Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 29 January 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;1Samueli31...Mwisho wa Kitabu cha 1 Samweli..



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

haleluyah Mungu wetu yu nmwema sana..
Tunamshukuru Mungu wetu kwa kutupa neema ya kumaliza kusoma/kupitia na kujifunza katika katika kitabu.
Leo tunamalizia na  1 Swamweli na kesho  tutaanza 2 Samweli
Ikimpendeza Mungu wetu...
Isiwe ndiyo mwisho wa kujifunza/kupitia/kurudia tena vitabu
vyote tulivyopitia huko nyuma,ni vyema kuwa tunarudia kusoma ili kujifunza na kuelewa zaidi,pia tusisite kuomba msaada kwa wengine pale tusipoelewa..
Mungu akatuongoze na kutupa shauku/kiu ya kutaka kujifunza zaidi na kuelewa na kutenda yote sawasawa na mapenzi yake...
Kuna swala "MUDA/NAFASI" ya kusoma ili nitaliongelea wakati mwingine lakini ukiamua kitu na ukamuomba Mungu hutokosa muda wa kusoma NENO..


Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wote wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa. Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia, “Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu. Alipokuwa akipanda mbegu, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila. Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi, zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina. Jua lilipochomoza, zikateketea; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka. Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka. Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikamea, zikakua na kuzaa: Moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia.” Kisha akawaambia, “Mwenye masikio na asikie!”

Ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwa nguvu zetu wala si kwa uwezo wetu,si kwamba sisi ni wema sana si kwamba sisi ni wazuri mno si kwa akili zetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii ni kwa neema/rehema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu..

Asante Baba wa Mbinguni  kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante Mungu wetu kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu.
utukuzwe Mungu wetu,unastahili sifa Baba wa Mbinguni,unastahili kuabudiwa Yahweh,unastahili kuhimidiwa Jehovah,unastahili kutukuzwa
Mungu Baba....
Matendo yako ni makuu sana,Matendo yako ni ya ajabu mno..
Neema yako yatutosha Mungu wetu..!


Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano. Naye akawaambia, “Nyinyi mmejaliwa kujua siri ya ufalme wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano, ili, ‘Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe.’”
Yahweh tunakuja mbele zako tukinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako..
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea..
Jehovah tunaomba utuepushe  katika majaribu Yahweh utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..
Baba wa Mbinguni tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu Yahweh utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..


Basi, Yesu akawauliza, “Je, nyinyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote? Mpanzi hupanda neno la Mungu. Watu wengine ni kama walio njiani ambapo neno lilipandwa. Lakini mara tu baada ya kulisikia, Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao. Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu walisikiapo hilo neno hulipokea kwa furaha. Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno, mara wanakata tamaa. Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaosikia hilo neno, lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda. Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: Wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia.”

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu Jehovha tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika ufanyaji/utendaji Mungu wetu nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako...
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo Mungu wetu nasi ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Baba wa Mbinguni tunaomba tusipungukiwe katika mahitaji yetu Jehovah ukatupe kama inavyokupendeza wewe..



Yesu akaendelea kuwaambia, “Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa debe au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara. Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa. Mwenye masikio na asikie!” Akawaambia pia, “Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa. Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.”

Mafalme wa amani tunaomba amani yako ikatawale katika maisha yetu
Yahweh tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka..
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Mungu wetu tunaomba ukatamalaki na kutuatamia,Yahweh ukatuongoze tutokapo/tuingiapo Baba wa Mbinguni tunaomba ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo vyote tunavyoenda kugusa/kutumia..
Mungu Baba tukawe salama moyoni Yahweh ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia Neno lako na kulitii..


Yesu akaendelea kusema, “Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani. Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika. Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: Kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke. Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika.”
Jehovah tukanene yaliyo yako,Mungu wetu ukaonekane popote tupitapo Yahweh na ikajulikane kwamba upo Baba wa Mbinguni..
Yahweh neema yako na fadhili zako ziwe nasi Baba wa Mbinguni Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu..
Jehovah ukatupe neema ya kufuata njia zako Baba wa Mbinguni tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote za maisha yetu..
Baba wa Mbinguni ukatufanye chombo chema Yahweh tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..


Tena, Yesu akasema, “Tuufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani? Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote. Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake.” Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia. Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.

Yahwe tunaomba ukawabariki na kuwaponya wagonjwa Mungu wetu ukawape uvumilivu na imani wanaowauguza..
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawape chakula wenye njaa Yahweh ukabariki mashamba/vyanzo vyao.
Mungu wetu tunaomba kuwavushe salama wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali Jehovah tunaomba ukawe tumaini kwa wote waliokata tamaa,waliokataliwa,wenye hofu na mashaka..
Mungu wetu tunaomba ukawafariji wafiwa ukawape moyo uvumilivu na nguvu..
Yahweh ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu wenye shida/tabu Mungu wetu ukawafungue walio katika vifungo vya yule mwovu Baba wa Mbinguni tazama walio magerezani pasipo na hatia Mungu wetu tunaomba ukawatendee na haki ikapatikane..
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea na kufuata njia zako
Mungu Baba ukawasamehe wale walio kwenda kinyume nawe Mungu wetu walionguka/potea Baba wa Mbinguni ukasikie kuomba kwao Yahweh ukawabariki na kuwatendea sawasawa na mapenzi yako..


Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvuke ziwa, twende ngambo.” Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Vilevile mashua nyingine zilimfuata. Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji. Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, “Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?” Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, “Kimya! Tulia!” Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa. Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?” Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, “Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?”

Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utufu hata Milele..
Amina..!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba akadumishe pendo lenu Yahweh akawatendee sawasawa na mapenzi yake..
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo ikawe nanyi Daima..
Nawapenda. 




Kifo cha Shauli na wanawe

(Kumb 10:1-12)

1Basi, Wafilisti walipigana vita dhidi ya Waisraeli; nao Waisraeli walikimbia mbele ya Wafilisti, na kuuawa katika mlima wa Gilboa. 2Lakini Wafilisti wakamzingira Shauli na wanawe, kisha wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-shua, wana wa Shauli. 3Vita vilikuwa vikali sana dhidi ya Shauli. Wapiga mishale walipomwona walimjeruhi vibaya. 4Ndipo Shauli alipomwambia mtu aliyembebea silaha, “Chomoa upanga wako unichome nife, ili watu hawa wasiotahiriwa wasije wakanichoma upanga na kunidhihaki.” Lakini huyo aliyembebea silaha hakuthubutu kwa sababu aliogopa sana. Hivyo, Shauli alichukua upanga wake mwenyewe, na kuuangukia. 5Halafu yule aliyembebea silaha alipoona kuwa Shauli amekufa, naye pia aliuangukia upanga wake, akafa pamoja na Shauli. 6Hivyo ndivyo Shauli alivyokufa, na wanawe watatu, pia na mtu aliyembebea silaha pamoja na watu wake wote katika siku hiyohiyo moja. 7Nao Waisraeli waliokuwa upande wa pili wa bonde, na wengine waliokuwa upande wa mashariki wa mto Yordani walipoona kuwa Waisraeli wamekimbia, naye Shauli na wanawe wamekufa, waliihama miji yao, wakakimbia. Wafilisti wakaenda na kukaa katika miji hiyo.
8Kesho yake, Wafilisti walipokwenda kuwateka nyara hao waliouawa walizikuta maiti za Shauli na wanawe mlimani Gilboa. 9Walikata kichwa cha Shauli na kumvua silaha zake; halafu waliwatuma wajumbe katika nchi yao yote ya Filistia kutangaza habari njema nyumbani mwa sanamu zao na kwa watu. 10Zile silaha zake waliziweka nyumbani mwa Maashtarothi; kisha wakautundika mwili wake kwenye ukuta wa mji wa Beth-sheani.
11Lakini wakazi wa mji wa Yabesh-gileadi waliposikia Wafilisti walivyomtendea Shauli, 12mashujaa wote waliondoka, wakasafiri usiku kucha, wakaondoa mwili wa Shauli na miili ya wanawe kutoka ukuta wa Beth-sheani; wakaja nayo mpaka Yabeshi na kuiteketeza huko. 13Baadaye, wakaichukua mifupa yao na kuizika chini ya mkwaju huko Yabeshi; nao wakafunga kwa muda wa siku saba.



1Samweli31;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: