Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 29 July 2015

Mazungumzo na mtangazaji Rose Chitallah kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU


Mubelwa Bandio na Rose Chitallah studioni
Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015

Katika kipindi hiki utasikia mahojiano yetu na watu mbalimbali kuhusu DEMOKRASIA kuelekea uchaguzi nchini Tanzania

Katika kipindi cha wiki hii tumebahatika kuungana na mtangazaji Rose Chitallah

Karibu

Mahojiano na Balozi Amina Salum Ali kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU


Mhe. Balozi Amina Salum Ali akifafanua jambo ndani ya Kilimanjaro Studio
Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015

Katika kipindi hiki utasikia mahojiano yetu na watu mbalimbali kuhusu DEMOKRASIA kuelekea uchaguzi nchini Tanzania

Katika kipindi cha wiki hii tumebahatika kuungana na Balozi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika nchini Marekani Mhe. Amina Salum Ali

Karibu

Sunday 26 July 2015

Mahojiano na Charles Magali ndani ya Washington DMV


Charles Magali akiwa ndani ya Kilimanjaro Studio zinazomilikiwa na Vijimambo Radio, Kwanza Production na NesiWangu Media
Ijumaa ya Julai 24, 2015, mwigizaji na mwimbaji wa muziki nchini
Tanzania Charles Magali alipata fursa ya kutembelea studio zetu zilizopo
Beltsville Maryland. Hapo akazungumza nasi kwa ufupi

Karibu umsikilize akihojiwa na Mbunifu na Mtayarishaji wa kipindi hiki Dj Luke Joe na Mubelwa Bandio

Wednesday 15 July 2015

Siku kama ya Leo da'Sandra-Neema Alizaliwa....!!!


Siku miezi miaka sasa.. Ni Furaha isiyo na kikomo kwetu kwa zawadi hii kubwa Mungu aliyotupatia
Mtoto kwa wazazi hakui atabaki kuwa mtoto tuu mpaka mwisho...

Hongera Sana da'Sandra-Neema(Dide)kwa kuongezeka mwaka mwingine..
Mungu azidi kukubariki,kukutendea,Kukulinda,Kukuongoza.
Akupe miaka Mingi ufanikishe ndoto Zako na Kazi aliyokutuma hapa Duniani...
Uendelee kuwa Baraka,Faraja kwetu kama wazazi na kwa Ndugu,Jamaa,Marafiki na Jamii pia.

Tunamshukuru Sana Mungu katika yote aliyokutendea na Anayoendelea kukutendea.
Mkono wake tumeuona/tunaendelea kuuona juu yako.
Tumejifunza mengi mno na tunaendelea kujifunza.

Shukrani kwa wazazi wetu kwa muongozo na mengine mengi..
Shukrani kwa ndugu/jamaa na Marafiki wote kwa kushirikiana nasi katika Maombi,Sala/Dua na malezi kwa ujumla..
Tunaamini mtoto halelewi na wazazi tuu..
Mungu azidi kuwabariki na kuwaongezea zaidi ya mnavyojitoa kwetu.

Mungu yu mwema sana..
Tunawapenda wote...
Happy birthday binti yetu Mpendwa Sandra-Neema(Didee)
Isaac family.


Kipindi cha Niambie Live



Karibu kwenye kipindi hiki cha NIAMBIE LIVE

Kipindi kinachozungumzia mambo mbalimbali yaliyochukua nafasi za juu kwenye mitandao ya kijamii.

Na mgeni mwalikwa ni Henry Kente

Ni Niambie Live....

KARIBU



Tuesday 14 July 2015

Kipindi cha JUKWAA LANGU, Julai 13, 2015


Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015
Katika kipindi hiki utasikia mahojiano yetu na watu mbalimbali akiwemo Katibu Uenezi na Itikadi wa CCM Ndg. Nape Nnauye kuhusu DEMOKRASIA kuelekea uchaguzi nchini Tanzania
KARIBU


Monday 13 July 2015

BALOZI LIBERATA MULAMULA AWAAGA TAMCO RASMI, ASEMA UMOJA NA MSHIKAMANO WAO NI MFANO WA KUIGWA NA JUMUIYA ZINGINE



Na Mwandishi wetu, Washington, DC
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na
aliyekua Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberata Mulamula
 siku ya Jumapili July 12, 2014 alijumuika na wanajumuiya ya
Kiislam ya DMV (TAMCO) katika futari ya pamoja iliyoandaliwa na
jumuiya hiyo na kutumia fulsa hiyo kuwaaga rasmi.



Katika hotuba yake. Mhe. Liberata Mulamula  aliwakuwakumbusha
alipokuja kwa mara ya kwanza kulitumikia Taifa kama Balozi wa Tanzania
nchini Marekani , Jumuiya hiyo ndio iliyomkaribisha kwa mara ya kwanza
hapa DMV na leo nimerudi tena kuagana nanyi rasmi. Mhe. Liberata
Mulamula aliwashukuru TAMCO kwa ushirikiano na mshikamano wao na
kuzitaka Jumuiya zingine za Watanzania ziige mfano wao kwani TAMCO ni
jumiya ya Kiislam iliyoimara, isiyotetereka na yenye uongozi makini.
Mhe. Balozi Liberata Mulamula aliushukuru uongozi wa TAMCO kwa
kumkaribisha aje azungumze na Watanzania wanajumuiya ya TAMCO na
kutumia fulsa hiyo kuwaaga rasmi.


Uongozi wa TAMCO ulimuzawadia Mhe. Balozi Liberata Mulamula zawadi na
yeye kutoa mchango wake wa mwaka kwa jumuiya hiyo inayo wakubali
Watanzania wote bila kubagua rangi, kabila wala dini.





 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kiislam ya Watanzania DMV
(TAMCO)Ustadh Ally Mohamed akimlaki Mhe. Katibu Mkuu Wizara ya Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulaula mara tu
alipowasili kwenye ukumbi wa park iliyopo Silver Spring, Maryland
nchini Marekani alipokuja yeye Mhe. Balozi akiambatana na mumewe Eng.
George Mulamula (hayupo pichani) na mwanae Alvin Mulamula (kulia)
kujumuika na wanajumuiya hao katika futari ya pamoja na kutumia futari
hiyo kuwaaga rasmi. Picha zote na Kwanza Production na Vijimambo
Blog.





 Mtunza fedha msaidizi wa TAMCO. Bi. Asha Hariz(kushotao)
akiongozana na Mhe. Liberata Mulamula kuelekea ukumbini siku ya
Jumapili July 12, 2015 siku Mhe. Balozi alipopata mwaliko wa Jumuiya
hiyo wa kufuturu pamoja na kuwaaga rasmi.


Mwenyekiti wa TAMCO ustadh Ally Mohamed akiongea machache na baadae
kumkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa Mhe. Balozi Liberata Mulamula kuongea na
wanajumuiya.





Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiongea na Wanajumuiya wa TAMCO na
kuwaaga rasmi.




Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Mhe. Balozi Liberata Mulamula akikabidhi mchango wake wa TAMCO wa
mwaka kwa mtunza fedha msaidizi ustadh Shamis Abdullah.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokea zawadi kutoka kwa mtunza fedha
msaidizi wa TAMCO bi. Asha Hariz.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokea zawadi kutoka kwa mtunza fedha
msaidizi wa TAMCO bi. Asha Hariz.



Picha ya pamoja

Sunday 12 July 2015

[AUDIOS] Hotuba mbalimbali kwenye mkutano mkuu wa CCM


Hotuba Ya Dr Ali Mohamed Shein kukubali kuwa mgombea wa CCM Zanzibar 2015



Hotuba Ya Dr Asha - Rose Migiro kukubali yatokeo ya mkutano Mkuu wa CCM 2015



Hotuba Ya Balozi Amina Salum Ali kukubali matokeo ya mkutano mkuu wa CCM 2015



Hotuba Ya Dr John Pombe Magufuli kukubali kuwa mgombea wa CCM 2015



Hotuba Ya Mwenyekiti Wa CCM Taifa Mhe. Jakaya Kikwete kufunga mkutano mkuu wa chama 2015