Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 2 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 24...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu na kumsifu daima..
Mtakatifu Baba wa Mbinguni..Asante kwa ulinzi wako usiku mzima ,Asante kwa kutuamsha tena,Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali  cha kuendelea kuiona leo hii..
Asante kwa wema wako na fadhili zako Baba wa mbinguni..
Tunakuja mbele zako  tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako mwako Mfalme wa Amani..Tunaomba ukaibariki siku hii iwe njema na yenye Amani,Upendo,Furaha na shukrani..
Ukabariki kazi zetu Baba Biashara,Masomo,Tuingiapo/tutokapo,vyombo vya usafiri,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!Vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakase na ukatutakase Miili yetu na Akili kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Mungu wetu tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe..kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwajua/kutojua..
Baba tunaomba na sisi ukatupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Roho mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda,kutambua/kujitambua na tuwe na kiasi..


Yahweh..!! tunaiweka Nchi hii tunayoishi mikononi mwako na wote tunaoishi humu..Baba wa mbinguni tunaomba utubariki na kutulinda katika yote..Baba wa Mbinguni nyoosha mkono wako wenye nguvu na kutugusa na kutuponya kiroho na ukawe mtala mkuu..Mfalme wa Amani bariki mji huu na ukuu wako ukaonekane..
Mfalme wa Amani tunaiweka Tanzania mikononi mwako ukawe mtawala mkuu na kuibariki na ukawabariki wa Tanzania wote popote walipo..Ukatamalaki na kuwaongoza katika maisha yao..
Tunaiweka mikononimwako Afrika na Dunia yote wewe Mungu ukatuongoze katika yote,ukatawale na kuwaongoza wanaotuongoza wakatuongoze katika haki na kweli..
Mfamle wa Amani ukuwaponye na kuwagusa wote wanaopitia Magumu/majaribu,shida/tabu, waliokatika vifungo mbalimbali Yahweh..!! ukawafungue wapate kupona kimwili na kiroho pia..


Asante kwa yote Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba mbingu na Nchi na vyote vilivyomo,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Jehovah nissi...!!Jehovah Rapha..!!Jehovah Jireh..!! Jehovaha Shammah..!!Jehovah Shalom....!!! Haleluyahhhhh...!!!


Mose akajenga madhabahu na kuiita, “Mwenyezi-Mungu ni Bendera Yangu”, akisema, “Inueni juu bendera ya Mwenyezi-Mungu! Mwenyezi-Mungu atapigana na Waamaleki kizazi hata kizazi!”
Amina..!!

Mungu wetu anatosha,Hakuna hatokuwepo kama yeye..Amini na kumtumainia yeye..atatenda alitenda na anaendelea kutenda..
Mungu aendelee kuwabariki...
Asanteni sana sana mnaopitia hapa Mungu awe nanyi Daima na msipungukiwe katika mahitaji yenu..
Nawapenda..Nawapendaa..!!



Agano linathibitishwa

1Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Njoni kwangu, wewe Aroni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli, mniabudu kwa mbali. 2Wewe Mose peke yako ndiwe utakayenikaribia, lakini wengine wasije karibu, na Waisraeli wasipande mlimani pamoja nawe.”
3Basi, Mose akaenda na kuwaambia watu wote maneno na maagizo yote Mwenyezi-Mungu aliyomwambia. Watu wote wakajibu kwa sauti moja, “Mambo yote aliyoyasema Mwenyezi-Mungu, tutayafanya.” 4Mose akayaandika maagizo yote ambayo Mwenyezi-Mungu alimpa. Kisha akaamka asubuhi na mapema, akajenga madhabahu chini ya mlima na kusimamisha nguzo kumi na mbili kulingana na idadi ya makabila kumi na mbili ya Israeli. 5Kisha akawatuma vijana wa Waisraeli wamtolee Mwenyezi-Mungu sadaka za kuteketezwa na kumchinjia sadaka za amani za ng'ombe. 6Mose akachota nusu ya damu ya wanyama hao na kuiweka katika mabirika, na nusu nyingine akairashia ile madhabahu. 7Kisha akachukua kitabu cha agano la Mwenyezi-Mungu, akakisoma mbele ya watu, nao wakasema, “Hayo yote aliyoyasema Mwenyezi-Mungu, tutayafanya, nasi tutakuwa watiifu.” 8Taz Mat 26:28; Marko 14:24; Luka 22:20; 1Kor 11:25; Ebr 9:19-20; 10:29 Mose akaichukua ile damu na kuwanyunyizia watu, akisema, “Hii ndiyo damu ya agano ambalo Mwenyezi-Mungu amelifanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.”
9Kisha Mose, Aroni, Nadabu na Abihu na wazee sabini wa Israeli wakapanda mlimani, 10wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa na kitu kama sakafu ya mawe ya johari ya rangi ya samawati, kikiwa safi kama mbingu angavu. 11Na Mungu hakuwadhuru hao viongozi wa watu wa Israeli. Walimwona Mungu, wakala na kunywa.
Mose mlimani Sinai

12Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Njoo kwangu juu mlimani, ungoje huko. Mimi nitakupa vibao viwili vya mawe vyenye sheria na amri nilizoandika kwa ajili ya kuwafunza Waisraeli.” 13Basi, Mose akaondoka pamoja na Yoshua, mtumishi wake, akaenda kwenye mlima wa Mungu. 14Mose aliwaambia wale wazee, “Tungojeni hapa mpaka tutakapowarudia. Aroni na Huri wako pamoja nanyi; yeyote aliye na tatizo na awaendee wao.”
15Basi, Mose akaenda mlimani, na wingu likaufunika mlima. 16Utukufu wa Mwenyezi-Mungu ukatua juu ya mlima Sinai na wingu likaufunika mlima kwa muda wa siku sita. Siku ya saba Mungu akamwita Mose kutoka katikati ya lile wingu. 17Utukufu wa Mwenyezi-Mungu ulionekana mbele ya macho ya watu wa Israeli kama moto unaowaka juu ya mlima. 18Taz Kumb 9:9 Mose akaingia ndani ya lile wingu, akapanda mlimani. Alikaa huko kwa muda wa siku arubaini, mchana na usiku.

Kutoka24;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: