Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 31 August 2014

Natumaini JumaPili Inaendelea Vyema;Burudani-Jamaican Gospel...!!!!!!

Wapendwa;Nimatumaini yangu Jumapili ilikuwa/inaendelea Vyema,Indelee kuwa na Amani,Upendo,Unyenyekuvu,Furaha na Upole kiasi....



Basi ,mimi Paulo mwenyewe nawasihi kwa upole na utaratibu wa Kristo;mimi niliye mnyenyekevu nikiwapo pamoja nanyi,bali nipokuwapo ni mwenye ujasiri kwenu;2;Naam, naomba kwamba nikiwapo, nisiwe na ujasiri kwa uthabiti ambao nahesabu kuwa nao juu ya wale wanaodhani ya kuwa sisi tunaenenda kwa jinsi ya kimwili 3; Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; 4;[Maana silaha za vita vyetu  si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;]
Neno La Leo;2Wakorintho 10:1-18
5;Tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu, na tukitekanyara kila fikira ipate kumtii Kristo 6;Tena  tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia. 7;Yaangalieni yaliyo mbele ya macho yenu.Mtu akijitumainia mwenyewe yakuwa ni mtu wa Kristo, na afikiri hivi pia nafsini mwake,Ya kwamba kama yeye alivyo mtu wa Kristo,vivyo hivyo sisi 8;Maana, ninapojisifu zaidi kidogo kwa ajili ya mamlaka yenu,[tuliyopewa na Bwana,tupate kuwajenga wala si kuwaangusha],sitatahayarika; 9;Nisije nikaonekana kana kwamba nataka kuwaogofya kwa  nyaraka zangu.......................

17;Lakini, yeye ajisifuye, na ajisifu katika Bwana. 18;Maana mtu mwenye kukubaliwa si yeye ajisifuye, bali yeye asifuwaye na Bwana.









"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe wote.

No comments: