Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 31 January 2013

Jikoni Leo,Shaba,Soda Mtungini na.....!!!!!!


    Kitu cha Shaba..Pilau..haswaa hii la Shughulini.....


Soda za kwenye Mtungi...nimezipata hukooo Ruhuwiko....

  Kitu Chipsi na Nyama Choma/kuku..... hapa Diet hakuna...

Waungwana;Jikoni Leo..Mambo kama hayo....
mimi sina meengi..zaidi  nasubiri kutoka kwako ..

Umeshawahi  Kula shaba/Pilau.Chakula cha Shughulini?...Nini ubaya wake na Nini Uzuri wake?

Karibuni sana kwa Maoni/Ushauli na Kuelimishana kwa upendo.

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Saaana.

Wednesday 30 January 2013

Watoto Na Mitindo;Pata na Video Hairstyle Slideshow!!!!


Aliye msuka huyu  ndiyo aliyekuwa akiwasuka watoto wangu..Nimefurahi kusikia bado yupo na anaendelea vyema na kazi zake kwa watoto...tena anawezana nao haswa...

Waungwana; Mimi naamini watoto wana Mitindo yao..pia wakipendeza wao wenyewe na wazazi tunakuwa na furaha sana..

Si Lazima au si wote wanapenda  watoto wasukwe..basi hata kama ana Nywele fupi..kuna Vibanio vyao pia wanapendeza sana......

Nao Watoto  kuna Umri wewe mzazi utamchagulia Mitindo ya Nywele lakini kuna Umri mwingine Mmmhh !!...inakuwa kazi ya ziada, Yeye/Wao hutaka hivi nawe unataka hivi..basi ni mabishano tuu..kama wapo wawili huwa wanaangaliana wao na kucheka au kuguna....hahahhaahhah imeshakukuta hii?

Karibuni sana kwa Maoni/Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.....

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.





Sunday 27 January 2013

Natumai mlikuwa na J'Pili yenye Kupendeza;Burudani-Bahati Bukuku-Dunia,Samehe!!!!!!!!!




Wapendwa natumaini mlikuwa na J'Pili yenye kupendeza.....

Tumalize J'Pili hii kwa.....Neno La Leo;Wakolosai;3:18-25;

[18]Ninyi wake,watiini waume zenu,kama ipendezavyo katika BWANA.

[19]Ninyi waume,wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao.

[20]Ninyi watoto,watiini wazazi wenu katika mambo yote;Maana jambo hili lapendeza katika BWANA

[21]Ninyi akina baba msiwachokoze watoto wenu,wasije wakakata tamaa......Endelea....


"Swahili NA Waswahili" MUNGU awabariki Saana.

Monday 21 January 2013

Jikoni Leo;Ugandan foods & Cuisines!!!!!!!



Waungwana;Jikoni Leo Tupo Uganda...Pata kujua Mapishi yao na Maandalizi yoote.
Mengi sina ukitaka kujua Uhondo wa Ngomaaa..Ingia Ucheze..

   "Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.

Sunday 20 January 2013

Wapendwa Nawatakia J'Pili Yenye Ushindi;Burudani-Geraldine Oduor - Wewe ni Mungu na Nyingine Nyingii!!!


Wapendwa Poleni na Snow natumaini hamjambo na kufurahia majira aliyoyaweka MUNGU na kushangilia. Ikiwa snow kama Greenland  Mchanga na Joto kama Sahara Baridi kama Himaya Mvua na Radi za Ikweta.Tusilalamike Nawatakia Kila la Kheri.....

Ujumbe huu  Wa kutia Moyo Nilitumiwa na Kaka yangu ALEX LUKUNDO Wa hapa COVENTRY .


Nami nimependa kushiriki nanyi  NA Kuongezea....Hasa mliokuwa kwenye Hali ya hewa kama hii isiwe sababau ya kukosa Kushiriki IBADA.




Wapendwa Muwe na J'Pili Njema, Yenye Unyenyekevu,Upendo,Busara ,Ushindi na Shukrani.Msijiwekee hazina duniani,nondo na kutu viharibupo,na wevi huvunja na kuiba;

Neno La Leo:Mathayo Mtakatifu:6:19-21;Kwakuwa hazina yako ilipo,ndipo utakapokuwapo na Moyo wako.

          "Swahili NA Waswahili" MUNGU Awabariki Sana.

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-Recipe of Basic Cupcakes for beginners - Mapishi ya (In swahili subtitle...!!!!!!!!



This is a video showing how to make basic Cupcakes for beginners, for East-African users and all the swahili speakers all around the world. It's also subtituled in English. Please, subscribe to our channel if you like it. We are working to offer you more video-recipes in swahili, in our Youtube channel and in our web-sitehttp://www.tupikepamoja.com/

Haya Waungwana si lazima kila kitu Mnunue......Jaribu mwenyewe na watoto watafurahi!!!!!!!

Jikoni Leo na Tupike Pamoja..Mmmmmhhhh Tamuuuuu Sanaaaaaaaaa.

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Saturday 19 January 2013

Chaguo La Mswahili Leo:Mambo ya Pwani;AT - Bi Harusi,Mzee Yussuf-Na hiili Kaseme,Offside Trick-Aambiwe na Nyingine nyingiii!

w

Waungwana;Chaguo la Mswahili Leo ni Mambo ya Mduara/Taarab..... Ralaralaaaaaa...lalalaaaahhhh..Mmmhh ....mimi sina Mengi kama wewe unayo Funguka /Ongea tuu.

Swali la Kizushi;-Eti nyimbo za Taarab/Mduara nyingi zinauchochezi,Ushari,Vidongo na Umbea ......Haswa sa siku hizi.Za Zamani nyingi zilikuwa Kimapenzi Zaidi......Unasemaje Muungwana?

         "Swahili NA Waswahili" Twende Soteeee sasa.