinental uliopo Houston, Texas nchini Marekani kwa ajili ya Pazi Reunion itakayofanyika siku ya Jumamosi March 14, 2015 katika uwanja wa mpira wa kikapu wa Pilgrim uliopo katika kanisa la Lutheran lililopo Houston. Wengine katika picha ni wenyeji wake waliompokea,  kutoka kushoto ni Willy Crrusa, Aika na Flora Mochiwa maarufu kama Madikodiko. Mchezaji mwingine anayekuja kwenye maadhimisho hayo ya Pazi toka nje ya Marekani ni Atiki Matata anayekuja siku ya Ijumaa March 13, 2015 akitokea Uingereza. Picha na VIJIMAMBO
 Richard Kasesela akitest uwanja wa mpira wa kikapu mara tu alipowasili uwanjani hapo mara tu baada ya kutoka uwanja wa ndege kushoto ni Davis mchezaji mwingine wa mchezo huo, Flora Mochiwa na Willy Crrusa wakiangalia kama bado wamo. Richard Kasesela richa ya kuwa mchezaji wa Pazi pia aliwahi kuwa Rais wa chama cha mpira wa kikapu Tanzania.
 Wachezaji wa mpira wa kikapu wakipata picha ya pamoja na Richard Kasesela.
 Mdau toka Columbus, Ohio akiwa tayari kushuhudia Pazi Reunion itayaofanyika siku ya Jumamosi March 14, 2015 ndani ya jiji la H-Town.
 Willy Crrusa katika picha ya pamoja na Andrew wakati wakiwa ndani ya madikodiko.
 Wageni wakipata chakula huku maongezi yakiendelea.
Andrew akipata picha ya pamoja na Richard Kasesela.

WaTanzania wa Houston Texas kurekodi kipindi kuhusu mauaji ya Albino Tanzania‏





Wadau kutoka New York katika moja ya vipindi vilivyorekodiwa.



Wadau wa North Carolina wakiwa kwenye kipindi kilichopata kurekodiwa.


Timu ya Vijimambo ikishiriana na Kwanza Production inapenda kwanza kutoa pongezi kwa Watanzania Houston kwa jitihada zao za kupambana na mauaji ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi
Pia inaandaa kipindi cha video kuongelea hili swala kwa mapana zaidi na kuangalia jinsi gani ya kukomesha mauaji haya ambayo yanaleta fedheha na aibu  ikiwemo ukiukaji wa haki za binadamu.

Kipindi kitarekodiwa siku ya Jumampili saa 8 mchana (2pm) mahali ni Extended Stay America chumba namba 224 anuani ni 2424 West Sam Houston Prkway, Houston, TX 77042. 

Kwa maelezo zaidi wasiana na 301 335 6383 asante


Ujumbe kutoka kwa ndugu zetu hapo chini.

Monday 9 March 2015

Mazungumzo na Mhe Samuel Sitta......Wizara na Kugombea Urais


Karibu katika sehemu hii ya pili ya mazungumzo na Mhe. Samuel Sitta (Mb)

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania mwaka 2014.

Aliketi nasi kuzungumzia kuhusu kazi zake kama Waziri wa Uchukuzi na pia nia yake ya kugombea Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu (2015)

Karibu


Sunday 8 March 2015

Nawatakia Jumapili njema Na Happy Women's Day;that's my king-.!!!Burudani-Your Name Brings Healing To Me - Planetshakers (Worship song with Lyrics)


Wapendwa;Natumaini Jumapili inaendelea Vyema..
Mungu andelee kuwa Bariki na Kuwalinda kila iitwapo Leo..

"Happy Women's Day"


That's My King..!!!!!!



"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe sana.

Saturday 7 March 2015

Stara T aachia wimbo wa Siku ya Wanawake Duniani



Msanii Stara T, ametoa wimbo mpya UWEZESHWAJI WA MWANAMKE ambao ni maalum kwa ajili ya siku ya kinamama dunia inayoadhimishwa Machi 8 ya kila mwaka.


Wednesday 4 March 2015

Jikoni Leo;Kenyan Mukimo Recipe How to make Mukimo - Jikoni Magic

Waungwana;"Jikoni Leo"Tujifunze kupika "Mukimo" chakula hiki kinapikwa/kuliwa sana na Ndugu zetu waKenya...
Mimi ni mmoja wa wapenzi wa chakula hiki,lakini sijawahi kupika huwa napikiwa na Rafiki yangu.
Vipi wewe Mpendwa/Muungwana umeshawahi kula/kupika Mukimo?
Kama bado jaribu natumai utakipenda.....


Twende wote sasa..


Shukarani/Thanks;Jikonimagic

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Monday 2 March 2015

Mazungumzo na Mhe Samuel Sitta (Pt I).......KATIBA


Karibu katika sehemu hii ya kwanza kati ya mbili za mazungumzo na Mhe. Samuel Sitta (Mb)
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania mwaka 2014.
Aliketi nasi kuzungumzia zaidi suala hili la Katiba hii pendekezwa, na mchakato mzima wa kuipata
Karibu