Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 19 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 19...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante

 kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Jehovah  Jireh..!Jehovah Nissi..!Jehovah Raah..!
Jehovah Rapha..!Jehovah Shammah..!Jehovah Shamlom..!
Emanuel-Mungu pamohja nasi..!!
Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni..!

“Sikiliza!” Asema Yesu, “Naja upesi pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake. Mimi ni Alfa na Omega, wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho.” Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, wapate kuwa na haki ya kula tunda la mti wa uhai, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake. Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona...



“Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!” Roho na Bibi arusi waseme, “Njoo!” Kila mtu asikiaye hili, na aseme, “Njoo!” Aliye na kiu na aje; anayependa, na achukue maji ya uhai bila malipo.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu tunaomba ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo Mungu wetu

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: Mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uhai, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki. Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: “Kweli naja upesi.” Amina. Njoo Bwana Yesu! Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amina.

Tazama wenye shida/tabu,watoto wako wanaokutafuta kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba  ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu  unajua haja za mioyo ya kila mmoja
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.





Jibu la Yobu

1Kisha Yobu akajibu:
2“Mtaendelea kunitesa mpaka lini,
na kunivunjavunja kwa maneno?
3Mara hizi zote kumi mmenishutumu.
Je, hamwoni aibu kunitendea vibaya?
4Hata kama ingekuwa nimekosa kweli,
kosa langu lanihusu mimi mwenyewe.
5Mnaishusha hadhi yangu mpate kujikuza;
mnanilaumu kwa kunyenyekezwa kwangu.
6Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,
na kuninasa katika wavu wake.
7Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’
Lakini sijibiwi.
Naita kwa sauti kubwa,
lakini sipati haki yangu.
8Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipite
amezitia giza njia zangu.
9Amenivua fahari yangu;
ameiondoa taji yangu kichwani.
10Amenivunja pande zote, nami nimekwisha;
tumaini langu amelingoa kama mti.
11Ameichochea ghadhabu yake dhidi yangu;
ameniona kuwa kama adui yake.
12Majeshi yake yanijia kwa pamoja;
yametengeneza njia ya kuja kwangu,
yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.
13Mungu amewaweka ndugu zangu mbali nami;
rafiki zangu wakuu wamenitoroka kabisa.
14Jamaa zangu na marafiki hawanisaidii tena.
15Wageni nyumbani mwangu wamenisahau;
watumishi wangu wa kike waniona kuwa mgeni.
Mimi nimekuwa kwao mtu wasiyemjua.
16Namwita mtumishi wangu lakini haitikii,
ninalazimika kumsihi sana kwa maneno.
17Nimekuwa kinyaa kwa mke wangu;
chukizo kwa ndugu zangu mwenyewe.
18Hata watoto wadogo hunidharau,
mara ninapojitokeza wao hunizomea.
19 Taz Sir 6:8 “Rafiki zangu wakuu wanachukizwa nami,
wale niliokuwa nikiwapenda wamenipa kisogo.
20Mwili wangu umebakia tu mifupa na ngozi,
nimeponea chupuchupu baada ya kupoteza yote.
21Nioneeni huruma,
nioneeni huruma enyi rafiki zangu;
maana mkono wa Mungu umenifinya.
22Kwa nini mnanifuatia kama Mungu?
Mbona hamtosheki na mwili wangu?
23“Laiti maneno yangu yangeandikwa!
Laiti yangeandikwa kitabuni!
24Laiti yangechorwa kwa chuma na risasi
juu ya jiwe ili yadumu!
25Najua wazi Mkombozi wangu anaishi,
mwishowe yeye atanipa haki yangu hapahapa duniani.
26Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivyo,
nitamwona Mungu kwa macho yangu mwenyewe.19:26 kwa macho yangu mwenyewe: Au Katika mwili huu.
27Mimi mwenyewe nitakutana naye;
mimi mwenyewe na si mwingine nitamwona kwa macho.
28“Nyinyi mwaweza kujisemea:
‘Tutamfuatia namna gani?
29Tutapataje kwake kisa cha kumshtaki?’
Lakini tahadharini na adhabu.
Chuki yenu yaweza kuwaletea kifo!
Mnapaswa kujua: Mungu peke yake ndiye hakimu.”



Yobu19;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: