Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label WaTanzania/Waswahili. Show all posts
Showing posts with label WaTanzania/Waswahili. Show all posts

Thursday 28 June 2018

UZINDUZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA UINGEREZA MJINI READING , JUNI 2018


Picha na Habari za Freddy Macha

Kwa miaka mingi imesikika mikutano ya vyama na vilivyodai kushirikisha Watanzania Uingereza. Ila mwaka huu Jumuiya mpya iliyoundwa (ATUK-" Association of Tanzania United Kingdom")- imeahidi kuweka chombo tofauti.


Akizindua hafla hiyo mjini Reading (tamka “redding”) Balozi Asha Rose Migiro, alisifu jitihada hasa za kitengo cha vijana waliosukuma kuelewana. Akahimiza kuwa serikali nzima kuanzia Mheshimiwa Rais, Wizara ya Mambo ya Nje na Ubalozi wako bega moja na ATUK.

Baadaye Joseph Warioba alieleza kuwa kitendo hiki kimefikiwa baada ya utafiti na mazungumzo ya muda mrefu kuhakikisha hakuna tena migongano. Tofauti ya sasa na zamani ni nini? Warioba alihimiza kuwa zamani wahusika waliendekeza maslahi binafsi na ulafi. ATUK tunaelezwa, inashirikisha Watanzania wa kila namna wakiwemo wataalamu, wafanyabiashara, wasomi, wasanii nk. Shughuli iliofanyika Jumamosi 23 Juni, 2018 – ulikusanya zaidi ya Watanzania, ndugu na marafiki zao zaidi ya 300 –kiasi kikubwa kinachodokeza matumaini makubwa.

1- BLOGA- Balozi Migiro akihutubia- pic by F Macha 2018Balozi Migiro akihutubia Watanzania Reading, Jumamosi 23 2018. Kulia kwake ni mwakilishi wa muda wa ATUK, Joseph Warioba na kushoto, Rose Kutandula, Afisa Utawala, Ubalozini.

2-BLOGA- Dk Hamidu Hassan akizungumza kuh wasomi- pic by F Macha 2018Dokta Hassan Hamidu akielezea umuhimu wa wasomi na wataalamu kujiunga kushirikiana kutekeleza ujenzi Nyumbani na Ughaibuni.

3-BLOGA- Mseto wa wageni na wananchi wakisikiliza- pic by F Macha 2018.jpgMseto wa wananchi na wageni wakisikiliza wazungumzaji wa sekta, taaluma na kanda mbalimbali za Uingereza

4-BLOGA- Mjasiria mali Hamidu Mbaga wa All Things African- pic by F Macha 2018.jpgMjasiria mali, Hamida Mbaga, mwenye kampuni ya “All Things African”, akionesha baadhi ya mavazi na bidhaa za Kitanzania anazozisambaza kila ncha ya Uingereza miaka mingi sasa.

5-BLOGA- Balozi Migiro akiwa na mpinzani wa adha ya UKEKETAJI - Devota Haule- pic by F Macha 2018Balozi Migiro (kulia) na mpigania haki za wanawake na adha ya UKEKETAJI, Devota Haule anayeishi Uingereza. Bi Haule ni piamjumbe wa Jumuiya ya wana afya (“health practitioners”) wa Kitanzania Uingereza, yenye zaidi ya wanachama hamsini.

6-BLOGA- Wataalamu mbalimbali - pic by F Macha 2018.jpgWataalamu mseto waliojumuika. Dokta Hassan Hamza, mwanamuziki Fab Moses (WASATU), Dokta Gideon Mlawa (aliyebobea masuala ya Kisukari) Saidi Kanda (WASATU) na Ammy Ninje- kocha wa muda wa Timu ya Taifa Stars. Nyuma yao kabisa, Dk Kazare Nakyoma, mganga wa wenye ulemavu wa akili.

7-BLOGA- Balozi akisalimiana na mmoja wa wageni waliohudhuria- pic by F Macha 2018.jpgBalozi akisalimiana na baadhi ya wageni waliohudhuria

8-BLOGA- Zuhura Mkwawa na Pauline Nzengula- pic by F Macha 2018.jpgWatanzania wengi walisafiri toka majimbo ya mbali Uingereza. Hapa ni Zuhura Mkwawa, mwakilishi Leicester na katibu wake, Pauline Nzengula.

9-BLOGA-Keki ya Ishara- pic by F Macha 2018Keki ya Ishara ya Uzinduzi baada ya kukatwa

10- BLOGA- Waganga na Wanadiplomasia- pic by F Macha 2018Dokta Hamza Hassan, Msaidizi Utawala Ubalozini, Husna Hemed, Balozi Migiro na Dokta Gideon Mlawa

11-BLOGA- Watoto waliotumbuiza - pic by S Mzuwanda 2018.jpgWatoto waliotumbuiza. Picha na Simon Mzuwanda

12-BLOGA-Mwanahabari wa ATUK- Simon Mzuwanda- pic by F Macha 2018.jpgMwanahabari mkuu wa ATUK- Simon Mzuwanda na kamera yake.

Tazama mahojiano na habari zaidi BAADHI YA WALIOSHIRIKI - “Kwa Simu Toka London” ( KSTL)


  1. MAHOJIANO NA JOE WARIOBA
https://www.youtube.com/watch?v=KRPAGkI2WvQ
  1. MAHOJIANO NA DEVOTA HAULE KUHUSU UKEKETAJI
https://www.youtube.com/watch?v=HBgL9IJ75oI&t=23s
  1. MAHOJIANO NA DOKTA GIDEON MLAWA –MTAALAMU WA KISUKARI
https://www.youtube.com/watch?v=uszuASkrSDQ&t=47s
  1. MJASIRIA MALI HAMISA MBAGA AKIZUNGUMZIA KUHUSU BIDHAA ZA KITANZANIA ULAYA
https://www.youtube.com/watch?v=YdiT9x0yguw&t=5s

5. NDOGO NDOGO ZA KIJANA EDWARD “HUNGAZ” CHACHA KUHUSU UMOJA WA WATZ

https://www.youtube.com/watch?v=TWmuDqP3MIM

6. TATHMINI YA MJUMBE WA ATUK- MOHAMMED MWAUPETE

https://www.youtube.com/watch?v=w_HJjmaTbGU











Tuesday 18 August 2015

Kipindi cha Jukwaa Langu Agosti 17 2015


Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015

Katika kipindi hiki utasikia mjadala wetu na wageni Jeff Msangi toka Toronto Canada na Darmatus Nambai aliyehudhuria studio kuhusu DEMOKRASIA na MABADILIKO kuelekea uchaguzi nchini Tanzania

KARIBU

Tuesday 4 August 2015

BALOZI LIBERATA MULAMULA ATINGA NDANI YA STUDIO YA KILIMANJARO


 Balozi Liberata Mulamula akiwasili nje ya jengo lenye studio ya Kilimanjaro tayari kuongea LIVE katika kipindi cha Jukwaa langu kinachorushwa kila siku ya Jumatatu kuanzia saa 12 jioni mpaka saa 2 usiku saa za Mashariki za Marekanui. anayemfungulia mlango ni Abdul Malik

 Balozi Liberata Mulamula akiingia ndani ya studio akiwa amesindikizwa Harriet Shangarai (kushoto) ambaye pia ni Mkurugenzi wa studio hiyo, kulia ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme na Abdul Malik
 Balozi Liberata Mulamula akipata maelezo kutoka kwa studio meneja ambaye pia ni mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi cha Jukwaa langu, Bwn. Mubelwa Bandio (hayupo pichani) Kushoto ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme akifuatilia maelezo hayo.
 Mhe. Liberata Mulamula akiendelea kusikiliza maelezo kutoka kwa meneja wa studio Mubelwa Bandio ambaye ni mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi cha jukwaa lako. Kati ni matangazaji maarufu wa Radio ya Times FM na aliyewahi kutangaza  Radio One Bi. Rose Chitalah ambaye pia anamsaidia Mubelwa Bandio katika utangazaji na kuchangia hoja mbalimbali katika kipindi cha Jukwaa langu.
 Balozi Liberata Mulamula akiendelea kujibu maswali ya watangazaji mahiri Mubelwa Bandio (kulia) na Rose Chitalah (hayupo pichani ) na wasikilizaji waliokua na shahuku ya kumuuliza maswali.
  Balozi Liberata Mulamula akiendelea kujibu maswali ya watangazaji mahiri Bwn. Mubelwa Bandio (hayupo pichani ) na Rose Chitalah (kushoto)
 Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme akisikiliza mahojiano na kunakili baadhi ya vipengele katika mahojiano hayo.
 Kutoka kushoto ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na mtangazaji mahiri Rose Chitalah wakiwa katika picha ya pamoja.
 Kutoka kushoto ni Dj Luke Joe, Meneja wa studio ya Kilimanjaro,  Mubelwa Bandio, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na mtangazaji mahiri Rose Chitalah wakipata picha ya kumbu kumbu na Balozi Liberata Mulamula anayemaliza muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marejkani na Canada na sasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Friday 13 March 2015

WaTanzania wa Houston Texas kurekodi kipindi kuhusu mauaji ya Albino Tanzania‏





Wadau kutoka New York katika moja ya vipindi vilivyorekodiwa.



Wadau wa North Carolina wakiwa kwenye kipindi kilichopata kurekodiwa.


Timu ya Vijimambo ikishiriana na Kwanza Production inapenda kwanza kutoa pongezi kwa Watanzania Houston kwa jitihada zao za kupambana na mauaji ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi
Pia inaandaa kipindi cha video kuongelea hili swala kwa mapana zaidi na kuangalia jinsi gani ya kukomesha mauaji haya ambayo yanaleta fedheha na aibu  ikiwemo ukiukaji wa haki za binadamu.

Kipindi kitarekodiwa siku ya Jumampili saa 8 mchana (2pm) mahali ni Extended Stay America chumba namba 224 anuani ni 2424 West Sam Houston Prkway, Houston, TX 77042. 

Kwa maelezo zaidi wasiana na 301 335 6383 asante


Ujumbe kutoka kwa ndugu zetu hapo chini.

Friday 25 April 2014

Maandalizi ya sherehe za Muungano Washington DC‏





Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Liberata Mulamula akizungumzia maandalizi ya sherehe za miaka 50 ya muungano ofisini kwake Washington Dc Jumatano, Aprili 23, 2014.
Photo: Sunday Shomari

Monday 9 December 2013

Mheshimiwa January Makamba akihutubia waTanzania DMV‏


Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mhe. January Makamba alipohutubia waTanzania na jamii zao waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara zilizofanyika Laurel Maryland Desemba 7, 2013 kwa uratibu wa blog ya VIJIMAMBO


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Wednesday 30 October 2013

Tanzania: Tunaweza kujitoa A. Mashariki

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete

Serikali ya Tanzania imesema inatafakari ushiriki wake ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na inaweza kujitoa ndani ya Jumuiya hiyo iwapo itaendelea kutengwa katika baadhi ya vikao.
Aidha imesema Tanzania haitambui vikao vinavyofanywa na nchi tatu zilizopo ndani ya Jumuiya hiyo ambazo zimekuwa zikizitenga Tanzania na Burundi.
Taarifa zinazohusiana
Tanzania, Afrika Mashariki, Afrika
Waziri anayehusika na masuala ya Afrika Mashariki wa Tanzania Samwel Sitta ameliambia Bunge la Tanzania kuwa makubaliano ya vikao hivyo vinavyofanywa na nchi za Kenya, Rwanda na Uganda yatatekelezwa na nchi hizo zinazofanya vikao hivyo kwa sababu vinafanyika nje ya utaratibu wa mkataba wa jumuiya hiyo.
Katika mikutano iliyofanyika hivi karibuni Tanzania na Burundi hazikualikwa kwenye vikao hivyo.
Kwa mujibu wa Waziri Sitta mikutano ya wakuu wa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda ambayo ilianza kwa kuitenga Tanzania ilifanyika Entebbe nchini Uganda mwezi Juni mwaka huu na kufuatiwa na mkutano wa pili uliofanyika Agosti mwaka huu huko Mombasa nchini Kenya ambapo nchi hizo tatu bila kuishirikisha Tanzania walizungumzia uanzishaji wa himaya moja ya forodha.
Mambo mengine waliyozungumza wakuu hao ilikuwa uanzishaji wa visa moja ya utalii kwa nchi zao na matumizi ya vitambulisho vya uraia ambavyo vitatumika kama hati za kusafiria miongoni mwa nchi hizo.
Aidha Waziri Sitta amesema ndani ya mikutano hiyo pia walizungumzia kuanzisha mchakato wa kuanzisha shirikisho la nchi hizo.
Tayari Tanzania imeanza mazungumzo na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kuangalia ni kwa namna gani zitaanzisha ushirikiano nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kama zinavyofanya nchi za Rwanda, Uganda na Kenya.
Habari kutoka;http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

Thursday 30 May 2013

Miezi,Wiki,Siku..TANO LADIES Imewadia..Usiku Wa Mwanamke wa Ki-TANZANIA,SHANGWE,VIFIJO..MWANAMKE UPO?

Sold out Event! .. God is Good!
Kitenge Tayari kwa Fundi Juma!
Usiku wa Mwanamke wa Ki TZ
Shangwe, Vifijo & Vigelegele!
Mwanamke Uko Wapi?!!







Sold out Event! .. God is Good!
Kitenge Tayari kwa Fundi Juma!
Usiku wa Mwanamke wa Ki TZ
Shangwe, Vifijo & Vigelegele!
Mwanamke Uko Wapi?!!





Wasikilize/waangalie...WANAWAKE WA SHOKA!!!!!!!!



Pia unaweza kuwatembelea Facebook;https://www.facebook.com/pages/TANO-Ladies/


   "Swahili NA Waswahili"Pamoja Daima.

Tuesday 16 April 2013

Yanayo endelea Facebook;Mwalimu Ndondole na Wengine...Jee Wewe Unasemaje?


NAMHOFIA MWANANGU... NAIHOFUA KAZI YANGU... NALIHOFIA TAIFA LANGU...... HASA PALE MBUNGE NA WAZILI WANAPOONA BANGI INAWEZA KUWA HALALI KULIMWA (MAANA YAKE NA MATUMIZI YAKE)

HIVI TANZANIA IMEKOSA VITEGAUCHUMI NA RASLIMALI KIASI CHA KUIFIKILI BANGI KAMA ZAO LA KUONGEZA KIPATO....?

MADHARA YA BANGI YANAPOFANANISHWA NA YALE YA SIGARA KUNA UELEWA HAPO?
HAWA NDIO VIONGOZI WETU WANAOFIKIRI KWA KINA KWA NIABA YETU...?

WANAJUA KWANINI WATU WANAFIKIA HATUA YA KUVUTA BHANGI.....?

BINAFSI NAOGOPA...........................................................?

  • Edgar Joel Naunga mkono hoja tunapoteza mapato mengi sana wakati watu wengi wanatumia na ina soko kubwa sana tungepata mapato mengi endapo ingetozwa kodi .
  • Leon Mhongole uwezo wa kufikiri wa wabunge wetu umeshuka sana inatishia maisha ya vizazi vijavyo..
  • Lusungu Ndondole Natamani watoto wa yule mbunge, waziri na Edgar Joel wawe wa kwanza kuanza kutumia hii kitu. Lakini nawaswas na UZALENDO WAO na KAMA WANA WATOTO........ Najiridhisha kwa KAZI ZAO haziwapi fursa ya KUTAFAKARI zaidi ya KUFIKIRI....
  • Lusungu Ndondole Bwana Leon Mhongole, sie wenye WATOTO, UZALENDO na IMANI............ ndio TUNAOTAFAKARI mpaka kufikia tulikofikia. Usiogope ni KAZI zao na MAKUZI yao yanawapotosha...
  • Edgar Joel Mi nilimwelewa sana Mbunge Lusungu Ndondole unajua tumbaku ina madhara makubwa sana na ni sumu lakini imeruhusiwa kwanini bangi nayo isiruhusiwe tafakari na jua kuwa inatumika sana sasa na watu wa rika lote sasa jiulize je tumepoteza vipi mapato..
  • Edwin Mvanda Nadhani watawala washalichoka taifa hili. Wanataka baadae tuwe na taifa lenye vichaa watupu.
  • Kukaye Moto hiyo ndio dawa ya vifua vikuu hamkujua nini hahahaahaha hapa ulaya inauzwa bei sana, karibu nchi zote zimeruhusu ..watu wananunua hapa madukani..Usiogope..acha watu wapate ajila zao kama zao lina kubali ..hiyo sio hatari kama kodi itakusanywa vizuri..Rushwa ni hatari kupita kajani hako
    16 hours ago · Edited · Like · 1
  • Jane Mkini Acha mbwembwe wewe mbona tumbaku inalimwa akat mshaambiwa ni hatari kwa afya zenu!!!!!!!!! Acha tu iruhusiwe hiyo bange ili kama kutatokea nginjanginja basi wajingawajinga wote tufe wabaki wenye akili zao labda kutajengwa taifa lenye usawa na haki.......
    7 hours ago · Like · 1
  • Lusungu Ndondole Dada Jane Mkini Hujaisoma POST sawasawa, kwa uwezo wako wa kutafakari watakaokufa ni wajinga au wavutabangi? Ndio maana nimeuliza UNAFANANISHA MADHARA YA BANGE NA YALE YA SIGARA? Fikiri tena na UTAFAKARI.
  • Lusungu Ndondole Shemeji yangu Kukaye Moto, najua we ni ADIKT WA UZUNGU ndio maana sishangai mchango wako.
  • Lusungu Ndondole Nina maswali muhimu kwa Kukaye Moto, UNAFANANISHA ULAYA NA TANZANIA? We umetokea pale Ipogoro, najua fika unaijua TZ vizuri, UNADIRIKI KUITAFAKARI TANZANIA KWA KUILINGANISHA NA UINGEREZA AU UJERUMANI? Vijana wa kitanzania wapo sawa KIELIMU, KIPATO, UTA...See More
  • Edwin Mvanda Watu hawajui, unapokua na vichaa na mateja wengi ndipo hata wewe uliye na kazi yako unakua katika risk zaidi. Vibaka wakizidi utapolwa na wala hutakua salama. Kwa sasa wafanyakazi wote wanalipa kodi pamoja na ya wote wasio na kazi. Yaani wewe uliyeajil...See More
    15 minutes ago · Like · 1
  • Lusungu Ndondole Kwa maswali yangu hayo kama UNAWATAKIA MEMA wanyalukolo wenzio huku utafikiri UPYA na KUTAFAKARI shemeji yangu Kukaye Moto. Huo UZUNGU ndio ULIOWAHARIBU hata viongozi wetu wakienda ulaya wanarudi wanafikiri na KUWAZA KIULAYA wakidhani watu wote wa TZ wameshafikia kiwango cha
  • Edwin Mvanda Ubinafsi utatuua. Huyu anayetetea bangi ananikumbusha hasira za popo anapokua mtini kalala. Popo anaposikia kishindo cha kitu kinapita chini hupatwa na hasira na hatua ambayo huchukua ni kutoa kinyesi ili kimfikie aliye chini ambaye anahisi ni adui yake, sasa anasahau kua kalala miguu juu kichwa chini ndipo hapo mwili mzima huloa mavi yake mwenyewe. Hivi ndivo tunataka kufanya tunapotetea bangi. Watch out guys.
  • Lusungu Ndondole Sawa kabisa kaka Edwin Mvanda. Tatizo la kuathiriwa na UZUNGU ndilo linalowatesa hata viongozi wetu wengi wakienda semina ULAYA na AMERIKA wakirudi WANAFIKIRI KIZUNGU na KUWAZA KIZUNGU ndio maana wanalopoka tuu wakidhani wote wamefikia MAENDELEO, MAHITAJI, MTAZAMO na MALENGO ya KIMAREKANI wamesahau kama wao wanawaongoza WAFRIKA ambao wengi bado HAWAJAFIKIA KIWANGO WANACHOWAFIKIRIA badala yake walitakiwa WATAFAKARI kwanza.

Like ·              Maoni/Ushauri,Nyongeza......
 Karibuni Sana na Tuelimishane Kwa Upendo.
                                                      "Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.
 ·