Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 27 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 6...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, kwa vile ahadi ya kuingia mahali pa pumziko bado ipo, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo. Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.” Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko.” Basi, hiyo ahadi ya kuingia bado ipo, maana wale waliohubiriwa Habari Njema pale awali walishindwa kuingia humo kwa sababu walikosa kutii.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Maonyo manne
1Mwanangu, kama umejitolea kumdhamini jirani yako,
ikiwa umetoa ahadi yako kwa ajili ya mtu huyo,
2umejibana kwa maneno yako mwenyewe,
umejinasa kwa ahadi uliyofanya.
3Ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzio,
lakini mwanangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi:
Mwendee mtu huyo mara moja umsihi akupe uhuru wako.
4Jitahidi usiache macho yako yapate usingizi,
wala kope za macho yako zisinzie.
5Jiokoe kwa kujitoa katika mtego huo,
mithili ya paa ama ndege amtorokavyo mwindaji.
6Ewe mvivu! Hebu ukamchungulie sisimizi,
fikiria namna yake ya kuishi ukapate hekima.
7Sisimizi hana kiongozi, ofisa, wala mtawala;
8lakini hujiwekea chakula wakati wa kiangazi,
hujikusanyia akiba wakati wa mavuno.
9Ewe mvivu, utalala hapo mpaka lini?
Utaamka lini katika usingizi wako?
10Wasema: “Acha nilale kidogo tu,
acha nisinzie kidogo!
Niache nikunje mikono nipumzike kidogo!”
11Wakati huo umaskini utakuvamia kama mnyanganyi,
ufukara utakufuata kama jambazi.6:11 Taz pia 24:33-34
12Mtu mwovu, mtu asiyefaa kitu,
huzururazurura akisema maneno mapotovu.
13Hukonyeza jicho kuwakosesha wengine,
huparuza kwa nyayo,
na kuashiria watu kwa vidole.
14Akiwa amejaa ulaghai moyoni hutunga maovu,
huzusha ugomvi kila mahali.
15Kutokana na hayo maafa yatamvamia ghafla,
ghafla atadhurika vibaya asiweze kupona tena.
16Kuna vitu sita anavyochukia Mwenyezi-Mungu;
naam, vitu saba ambavyo ni chukizo kwake:
17Macho ya kiburi,
ulimi mdanganyifu,
mikono inayoua wasio na hatia,
18moyo unaopanga mipango miovu,
miguu iliyo mbioni kutenda maovu,
19shahidi wa uongo abubujikaye uongo,
na mtu achocheaye fitina kati ya ndugu.

Onyo dhidi ya uasherati
20Mwanangu, shika maagizo ya baba yako,
wala usisahau mafundisho ya mama yako;
21yaweke daima moyoni mwako,
yafunge shingoni mwako.
22Yatakuongoza njiani mwako,
yatakulinda wakati ulalapo,
yatakushauri uwapo macho mchana.
23Maana amri hiyo ni taa,
na sheria hiyo ni mwanga.
Maonyo hayo na nidhamu yatuweka njiani mwa uhai.
24Yatakulinda mbali na mwanamke mbaya,
yatakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.6:24 Taz 5:5 maelezo.
25Usimtamani mwanamke huyo kwa uzuri wake,
wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.
26Mtu hupoteza kipande cha mkate kwa malaya,
lakini kwa mke wa mtu mwingine utapoteza uhai wako wote.
27Je, waweza kuweka moto kifuani
na nguo zako zisiungue?
28Je, waweza kukanyaga makaa ya moto
na nyayo zako zisiungue?
29Ndivyo alivyo mwanamume alalaye na mke wa mwenzake;
yeyote anayemgusa mwanamke huyo hataacha kuadhibiwa.
30Watu hawambezi sana mtu akiiba kwa sababu ya njaa;
31lakini akipatikana lazima alipe mara saba;
tena atatoa mali yote aliyo nayo.
32Mwanamume anayezini na mke wa mtu hana akili kabisa;
huyo hujiangamiza yeye mwenyewe.
33Atapata majeraha na madharau;
fedheha atakayopata haitamtoka.
34Maana wivu wa mume humfanya kuwa mkali kabisa;
wakati atakapolipiza kisasi hana cha kuhurumia.
35Hatakubali fidia yoyote;
wala kutulizwa na zawadi zako nyingi.

Methali6;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: