Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Ukatili. Show all posts
Showing posts with label Ukatili. Show all posts

Tuesday 18 October 2011

AIBU GANI HII BADO INAENDELEA KULIKUMBA TAIFA LETU!!




Jeshi la Polisi nchini (PT) kupitia Inspekta Generali wake Said Mwema(Pichani) imetangaza dau la Shilingi Milioni 5 kwa mtu yeyote atakaefanikisha kupatikana kwa mtu aliyemjeruhi mtoto Adam Robert (14) ambaye ni Albino huko Geita ambapo mtu asiyejulikana alimvamia mtoto huyo na kuanza kumkata kata mikono na kisha kutoweka na vidole vya Albino huyo.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia mwishoni mwawiki katika Kijiji cha Nyaruguguna, Kata na Tarafa ya Nyang'hwale ambapo mlemavu huyo, Adam Robert (14), mwanafunzi wa darasa la nne, alivamiwa na kukatwa mkono wa kulia na kisha kunyofolewa vidole vitatu vya mkono wa kushoto.
Ni jambo la kusikitisha sana kuona vitendo hivi vinaendelea kutokea na mwisho wa siku jeshi linataka kutumia fedha za walipa kodi kwa ajili ya kuwapata wahalifu hao, mi nadhani hii njia sio sahihi, sidhani kama Jeshi la polisi wanashindwa kuwapata hawa wanaowatuma wahalifu kwenda kuwadhuru maalbino hawa. Jambo la msingi hapa sio kutangaza dau ni kuhakikisha wale wanaowatuma ndio wanakamatwa na ninaamini jeshi la polisi likishirikiana na usalama wa Taifa inawezekana kuwakamata hawa na kuwatokomeza kabisa, usalama wa Taifa wanafanya kazi gani kama sio pia na kuangalia usalama wa Watanzania hawa!
Ni aibu kubwa kwa Taifa letu vitendo hivi vinavyoendelea.
                                                            
                                                                          Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog
                                                             Asante sana kaka Kapinga.

Saturday 17 September 2011

Ukatili Mbeya!!!!!!!!

VITENDO HIVI VYA KIKATILI VYA WATU KUPIGWA NONDO VITAISHA LINI MBEYA?

Bwana Elia Daudi Mwalonde mkazi wa Uyole akiwa hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya wodi namba 1 baada ya kupigwa nondo hivi karibuni.

Bwana Zefania Mwangwale mwenye umri wa miaka 31 mkazi wa Uyole akiwa katika hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya baada ya kupigwa nondo pia.

Vitendo vya watu kupigwa nondo kwa Jiji la Mbeya vimekua kama ni vitendo vya kawaida, ni jambo la kusikitisha sana kwa sababu kila mwaka lazima hivi vitendo vitokee na kupelekea watu wengi wa jiji la Mbeya kuishi katika maisha ya wasi wasi sana.
KAPINGAZ Blog inapenda kuviomba vyombo vyote vya usalama Jijini Mbeya kuona kama hivi vitendo kama ni janga kubwa kwa watu wa Mbeya.