Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 23 November 2015

MISA TAKATIFU YA KUMBUKUMBU YA NYAMITI LUSINDE BALTIMORE, MARYLAND




 Picha ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde ikiwa kanisani
siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 siku ilikofanyika misa takatifu ya
kumbukumbu na kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe.
Wilson Masilingi akiwa ameongozana na mkewe pamoja na mwanae. Nyamiti
alikua mfanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani alipatwa na
mauti alipokua likizo Tanzania katika hospitali ya Kariuki alipokua
amekwenda kwa matibabu baada ya kuugua ghafla alipokua huko na baadae
kuaga Dunia Novemba 17, 2015. Picha na Vijimambo/Kwanza
Production




Father Honest Munishi akiongoza misa takatifu ya kumbukumbu ya
mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 na
kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson
Masilingi akiwa ameongozana na mkewe pamoja na mwanae. 


Father Lehandry Kimario akisaidiana na Father Honest Munishi katika
kuongoza misa takatifu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde
iliyofanyika siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 Baltimore, Maryland
nchini Marekani.
Mhe. Balozi Wilson Masilingi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
nchini Marekani akiwa na mkewe Marystella Masilingi wakifuatilia misa
takatifu ya kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde
iliyofanyika siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 Baltimore, Maryland
nchini Marekani.
Balozi Mhe. Wilson Masilingi akiongea machache jinsi alivyomjua
Nyamiti na kutoa shukurani zake kwa watu mbalimbali ikiwemo kamati
iliyowezesha kufanikisha misa hiyo na shukurani za pekee kwa Father
Honest Munishi na Father Lehandry Kimario.
Kulia ni Sima Kazaura akisoma soma la kwanza huku akiwa
amesindikizwa na Dorothy.
Kulia ni Farida Sarita akisoma soma la pili huku akiwa
amesindikizwa na Dorothy.
 Mshereheshaji Tuma akiongea jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu
Nyamiti.
 Kulia ni Rosemary Commodores akisoma wasifu wa marehemu.
 Kulia ni Afisa Ubalozi Suleiman Saleh akitoa salamu za
Ubalozi, kushoto ni mkewe.
 Dorothy akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu Nyamiti.
 Sima Kazaura akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu
Nyamiti
 Patrick Kajale akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu
Nyamiti
Eddah Gachuma akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu Nyamiti
Dj Luke akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu Nyamiti
Joyce akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu Nyamiti
Pius Mtalemwa kiongozi wa kanisa la ibada ya Kiswahili DMV
akihitimisha kwa kutoa shukurani kwa wote.


Nelson Masilingi, mtoto wa Mhe. Balozi akifuatilia misa takatifu ya
kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde.


Mwambata wa Jeshi Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Canada
Col. Adolph Mutta akiwa na mkewe wakifuatilia misa takatifu ya
kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde.


Watu mbalimbali waliohudhuria misa.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

No comments: