Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 24 August 2014

Tumalizie JumaPili hii Kwa Amani na Baraka;Burudani-Angalia baba,Pamoja na Wewe-Elisha Muliri!!!!!!!

Natumaini Jumjapili hii ilikuwa Njema,Mungu azidi Kuwabariki,Kuwa na Imani,Kusifu,Kuabudu,Kushukuru na Kutukuza...
Akaanza kufundisha tena kando ya bahari.Wakamkusanyikia mkutano mkubwa mno,hata yeye akapanda chomboni, akakaa baharini,mkutano wote ulikuwako juu ya nchi kavu kando ya bahari.2;Akawafundisha mambo mengi kwa mifano,akawaambia katika mafundisho yake.
Neno La Leo;Marko Mtakatifu4:1-40
3;Sikilizeni;Tazama mpanzi alitoka kwenda kupanda;4;Ikawa alipokuwa akipanda, Mbegu nyingine  ilianguka kando ya njia, wakaja ndege wakaila.5;Nyingine ikaanguka penye mwamba,Pasipokuwa na udongo mwingi,;Mara ikaota kwakuwa na udongo hapa;6;Hata jua lilipozuka iliungua, na kwa kuwa haina mizizi ikanyauka.7;Nyingine ikaanguka penye miiba;Ile miiba ikamea ikaisonga, isizae matunda.8;Nyingine zikaanguka penye udongo ulio  mzuri,zikazaa matunda,Zikimea na kukua, na  kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.9;Akasema, Aliye na masikio ya kusikilia, na asikie.


Mfano Wa Mpanzi:1-9


Shabaha Ya Mifano:10-13[Mat13:10-17[Luka:8:9-10]


Yesu anafafanua mfano wa Mpanzi:13-20[Mat 13:18-23][Luka 8:11-15]

Taa iliyofunikwa:21-25[Luka 8:16-18]

Mfano wa Mbegu inayoota:26-29

Mfano wa Mbegu ya Haradali:30-34[Mat 13:31-32,34][Luka 13:18-19]


Yesu anaamuru dhoruba itulie:35-40[Mat 8:23-27][Luka 8:22-25]




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Ahsante kwa neno. Naamini nawe ilikuwa jumapili yenye baraka pia.

Rachel Siwa said...

Ahsante nawe Kadala..ilikuwa nzuri.