Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 12 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..12...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote..

Asante Mungu wetu Baba yetu,Asante kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako usiku na siku zote umekuwa nasi Jehovah..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa Kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwa uwezo wetu wala nguvu zetu ni kwa Neema/Rehema yako tuu Mungu wetu sisi kuwepo leo hii na kuweza kufanya yote haya tufanyayo..

Tazama Jana imepita Baba wa Mbinguni Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..
Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Yahweh..

Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Roho mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Utuepushe na majaribu ya yule mwovu na kazi zake..Utuokoe na kutufunika na Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase  Miili yetu na Akili zetu kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Tukaanze nawe Bwana wetu katika wiki hii..yote tunayoenda kufanya/kutenda yakaendane na matakwa yako Jehovah..

ukaonekane kwenye maisha yetu Yahweh..!ukatupe hekima,Busara katika kuamua na kutenda,tukapate kutambua/kujitambua..
Tukaelewe na kulijua Neno lako,Tukafuate na  tukatii sheria zako na Amri zako

Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Kila kuhani mkuu ambaye huchaguliwa miongoni mwa watu hupewa jukumu la kushughulikia mambo ya Mungu kwa niaba ya watu, kutolea zawadi na tambiko kwa ajili ya dhambi. Maadamu yeye mwenyewe ni dhaifu, anaweza kuwatendea kwa huruma wale wasiojua kitu na wanaofanya makosa. Kwa sababu hiyo anapaswa kutoa tambiko si tu kwa ajili ya watu, bali pia kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe. Hakuna mtu awezaye kujifanya mwenyewe kuwa kuhani mkuu. Kila mmoja huteuliwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kama alivyokuwa Aroni. Hali kadhalika naye Kristo; yeye hakujitwalia mwenyewe heshima ya kuwa kuhani mkuu, bali Mungu alimteua na kumwambia: “Wewe ni Mwanangu; mimi leo nimekuwa baba yako.” Alisema pia mahali pengine: “Wewe ni kuhani milele, kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.” Yesu alipokuwa anaishi hapa duniani, kwa kilio kikuu na machozi, alisali na kumwomba Mungu ambaye alikuwa na uwezo wa kumwokoa kifoni; naye alisikilizwa kwa sababu ya kumcha Mungu. Lakini, ingawa alikuwa Mwana wa Mungu, alijifunza kutii kwa njia ya mateso. Na alipofanywa mkamilifu, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii, naye Mungu akamteua kuwa kuhani mkuu kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.
Ukatuongoze ee Mungu wetu na ukatubariki na kubariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo nasi utupe neema ya kuwabariki wenyekuhitaji..

 Neno lako likawe Mwanga kwenye maisha yetu likawe faida na likatufae sisi na wengine pia..
Wale walio asi wakapate kurudi kundini na kuwa pamoja katika kuamini na kujifunza zaidi..



Tunayo mengi ya kusema juu ya jambo hili, lakini ni vigumu kuwaelezeni, kwa sababu nyinyi si wepesi wa kuelewa. Kwa wakati huu nyinyi mngalipaswa kuwa waalimu tayari, lakini mnahitaji bado mtu wa kuwafundisheni mafundisho ya mwanzo juu ya neno la Mungu. Mnahitaji maziwa badala ya chakula kigumu. Kila anayepaswa kunywa maziwa ni mtoto bado, hajui uadilifu ni nini. Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu waliokomaa, waliofunzwa kwa vitendo kubainisha mema na mabaya.

.Baba wa Mbinguni ukaonekane kwenye Maisha yetu na tusipungukiwe na mahitaji yetu..

Tunayaweka haya yote mikononi mwako,Tukiamini wewe ni Mungu wetu hatuna Mungu mwingine..
Yote tuliyoyanena na kutonena Baba unayajua na unatujua kuliko tunavyojijua..
Mungu wetu ukatupe sawasawa na mapenzi yako..


Sifa na Utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..

Amina..!
Mungu aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake..
Niwashukuru sana kwakunisoma/kupita hapa..
Nawapenda.

Kuwatakasa wanawake baada ya kujifungua

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2“Waambie watu wa Israeli hivi: Mwanamke akipata mimba, akajifungua mtoto wa kiume, atakuwa najisi kwa muda wa siku saba kulingana na siku zake zihusikanazo na hali ya wanawake. 3#Taz Mwa 17:12; Luka 2:21 Mtoto huyo atatahiriwa katika siku yake ya nane. 4Kisha mama mtoto ataendelea kuwa najisi kwa muda wa siku thelathini na tatu. Wakati huo, kamwe asiguse chochote kilichowekwa wakfu wala kuingia mahali patakatifu mpaka siku za kutakasika kwake zitakapotimia. 5Lakini, kama amejifungua mtoto wa kike, basi, atakuwa najisi kwa muda wa majuma mawili kama ilivyo anapokuwa katika siku zake. Ataendelea katika kutakasika kwake kwa muda wa siku sitini na sita.
6“Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, iwe amepata mtoto wa kiume au wa kike, atamletea kuhani mlangoni mwa hema la mkutano mwanakondoo wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na kinda la njiwa au hua, kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi. 7Kuhani atamtolea mbele ya Mwenyezi-Mungu na kumfanyia huyo mama ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu. Hivyo huyo mwanamke atakuwa safi kutokana na damu yake. Huo ni mwongozo kuhusu mwanamke yeyote anayejifungua mtoto wa kiume au wa kike.
8 # Taz Luka 2:24 “Kama hawezi kutoa mwanakondoo, basi, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa; mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuondolea dhambi. Kuhani atamfanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.”

Mambo Ya Walawi12;1-8


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: