Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Mkesha. Show all posts
Showing posts with label Mkesha. Show all posts

Friday 30 December 2011

MKESHA MKUBWA WA KULIOMBEA TAIFA -ZANZIBAR!!!!!!!!


                       
                                                 
Mwenyekiti wa Kamati ya Mkesha wa Kuliombea Taifa Mchungaji Saimon Mputa katikati akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu maandalizi ya Mkesha huo katika ukumbi wa Habari Maelezo Raha Leo,Mjini Zanziba kushoto kwake ni Katibu wa Kamati Mchungaji Edward Mashimba na kuliani kwake ni Mjmbe wa kamati hiyo Askofu Obeid Fabian
                                      
                                                       
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar 29/12/2011

Wananchi wa Zanzibar wameombwa kushiriki katika Dua maalum ya
Mkesha wa kuliombea taifa la Zanzibar ilioandaliwa na Umoja wa Makanisa
Zanzibar ambapo Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Add
anatarajiwa kuwa Mgeni.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mkesha
huo Mchungaji Simon Mputa alipokuwa akizungumza na waandishi wa
habari katika Ukumbi wa Habari Maelezo uliopo Raha leo Mjini Zanzibar.

Amesema dua hiyo ambayo inatarajiwa kufanyika kuanzia majira ya usiku
wa kuamkia Mwaka 2012 katika Uwanja wa Mao tse Tung lengo lake kuu
ni kuliombea taifa kuepukana na majanga mbali mbali ambayo yanaweza
kulikumba Taifa hilo.

Mchungaji Simon amesema sambamba na kuliombea taifa pia kutafanyika
maombi maalum ya shukrani kwa Mungu juu ya kupatikana kwa Serikali ya
Umoja wa kitaifa Zanzibar pamoja na kuwaombea viongozi wake hekima na
busara katika uongozi wao

Aidha ameongeza kuwa kuna haja ya wananchi kukaa kwa pamoja na
kuweza kumuomba Mungu ili kuyaepusha majanga yaliyoikumba Tanzania
mwaka 2011 yasiweze kutokea tena katika Mwaka mpya wa 2012

Ameyataja majanga hayo kuwa ni pamoja na ajali ya kuzama kwa Mv.
Spice Islanders Zanzibar na Mafuriko yaliyoikumba mikoa ambali mbali ya
Tanzania Bara ikiwemo Dar es Salaam na kusababisha vifo vya wananchi
wengi.

Kwa upande wake Katibu wa Mkesha huo Mchungaji Edward Mashimba
amesema maandalizi ya Mkesha huo yamekamilika na kuwataka wananchi
wa Zanzibar kushiriki kwa wingi bila kujali itikadi za dini wala siasa zao.

Mchungaji Saimon amesema Maombi hayo ni maombi shirikishi ambayo
hapo awali yalikuwa yakifanywa na watu wachache lakini kutokana na
mwamko wa watanzania kumesababisha maombi hayo kufanyika katika
viwanja ili kukidhi haja ya wageni wanaoshiriki

Naye Mraribu wa Tamasha hilo hapa Zanzibar Allen Mbaga amesema

Mkesha wa Maombi wa kuliombea Taifa utafanyika katika mikoa mbali
mbali ya Tanzania Bara na Visiwani ambapo washiriki wa Zanziabar
watapata burudani mbali mbali kutoka kwa vikundi vya Kwaya huku
huduma ya za vitafunwa na vinywaji vikiwa vinapatikana Uwanjani hapo.

IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

Wednesday 28 December 2011

MKESHA MKUBWA WA KULIOMBEA TAIFA LA TANZANIA KUFANYIKA UWANJA WA TAIFA DESEMBA 31 MWAKA HUU, SERIKALI YAPONGEZWA KUKATAA USHOGA.


Umoja wa makanisa ya Kikiristo Tanzania (Tanzania ChristianFellowship of Churches) umeandaa mkesha mkubwa kwa ajili ya dua maalum kwa taifa kwa lengo la kumshukuru Mungu kwa kulivusha taifa katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru na kuanza kipindi kingine ambapo mgeni rasmi katika mkesha huo atakuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Mkesha mkuu kutoka Tanzania Christian Fellowship of Chrches Askofu Godfrey Emmmanuel Malasi amesema watanzania wanapaswa kujua Mungu anakusudi gani na taifa la Tanzania katika kipindi hiki ambacho Taifa limetimiza miaka 50 ya uhuru na kuanza kipindi kingine na kutoa wito kwa kila mtanzania kufanya kazi kwa bidii na kushiriki katika uchumi wa taifa.
Amesema serikali inazo sera nzuri za kuweza kuwamilikisha wananchi rasilimali ziliizopo nchini ili waweze kuishi maisha bora na kuongeza kuwa wananchi wanapaswa kutambua majira na wakati uliopo sasa wakati taifa linapoanza miaka 50 mingine ya uhuru kwa kuzitumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo.
“Kila mmoja anapaswa kushiriki na kushirikishwa kikamilifu katika uchumi wa taifa letu ambalo sasa limemaliza miaka 50 ya uhuru, kila mtu anapaswa kutambua nafasi yake, tusikae kwa kubweteka, tusikae kwa kulalamika kila mtu ajue ni wakati wa kumiki na kurithishwa rasilimali zilizopo katika taifa hili”
Amesema mwaka huu dua maalum kwa taifa litafanyika katika mikoa 14 ya Tanzania ikiwemo Dar es salaam, Arusha, Mwanza,Kilimanjaro, Singida Iringa, Mbeya ,Iringa, Kagera, Dodoma, Ruvuma, Tabora,Tanga na visiwa vya Zanzbar na Pemba.
Amefafanua kuwa katika mkesha huo viongozi mbalimbali wa taifa ,vyama vya siasa na balozi mbalimbali zipatazo 37 zilizopo nchini zimearikwa kushiriki mkesha huo na kuongeza kuwa tayari baadhi ya balozi zimethibitisha kushiriki mkesha huo.
Kuhusu maadalizi ya mkesha huo askofu Godfrey Malasi amesema yanaendelea vizuri na kutoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika dua hiyo maalum na kuongeza kuwa mkesha huo utaambatana na tukio maalum la watoto 50 kusimama uwanjani na kutamka maneno ya kupokea miaka 50 ijayo ikiwa ni ishara ya kupokea kizazi huru cha watanzania.
Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa kamati ya mkesha mkuu wa Taifa Askofu Keneth Damas ameipongeza serikali kwa kuwa na msimamo wa kupinga suala la ndoa za jinsia moja (ushoga) katika mikutano ya kimataifa iliyofanyika hivi karibuni na kuuita uamuzi huo kuwa ni ushindi mkubwa kwa taifa la Tanzania na watu wake katika kuheshimu utu na utamaduni wa taifa na uukataaji wa vitendo vya udhalilishaji na kuongeza kuwa wao kama viongozi wa dini wataendelea kuonya na kufundisha watu wajue athari za dhambi hiyo.
“Sisi kama viongozi wa makanisa katika nchi hii tunapinga kwa nguzu zote vitendo vya ushoga ndani ya taifa letu, vitendo vya ushoga ndivyo vilivyosababisha Sodoma na Gomora kuchomwa moto kwa kuwa vilimchukiza sana Mungu, Sisi kama viongozi wa dini katika kizazi chetu na vizazi vijavyo hatutaki kufikia hapo na kuona taifa letu likichomwa moto”