Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 13 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 11...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa Matendo yake makuu kwetu..
Yeye anatujua kuliko tunavyojijua,Yeye ni Mungu wetu na Kimbilio letu,Yeye aliyetupa Kibali cha kuendelea kuiona Leo hii..Yeye ni Muumba wetu na Muumba wa Mbingu na Nchi..Yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,Yeye ni Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Yeye ni Alfa na Omega..Yeye ni Mlinzi mkuu na Mtawala,Amani,Furaha,Upendo na Fadhili zipo kwake..Yeye akisema ndiyo hakuna wakusema siyo..Yeye atosha Maishani kwetu.ukimuita aitika,ukimuomba anakupa,ukifuata njia zake na kumuabudu yeye hutojuta..



Mungu si mtu, aseme uongo, wala si binadamu, abadili nia yake! Je, ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?[Hesabu 23:19]
Asante Baba wa mbinguni kwa Neema/Rehema yako uliyotupa..Tazama Jana imepita Baba Leo ni Siku mpya na Kesho ni siku nyingine..
Jehovah..!! tunaomba uibariki siku hii ikawe njema , yenye Amani na kukupendeza wewe..Ukabariki kuingia kwetu na kutoka kwetu,Vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Baba..
Tunaomba ukabariki Vilaji/Vinywaji, Kazi zetu,Biashara,Masomo na Vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakasase kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..

Baba tunakwenda kinyume na adui mwovu na kazi zake zote..Tunaomba ukatuokoe,kutulinda na kutufunika na Damu ya Mwokozi wetu Bwana Yesu Kristo..
Baba tukuja mbele zako na kujinyeyekeza tunaomba utusamehe pale tulikwenda kinyume nawe..kwakuwaza,kwakunena,kwakujua/kutojua..Mfalme wa Amani tunaomba utupe nasi Neema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Roho mtakatifu akatuongoze vyema katika yote..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Jehovaha..!!!Ukawaguse na kuwaokoa wote wanaopitia magumu/mapito,shida/tabu,Wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliokata tamaa,waliokataliwa na wakapate tumaini lako..
ukawaponye kimwili na kiroho pia..

Tunayaweka haya mikononi mwako Yahweh..Sifa na Utukufu ni wako Daima.
Tunashukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu leo na hata milele.


11Maandiko Matakatifu yasema: “Kila anayemwamini hataaibishwa.[Waroma10;11]
Amina..!!
Muwe na wakati mwema..nawapenda.


Tangazo la kuuawa wazaliwa wa kwanza wa Wamisri

1Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Bado kuna pigo moja nitakalomletea Farao na nchi ya Misri. Baadaye atawaacheni mwondoke hapa. Tena atakapowaacheni mwondoke, yeye mwenyewe atawafukuza mwondoke kabisa. 2Waambie Waisraeli sasa wasikie vizuri kwamba kila mmoja wao, mwanamume kwa mwanamke, ni lazima amwombe jirani yake vito vya fedha na dhahabu.” 3Mwenyezi-Mungu akawafanya Waisraeli wapendeke mbele ya Wamisri. Tena, Mose mwenyewe akawa mtu mashuhuri sana nchini Misri, na mbele ya maofisa wa Farao na watu wote.
4Mose akamwambia Farao, “Mwenyezi-Mungu asema hivi: ‘Panapo usiku wa manane leo, nitapitia katikati ya nchi ya Misri. 5Nitakapopita, kila mzaliwa wa kwanza nchini Misri atakufa: Kuanzia mzaliwa wa kwanza wako wewe Farao ambaye ni mrithi wako, hadi mzaliwa wa kwanza wa mjakazi anayesaga nafaka kwa jiwe. Hata wazaliwa wa kwanza wa mifugo nao wote watakufa. 6Kutakuwa na kilio kikubwa kote nchini Misri, kilio ambacho hakijapata kutokea, wala hakitatokea tena. 7Lakini miongoni mwa Waisraeli hakuna mtu, mnyama au mbwa wao atakayepatwa na madhara yoyote, ili upate kutambua kwamba mimi Mwenyezi-Mungu hutofautisha kati ya Waisraeli na Wamisri.’” 8Mose akamalizia kwa kumwambia Farao, “Watumishi wako hawa watanijia na kuinama mbele yangu kwa heshima, wakinisihi niondoke nchini Misri, mimi pamoja na watu wote wanaonifuata. Baada ya hayo, nitaondoka.” Kisha Mose, huku akiwa ameghadhabika, akaondoka kwa Farao.
9Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Farao hatakusikiliza, ili maajabu yangu yapate kuongezeka nchini Misri.” 10Basi, Mose na Aroni walifanya maajabu hayo yote mbele ya Farao. Lakini Mwenyezi-Mungu alimfanya Farao kuwa mkaidi, akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke nchini mwake.

Kutoka11;1-10

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: