Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 3 August 2014

Nawatakia JumaPili Njema;Burudani-Living Water Worship Team Yesu U Mwema,Sifa ni kwako,Yehova Mwenye Nguvu Zote..!!!!!!!!


Wapendwa;Nawatakia Jumapili Njema Yenye Kusifu,Kuabudu,Kutukuza,Kushukuru,Kuwa na Matumaini na Kupendana......
5.Naam, na kwa sababu hiyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,6.Na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa, 7. Na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo.....


Neno La Leo;Waraka Wa Pili Wa Petro;1:1-21

19.Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa ing'aayo mahali penye giza, mwafanya vema, mpaka kutakapo pambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu.20.Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu furani tu.21.Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu;bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa MUNGU,Wakiongozwa na roho mtakatifu.






"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima

No comments: