Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 30 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..3...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote..

Asante Baba wa mbinguni kwa wema na fadhili zako..
Asante kwa ulinzi wako usiku wote na wakati wote..
Asante kwa kutuamsha salama na wenye Afya..
Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuina leo hii..
Tunashuka mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Jehovah..!

Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Baba wa Mbinguni nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..

Yahweh..!utuepushe na majaribu utuokoe na yule mwovu na kazi zake..
Baba wa Mbinguni ututakase Miili yetu na Akili zetu na utufunike kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Mungu wetu ukatamalaki katika nyumba zetu na ukatuatamie na kutubariki katika yote..

Baba wa Mbinguni ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo,vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri,Tuingiapo/tutokapo, tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!

Tazama wenye shida/tabu,wanaopitia magumu/majaribu ,walio kwenye vifungo mbalimbali,Wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliokata tamaa,waliokataliwa,wenye Hofu/mashaka Baba wa mbinguni ukawaguse na mkono wako wenye nguvu,ukawaponye na kuwaokoa katika mapito yao, Mfalme wa Amani ukaonekane kwenye mahitaji yao..
Baba wa Mbinguni wapate kupona kimwili na kiroho na ukawape sawasawa na mapenzi yako..

Nyinyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa na dhambi zenu. Wakati ule mliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, mkawa mnamtii mtawala wa pepo wenye nguvu wa anga, pepo ambao huwatawala sasa watu wasiomtii Mungu. Na hata sisi sote tulikuwa kama wao; tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kidunia na kufanya tu mambo yale yaliyoipendeza miili na akili zetu. Kidunia, sisi kama vile pia wao, tulistahili ghadhabu ya Mungu. Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa mapendo yasiyopimika, hata, ingawa tulikuwa tumekufa kwa sababu ya dhambi, alitufanya hai pamoja na Kristo. Kwa neema ya Mungu nyinyi mmeokolewa. Kwa kuungana na Kristo Yesu, Mungu alitufufua pamoja naye, tukatawale pamoja naye mbinguni. Ndivyo alivyopenda kuonesha kwa watu wa nyakati za baadaye ukuu wa neema yake aliyotujalia kwa ukarimu katika kuungana kwetu na Kristo Yesu. Maana, kwa neema ya Mungu mmekombolewa kwa njia ya imani. Jambo hili si matokeo ya juhudi zenu, bali ni zawadi ya Mungu. Wala halitokani na matendo yenu wenyewe, asije mtu akajivunia kitu. Sisi ni viumbe vyake Mungu, na kwa kuungana na Kristo Yesu, alituumba kwa ajili ya kuishi maisha ya matendo mema aliyotutayarishia tuyatende.
Baba wa Mbinguni ukatupe Hekima, Busara katika yote tusiwe watu wakujisifu,kujivuna,kutaka mambo yetu wenyewe yasiyompendeza Mungu, tusiwe wenye kiburi,dharau,kujiona na wenye chuki na kisasi..
tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Tunashukuru na kuyaweka haya yote mikononi mwako..
Tukiamini wewe ni Mungu wetu..
Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe..
Amina..!
Asanteni sana wote mnaopitia Hapa..
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea..
msipungukiwe na mahitaji yenu..
Mungu wetu yu mwema sana
na akawaguse na mkono wake wenye nguvu..
Nawapenda.



Sadaka za muungano

1“Kama mtu anatoa sadaka ya amani, na sadaka yake ni ng'ombe dume au jike basi, mnyama huyo asiwe na dosari mbele yangu. 2Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha mnyama huyo na kumchinja mlangoni mwa hema la mkutano. Hao makuhani wazawa wa Aroni watainyunyizia madhabahu damu yake pande zake zote. 3Mafuta yote yanayofunika na yaliyo juu ya matumbo ya mnyama wa sadaka hiyo ya amani atayateketeza kama sadaka anayotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto. 4Atatoa pia zile figo mbili na mafuta yake pamoja na ile sehemu bora ya ini. 5Wazawa wa Aroni wataiteketeza madhabahuni pamoja na sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni; hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumpendeza Mwenyezi-Mungu.
6“Kama sadaka hiyo ya kufanya amani unayomtolea Mwenyezi-Mungu ni kutoka kundi la kondoo au mbuzi, basi achaguliwe dume au jike asiye na dosari. 7Kama mtu atatoa mwanakondoo kuwa sadaka yake, basi, atamtolea mbele ya Mwenyezi-Mungu, 8akiweka mkono wake juu ya kichwa cha mnyama huyo na kumchinja mbele ya hema la mkutano. Makuhani wazawa wa Aroni watainyunyizia madhabahu damu yake pande zake zote. 9Kisha, kutoka katika sadaka hiyo ya amani anayotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto, atamtolea sehemu zifuatazo: Mafuta yake, mkia wenye mafuta mzima uliokatwa karibu kabisa na uti wa mgongo pamoja na mafuta yote yanayofunika matumbo na mafuta yote yaliyo kwenye matumbo, 10zile figo mbili na mafuta yake pamoja na sehemu bora ya ini. 11Kuhani ataviteketeza hivyo vyote juu ya madhabahu kama chakula anachotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto.
12“Kama sadaka yake ni mbuzi, basi, atamtolea mbele ya Mwenyezi-Mungu 13akiweka mkono wake juu ya kichwa cha mnyama huyo na kumchinja mbele ya hema la mkutano. Wazawa wa Aroni watainyunyizia madhabahu damu yake pande zake zote. 14Kisha, mafuta yote yanayofunika matumbo 15na zile figo mbili na mafuta yake pamoja na sehemu bora ya ini, atamtolea Mwenyezi-Mungu sadaka ya kuteketezwa kwa moto. 16Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula kinachotolewa kwa Mwenyezi-Mungu kwa moto kutoa harufu ya kumpendeza Mungu. Mafuta yote ni ya Mwenyezi-Mungu. 17Ndiyo maana siku zote na mahali popote mtakapokaa ni lazima kushika kanuni hii. Kamwe msile mafuta wala damu.”

Mambo Ya Walawi 3;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: