Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 5 July 2017

Kikombe Cha Asubuhi;kitabu cha Hesabu..2

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote..
Mtakatifu..!Mtakatifu..!Mtakatifu..! Baba wa Mbinguni,Mungu wetu na Baba yetu..Muumba wetu na Muumba Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo,
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..!
Yahweh..!Jehovah..!El shaddai..!Elohim..!Muweza wa Yote..!
Asante kwa wema na fadhili zako Baba..
Asante kwa ulinzi wako wakati wote na kutuamsha salama na wenye afya
Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendele kuiona Leo hii..
Si kwa uwezo wetu wala nguvu zetu..si kwamba sisi ni wema sana..
Ni kwa Neema/rehema zako Mungu Baba na Mapenzi yako kwetu..
Si kwamba waliotangulia/ni wabaya mno au si wema Baba..
Imekupendeza wewe Mungu wetu ...!!

Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: Ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake. Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
Tunakuja mbele zako Mungu Baba tukijinyenyekeza,tukijishusha na tukijiachilia mikononi mwako Jehovah..
 Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mungu wetu
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..Mungu Baba..
Tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale waliotukosea..
Utuepushe na majaribu na utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu kwa Damau ya Mwanao Mpendwa..
Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona...


Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu. Yeye ametufungulia njia mpya, njia ya uhai, kupitia lile pazia, yaani mwili wake mwenyewe. Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa kutokana na dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi. Tuzingatie kabisa tumaini letu tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu. Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema. Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, siku ile ya Bwana inakaribia. Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna tambiko iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi. Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga. Mtu yeyote asiyetii sheria ya Mose, huuawa bila huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu. Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani? Maana tunamfahamu yule aliyesema, “Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza,” na ambaye alisema pia, “Bwana atawahukumu watu wake.” Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno! Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, nyinyi mlistahimili. Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo. Mlishiriki mateso ya wafungwa na mliponyanganywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele. Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatia tuzo kubwa. Mnahitaji kuwa na uvumilivu ili muweze kutimiza matakwa ya Mungu na kupokea kile alichoahidi. Maana kama yasemavyo Maandiko: “Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia. Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye.” Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tumo na wale wanaoamini na kuokolewa.
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tupate kutambua/kujitambua
na tukawe na kiasi..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yake...

Mungu wetu tunayaweka maisha yetumikononi mwako..
Tunaomba utubariki na ukabariki vyote tunavyoenda kufanya/kutenda..
Mungu wetu ukatuongoze tukatende kama itakavyokupendeza wewe..
Ukabariki kuingia kwetu/kutoka kwetu vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Mungu Baba ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu na ukatupe kulingana na mapenzi yako
Asante Mungu wetu tunarudisha sifa na utukufu ni wako..
tunayaweka haya yote mikononi mwako tukiamini na kushukuru...

Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!
Asanteni wapendwa/waungwana kwakuwa pamoja..
Mungu Baba akaonekane kwenye maisha yenu..
Mungu awabariki muingiapo/mtokapo..
Msipungukiwe katika mahitaji yenu kama ikatavyompendeza yeye..
Nawapenda.



Kupangwa kwa makabila

1Mwenyezi-Mungu aliwapa Mose na Aroni, maagizo yafuatayo: 2“Waisraeli watapiga kambi zao, kila mmoja akikaa mahali penye bendera yake, penye alama za ukoo wake. Watapiga kambi zao kulizunguka hema la mkutano.
3“Wale watakaopiga kambi upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua watakuwa kikundi cha watu walio chini ya bendera ya Yuda na kiongozi wao atakuwa Nashoni mwana wa Aminadabu, 4kikosi chake kulingana na hesabu ni wanaume 74600. 5Wale watakaofuata kupiga kambi baada ya watu wa Yuda watakuwa kabila la Isakari, kiongozi wao akiwa Nethaneli mwana wa Suari, 6kikosi chake kulingana na hesabu ni wanaume 54,400. 7Kisha kabila la Zebuluni, kiongozi wao akiwa Eliabu mwana wa Heloni, 8kikosi chake kulingana na hesabu ni wanaume 57,400. 9Jumla yote ya watu watakaokuwa katika kambi ya Yuda kulingana na makundi yao ni watu 186,400. Hao ndio watakaotangulia kusafiri.
10“Kwa upande wa kusini, wale walio chini ya bendera ya kundi la Reubeni kulingana na makundi yao, kiongozi wao akiwa Elisuri mwana wa Shedeuri, 11kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 46,500. 12Kisha wale watakaopiga kambi kando ya watu wa Reubeni watakuwa ni watu wa kabila la Simeoni, kiongozi wao akiwa Shelumieli mwana wa Suri-shadai, 13kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 59,300. 14Hatimaye kabila la Gadi, kiongozi wao akiwa Eliasafu mwana wa Reueli, 15kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 45,650. 16Jumla ya wanaume watakaokuwa katika kambi ya Reubeni kulingana na makundi yao ni watu 151,450. Hawa ndio watakaokuwa katika msafara wa pili.
17“Halafu, kambi ya kabila la Walawi, ikiwa katikati ya kambi zote, na wakiwa wamebeba hilo hema la mkutano, wataondoka; kila kundi litasafiri kwa kufuata nafasi yake chini ya bendera yao.
18“Kwa upande wa magharibi, wale walio chini ya bendera ya kundi la Efraimu watapiga kambi kulingana na makundi yao, kiongozi wao akiwa Elishama mwana wa Amihudi, 19kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 32,200. 20Mara tu baada ya Waefraimu litafuata kabila la Manase: Kiongozi wake akiwa Gamalieli, mwana wa Pedasuri, 21kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa watu 32,000. 22Hatimaye kabila la Benyamini: Kiongozi wake ni Abidani, mwana wa Gideoni, 23kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 35,400. 24Jumla ya watu watakaokuwa katika kambi ya Efraimu kulingana na makundi yao ni watu 108,100. Kundi hili la Efraimu litakuwa katika msafara wa tatu.
25“Kwa upande wa kaskazini, watapiga kambi katika makundi yao wale walio chini ya bendera ya Dani, kiongozi wao atakuwa Ahiezeri, mwana wa Amishadai, 26kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 62,700. 27Kisha wale watakaopiga kambi baada yao watakuwa watu wa kabila la Asheri, kiongozi wao akiwa Pagieli mwana wa Okrani, 28kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 41,500.
29“Hatimaye watu wa kabila la Naftali, kiongozi wake akiwa Ahira mwana wa Enani, 30kikosi chake kulingana na hesabu, kitakuwa na watu 53,400. 31Jumla ya watu watakaokuwa katika kambi ya Dani kulingana na makundi yao ni watu 157,600. Kundi hili la Dani litakuwa katika msafara wa mwisho, bendera baada ya bendera.”
32Hao ndio Waisraeli waliohesabiwa kulingana na koo zao, katika kambi na vikosi vyao; wote walikuwa 603,550. 33Lakini Walawi hawakuhesabiwa miongoni mwa watu wa Israeli kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Mose.
34Hivyo ndivyo, Waisraeli walivyofanya kila kitu kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Mose. Walipiga kambi zao, kufuata bendera zao na walisafiri kila mmoja akiandamana na jamaa yake kwa kufuata ukoo wake.

Hesabu2;1-34


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: