Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 1 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 23...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tunamshukuru sana Mungu wetu kwa Neema/Rehema hii ya kutuchagua tena kuendelea kuiona siku/wiki/mwezi huu..si kwa uwezo wetu bali ni kwa mapenzi yake..
Tunaomba Baba wa Mbinguni ukatubariki,Tazama  mwezi/wiki/siku mwingine/nyingine tena Baba tukakuja mbele zako tukishukuru kwa mema yote uliyotutendea na unayoendelea kututendea..Asante kwa pumzi na afya,Asante kwa ridhiki zako ,wema na fadhili zako,Asante kwa yote na tunaanza nawe Baba wa mbinguni kwa kila jambo, maisha yetu yapo mikononi mwako,Tunaomba ukatubariki na kututendea sawasawa na mapenzi yako..Tunaomba utuokoe na mwovu na kazi zake zote..Tunaomba utubariki tuingiapo/tutokapo,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Baba, kazi zetu,Biashara,Masomo,vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona...Baba ukatutakase Akili na Miili yetu pia..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda,kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi...
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mfalme wa Amani kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Tunaomba na sisi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea na tuwe na kiasi ili tusikwazane tena..
Tunawaweka mikononi mwako wote wanaopitia magumu/majaribu..Baba tazama wenye Shida/Tabu, wagonjwa,Wafiwa ukawe mfariji wao,waliokatika vifungo mbalimbali, waliokataliwa,waliokata tamaa,wenye mashaka/hofu,waliomizwa moyoni,Baba wa mbinguni ukawaguse na kuwaponya..
Tazama Yatima na wajane,wanaotafuta watoto Mfalme wa Amani,wanaotafuta wenza mke/mume ukawapatie walio wao na kuwabariki katika mahitaji yao..
Baba tunaomba ukabariki Ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo ukazifanye baraka na kuweza kusaidia wengine..
Yesu Anakataliwa na Wayahudi...!!
Huko Yerusalemu kulikuwa na sikukuu ya kutabaruku. Wakati huo ulikuwa wa baridi. Naye Yesu akawa anatembea hekaluni katika ukumbi wa Solomoni. Basi, Wayahudi wakamzunguka, wakamwuliza, “Utatuacha katika mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiwe Kristo, basi, tuambie wazi.” Yesu akawajibu, “Nimewaambieni, lakini hamsadiki. Kazi ninazozifanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia. Lakini nyinyi hamsadiki kwa sababu nyinyi si kondoo wangu. Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata. Mimi nawapa uhai wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu. Baba yangu ambaye ndiye aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote, wala hakuna awezaye kuwatoa mikononi mwake Baba. Mimi na Baba, tu mmoja.” Basi, Wayahudi wakachukua mawe ili wamtupie. Yesu akawaambia, “Nimewaonesheni kazi nyingi kutoka kwa Baba. Ni ipi kati ya hizo inayowafanya mnipige mawe?” Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa ajili ya kazi njema, ila kwa sababu ya kumkufuru Mungu! Maana wajifanya kuwa Mungu hali wewe ni binadamu tu.” Yesu akawajibu, “Je, haikuandikwa katika sheria yenu: ‘Mimi nimesema, nyinyi ni miungu?’ Mungu aliwaita miungu wale waliopewa ujumbe wake; nasi twajua kwamba Maandiko Matakatifu yasema ukweli daima. Je, yeye ambaye Baba alimweka wakfu na kumtuma ulimwenguni, mnamwambia: ‘Unakufuru,’ eti kwa sababu nilisema: ‘Mimi ni Mwana wa Mungu?’ Kama sifanyi kazi za Baba yangu, msiniamini. Lakini ikiwa ninazifanya, hata kama hamniamini, walau ziaminini hizo kazi, mpate kujua na kutambua kwamba Baba yuko ndani yangu, nami niko ndani yake.” Wakajaribu tena kumkamata lakini akachopoka mikononi mwao. Yesu akaenda tena ngambo ya mto Yordani, mahali Yohane alipokuwa akibatiza, akakaa huko. Watu wengi walimwendea wakasema, “Yohane hakufanya ishara yoyote. Lakini yale yote Yohane aliyosema juu ya mtu huyu ni kweli kabisa.” Watu wengi mahali hapo wakamwamini.
Mwamini Mungu ndugu yangu..katika shida zako mwite yeye,katika Raha,Furaha mshukuru yeye...Yeye asiye lala wala kusinzia hatokuacha daima, binadamu hubadirika lakini Mungu yeye habadiriki kamwe ukimtumainia yeye na kufuata njia zake kamwe hutojuta....
Sifa na utukufu ni wako Mungu wetu, tunayaweka yote mikononi mwako,tukishukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu..
Amina..!!
Asanteni sana kwa wote mliopita hapa Mungu Baba muweza wa yote aendelee kuonekana katika mahitaji yenu na aendelee kuwabariki..
Nawapenda.

Haki na usawa

1“Usitoe habari za uongo. Usishirikiane na mtu mwovu ili kuwa shahidi mbaya. 2Usifuate genge la watu kutenda uovu, wala usijumuike na genge la watu kutoa ushahidi mahakamani ili kupotosha haki. 3Taz Lawi 19:15 Usiwe na upendeleo katika kesi ya maskini.
4“Ukimkuta ng'ombe au punda wa adui yako amepotea, utamrudishia mwenyewe. 5Ukimwona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, msaidie mtu huyo kumsimamisha punda wake, wala usimwache na kwenda zako.
6“Usiipotoshe haki anayostahili maskini katika kesi yake. 7Jitenge mbali na mashtaka ya uongo wala usiwaue wasio na hatia na waadilifu, maana mimi sitamsamehe mtu mwovu. 8Usipokee rushwa, maana rushwa huwapofusha wakuu na kupotosha mambo ya wenye haki.
9“Usimdhulumu mgeni; nyinyi mwajua hali ya kuwa mgeni, maana mlikuwa wageni nchini Misri.

Mwaka wa saba

10“Kwa muda wa miaka sita utapanda mashamba yako na kuvuna mazao yake. 11Lakini mnamo mwaka wa saba, utayaacha mashamba yako bila kupanda mbegu, ili maskini miongoni mwa watu wako wapate chakula kilichosalia humo, na wanyama wa porini wale. Utafanya vivyo hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
12“Kwa siku sita utafanya kazi zako, lakini siku ya saba utapumzika, ili ng'ombe wako na punda wako pia wapate kupumzika; na watumwa wako na watumishi wa kigeni wapate kustarehe. 13Yazingatie yote niliyokuambia. Usiyataje hata kidogo majina ya miungu mingine; hayo yasisikike kinywani mwako.
Sikukuu tatu kubwa

(Kut 34:18-26; Kumb 16:1-17)

14“Mara tatu kila mwaka mtafanya sikukuu kwa heshima yangu. 15Taz Kut 12:14-20; Lawi 23:6-8; Hes 28:17-25 Mtaadhimisha sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu: Kama nilivyowaagiza, mtakula mikate isiyotiwa chachu kwa siku saba wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kwa sababu katika mwezi huo mlitoka Misri. Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu. 16Taz Lawi 23:15-21, 39-43; Hes 28:26-31 Mtaadhimisha sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mtaadhimisha sikukuu ya kukusanya mavuno23:16 sikukuu ya kukusanya mavuno: Au sikukuu ya vibanda. mwishoni mwa mwaka mnapokusanya mazao ya kazi zenu. 17Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakusanyika mbele zangu mimi Bwana Mwenyezi-Mungu.
18“Usinitolee damu ya tambiko yangu pamoja na mkate uliotiwa chachu, wala usiyaache mafuta ya sikukuu yangu yabaki mpaka asubuhi.
19 Taz Kut 34:26; Kumb 14:21; 26:2 “Mazao ya kwanza ya ardhi yako utayaleta nyumbani kwangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.
“Usimchemshe mwanakondoo au mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.23:19 desturi hiyo ilifanyika katika mila za kidini za Wakanaani.

Ahadi na maagizo

20“Tazameni, mimi namtuma malaika awatangulie safarini ili awalinde na kuwafikisha katika nchi niliyowatayarishia. 21Msikilizeni na kutii atakachosema, wala msimwasi, kwani hatawasamehe uasi wenu maana nimemtuma kwa jina langu. 22Lakini mkimsikiliza kwa makini na kufanya yote asemayo, mimi nitakuwa adui wa adui zenu na mpinzani wa wapinzani wenu. 23Malaika wangu atakapowaongoza na kuwafikisha katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi na Wayebusi, nami nikawaangamiza hao wote, 24msiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala msiige mambo yao. Bali mtawaangamiza kabisa na kuzivunjavunja nguzo zao. 25Mtanitumikia mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, nami nitawabariki kwa chakula na maji na kuyaondoa magonjwa kati yenu. 26Hakutakuwa na mwanamke yeyote atakayepoteza mimba wala kuwa tasa katika nchi yenu. Nami nitawajalia maisha marefu.
27“Nitapeleka kitisho mbele yenu na kuwavuruga watu wote mtakaowakabili, na adui zenu nitawafanya wageuke na kuwakimbia. 28Nitapeleka manyigu mbele yenu ambao watawafukuza Wahivi, Wakanaani na Wahiti. 29Sitawaondoa watu hao katika mwaka mmoja, nchi isije ikabaki tupu na wanyama wa porini wakaongezeka mno na kuwazidi nguvu. 30Lakini nitawaondoa kidogokidogo mpaka hapo mtakapoongezeka na kuimiliki nchi hiyo. 31Mipaka ya nchi yenu itakuwa kutoka bahari ya Shamu hadi bahari ya Mediteranea, na kutoka jangwani mpaka mto Eufrate, maana nitawatia wakazi wa nchi hiyo mikononi mwenu, nanyi mtawafukuza wawaondoke. 32Msifanye agano lolote nao, wala na miungu yao. 33Msiwaruhusu waishi nchini mwenu wasije wakawafanya mtende dhambi dhidi yangu; maana kama mkiitumikia miungu yao, hakika hiyo itakuwa mtego wa kuwanasa.”

Kutoka23;1-33

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: