Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 31 March 2014

Jikoni Leo; Nyama Choma - How to Eat Your Meat the East African Way,Tanzanian Mishkaki - Beef and Chicken Kebabs

Waungwana;"Jikoni Leo" Mmmmmmhhh mambo ya mitaani Bongo Tanzania....
Lakini wa Ughaibuni/Ng'ambo..hasa U.K. Hali ya hewa kwa sasa si mbaya saaana..unaweza kufanya mambo haya.





Shukrani;Mark Wiens

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Sunday 30 March 2014

Nawatakia JumaPili Njema na Happy Mother's Day;Burudani kutoka -African Gospel.....[Mchanganyiko]!!!!!!!!


Happy Mother's Day to all mothers, may GOD bless you.
Natumaini Jumapili hii inaendelea vyema..

Lakini  yanenaje?Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.

Neno La Leo;Warumi:10:5-15

Tena wahubirije, wasipopelekwa?kama ilivyoandikwa,Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema. 




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana

Saturday 29 March 2014

Jikoni Leo;Afya na Jamii-How to be slim _ BBC DOCUMENTARY_health documentary!!!!!

Waungwana ni "Jikoni Leo"; Tuangalie Afya zetu na Vyakula,Vinaweza kuwa Sumu au Dawa......


Sina mengi twende Pamoja...


"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Tuesday 25 March 2014

Monday 24 March 2014

[AUDIO]: Mdau Boniface Makulilo akijadili suala la Scholarship katika kipindi cha NJE-NDANI‏

Mdau Ernest Makulilo ambaye huandika kuhusu masuala ya Scolarship HAPA na pia kutoa video za suala hili HAPA
UNATAKA SCOLARSHIP?
Unajua pa kuzipata?
Unajua namna ya kuzipata?
Masharti yake je?
Makosa yanayofanywa na wengi?
Tofauti ya Scholarships za Undergraduate na Graduates wazijua?
Yapi ya kuchunga wakati wa kutafuta scholarships?
Boniface Makulilo ambaye amenufaika na scholarship hizi na kuandika kuzihusu kwa miaka ipatayo sita anaungana na Mubelwa Bandio wa Jamii Production kujadili hili.
Kuna mengi mema ya kujifunza.
KARIBU

NJE-NDANI ni kipindi kutoka Jamii Production Washington DC kinachokujia moja kwa moja (LIVE) kila Jumamosi kuanzia saa 6 mpaka 8 mchana (saa za Marekani mashariki) ambacho kinaleta Habari na Taarifa kuhusu yale yanayotokea na kuwagusa waAfrika walio NJE na NDANI ya Afrika.

Sunday 23 March 2014

Nawatakia JumaPili yenye Furaha Na Shukrani;Burudani Kutoka- African Mega Praise....!!!!!!

GOD can do Anything, Anytime, Anywhere in His time!!!!!!
Nawatakia JumaPili Yenye,Furaha,Shukrani,Matumaini,Amani na Baraka....

Nitamhimidi BWANA kila wakati,Sifa zake zi kinywani mwangu daima...

Neno La Leo;Zaburi:34:1-12

Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima,Apendaye siku nyingi apate kuona mema?




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Saturday 22 March 2014

[AUDIO]: DAKIKA 90: Kupotea kwa Air Malaysia na takwimu za usalama wa anga duniani‏

Ndege aina ya Boeing 777 ya Malaysia Airlines ikiruka kutoka Roissy-Charles de Gaulle Airport nchini Ufaransa mwaka 2011.
Photo Credits: PressTv
Wakati harakati za
kutafuta ndege ya Shirika la ndege la Malaysia iliyopotea zikizidi kushika kasi
na kuvunja rekodi ya kushirikisha mataifa mengi duniani, baadhi ya takwimu
kuhusu hali ya usalama wa safari za anga duniani zimezidi kuibuka na kufungua
macho ya wengi waliokuwa wakiamini kuwa tukio hili ni la kwanza na / ama
miongoni mwa machache kupata kutokea duniani.


Mtandao wa Usalama wa safari za Anga ama Aviation Safety Network
ilitoa orodha ya ndege zilizopotea tangu kumalizika kwa vita kuu ya pili ya
dunia.



Kwa mujibu wa takwimu hizo, ndege 88 zimepotea
tangu mwaka 1948, hivyo kufanya wastani wa ndege zinazopotea na kutopatikana
wala miili ya abiria kuwa 1.33 kwa mwaka.


Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90
ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es
Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30
AM).

Tuesday 18 March 2014

IskaJojo Studios; Ilimuhoji Miriam Kinunda Author of Taste of Tanzania Cookbook‏


IskaJojo Studios; Ilimuhoji "Miriam Kinunda" Mwandishi wa kitabu cha mapishi a Taste of Tanzania: Modern Swahili Recipes for the West.
Akieleza historia yake fupi ya kazi na mapishi na mengineo yanayoweza mnufaisha yoyote anayetaka kuandika kitabu na kufanikisha.



Miriam Kinunda - Taste of Tanzania  Na  IskaJoJo Studios 


"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Monday 17 March 2014

Boniface Makulilo azungumzia maisha katika jeshi la Marekani kwenye kipindi cha NJE-NDANI‏

Boniface Makulilo alipokuwa katika Jeshi la Maji la Marekani (Navy)
Mtanzania Boniface Makulilo ametumikia Jeshi la Maji (NAVY) hapa
Marekani kwa miaka miwili na sasa ni mwanajeshi mstaafu (Veteran)

Amezungumza
na Mubelwa Bandio wa Jamii Production kuhusu maisha yake ya jeshini na
namna ambavyo watu toka nje ya nchi wanaweza kunufaika na mafao yaliyopo
jeshini.

Ameeleza mengi ya manufaa ambayo wengi hatuyajui kuhusu maisha katika jeshi hilo.

Karibu uungane nasi

NJE-NDANI ni kipindi kutoka Jamii Production Washington DC kinachokujia moja kwa moja (LIVE) kila Jumamosi kuanzia saa 6 mpaka 8 mchana (saa za Marekani mashariki) ambacho kinaleta Habari na Taarifa kuhusu yale yanayotokea na kuwagusa waAfrika walio NJE na NDANI ya Afrika.

Sunday 16 March 2014

Nawatakia JumaPili Njema na Furaha;Burudani kutoka kwa Beatrice Kitauli-YESU Unipendaye[TENZI],Imbombo Inunu mwa JESU na Nyingine!!!

Wapendwa;Nimatumaini yangu Jumapili inaendelea vyema..

Heri kila mtu amchaye BWANA,Aendaye katika njia yake.


Neno La Leo;Zaburi:128:1-6

Tazama,atabarikiwa hivyo,yule amchaye BWANA......





"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

Saturday 15 March 2014

[AUDIO]: DAKIKA 90 ZA DUNIA: Mfungwa aliyekuwa akisubiria KIFO aachiwa huru‏


Picha iliyopigwa na mwanasheria wake, ikimuonyesha Bwn Ford, siku ya kwanza kama mtu huru baada ya miaka 30 jela kwa kosa ambalo hakufanya. Photo Credits: theatlantic.com
Wiki hii, mmoja wa wafungwa nchini Marekani, ambaye alikuwa kwenye orodha ya wanaosubiri kunyongwa kutokana na kuhukumiwa kifo kwa mauaji  aliyotuhumiwa kufanya mwaka 1984 aliachiwa huru baada ya Jaji kukubali kuwa hakukuwa na ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa ni yeye aliyeshiriki mauaji hayo.

Sasa, mfungwa huyu atalipwa dola 25,000 kwa kila mwaka aliotumikia kifungo hicho, lakini, kwa mujibu wa sheria ya Louisiana, kiwango cha juu anachoweza kulipwa ni dola 250,000

Ina maana, atalipwa kwa miaka 10 tu kati ya 30 aliyokaa gerezani

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Tuesday 11 March 2014

[AUDIO]: Kipindi cha FAMILIA. Siku ya wanawake duniani‏

Karibu katika kipindi cha FAMILIA kutoka Jamii Production.
Kipindi hiki kilirushwa moja kwa moja (live) Jumamosi Machi 8, 2014

Katika kipindi cha wiki hii, mjadala ulijikita zaidi katika SIKU YA WANAWAKE DUNIANI ambapo wageni Mary Ndaro akiwa Wichita Kansas na Mch. Tumaini Mwanyonga  walijadili kwa mapana suala hili.

Wamegusa mengi mema ambayo ni muhimu kuyasikiliza.





Photo Credits: happyholidays2014.com

Monday 10 March 2014

Jikoni Leo; Njoo Tupike Na Chef Kile-Kuchoma Ndizi Mzuzu kwa Oven na Mengine!!!!!

Waungwana;"Jikoni Leo" Tupo na Njoo Tupike Na Chef Kile.

Vijiwe/Vibaraza vya Mapishi kwa sasa Vinakuwa Kwa Kaaasi.
Sasa kama wewe ni Mpishi/Unapenda Kujifunza ,Mpenzi wa mapishi mbalimbali Wakati ndiyo huu.
Nisiwachoshe na Maneno Meengi...
Twende Sote sasa;"Jikoni Leo" Na....





Jee kuna faida/umejifunza kitu hapa?

Mimi hii ya Ndizi  Mzuzu kwa Oveni nimeondoka nayo/Nimejifunza!!!!

Zaidi ingia;youtube.Njoo Tupike /http://www.njootupike.com/

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 9 March 2014

JumaPili hii Tusifu Na Kuabudu;Burudani-Mr&Mrs Goodluck Sandy-Alipo BWANA,Viumbe Vyote,Hakuna mwingine Tena,MUNGU U Mwema,Hakuna wa Kufanana na YESU!!!!!

Hatuja chelewa saana,Wapendwa Waungwana..WANAWAKE JUU!!



Wapendwa; Nawatakia JumaPili Njema, Yenye Kusifu na Kuabudu,Imani,Furaha,Amani,Tumaini,Subira,Uvumilivu,Hekima,Busara na UPENDO!!!!


Wanafunzi waliposikia,walishangaa mno,wakisema,Ninani basi awezaye kuokoka?



Neno La Leo;Mathayo Mtakatifu:19:23-30


YESU akawakazia macho,akawaambia,kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa MUNGU yote yanawezekana.


Lakini wengi walio wa  kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Friday 7 March 2014

International Women's Day 2014 - UDSM female staff.

Wanawake tunaweza.. Mamaaa GerryHans nawatakia wanawake woote kila la kheri ktk kusherehekea siku ya wanawake duniani. Kina Mama oyeeeee...

Picha na Mpiga picha Wetu;Phoibe Penza- Mshana[Mwanapenza]


Kama unapicha,Ujumbe wowote,Usisite kututumia kwa Email;rasca@hotmail.co.uk

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.