Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 18 January 2015

Muendelee vyema na Jumapili hii;Msipungukiwe na Amani, Upendo;Burudani-MAAGANO,EE BWANA NIMESKIA,MSALABA NITAULINDA,KIU YANGU BWANA BY AIC MAMAJUSI CHOIR


Wapendwa muendelee na juma pili hii vyema,Baraka,Amani,Upendo,Busara na Hekima vitawale..
Mungu azidi kutuongoza katika kunena,kutenda na katika yote..............


22Wanajidai kuwa wenye hekima, kumbe ni wapumbavu. 23Wanaacha kumwabudu Mungu aishiye milele, na badala yake, wanaabudu sanamu zilizo mfano wa binadamu ambaye hufa, mfano wa wanyama, ndege, au wanyama watambaao.








Neno La Leo;Warumi:1:18-32
Kosa la binadamu
 24Kwa sababu hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya za mioyo yao na kufanyiana mambo ya aibu kwa miili yao. 25Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina. 26Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile. 27Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke, wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu. 28Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya. 29Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya, 30na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao; 31hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine. 32Wanajua kwamba sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.

Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe sana.

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Amani itawale ndani nyumba yenu.

Rachel Siwa said...

Ameeeen..!!!!
da'Yasinta asante.