Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Matangazo/Imani. Show all posts
Showing posts with label Matangazo/Imani. Show all posts

Monday 3 August 2015

Mkutano wa Injili Washington DC [Aug 14 - 16 2015]


Kanisa la The Way of the Cross Gospel Ministries linapenda kuwaalika katika siku tatu za mkutano wa uamsho utakaofanyika hapa Washington DC.

Ni kati ya Agosti 14-16 2015




Mtumishi wa Mungu Emmanuel Mgaya ama Masanja Mkandamizaji alipohudumu kwa waumini wa jiji la Washington DC na vitongoji vyake siku ya Jumapili 07/07/2013 katika kanisa la THE WAY OF THE CROSS GOSPEL MINISTRIES

Monday 11 August 2014

CITE SUMMER CONFERENCE 2014 COVENTRY WEST MIDLANDS UK WITH MWL.MWAKASEGE.[Tujikumbushe Picha za Mkutano na Mchungaji Daniel Kulola,Uliofanyika Coventry]



Picha hizi za chini ni mkutano wa zamani kidogo na Mchungaji Daniel Kulola,Ulifanyika Coventry UK.
Si vibaya tukijikumbusha.....



























Picha kutoka Maktaba ya Swahili Na Waswahili

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Monday 9 September 2013

REVIVAL GOSPEL CONFERENCE.!!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu, tunakaribisha wote walio miji jirani kuhudhuria kongamano hili kubwa lenye baraka, Kutakuwa na wahudumu mbali mbali watakaoshiriki na kufundisha kuhusu Ukuu wa Mungu, walete watu wenye mahitaji mbali mbali nao wataenda kuguswa na Nguvu za Mungu. Chakula kitakuwepo,

Watakaosafiri na kutaka Maelekezo jinsi ya kufika tafadhali wasiliana nasi

484-751-7038

Barikiwa.

Kwa Maelezo zaidi ingia;

Friday 9 August 2013

Tamasha kubwa la muziki wa Injili kufanyika Washington DC kesho!!!!


 Waimbaji wanaofanya vema kwenye muziki wa Injili Afrika Mashariki, Upendo Kilahiro na Christina Shusho, watatumbuiza katika Tamasha kubwa la Injili litakalofanyika Jumamosi hii jijini Washington DC

 Kama walivyoongea kwenye VIDEO HII, waimbaji hao wamekamilisha maandalizi ya tamasha hilo ambalo pia litashirikisha waimbaji wenyeji wa hapa Marekani.
 

 Tamasha hilo kubwa lililo sehemu ya Maadhimisho ya miaka mitano ya kanisa la The Way of The Cross Gospel Ministries litafanyika siku ya Jumamosi kuanzia saa kumi kamili mpaka saa tatu usiku (6:00pm - 9:00pm) na kiingilio kwenye tamasha hilo kitakuwa ni dola kumi ($10) kwa watu wazima, bure kwa watoto.

 Anwani ambapo litapofanyika tamasha hilo ni

 The Way of the Cross Gospel Ministries 

 (at University United Methodist Church) 

 3621 Campus Drive 

 College Park, MD 20740 

 Kwa maelezo zaidi unaweza kuwasiliana na

 Mch. Ferdnand Shideko +1 240 476 6718 ama

 Ms Flora Mnkande +1 240 217 6335

 Waimbaji hawa wote watatumbuiza nyimbo zao za zamani na mpya na wanawaalika watu wote kujumuika nao na waimbaji wenyeji kuweza kupata BARAKA kwa njia hii ya uimbaji

   

   
Zaidi utayapata; http://www.changamotoyetu.blogspot.com
 http://www.youtube.com/user/mutwiba

Thursday 8 August 2013

Shusho, Kilahiro kuhudumu Washington DC wiki hii!!!!!



 Watumishi wa Mungu Christina Shusho na Upendo Kilahiro, mwishoni mwa wiki hii watahudumu katika jiji la Washington DC na Vitongoji vyake (DMV).

 Shusho na Kilahiro ambao ni miongoni mwa waimbaji mahiri wa muziki wa Injili Afrika Mashariki, wameshawasili Washington DC tayari kwa huduma hiyo ambayo ni sehemu siku tatu za  Maadhimisho ya miaka mitano ya kanisa la The Way Of The Cross Gospel Ministries.

 Maadhimisho haya yataanza siku ya Ijumaa na kumalizika Jumapili

 Maadhimisho haya yatafanyika
The Way of the Cross Gospel Ministries
(at University United Methodist Church)
3621 Campus Drive
College Park, MD 20740


 Hii inakuwa ni mara ya pili kwa watumishi hawa kuhudumu pamoja kanisani hapo katika kipindi cha miaka miwili, ambapo mwaka 2011waliungana na Upendo Nkone kuhudumu katika Mkutano mkubwa wa Injili ulilofanyika kanisani hapo.

  Watazame na kuwasikiliza wanavyoelezea siku hizo



Mengi utayapata; http://www.changamotoyetu.blogspot.com
 http://www.youtube.com/user/mutwiba