Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 8 March 2018

Heri ya siku ya wanawake Duniani..[Happy Women's Day]





Heri ya siku ya wanawake Duniani
:Mwanamke simama kwenye nafasi yako.
Usiyumbe uwe imara kwenye majukumu yako kama Mama,Mke,Dada,Shangazi ...
Pangilia muda wako vyema .
Simama kwenye maombi/sala(Imani)
Kwenye kujifunza,kujituma,kujiheshimu na kuheshimu wengine.
Tuwe jasili,nidhamu na si nidhamu ya woga.
Tuwe na misimamo makini katika maamuzi na utendaji.
Hatua moja inaanzia hapo ulipo.
Tupunguze kulalamika.
Mungu atusaidie na kutuongoza

               “Rachelsiwa “        
                           ~
       “Basi, mwanamke mmoja miongoni mwa wake za wanafunzi wa manabii akamwendea Elisha, akamwambia, “Mtumishi wako, mume wangu amefariki, na kama ujuavyo, alikuwa mcha Mungu, lakini aliyemwia fedha amekuja kuwatwaa wanangu wawili wawe watumwa wake.” Elisha akamwuliza, “Sasa nikusaidieje? Niambie kile ulicho nacho nyumbani.” Mama huyo mjane akamjibu, “Mimi mtumishi wako sina kitu chochote ila chupa ndogo ya mafuta.” Elisha akamwambia, “Nenda kwa jirani zako uazime vyombo vitupu vingi kadiri utakavyopata. Kisha uende, wewe pamoja na wanao, mjifungie ndani ya nyumba, na muanze kujaza mafuta. Kila chombo mnachojaza, kiwekeni kando.” Akaenda na kujifungia ndani ya nyumba na wanawe na kuanza kumimina mafuta ndani ya vyombo. Vilipojaa vyote, akamwambia mwanawe mmojawapo, “Niletee chombo kingine.” Mwanae akamjibu, “Vyote vimejaa!” Hapo mafuta yakakoma kutiririka. Akarudi kwa mtu wa Mungu na kumweleza habari hizo. Naye mtu wa Mungu akamwambia, “Nenda ukauze hayo mafuta na kulipa madeni yako, ndipo wewe na wanao mtaishi kwa kutumia hayo yatakayobaki.””
‭‭2 Wafalme‬ ‭4:1-44

"Swahili Na Waswahili"Happy Women's Day.




No comments: