Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 30 November 2014

Nawatakia Jumapili Njema;Burudani-Angela Chibalonza- Uliniumba nikuabudu na Nyingine....

Wapendwa;Natumaini jumapili ilikuwa/ inaendelea Vyema,
1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,
tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!

Neno La Leo;Zaburi:95;1-11
Utenzi wa kumsifu Mungu
1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,
tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!
2Twende mbele zake na shukrani;
tumshangilie kwa nyimbo za sifa.
3Maana Mwenyezi-Mungu, ni Mungu mkuu;
yeye ni Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4Vilindi vyote vya dunia vimo mikononi mwake,
vilele vya milima ni vyake.
5Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya;
kwa mikono yake aliiumba nchi kavu.
6Njoni tusujudu na kumwabudu;
tumpigie magoti Mwenyezi-Mungu, Muumba wetu!
7 Maana yeye ni Mungu wetu,
nasi ni watu wa kundi lake,
ni kondoo wake anaowachunga.
Laiti leo mngesikiliza sauti yake:
8“Msiwe wakaidi kama kule Meriba,
kama walivyokuwa kule Masa jangwani,
9wazee wenu waliponijaribu na kunipima,
ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.
10Kwa miaka arubaini nilichukizwa nao,
nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka!
Hawajali kabisa njia zangu!’
11 Basi, nilikasirika, nikaapa:
‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko!’”
Bible Society of Tanzania



"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Friday 28 November 2014

Jikoni Leo; Na Mswahili-Chef Issa[Issa Kapande]..

Waungwana;"Jikoni Leo"Tuangalie/Tujifunze na Mpishi wa Leo ni Mswahili, kaka yetu huyu Isaa Kapande...
Mapishi ya Viazi...Mmmhh kila mtu anaupishi wake si vibaya tukijufunza Mapishi mbalimbali.
Hata nawe kama ni mpishi/unapenda mapishi usisite kutushirikisha nasi tukajifunza kupitia mapishi yako.Tutumie kupitia Email;rasca@hotmail.co.uk
Pia usisite kuuliza pale ulipokwama/shindwa...kama wewe unajua hiki na kuna wengine wanajua kile,   Tunaweza kujifunza kupitia wengine.

Mimi natatizwa/siwezi kupika hafu keki[Half cake]..kama maandazi lakini yale yanakuwa Magumu na yamekatika katika..
Tanzania/Dar... mara nyingi yanashushiwa/kinywaji cha Tangawizi...
Msaada waungwana mwenye kuyajulia......










Shukran;Zaidi-activechef/http://activechef.blogspot.co.uk/

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 23 November 2014

Muendelee Na Jumapili hii Vyema;Burudani-Freedom (Live from Faith Christian Center) - Kenneth Reese

Wapendwa nawatakia jumapili njema,yenye Baraka,Furaha,Upendo,Amani,Shukrani,Upole kiasi......
34Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi. 35Mkipendana, watu wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu.”

Neno La LeoYohana:13:1-36.
Amri mpya
31Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake. 32Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara. 33“Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: ‘Niendako nyinyi hamwezi kwenda!’ 34Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi. 35Mkipendana, watu wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu.”
Bible Society of Tanzania

I wanna clap a little louder than before,I wanna sing a little louder than before,
I wanna Jump higher than before,I wanna shout louder than before.........Hallelujah..!!!!




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Wednesday 19 November 2014

MISHUMAA YA KALE...Kipindi kipya kutoka VIJIMAMBO na KWANZA PRODUCTION


Photo Credits: Ye Olde Vivyl Shoppe
Baada ya pilika za wiki nzima, na mchamchaka wa maisha, sasa unakuja wakati wa kuburudika na muziki halisi wa zamani.

Katika kipindi hiki, utaweza "kuruka majoka" na "kula mangoma" kwa kusikiliza nyimbo ziliotamba miaka ya zamani, kupata historia ya wasanii na vikundi mbalimbali na pia kusikiliza mazungumzo na maDj na wasanii mbalimbali wa zamani.

Ungana na MixMaster Dj Luke Joe kwenye "one and two" na Mubelwa Bandio nyuma ya kipaza sauti kwenye kipindi kipya cha MISHUMAA YA KALE kitakachokujia kila Ijumaa kuanzia saa 11 kamili jioni mpaka saa 1 kamili usiku kwa majira ya Marekani ya Mashariki (5:00pm - 7:00pm EST)

Ungana nasi kupitia www.kwanzaproduction.com

MixMaster DJ Luke Joe. Photo Credits: IskaJojo Studios
Mubelwa Bandio



Wednesday 12 November 2014

Jikoni Leo,Wanaopenda kujifunza ya Waswahili-Jiko yetu...!!!!


Waungwana;"Jikoni Leo" Na Wanaojifunza ya Waswahili...
Mengi sina tuendelee kujifunza...[Hongera zao]



Thanks/Shukrani;Brennan Waters

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Tuesday 11 November 2014

Discussion on USAID African Diaspora Marketplace III

Discussion with Jeffrey L. Jackson, Senior Private Sector Advisor, USAID.
Barbara Span, Vice President, Global Public Affairs, Western Union,
Eric-Vincent Guichard, CEO, Homestrings and Zelalem Dagne, ​
CEO, Global Tracking before the launch of the African Diaspora Marketplace III (ADM III), on October 27th 2014 at The Embassy of Tanzania in Washington, DC