Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 17 January 2017

Saalam za Mwaka Mpya Wapendwa/Waungwana...Muwe na wiki Njema yenye Baraka..(Hata mimi nasema yu mwema Mungu)Burudani Atosha Kisaava..!!!


Habari za siku Wapendwa/Waungwana,Heri ya Mwaka Mpya.!!!
natumaini wote mmeupokea vyema na Mungu aendelee kututendea sawa sawa na mapenzi yake.
Yeye yu Mwema sana, Ije mvua lije Jua atabaki kuwa Mungu..
Ukikosa,Ukipata endelea kumuomba Na Kumtukuza yeye tuu maana yeye Atosha.
Tupo pamoja Wapendwa /Waungwana..ni mambo yanaingiliana tuu,kikubwa uzima...

AHADI YA MUNGU NI YA KWELI



              Neno La Leo;Waebrani 6:13-20

Ahadi ya Mungu ni ya kweli
13Mungu alipompa Abrahamu ahadi, aliapa kwa jina lake mwenyewe, maana hakuna aliye mkuu kuliko Mungu ambaye kwa huyo angeweza kuapa. 14Mungu alisema: “Hakika nitakubariki na nitakupa wazawa wengi.” 15Abrahamu alisubiri kwa uvumilivu na hivyo akapokea kile alichoahidiwa na Mungu. 16Watu wanapoapa, huapa kwa mmoja aliye mkuu kuliko wao, na kiapo husuluhisha ubishi wote. 17Naye Mungu aliimarisha ahadi yake kwa kiapo; na kwa namna hiyo akawaonesha wazi wale aliowaahidia kwamba hatabadili nia yake. 18Basi, kuna vitu hivi viwili: Ahadi na kiapo, ambavyo haviwezi kubadilika na wala juu ya hivyo Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hiyo sisi tuliokimbilia usalama kwake, tunapewa moyo wa kushikilia imara tumaini lililowekwa mbele yetu.19Tunalo tumaini hilo kama nanga ya maisha yetu. Tumaini hilo lapenya mpaka mahali patakatifu mbinguni. 20 Yesu mwenyewe ametangulia kuingia humo kwa ajili yetu na amekuwa kuhani mkuu milele, kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.



"Swahili Na Waswahili"Mungu yumwema, Mbarikiwe.

No comments: