Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 17 September 2011

Pole Zanzibar PoleTanzania!!!!!!!!

Ukatili Mbeya!!!!!!!!

VITENDO HIVI VYA KIKATILI VYA WATU KUPIGWA NONDO VITAISHA LINI MBEYA?

Bwana Elia Daudi Mwalonde mkazi wa Uyole akiwa hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya wodi namba 1 baada ya kupigwa nondo hivi karibuni.

Bwana Zefania Mwangwale mwenye umri wa miaka 31 mkazi wa Uyole akiwa katika hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya baada ya kupigwa nondo pia.

Vitendo vya watu kupigwa nondo kwa Jiji la Mbeya vimekua kama ni vitendo vya kawaida, ni jambo la kusikitisha sana kwa sababu kila mwaka lazima hivi vitendo vitokee na kupelekea watu wengi wa jiji la Mbeya kuishi katika maisha ya wasi wasi sana.
KAPINGAZ Blog inapenda kuviomba vyombo vyote vya usalama Jijini Mbeya kuona kama hivi vitendo kama ni janga kubwa kwa watu wa Mbeya.

Thursday 15 September 2011

Waswahili Wetu Leo, Mkubwa na Wanawe/Miaka50 ya Uhuru!!!!!!!!

Haya Mpedwa wewe umejiandaaje na Miaka 50 ya Uhuru?
Sikiliza hayo maneno ya Waswahili, Chura anapenda Maji lakini si ya Moto.
Watoto wa Kiswahili wanatimbwilika/kucheza.Tanzania Kiroho Safi!!!!!!
Je wewe una Amani, Uko Huru? Kila la Kheri.

Wednesday 14 September 2011

Wanaume na Mitindo,Leo tupo Igunga!!!

                       Huyu baba kavaa shanga na katupia kikoi.
                Kijana Kasuka,shanga hakukosa na katupia kikoi,anasalimia kwa mapozi kabisa.
              Hawa wamejifunika vikoi, sijui hii ya mwisho nyeusi ni kaniki au....
Haya wapendwa Leo tupo Igunga,Tanzania.Kama uonavyo wanaume wa huko na Mitindo.
Sijajua kama hii ndiyo Mitindo ya Asili au yakisasa,Maana nasikia kunamitindo ya Asili,kama ndivyo,
Hongereni kwa kuendeleza Mila ambayo wengine wanameacha.

Wapendwa sina la zaidi nawasikiliza ninyi, Vipi kuhusu mitindo hii wewe unaionaje?
Na je kama Mitindo hii niya kiasili vipi kwenye Harusi au Sherehe za Kitaifa mtu akitinga si itakuwa mwake?





Karibuni sana Waungwana.











Saturday 10 September 2011

Poleni sana Wapendwa wetu Zanzibar,Mungu awatie nguvu kwa wakati huu Mgumu!!!

MELI YA LCT SPICE ISLANDERS YAZAMA KATIKA BAHARI YA HINDI PWANI YA NUNGWI LEO USIKU.



Meli ya LCT SPICE ISLANDERS imebinuka na kuzama katika Bahari ya Hindi huko Pwani ya Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja ikielekea Pemba.

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu, Issa Haji Ussi amesema tukio hilo limetokea saa 8:30 za usiku ambapo meli hiyo ilikuwa imebeba abiria 610 pamoja na mizigo.
Naibu Waziri huyo amesema meli hiyo imeondoka katika Bandari ya Malindi Unguja ikiwa katika hali ya uzima,lakini katikati ya safari ikapata hitilafu na kusababisha kubiruka na hatimaye kuzama.

Hadi sasa haijaweza kufahamika idadi kamili ya watu waliofariki,lakini vyombo vya uokozi vimefika katika eneo la tukio kutoa msaada.

Naibu Waziri Issa amesema Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya usafiri vya binafsi boti ziendazo kasi zimekwenda eneo la tukio kutoa msaada unahitajika.Jeshi la Polisi Tanzania limetuma Helkopta yake kwenye eneo la tukio

Awali, amesema Mamlaka zinazohusika zilipata taarifa za kuzama kwa meli hiyo baada ya Meli ya Mv Jitihada inayomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuripoti kuzama kwa meli ya Spice Islanders ambayo ililazimika kukatisha safari yake kuelekea Kisiwani Pemba na kwenda kwenye tukio.

Serikali imesema taarifa zaidi zitakuwa zikitolewa na wananchi wameombwa kuwa watulivu.

Habari kwa msaada wa Kapingaz.

Wednesday 7 September 2011

Watoto wa Shule na Tamaa!!!!!

                       Hawa wanandika kwenye ubao na chaki.
                                  Hawa wanamsikiliza mwalimu kwa tabasamu.
                                Hawa wamenyoosha mkono ili wapewe nafasi ya kujibu/kuuliza.
Baadhi ya Shule  zimeshafunguliwa hapa U.k.
watoto wa shule kila kona sasa, lakini baadhi yao walivyo jiremba mmhh,
mpaka  kugundua kama ni mwanafunzi ipo kazi.

Hili pia lipo kwa baadhi ya shule Afrika/Tanzania, hasa hizi shule za kulipia.
Sijui ndiyo kwenda na wakati auu....... Ninawaza tuu!!!!!


Mpendwa unafikiri kwa nini  baadhi ya watoto wa Shule wanakuwa na Tamaa?[1].Ni utoto tuu wakikuwa wataacha,Kutoridhika na maisha yao au...?[2.] Nivyema kwa watoto wa Shule kuvaa sare za shule au kutovaa sare kila mmoja aje na nguo zake?
[3.]Kupata chakula cha aina moja Shule au kila mtu ajitegemee.

Karibuni sana kwa Maoni,Kuelimishana katika malezi ya watoto wetu!!!!!!