Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 17 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 34...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu...

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na Fadhili zako, Asante kwa ulinzi wako na kutuamsha salama, Asante kwa kutupa Kibali cha kuendelea kuiona siku hii..
Tunakuja mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Baba Mungu tunaomba nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe walio tukosea..
Roho mtakatifu akatuongoze tupate kutambua na kujitambua na tuwe na kiasi..
Baba tunaomba utulinde na kutuokoa na yule mwovu na kazi zake zote..ukatutakase Miili yetu na Akili zetu na utufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Tunajua kwamba kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, kwa sababu Mwana wa Mungu humlinda salama, na yule Mwovu hawezi kumdhuru. Tunajua kwamba sisi ni wake Mungu ingawa ulimwengu wote unatawaliwa na yule Mwovu. Twajua pia kwamba Mwana wa Mungu amekuja, akatupa elimu ili tumjue Mungu wa kweli; tuishi katika muungano na Mungu wa kweli – katika muungano na Mwanae, Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na huu ndio uhai wa milele. Watoto wangu, epukaneni na sanamu za miungu!

Asante Mungu wetu kwa Upendo wako kwetu ,Nasi ukatupe moyo wa upendo kwa wengine, tukawe na upendo wa kweli..

Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu. Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo. Na Mungu alionesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uhai kwa njia yake. Hivi ndivyo upendo ulivyo: Si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu. Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.

Asante kwa ridhiki zetu Baba wa Mbinguni tunaomba ukazibariki nasi tuweze kuwabariki wengine wenye kuhitaji..
Asante kwa kazi zetu,Biashara,Masomo tunaviweka mikononi mwako Baba wa mbinguni tunaomba ukabariki na kutuongoza vyema..
Mfalme wa Amani ukabariki tuingiapo/tutokapo, vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!
Vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Jehovah..! Ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Mfalme wa Amani tazama wenye shida/tabu, wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao,waliokwenye vifungo mbalimbali, wanaopitia magumu/majaribu yoyote Mungu wetu, Baba yetu, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.. Tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu na uponyaji..wakapate kupona kimwili na kiroho pia..ukaonekane kwenye mapito yao Baba..
Maisha yetu yapo mikononi mwako Baba wa Mbinguni hatuna Mungu mwingine, hakuna wa kuabudiwa ila ni wewe tuu Mfalme wa Amani.. wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho, wewe ni Alfa na Omega..Sifa na utukufu ni wako Jehovah Jireh...!!

Tunayaweka haya yote mikononi mwako, Tunashukuru na kukuabudu Mungu wetu..
Amina..!!

Asanteni kwakutembelea hapa..
Mungu aendelee kuwabariki na kubariki kazi zenu na familia zenu..

Awape sawasawa na mapenzi yake..
Nawapenda.

Vibao vipya vya agano

(Kumb 10:1-5)

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitayaandika maneno yale yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza ulivyovivunja. 2Uwe tayari kesho asubuhi, uje kukutana nami mlimani Sinai. 3Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane popote mlimani; wala kondoo au ng'ombe wasilishwe karibu yake.” 4Basi, Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza. Akaondoka asubuhi na mapema, akapanda mlimani Sinai, kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru, akiwa na vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake. 5Mwenyezi-Mungu akashuka katika wingu, akasimama pamoja na Mose, akalitaja jina lake, “Mwenyezi-Mungu.” 6Taz Kut 20:5-6; Hes 14:18; Kumb 5:9-10; 7:9-10 Kisha Mwenyezi-Mungu akapita mbele ya Mose akitangaza tena, “Mwenyezi-Mungu; mimi Mwenyezi-Mungu, ni Mungu mwenye huruma na neema; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili na uaminifu. 7Mimi nawafadhili maelfu,34:7 maelfu: Au Maelfu ya vizazi. nikiwasamehe uovu, makosa na dhambi; lakini kwa vyovyote vile sitaacha kumwadhibu mwenye hatia; nawapatiliza watoto na wajukuu uovu wa baba na babu zao, hata kizazi cha tatu na nne.”
8Mose akainama chini mara, akamwabudu Mungu. 9Kisha akasema, “Ee Bwana wangu, kwa vile umenijalia fadhili mbele zako, nakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na dhambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.”

Agano lafanywa upya

(Kut 23:14-19; Kumb 7:1-5; 16:1-17)

10Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Sasa ninafanya agano na watu wako. Nitatenda maajabu mbele yao ambayo hayajapata kutendwa duniani kote, wala katika taifa lolote. Na watu wote mnaoishi kati yao wataona matendo yangu makuu. Maana nitafanya jambo la ajabu kwa ajili yako.
11“Shikeni amri ninazowapa leo. Nitawafukuza mbele yenu Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. 12Jihadharini msije mkafanya agano na wakazi wa nchi mnayoiendea, maana hilo litakuwa mtego miongoni mwenu. 13Taz Kumb 16:21 Lakini mtazibomoa madhabahu zao na kuzivunja nguzo zao za ibada na sanamu zao za Ashera.34:13 Ashera: Mungu wa kike aliyeabudiwa na wananchi wa Kanaani. 14Msiabudu mungu yeyote mwingine, maana mimi Mwenyezi-Mungu najulikana kwa jina: ‘Mwenye Wivu,’ mimi ni Mungu mwenye wivu. 15Msifanye mikataba yoyote na wakazi wa nchi hiyo, maana watakapoiabudu miungu yao ya uongo na kuitambikia, watawaalikeni, nanyi mtashawishiwa kula vyakula wanavyoitambikia miungu yao, 16nao wavulana wenu wakaoa binti zao, na hao binti wanaoabudu miungu yao, wakawashawishi wavulana wenu kufuata miungu yao.
17 Taz Kut 20:4; Lawi 19:4; Kumb 5:8; 27:15 “Msijifanyie miungu ya uongo ya chuma.
18 Taz Kut 12:14-20; Lawi 23:6-8; Hes 28:16-25 “Mtaiadhimisha sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu. Kwa muda wa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu,34:18 mwezi wa Abibu: Ni kati ya Machi na Aprili katika kalenda yetu. kama nilivyowaamuru, kwa sababu katika mwezi huo wa Abibu mlitoka Misri. 19Taz Kut 13:2 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume ni wangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wako wote, wa ng'ombe na wa kondoo. 20Mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa kunitolea kondoo. Kama hutamkomboa utamvunja shingo. Watoto wenu wote wa kiume ambao ni wazaliwa wa kwanza mtawakomboa. Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu.
21“Siku sita mtafanya kazi zenu, lakini siku ya saba mtapumzika, hata ikiwa ni wakati wa kulima au kuvuna. 22Taz Kut 23:16 Mtaadhimisha sikukuu ya majuma34:22 majuma: Au Pentekoste. mwanzoni mwa majira ya mavuno ya ngano, na sikukuu ya kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka. 23Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakusanyika mbele yangu mimi Bwana Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli. 24Nitayafukuza mataifa mengine mbele yenu na kuipanua mipaka yenu. Hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yenu wakati mnapokusanyika kuniabudu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu mara tatu kila mwaka.
25“Msinitolee damu ya tambiko yangu pamoja na chachu; wala tambiko ya sikukuu ya Pasaka isibakizwe mpaka asubuhi.
26 Taz Kumb 24:21; 26:2 “Mazao ya kwanza ya ardhi yako utayaleta nyumbani kwangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.
“Usimchemshe mwanakondoo au mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.”
27Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Andika maneno haya, maana kulingana na maneno haya, ninafanya agano nawe na watu wa Israeli.” 28Mose alikaa huko mlimani pamoja na Mwenyezi-Mungu siku arubaini, mchana na usiku; hakula chakula wala kunywa maji. Aliandika maneno yote ya agano na zile amri kumi.

Mose anashuka kutoka mlimani Sinai

29 Taz 2Kor 3:7-16 Mose alipokuwa anashuka mlimani Sinai akiwa na vile vibao viwili vyenye maneno ya agano mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa unangaa kwa sababu alikuwa ameongea na Mwenyezi-Mungu. 30Aroni na watu Waisraeli wote walipomwona waliogopa kumkaribia, kwani uso wake ulikuwa unangaa. 31Lakini Mose alimwita Aroni na viongozi wa jumuiya ya Waisraeli waende karibu naye, kisha akazungumza nao. 32Baadaye Waisraeli wote wakaja karibu naye, naye akawapa amri zote ambazo Mwenyezi-Mungu alimpa kule mlimani Sinai. 33Mose alipomaliza kuzungumza na watu aliufunika uso wake kwa kitambaa. 34Lakini ikawa kwamba kila mara Mose alipokwenda kuongea na Mwenyezi-Mungu katika hema la mkutano, alikiondoa kile kitambaa mpaka alipotoka nje. Na alipotoka nje aliwaambia Waisraeli mambo yote aliyoamriwa, 35nao Waisraeli waliuona uso wake unangaa. Ndipo Mose alipoufunika tena uso wake kwa kitambaa mpaka alipokwenda kuongea na Mwenyezi-Mungu.

Kutoka34;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: