Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 5 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 27...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa wema na fadhili zake kwetu..
Mungu wetu, Baba yetu, Muumba wetu, Muumba Mbingu na Nchi, Muumba wa vyote vilivyopo, Mume wa Wajane, Baba wa Yatima,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Yahweh..!! Jehovah nissi..!, Jejovah rapha..!, Jehovah shalom..! Jehovah jireh..! Jehovah Shammah..!Jehovah Rohi..!!
Asante Baba kwa wema na fadhili zako, Asante kwa ulinzi wako usiku mzima,Asante kwakutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii Baba wa Mbinguni..

Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kuomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua,kutojua Mfalme wa Amani tunaomba na sisi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe wale waliotukosea..
Baba tunaomba utuokoe na Mwovu na kazi zake zote, zikashindwe na ututakase  Miili yetu na Akili zetu na Utufunike  kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Baba ukatuponye rohoni na Roho mtakatifu akatuongoze katika yote na tupate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..

Tukapendane na kusaidiana katika kweli,tusiwe watu wa kujikweza na kujitapa,tusiwe wenye kuhukumu, tusiwe watu wa kisasi,tusiwe wenye kiburi na kukoseana adabu.

Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Tukawe na Imani na kuwaombea wengine, Tukawe wavumilivu na wenye kushukuru..



Kwa hiyo, ndugu zangu, maadamu Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: Mtoleeni Mungu miili yenu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu. Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu na kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu. Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni nyinyi nyote: Msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kadiri ya kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.

Mfalme wa Amani tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu wote wanaopitia magumu/majaribu,shida/tabu,waliokwenyevifungo mbalimbali,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao, wanaotafuta watoto,wanaotafuta mume/mke,waliokata tamaa,wenye hofu na mashaka,wanaugua rohoni,waliokataliwa na walio njia panda hawaelewi waanzie wapi waishie wapi..maisha yamekuwa magumu hawana kazi wala biashara Baba ukawape ubunifu, Maarifa na ukawape hekima na busara kwenye maamuzi...

Mfalme wa Amani tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo, ukabariki tuingiapo/tutokapo,vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..
Ukamguse kila mmoja na kumbariki naye aweze kumbariki mwingine, iwe kwa chakula, iwe kwa kumuombea mwinzie, iwe kwa pesa, iwe kwa kumtakia maneno ya baraka na kumsamehe kabisa yule aliye mkosea na alikuwa kikwazo kwenye moyo wake..

Baba ukatende na kuponya mioyo yao, ukamalize kabisa uchungu moyoni, ukawape neema ya kupendana na kutakiana amani ya moyo..na wakawe na kiasi ili wasije kukwazana tena..

Ndugu yangu mpendwa yakabidhi hayo mapito yako kwa Mungu na umuombe akupe neema ya kutua hiyo mizigo uliyobeba..yanini kujitesa na mizigo mizito na yupo awezaye kukutua?Yanini kujitafutia mateso na kuugua rohoni na mponyaji yupo?
Mkabidhi Mungu nawe uwe huru na mwepesi..
Mungu wetu atupenda na alimtoa mwanawe mpendwa Bwana wetu Yesu Kristo aliteseka ili sisi tupate kupona..

Matafuteni Bwana maadam anapatikana..
Kwa Mungu yote yanawezekana...
Sifa na utukufu tumrudishie Mungu wetu, Tunakushuru Mungu wetu na tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Amina..!
Asante kwa wote mnaotembelea hapa
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea zaidi..
Nawapenda.

Madhabahu

(Kut 38:1-7)

1“Utatengeneza madhabahu kwa mbao za mjohoro. Madhabahu hiyo itakuwa ya mraba, urefu wake mita27:1 mita: Vipimo hivyo awali ni dhiraa, urefu wa kutoka kiwiko cha mkono hadi ncha ya kidole cha kati. mbili na robo, na upana wake mita mbili na robo; kimo chake kitakuwa mita moja na robo. 2Katika kila pembe ya madhabahu hiyo utatengeneza upembe ambao utakuwa umeundwa kutokana na madhabahu yenyewe. Madhabahu hiyo yote utaipaka shaba. 3Utaitengenezea vyombo vyake: Vyungu vya majivu, sepetu, na mabirika, na nyuma na visahani vya kuchukulia moto. Vyombo vyake vyote utavitengeneza kwa shaba. 4Kisha utatengeneza wavu wa shaba wenye pete nne za shaba kwenye pembe zake nne. 5Wavu huo utauweka kwenye ukingo wa madhabahu upande wa chini ili ufike katikati ya madhabahu. 6Utatengeneza pia mipiko ya mjohoro ya kuibebea madhabahu; nayo utaipaka shaba. 7Mipiko hiyo itaingizwa kwenye zile pete kila upande wa madhabahu, wakati wa kuibeba. 8Utaitengeneza madhabahu kwa mbao, na iwe yenye mvungu ndani, kulingana na mfano niliokuonesha mlimani.

Kitalu cha hema la mkutano

(Kut 38:9-20)
9“Utatengeneza ua wa hema la mkutano. Upande wa kusini wa ua kutakuwa na vyandarua vilivyotengenezwa kwa kitani safi iliyosokotwa ambavyo vitakuwa na urefu wa mita 44 kwa upande mmoja. 10Vyandarua hivyo vitashikiliwa na nguzo ishirini za shaba zenye vikalio vya shaba. Lakini kulabu za nguzo hizo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha. 11Hali kadhalika upande wa kaskazini, urefu wa chandarua utakuwa mita 44, na nguzo zake 20 za shaba, lakini kulabu za nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha. 12Upande wa magharibi wa ua utakuwa na chandarua chenye urefu wa mita 22, na nguzo zake 10 na vikalio vyake 10. 13Upande wa mashariki kuliko na mlango, ua utakuwa na upana wa mita 22. 14Chandarua cha upande mmoja wa mlango kitakuwa na upana wa mita 6.5, pamoja na nguzo tatu na vikalio vyake vitatu. 15Vilevile katika upande wa pili wa mlango chandarua kitakuwa mita 6.5, pamoja na nguzo tatu na vikalio vyake vitatu. 16Mlango wenyewe wa ua utakuwa na pazia zito lenye urefu wa mita 9, lililotengenezwa kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kutariziwa vizuri. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne zenye vikalio vinne. 17Nguzo zote kuuzunguka ua zitashikamanishwa kwa fito za fedha, kulabu zake zitakuwa za fedha na vikalio vyake vitakuwa vya shaba. 18Ua huo utakuwa na urefu wa mita 44, upana wa mita 22, na kimo cha mita 2.25. Vyandarua vyake vitakuwa vya kitani safi na vikalio vyake vya shaba. 19Vyombo vyote vya hema takatifu vya matumizi ya kila aina, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua vitakuwa vya shaba.

Taa
(Lawi 24:1-4)

20“Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi kwa ajili ya taa, kuwe na taa inayowaka daima. 21Hiyo itakuwa ndani ya hema la mkutano nje ya pazia hilo mbele ya sanduku la maamuzi27:21 maamuzi: Au agano; Kiebrania: Eduti. na Aroni na wanawe wataitunza mbele yangu tangu jioni mpaka asubuhi. Agizo hili sharti lifuatwe daima na Waisraeli wote, kizazi hata kizazi.
Kutoka27;1-21


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: