Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 25 January 2015

Msimu wa pili wa Darasa la Kiswahili waanza rasmi DMV


Sehemu ya wanafunzi, wazazi, mwalimu na viongozi wa jumuiya waliohudhuria siku ya kwanza ya darasa la Kiswahili DMV
Awamu ya pili ya Darasa la Kiswahili kwa watoto waishio Washington DC na vitongoji vyake umeanza Jumamosi ya Januari 24, 2015.
Rais wa Jumuiya Bw Iddi Sandaly alipata fursa ya kuzungumza nasi kwa ufupi kuhusu darasa hilo.

Karibu umsikilize



Sehemu ya wanafunzi wakimsikiliza Mwalimu Asha Nyang'anyi. Kushoto kwake ni Katibu wa Jumuiya ya waTanzania hapa DMV Said Mwamende
Baadhi ya wazazi wakiwa nje ya darasa wakati watoto wakiendelea na mafunzo
Baadhi ya wazazi waliokuwa ndani ya darasa wakati watoto wakiendelea na mafunzo

Friday 23 January 2015

Mahojiano na JhikoMan kuhusu wimbo wake mpya...Africa Arise


Karibu katika mahojiano kati ya Mubelwa Bandio na Jhiko Manyika a.k.a JhikoMan aliyejiunga nasi moja kwa moja kutoka Bagamoyo Tanzania

Alizungumzia wimbo wake mpya wa Africa Arise, ambao amemshirikisha Peter Morgan wa kundi la Morgan Heritage.

Amezungumza mengi kuuhusu

Karibu usikilize hapa chini



Pia unaweza kurejea mahojiano kati yao wakati JhikoMan akiwa ziarani Ulaya mwaka 2014. Alizungumza mengi kuhusu muziki wa reggae Tanzania lakini pia aligusia "projects" mbalimbali ambazo ziko njiani kuja

Monday 19 January 2015

Huyu na Yule...........Mahojiano na Dr na Mama Williams


Karibu kwenye mahojiano ya Dr na Mama Williams.

Waasisi wa AHEAD Inc. Taasisi ambayo iliasisiwa mwaka 1985 na inajishughulisha kubadili maisha ya wengi nchini Tanzania kupitia Elimu, Stadi za Maisha, Afya ya Mama na Mtoto na pia kuzisaidia jamii mbalimbali..

Wamezungumzia mengi kuhusu namna walivyofika Tanzania kwa mara ya kwanza 1974. Kilichowapeleka, walivyoamua kubaki huko mpaka sasa, shughuli za Taasisi yao na mengine mengi

Karibu

Huyu na Yule ni kipindi kinachotayarishwa na Vijimambo Blog na kuzalishwa na Kwanza Production

Kwa mawasiliano, maoni ama ushauri, tafadhali wasiliana nasi kupitia kwanzaproduction at gmail.com



Sunday 18 January 2015

Muendelee vyema na Jumapili hii;Msipungukiwe na Amani, Upendo;Burudani-MAAGANO,EE BWANA NIMESKIA,MSALABA NITAULINDA,KIU YANGU BWANA BY AIC MAMAJUSI CHOIR


Wapendwa muendelee na juma pili hii vyema,Baraka,Amani,Upendo,Busara na Hekima vitawale..
Mungu azidi kutuongoza katika kunena,kutenda na katika yote..............


22Wanajidai kuwa wenye hekima, kumbe ni wapumbavu. 23Wanaacha kumwabudu Mungu aishiye milele, na badala yake, wanaabudu sanamu zilizo mfano wa binadamu ambaye hufa, mfano wa wanyama, ndege, au wanyama watambaao.








Neno La Leo;Warumi:1:18-32
Kosa la binadamu
 24Kwa sababu hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya za mioyo yao na kufanyiana mambo ya aibu kwa miili yao. 25Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina. 26Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile. 27Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke, wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu. 28Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya. 29Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya, 30na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao; 31hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine. 32Wanajua kwamba sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.

Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe sana.

Saturday 17 January 2015

Jikoni Leo;Bi Manjula[Manjula's Kitchen]-Moong Dal Vadas ( Bhajia, Pakoras, Lentil Fritters),Vegetable Rice Cutlets - Indian Appetizer, Recipe by Manjula




Ingredients
1 cup split wash moong dal (available in Indian grocery stores)
1 cup potatoes boiled peeled and shredded
Approx. 2 tablespoon finely chopped cilantro (hara dhania)
1 green chili minced adjust to taste
1 tablespoon finely grated ginger
1 teaspoon cumin seeds (jeera)
1/8 teaspoon asafetida (hing)
1/8 teaspoon of baking soda
1 teaspoon salt adjust to taste
Oil to fry



Ingredients
2 cups cooked rice
1 small potato peeled and cut in small pieces
1 cup mixed vegetables cut into very small pieces (green beans, bell pepper and carrot)
2 teaspoon ginger chopped
1/2 teaspoon red chili powder, adjust to taste
1-1/2 teaspoons salt
1 teaspoon cumin seeds
1 tablespoon corn starch
Oil to fry

View full recipe at: http://www.manjulaskitchen.com

Manjula's Kitchen

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Wednesday 14 January 2015

Hongera sana kaka Isaac kwa siku kuu hii yako...Happy Birthday..!!!!!



Siku Kama ya Leo kaka Isaac Isaac alizaliwa..
Hongera sana kaka Isaac kwa siku kuu hii kwako..
Nasi tunaungana pamoja nawe katika siku hii...
Mungu azidi kukulinda,Kukutendea,kukuonyesha njia,kukuepusha na majaribu yote,
Akujaalie miaka mingi yenye Baraka,Amani,Upendo,Furaha,Ushindi, Afya njema na Ufanikishe Ndoto zako.
Usipungukiwe na kicheko,Shuhuda,Shukrani,
Mafanikio yako yawe chachu na msaada kwa wenye kuhitaji.
Uendelee kuwa baraka kwetu na jamii pia.
Mungu ni mwema sana na tunajivunia kuwa nawe siku zote.
Tunakupenda sana na Mungu awe nawe Daima.
Wako;Rachel siwa,Sandra-Neema,Tracey-Sarah.




"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Monday 12 January 2015

HUYU NA YULE........Mahojiano na Dr Talib Ali


Karibu katika kipindi cha HUYU NA YULE ambapo wiki hii tumeongea na Dk Talib Ali

Yeye ni mwanzilishi wa Avatar Dental Care iliyopo Leesburg Virginia.

Ameeleza mengi kuhusu kazi zake na mikakati aliyonayo baadae
Pia, ametoa punguzo la 50% kwa waTanzania watakaoenda kutiiwa kwake, pamoja na mpango wa malipo ya awamu kuwzesha watu kumudu gharama hizo

Karibu
Huyu na Yule ni kipindi kinachotayarishwa na Vijimambo Blog na kuzalishwa na Kwanza Production

Kwa mawasiliano, maoni ama ushauri, tafadhali wasiliana nasi kupitia kwanzaproduction at gmail.com
.

Friday 9 January 2015

Monday 5 January 2015

HUYU NA YULE.......Mahojiano na Dr Crispin Semakula

Karibu katika kipindi cha HUYU NA YULE ambapo wiki hii tumeongea na Dr Crispin Semakla.

Daktari wa mahgonjwa ya kisukari, shinikizo la damu na pia Mwalimu wa Afya katika Chuo Kikuu nchini Marekani

Pia ni mwanzilishi wa Access Medical and Dialysis Center iliyopo Dar Es Salaam

Ameeleza mengi kuhusu maradhi anayoshughulika nayo na pia kituo chake.


Huyu na Yule ni kipindi kinachotayarishwa na Vijimambo Blog na kuzalishwa na Kwanza Production

Kwa mawasiliano, maoni ama ushauri, tafadhali wasiliana nasi kupitia kwanzaproduction at gmail.com

Sunday 4 January 2015

Heri Ya Mwaka Mpya Na Muwe na Jumapili Njema;Burudani-10,000 Reasons (Bless the Lord) - Matt Redman,COVERED | Official Planetshakers Video

Wapendwa/Waungwana;Nimatumaini yangu mmevuka salama mwaka 2014 na mmeanza vyema mwaka huu mpya wa 2015.
Nawatakia kila lililo Jema,Furaha,Amani,Upendo,Mafanikio,Ushindi.
Wanaotafuta wenza Mungu akawaonyeshe walio wao,Wanaohitaji Watoto Mungu akawabariki,Uwe mwaka wa Shuhuda na Mkono wa Mungu ukawaguse wenye Shida/Tabu.
Mungu akaonekane kwa kila muhitaji.
Tuwe na Upendo wa kweli,Tusameheane,Tuchukuliane,Tusibebe mizigo isiyo ya lazima.
Tusahau yaliyopita na Tuanze upya.
Mungu ni Mwema sana.
Nawapenda wote.



1Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia. 2Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho ya Mungu ilikuwa ikitanda juu ya maji.
3Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa.4Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza, 5mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza.
Neno La Leo;Mwanzo1:1-31
26Kisha Mungu akasema, “Tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; atawale samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vitambaavyo.” 27 Basi, Mungu akaumba mtu kwa mfano wake; naam, kwa mfano wake Mungu alimuumba. Aliwaumba mwanamume na mwanamke. 28Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.”
Bible Society of Tanzania

You have removed my shame,
You take as I am
You call me justified,
Now I am covered by Your grace







"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Friday 2 January 2015

Maelezo ya Mwanasheria wa Uhamiaji kuhusu sheria mpya za uhamiaji nchini Marekani


Mwanasheria wa uhamiaji Fatmata Barrie akizungumza na wanaDMV kwenye mkesha wa mwaka mpya
Katika mkesha wa mwaka mpya (2014-2015), Jumuiya ya waTanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia , kulikuwa na matukio mbalimbali.

Moja wapo lilikuwa ni maelezo ya mwanasheria wa uhamiaji Fatmata Barrie kuhusu maamuzi mapya ya serikali ya Marekani kwenye sheria za uhamiaji.

Karibu umsikilize