Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 30 November 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Waamuzi 14...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuiona leo hii..
Si kwa akili zetu,wala si kwa nguvu/utashi wetu,si kwamba 
tumetenda mema sana zaidi ya wengine walikuotangulia/kufa,
wengine wapo hoi vitandani wanatamani hata kutubu na kuita
jina la Mungu lakini hawana kauli,wengine hawajitambui...

Ni kwa Neema/rehema zako,Ni kwa mapenzi yako Baba wa Mbinguni sisi kuwa hivi tulivyo  leo hii..
Wapendwa tuitumie vyema nafasi hii,tumtangulize Mungu katika
yote,yeye ndiye Mungu wa uponyaji,Mungu wetu anaweza..
Mungu wetu ana nguvu,Mungu wetu anaponya,Mungu wetu anabariki,
Mungu wetu anatenda,anasikia,anajibu,anaokoa,kwakwe yeye hakuna
lisilowezakana,yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,Alfa na Omega..!!


Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu, na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkipo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo. Kila wakati ninaposali, nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu, maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu. Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo. Ndugu, upendo wako umeniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.


Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako..
 Jehovah tunaomba utesamehe makosa yetu yote tuliyoyafanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Yahweh nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote
waliotukosea,Mungu wetu tunaomba utuepushe katika majaribu
Yahweh tunaomba utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..
Baba wa Mbinguni tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu..
Mungu wetu tunaomba utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi
wetu Yesu Kristo wa Nazareti,yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate
kupona...

Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Yahweh ukatupe ubunifu,maarifa katika ufanyaji/utendaji
Mungu wetu tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki
wenye kuhuitaji...
Yahweh tusipungikiwe katika mahitaji yetu Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe..

Mfalme wa Amani tunayaweka maisha yetu mikononi mwako

Baba wa Mbinguni tunaomba baraka zako katika nyumba/ndoa
zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Yahweh tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Mungu wetu tunaomba ukatamalaki na kutuatamia,Baba wa Mbinguni
ukatupe neema ya kufuata njia zako,tukasimamie Neno lako Amri na sheria zako siku zote za maisha yetu..
Yahweh ukatupe neema ya subira,amani,fadhili,utuwema,busara,Hekima,upendo
ukatawale kati yetu,tuchukuliane na kusameheana..
Tuonyane/tuelimishane kwa upendo..

Mungu wetu ukaonekane popote tupitapo,tukanene yaliyo yako,tukapate kutambua/kujitambua..

Ukatufanye chombo chema Yahweh nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..



Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika kuungana na Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya. Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake. Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni. Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia. Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe. Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Injili. Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika. Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. Na sasa yeye si mtumwa wa kawaida, ila ni bora zaidi ya mtumwa: Yeye ni ndugu yetu mpenzi. Ni wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi, kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana. Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe. Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi. Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako). Naam, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo. Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba. Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.

Mungu wetu tunawaweka ndugu zetu wanaopitia magumu/majaribu
mbali mbali Baba tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Mungu wetu tunaomba uponyaji wako kwa wagonjwa,Yahweh tunaomba
ukawapatie chakula na ukabariki mashamba yao wote wenye njaa..
Jehovah tunaomba ukawaguse wenye shida/tabu,waliokata tamaa,
walio na hofu,mashaka Baba ukawe tumaini lao..
Mungu wetu ukawafungue wote waliokatika vifungo vya yule mwovu..
Baba tunaomba ukawasamehe wale wote waliokwenda kinyume nawe
Mungu wetu tunaomba ukawape neema ya kujiombea na kufuata njia zako
Baba tunaomba ukasikie kilio cha watoto wako wanaokuomba kwa 
bidii na imani,Wafiwa ukawe mfariji wao..
Ee Mungu wetu tunaomba upokee sala/maombi yetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hat Milele..
Amina..!



Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu. Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu. Nawatakieni nyinyi nyote neema ya Bwana Yesu Kristo.


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwa kuwa nami
Mungu mwenyezi akawaguse kwa mkono wake wenye nguvu
akawabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye..
Nawapenda.

Matendo ya kwanza ya ushujaa ya Samsoni


1Siku moja, Samsoni aliteremka na kwenda Timna ambako alimwona msichana mmoja Mfilisti. 2Aliporudi nyumbani akawaambia wazazi wake, “Nimemwona msichana mmoja Mfilisti huko Timna. Niozeni msichana huyo.” 3Lakini wazazi wake wakamwambia, “Je, hakuna msichana yeyote miongoni mwa ndugu zako au kati ya watu wetu hata uende kuoa kwa Wafilisti wasiotahiriwa?” Lakini Samsoni akamwambia baba yake, “Niozeni msichana huyo, maana ananipendeza sana.”
4Wazazi wake hawakujua kwamba huo ulikuwa mpango wa Mwenyezi-Mungu ambaye alikuwa anatafuta kisa cha kuchukua hatua dhidi ya Wafilisti. Wakati huo, Wafilisti waliwatawala Waisraeli.
5Samsoni na wazazi wake waliondoka kwenda Timna. Walipofika huko kwenye mashamba ya mizabibu, mwanasimba mmoja akatokea akamngurumia Samsoni. 6Basi, roho ya Mwenyezi-Mungu ikamwingia Samsoni kwa nguvu, akamrarua simba huyo kama mtu araruavyo mwanambuzi. Naye Samsoni hakuwaambia wazazi wake kisa hicho. 7Kisha akateremka akaenda kuzungumza na yule msichana; huyo msichana alimpendeza sana Samsoni. 8Baada ya siku chache alirudi huko Timna kumchukua huyo msichana. Alipokuwa njiani akageuka pembeni kuuona mzoga wa yule simba, na kumbe kulikuwa na nyuki ndani ya mzoga na asali. 9Basi, akapakua asali kwa mikono yake akawa anakula huku akiendelea na safari yake. Aliporudi kwa wazazi wake, akawapa asali kidogo nao wakala. Lakini hakuwaambia kwamba alitoa asali hiyo ndani ya mzoga wa simba.
10Baba yake akaenda nyumbani kwa yule msichana, naye Samsoni akafanya karamu huko, kama walivyofanya vijana wakati huo. 11Wafilisti walipomwona Samsoni wakamletea vijana thelathini wakae naye. 12Samsoni akawaambia, “Nitatega kitendawili. Kama mkiweza kutegua kitendawili hicho kwa muda wa siku saba za sherehe za harusi, basi, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi thelathini ya sikukuu. 13Lakini msipoweza kukitegua, nyinyi mtanipa mavazi thelathini ya kitani na mavazi thelathini ya sikukuu.” 14Nao wakamwambia, “Haya tega tusikie.” Samsoni akawaambia,
“Kwa mla kukatoka mlo
kwa mwenye nguvu, utamu.”
Baada ya siku tatu hao vijana walikuwa bado hawajaweza kutegua hicho kitendawili.
15Basi siku ya saba14:15 siku ya saba: Hati nyingine za kale: Siku ya nne. wakamwambia mke wa Samsoni, “Mbembeleze mumeo ili atuambie maana ya kitendawili hicho, la sivyo tutakuteketeza kwa moto wewe pamoja na nyumba ya baba yako. Je, mlitualika hapa kuja kutunyanganya mali zetu?” 16Mke wa Samsoni akamwendea Samsoni, huku machozi yanamtiririka, akamwambia, “Kwa kweli unanichukia; hunipendi hata kidogo. Umewategea kitendawili watu wangu na hukuniambia maana yake.”
Samsoni akamjibu, “Mimi sijawaeleza hata wazazi wangu. Sasa nitawezaje kukuambia wewe?” 17Lakini aliendelea kulia katika muda wao wote wa siku saba za sherehe za harusi. Siku ya saba Samsoni akamwambia mkewe kile kitendawili kwani alimbana sana. Mkewe akaenda haraka akawaambia watu wake. 18Siku hiyo ya saba, kabla ya jua kutua, wakamwambia Samsoni,
“Ni kitu gani kitamu kuliko asali?
Ni nani mwenye nguvu kuliko simba?”
Samsoni akawajibu, “Kama hamngejishughulisha na mtamba wangu hamngeweza kukitegua kitendawili changu.”
19Hapo roho ya Mwenyezi-Mungu ikamjia Samsoni kwa nguvu, naye akaenda mjini Ashkeloni, akawaua watu thelathini, kisha akachukua mavazi yao ya sikukuu, akawapa wale waliotegua kitendawili chake. Halafu akaondoka, akaenda nyumbani kwa wazazi wake akiwa na hasira kali. 20Basi, wakamwoza mwanamke wake kwa kijana mmoja ambaye alikuwa mdhamini wa Samsoni katika harusi.

Waamuzi 14;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.


No comments: