Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 13 February 2013

Da'Naomi Nyembo Atimiza miaka 5.!!!!!!!!

Mwenyewe da'Naomi Nyembo..
 
Ahhh..ndiyo nina miaka 5........

Mapothii na Rafiki.....

Urafiki hauchagui Rangi,Utaifa, Dini wala kabila..mbele za MUNGU wote ni watoto wake....

Zawadi kwa Wapendwa Marafiki na Wanafunzi wenzie..Tujifunze kushirikisha watoto katika Utoaji na si Kupokea tuu.


Ahhhhh mwenyewe  da'Rabiah..Mzaa Chemaaaa..mamake Naomi na Nadia..Muke ya Nyembo ...Mutoto ya Abuu Jumaa Mujukuu wa Tuwa!!!!

Waungwana Mtoto wetu
NAOMI NYEMBO..Ametimiza miaka 5..

Wazazi/Familia.Inamshukuru sana MUNGU kwa zawadi ya kuwa na NAOMI..MUNGU azidi kumlinda na kumbariki kwa kila jambo.Awe Baraka kwao na kwa Jamii Pia.

Da' NAOMI nasi tunakutakia kila lililojema naAmani kila iitwapo Leo, Uwe mtoto mwema  na Ufanikishe Malengo yako.
Uwe Kichwa na si Mkia,Ukue na Kuongezeka Imani.


Wazazi/walezi hatua gani ya makuzi ya mtoto wako huwezi kuisahau?
Alitambaa/hakutambaa,Alichelewa kutembea,Alikuwa Mlizi/kulia sana,Kutokulala,Utundu,Kupenda/kutopenda Kula na...............

"Swahili NA Waswahili"Upendo na Umoja.

Sunday 10 February 2013

Natumaini mlikuwa na J'Pili Tulivu..Pole kwa Wote waliopatwa na Msiba;Burudani - Ambassadors of Christ Choir Rwanda, Ni Kwanini? na Nyingine Nyingii!!!!

Wapendwa J'Pili ya Leo tuwaombee wenzetu waliopatwa na Misiba shida na Tabu..MUNGU awape Nguvu kwa wakati huu Mgumu kwenu..

Kuna mwenzetu Amefiwa na MUME na Mwingine Amefiwa na BABA yake Mdogo Na Wengine wote waliopoteza Wapendwa wao.....

Tumshukuru MUNGU  siku zote kwa ajili yenu  nyote,tukiwataja katika maombi yetu.

Neno La Leo;Waraka wa Kwanza wa Paulo Mtume kwa WATHESALONIKE:1:1-7
.Wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya upendo, na saburi yenu ya tumaini lililo katika BWANA wetu YESU Kristo, mbele za MUNGU Baba yetu.....Endelea....

"Swahili NA Waswahili"
Mbarikiwe Sana.

Friday 8 February 2013

Ya Kale ni Dhahabu;Burudani(Congo-Soukous)Yondo Sister!!!!!!

   Hahahaahahaha ni wake za watu na ni  mama  za watu sasa....Mke wa Mheshiwa Mbunge alianza zamani kupigilia Suti!!!!!!!
Hahahahaha....Siku Hazigandiiiii mwehhh


Waungwana;Mambo hayo...kama kuna uliyemtambua hapo baelezeee..Tuambieee..


YOndooooo sister ................Tusindikizie Salamu Leo!!!!


Unayo yako/zako za zamani unapenda  kuungana nasi katika kukumbushana? tutumie kupitia email;rasca@hotmail .co.uk

Karibuni Woooteee....hahaaha .

"Swahili Na Waswahili"
Kwaheriiiiii

Wednesday 6 February 2013

President Obama's Message to the People of Kenya!!!!!



HABARI YAKOOOOOO!!!!

Waungwana;Ujumbe huu kutoka kwa Rais Obama, kwa Ndugu zetu Wa-Kenya...
kunalolote unataka kuongezea?..Maoni/Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

"Swahili Na Waswahili" KWAHERIIIIIIIIII

Monday 4 February 2013

Jikoni Leo;HOW TO BE HEALTHY ON AN AFRICAN DIET - @ZiggyZB! !!!!!!!

w

Waungwana;Jikoni Leo..Mambo hayoo Mikarangizooo haya faii.....

Hellooo Hi-iii!!......Na Wawwwwooh oohhh

DIET DIET...Waungwana.Mimi sina mengi..mwenye masikio na asikie..na Mwenye Macho.....

Mimi  naanza tena.....Mhhh...Jamani si mchezo..inahitaji ujinyanyase haswaaa!!!!

Unalo la kuongezea?..Maoni/Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

Kula ni Muhimu Lakini kwa kiasi...

"Swahili NA Waswahili" Pamoja saana.

Sunday 3 February 2013

Muwe na J'Pili ya Matumaini na Amani;Burudani-Suma Mwakalibule - Indumbula na Nyingine nyingii!!!!!!!!



Wapendwa;Nawatakia J'Pili ya Matumaini,Amani,Haki na Upendo...Wamtumainio BWANA ni kama mlima Sayuni,Ambao hautatikisika,wakaa milele...Neno La Leo:Zaburi 125:1-5:Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,Ndivyo BWANA anavyozunguka watu wake,Tangu sasa na hata milele.........Endelea.

"Swahili NA Waswahili"
Amani ikae na Nanyi.

Saturday 2 February 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Mchanganyiko-BOZI BOZIANA,Franco&Sam Mangwana,Madilu...Mmmhh..Mooto!!!!!




Waungwana;Chaguo La Mswahili Leo..Mhhhhh...motoo.mambo mchanganyiko.ya Kitambo kidogo....

Vipi hizi zinakukumbusha nini/wapi?.Zina kubamba/kuzipenda? Au hukupata kuzisikia?...

Twende sote sasaa.....Balobakiee..na Imalobato lembiyeeeh........kusemasema walisema tumechokaaa..Muongo na mulozi ni watu wa kuchomaaaah.......
Kujulikana kumbetabu mwana mbokaaa... Ukiwa shantii  kama Mushedo wanashangaaaa....ukitembea peke yako wanasema wewe ndiyo mbayaaaa....Kujulikana kuna mamboooo....Lwambo wetu Franco wandugu eeehhhh.......

Rafiki yake ananiaeeehh...wewe Mangwana ee...usiwafuate endelea jamani eehh...Ukipata Tabu omba kwa MUNGU eeeehhh Alafu MUNGU pekee  yeye Milele na Milele eeehhh........

Wewe na mimi kisa gani ayaahh Ndugu nimekosea nini Angalia  Makambooo eee....kama kuna mambo unielezee Taratibuuu eeehh kukorofisha mbele ya watu sitakieeeeehh sikia eeeeehhh.........

"Swahili NA Waswahili"Pamoja sana.