Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Watoto na Vituko. Show all posts
Showing posts with label Watoto na Vituko. Show all posts

Monday 27 February 2012

Mtoto Wetu Leo-Sabrina!!!!!!

katika Poziii
Alikuwa MC
Mifugo ni adimu kwao,weee paka njoo hapa!!!
Kwanini jana ulikimbia?utahama humu oohh,haya niamkie..
                                          Kama hutaki ngoja nikuamkie wewe!!!
Waswahili wanasema vyakurithi Vinazidi jee ni kweli?
Jee Watoto wanaweza kurithi Vituko,Ucheshi,Upole na Ugomvi?
Na kwanini baadhi ya misemo ya watoto inafanana kama Maji,kuwa Mma,Nyonyo na.....?
Kunawakati unaweza cheka na Mtoto mdogo au Kulia kwa mambo yake!!!!
Wengine hawapendi kula,kulala Usiku na mambo mengi.Pia kuwa na Mtoto kuna Raha yake!!

Kama wewe huna Mtoto na Unahitaji,Mungu yu Mwema  Uskate Tamaa!!!!

Tuesday 20 September 2011

kweli kulea Kazi!!!!!!!

Hata sijui nini anatafuta huko jamani, Mmmmhhh Tumetoka mbali sana.
Mpendwa unayakumbuka makabati ya vyombo ya Zamani yenye wavu kama wa dirisha?
mama yangu aliweka Ufuta huko,umetengenezwa kama vigorori hivi,mimi na kaka yangu tulikuwa tunautaka,
mama akasema tutapewa tukimaliza kula chakula,tumemaliza chakula mama kaondoka,lakini tunajua ulipo,mwenzangu  mimi nikaambiwa niupandie, hahahahaha kama wewe BINGWA panda,Sifa zikaniponza, nikaupandia weee nikala mweleka wa nguvu na kabati juu yangu, wenzangu wakatimua mbio,badala ya kuniokoa, Sasa na huyu naye yange mkuta yaliyonikuta jee? Kweli Kulea Kazi jamani, Wazazi /Walezi tuwe makini sana na Watoto.

Mpendwa huna kisanga kilichokukuta unachokumbuka?
Hujapitia mambo yakutaka  kuwa Bingwa/Mshindi?.

Karibuni sana.











Saturday 9 July 2011

Mtoto Wetu leo ni Arianna Mbwambo!!!!!!!

                                            dada Arianna katika poziiii
                               Nina mapozi yakutosha.
                                 Nikibeba kipochi jee?

Watoto wa leo na mapozi yao!Wapendwa hivi hawa watoto haya mapozi wanayatoa wapi?
wanayaona kwenye Tv,kwa Wazazi/walezi,kwa rafiki zao au.......

Hata wakubwa nao wana mapozi ,Wengine kunyanyua mguu juu,kushika kiuno,kuweka dole,mikono kifuani na....
zile picha zetu za Studio kushika maua,je mpendwa wewe unazo?.



Karibuni sana Waungwana!!!!!

Sunday 5 June 2011

Mtoto Wetu Leo ni Frank- Jayden!!!!!!!!!!!!!!!!

 Hapa anawaza leo nianze na  Mchezo upi au nikacheze wapi Sijui?
 Nimekuja kunywa maji tuu,Wao wameshanibana nisiende tena kucheza je hii ni haki jamani?
 Nimeshindwa kutoka tena,ahhh ngoja nioge zangu tuu!!!!!
 Sasa watajuta kunifungia ndani ,mimi naungana na huyu ni kelele tuu mpaka kieleweke!!!!!!
 Wakaona wanitoe kidogo hata kwa Mangi nipate walau Soda!!!!!!!
 Hapa sasa mambo poa watu wangu, Asanteni kwa Ofa baba na mama!!!!!!!!
Ngoja nikatafute Elimu , Eti yule babu wanaemuita sijui NYERERE [R.I.P] Nimeambiwa alisema Elimu ni Uti wa Mgongo,Sasa sijui kama nikweli au maneno tuu.

Waungwana kila Mtoto anavituko vyake,Hata wewe kwenye Utoto wako ulipitia mambo mengi  sana mpaka kufikia hapo ulipo.Katika hayo ya Mtoto wetu Frank-Jayden, Umeguswa/kumbushwa na  nini katika Maisha ya Utoto?. Karibuni sana kwa Ushauri na kuelimishana katika malezi ya Watoto wetu!!!!!!!

Saturday 28 May 2011

Usingizi Unaraha yake!!!!!!!!

Kuna asiyependa kulala?Usingizi nao ni Starehe jamani au mnasemaje?Nawatakia mwisho wa wiki mwema.