Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 30 October 2013

Tanzania: Tunaweza kujitoa A. Mashariki

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete

Serikali ya Tanzania imesema inatafakari ushiriki wake ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na inaweza kujitoa ndani ya Jumuiya hiyo iwapo itaendelea kutengwa katika baadhi ya vikao.
Aidha imesema Tanzania haitambui vikao vinavyofanywa na nchi tatu zilizopo ndani ya Jumuiya hiyo ambazo zimekuwa zikizitenga Tanzania na Burundi.
Taarifa zinazohusiana
Tanzania, Afrika Mashariki, Afrika
Waziri anayehusika na masuala ya Afrika Mashariki wa Tanzania Samwel Sitta ameliambia Bunge la Tanzania kuwa makubaliano ya vikao hivyo vinavyofanywa na nchi za Kenya, Rwanda na Uganda yatatekelezwa na nchi hizo zinazofanya vikao hivyo kwa sababu vinafanyika nje ya utaratibu wa mkataba wa jumuiya hiyo.
Katika mikutano iliyofanyika hivi karibuni Tanzania na Burundi hazikualikwa kwenye vikao hivyo.
Kwa mujibu wa Waziri Sitta mikutano ya wakuu wa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda ambayo ilianza kwa kuitenga Tanzania ilifanyika Entebbe nchini Uganda mwezi Juni mwaka huu na kufuatiwa na mkutano wa pili uliofanyika Agosti mwaka huu huko Mombasa nchini Kenya ambapo nchi hizo tatu bila kuishirikisha Tanzania walizungumzia uanzishaji wa himaya moja ya forodha.
Mambo mengine waliyozungumza wakuu hao ilikuwa uanzishaji wa visa moja ya utalii kwa nchi zao na matumizi ya vitambulisho vya uraia ambavyo vitatumika kama hati za kusafiria miongoni mwa nchi hizo.
Aidha Waziri Sitta amesema ndani ya mikutano hiyo pia walizungumzia kuanzisha mchakato wa kuanzisha shirikisho la nchi hizo.
Tayari Tanzania imeanza mazungumzo na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kuangalia ni kwa namna gani zitaanzisha ushirikiano nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kama zinavyofanya nchi za Rwanda, Uganda na Kenya.
Habari kutoka;http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

Tuesday 29 October 2013

JAMII PRODUCTION YAZINDULIWA RASMI‏ !!




Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara alipokuwa akisisitiza jambo wakati wa mahojiano mafupi aliyofanya na Jamii Production kabla ya KUZINDUA RASMI shughuli za kutayarisha na kusambaza matangazo ya Radio na Video.



Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akiwa na waanzilishi wa Jamii Production, Mubelwa Bandio (kulia) na Abou Shatry (kushoto)

Naam....
Kwa baraka za Mhe. Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt
Fenella Mukangara, JAMII RASMI IMEZINDULIWA RASMI Oktoba 26, 2013,
alipotutembelea kuangalia utendaji wetu na kuizindua rasmi hapa ofisini
kwetu Washington DC.
Hii ilikuwa ni ZAIDI YA TUKIO.
Ilikuwa ni BARAKA KWETU na tunamshukuru kila aliyewezesha hili.
NA SASA.....
Kazi ya kutekeleza yale yaliyousiwa na Mhe Waziri, yaliyo yaliyo msingi
wa kituo chetu, yale yaliyo MAHITAJI ya walaji (hadhira yetu) NA WAJIBU
WA FANI YETU ndio imeanza.
Na......
Hakuna litajalokuwa na maana kama hatutajua namna ambavyo utendaji wetu unaathiri maisha yako kwa namna CHANYA na HASI
Wewe (msikilizaji, mtazamaji na msomaji wetu) ni mdau mkubwa wa kufanikisha hili.
Tuzidi kushirikiana
TWAWAPENDA



Msimamizi wa vipindi na mpigapicha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry akisisitiza jambo kabla ya kuwasili kwa mgeni rasmi


Mtayarishaji na Mtangazaji wa kipindi cha FAMILIA Georgina Lema akiwa "kitini"


Mmoja wa wawezeshaji wakuu wa Jamii Production Bwn Isidory Lyamuya wa Prestige Health Services akijaribu vitendea kazi vya kituo


Mhe. Waziri Mukangara akipokea maelezo ya utendaji wa kituo. Kushoto ni Afisa Ubalozi Mindi Kasiga

 
Mhe. Waziri akisikiliza RISALA ya Jamii Production 



 Mhe. Waziri Mukangara akijibu risala ya Jamii Production


Bwn Isidory Lyamuya akipata akipata picha ya pamoja na Mhe. Waziri kwa msaada anaotoa kufanikisha kazi za Jamii Production



Bwn Isidory Lyamuya akipata mkono wa pongezi toka kwa Mhe. Waziri kwa msaada anaotoa kufanikisha kazi za Jamii Production

Abou Shatry akipongezwa na Mhe Waziri Mukangara


"Mwanamama" Georgina Lema wa kipindi cha FAMILIA akipata kumbukumbu na Mhe. Waziri


 Mkurugenzi wa Mambo Jambo Radio Bwn Julius Makiri ambaye aliungana nasi katika uzinduzi huu rasmi akipata kumbukumbu na Mhe. Waziri



 Mhe. Waziri Dkt Fenella Mukangara na Afisa Habari katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Mindi Kasiga pamoja na wanaJAMII

 


Hakuna ZAWADI kubwa sawa na kilichofanyika. Na zawadi pekee tuliyonayo ni UPENDO. Ambao hauonyesheki wala haupimiki.

Lakini....tunapenda POPOTE UWAPO, UKUMBUKE SIKU YA LEO.
Na hivyo..twaomba KIKOMBE hiki kiwe kumbukumbu ya tukio hili kubwa kwetu

Abou Shatry akiwa mahala anapopatawala zaidi...


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 27 October 2013

Nawatakia J'Pili yenye Baraka;Burudani-Kijitonyama Choir,Ndani Ya Safina,Hakuna Kama Wewe!!!

Nimatumaini yangu J'Pili hii inaendelea vyema.. Iwe Yenye Neema,Baraka,Upendo na Amani....

BWANA akamwambia Nuhu,Ingia wewe na Jamaa yako yote katika Safina; kwa maana nimekuona wewe u mwenye haki mbele zangu katika kizazi hiki... 
Neno La Leo;Mwanzo:7:1-24


Ndani Ya Safina aahhh....ndani ya Safiiina aa humo ndani ya Safina oooohh kuna upendo mwingiiii..........Mhhhh..Wanyakyusa kwa Waheheeee..Wasambaa kwa wadigoooo..Njoni wote Tuingieee...






"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana

Saturday 26 October 2013

chaguo La Mswahili Leo;Mrisho Mpoto!!!!

Waungwana ni wakati mwingine tena wa "Chaguo La Mswahili"Leo chaguo limeangukia kwa kaka Mrisho Mpoto[HOME BOY]Mpoto kama ukimsikiliza juu juu..huwezi kumuelewa kabisa na ukashangaa huyu naye anaimba nini?Lakini ukitulia na kumsikiliza maneno anayotumia utakubaliana nami..Maneno yake ni Vichocheo,Mafunzo,Maisha Na Jamii inayotuzunguka...
Mhhh..mimi Mpoto ananikosha/nibamba/Kupenda kazi zake,,,Vipi wewe mwenzangu?


Iyeeehhh Mjomba Iyeehh...!!..Bora kujenga darajaaaa...!!
Mjomba hapa Nyumbani Tuna hadithi  na misemo mingi kujihakiki,Maana lake mtu halimtapishi Lakini kukumbatia maji kama jiwe ni ujingaaa...
Twende Sote sasa....








"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA: Msiba wa Martha Shani DC


Katika kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA wiki hii... Kutoka nchini Marekani, tuanze na habari za msiba ulioikumba jamii ya waTanzania waishio maeneo ya Washington DC.

Marehemu Martha Shani

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).a


Hii ilikuwa ripoti ya Oktoba 26, 2013 





*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Wednesday 23 October 2013

Tuesday 22 October 2013

MAENDELEO YA MSIBA WA BI MARTHA SHANI WASHINGTON DMV


                                          Marehemu Martha Shani[1976-2013]
Marehemu Bi Martha akiwa na mumewe Alex Pamoja na watoto wao Jose naChris 
                                         
                                   
NDUGU YETU ALEX KASSUWI BADO ANAHITAJI MSAADA WETU WA HALI NA MALI ILI KUWEZESHA KUSAFIRISHA MWILI WA MPENDWA MKE WAKE ALIYEFARIKI GHAFLA SIKU YA JUMAMOSI OCT 19, 2013.

KUTOA NI MOYO NA CHOCHOTE UTAKACHOWEZA KITASAIDIA NA HATIMAE KUWEZESHA SAFARI HII NDEFU YA KUMPELEKA MAREHEMU KATIKA MAPUMZIKO KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE TANZANIA

GHARAMA ZA MSIBA KUSAFIRISHA MAREHEMU NA FAMILIA YAKE NI $19,500

FEDHA ZILIZOPATIKANA HADI SASA NI $4,300
ZILIZOBAKI $ 15,200

TAFADHALI TUMA RAMBI RAMBI ZAKO KUPITIA ACCOUNT IFUATAYO :-
# 446030759150 BANK OF AMERICA,MD
ROUTING # 052001633
MAJINA KWENYE ACCOUNT NI ALEX KASSUWI & FAITH ISINGO

CHEKI ZINAWEZWA ANDIKWA KWA ALEX KASSUWI AU FAITH ISINGO.

PIA UNAWEZA KUTOA RAMBIRAMBI ZAKO KWA KUFIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU AMBAKO NDIKO MSIBA UPO
ADDRESS NI

482 ARWELL CT
FREDERICK, MD,21703

AU WAWEZA WASILIANA NA MMOJA YA WANAKAMATI HAPO CHINI NA KUMUELEKEZA UPO WAPI ILI AWEZE KUKUSANYA MCHANGO WAKO

Tino Malinda -240-565-7133
Dickson Mkama - 301-661-6207
Mariam Mtunguja - 240-422-1852
Quizella Ntagazwa - 240-602-5011
MV Mtunguja- 240-593-0575
Victor Marwa - 240-515-6436
Faith Isingo - 240-705-1055
Julius Manase-240-393-8445

UKISOMA UJUMBE HUU TAFADHALI MTAARIFU NA MWENZIO, MZIGO HUU NI WETU SOTE NA KWA PAMOJA TUNAWEZA

HAKUNA KIDOGO PALIPO NA NIA. NA HAKUNA KIKUBWA PALIPO NA UMOJA.

Sunday 20 October 2013

Tumalizie J'Pili hii Vyema;Burudani- The Whispers Band-Nina Baba yangu asiyeshindwa kamwe na Nyingine!!!

Wapendwa muendelee na J'Pili kwa Amani,Furaha na Bidii....
Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?

Neno La Leo;Mithali:22:29 na Muhubiri:9:10






"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

TAHADHARI: UTAPELI MWINGINE WAINGIA NCHINI; Sasa wanatumia mitandao ya Internet ya Kuomba ajira, TAFADHALI soma taarifa hii usije ukalizwa.



Kuna UTAPELI mpya umeingia Nchini, kuna watu ambao wanajifanya wana makampuni na wanatafuta watu wa kazi namaanisha wanatangaza nafasi za kazi, nafasi hizo za kazi huzitangaza kupitia mitandao ya Internet ambayo huwa ina maeneo ya kutangaza nafasi za ajira, nitashindwa kuitaja mitandao hiyo kwa kuwa sio utaratibu ila wewe ambaye unajua kuwa kuna mitandao ambayo inatangaza ajira kupitia njia ya Internet ujue ndio hiyo ambayo tunaiongelea hapa.

Matukio yenyewe yanakuwaje: Watu hao hutangaza nafasi za kazi mbali mbali kupitia mitandao hiyo kwa kuandika wana makampuni na wanatafuta watu kwa nafasi mbambali kwenye makampuni yao feki, kwa kutambua watanzania wengi wana shida ya ajira hutangaza nafasi ambazo wanaamini wengi wataziomba na kuweka vigezo vya chini sana hasa eneo la Elimu na uzoefu kwa kuamini wengi wataomba, baada ya hapo, wewe mwenye shida ya ajira ukishatuma CV yako ambayo itakuwa pia inaonyesha mawasiliano yako, wao hutumia mwanya huo kukutumia ujumbe mfupi (SMS) na kujifanya wao ni wafanyakazi wa kampuni husika ambayo imetangaza nafasi hiyo na kujidai  wanaweza kukusaidia kuipata kazi hiyo na kukutaka uwatumie hela ili wakufanyie mpango na kukutumia maswali ambayo utaulizwa kwenye INTERVIEW na majibu yake, hawa jamaa kwa kutambua shida ya Watanzania hawasemi wanataka kiasi kikubwa huwa wanataka kiasi cha Elfu kumi hadi Hamsini, wanafanya hivyo kwa kutambua wewe mtafuta ajira unaweza ukakipata kiasi hicho.

Matapeli hao hudiriki kukwambia na kiasi cha mshahara ambao utalipwa kwenye kazi hiyo ili kukutamanisha utume hiyo hela, simu hiyo ambayo imekutumia ujumbe huo ukiipigia huwa haipatikani na ikipatikana haipokelewi na wanakua wameziregister kwa majina ambayo wanakuaminisha ni yao kumbe ni majina ya uongo ya kutapelia watu.

Mpaka sasa wameshawaliza watu wengi sana kwa hiyo wewe mdau kuwa makini sana wakati unaomba ajira kupitia mitandao mbalimbali ya Internet, ukiona unaombwa hela baada ya kuomba ajira kupitia mitandao hiyo ujue ndio hao matapeli.

KUWA MAKINI EWE MTANZANIA

IMETOLEWA NA:
MDAU MPENDA HAKI

Saturday 19 October 2013

Kukamatwa kwa mtuhumiwa wa mauaji ya Omar Sykes Washington DC‏


Eneo la tukio Washington DC ambapo Omar Sykes (picha ya ndani) aliuawa.
Photo Credits: National Review Online


Jumanne wiki hii, idara ya Polisi Washington DC (Metropolitan Police Department) ilitangaza kukamatwa kwa mtuhumiwa mmoja kati ya wawili waliokuwa wakitafutwa kwa mauaji ya mwanafunzi mTanzania aliyekuwa akisoma katika chuo kikuu cha Howard hapa jijini.

Omar Sykes (22) aliuawa usiku wa Julai 4 mwaka huu nje kidogo ya maeneo ya chuo hicho alipokuwa pamoja na mwenzake.

Wakiwa mtaa mmoja toka chuoni, wanafunzi hao walivamiwa na watu wenye silaha waliotaka kuwapora, na katika harakati hizo, Omar alipigwa risasi
kifuani na kufariki.


Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).



Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es
Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC


Hii ilikuwa ripoti ya Oktoba 19, 2013



--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"


Tuesday 15 October 2013

Mahojiano na wadau wa darasa la Kiswahili Washington DC‏

Photo Credits: Panafricanvisions.com
Kiswahili inaaminika kuwa lugha asili ya Afrika inayozungumzwa na watu wengi kusini mwa jangwa la sahara.

Kama
tunavyojua, ni lugha ya taifa kwa nchi za Tanzania naKenya, na pia
yazungumzwa kwenye nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi,
Rwanda, Uganda na visiwa vya Comoro.

Ikizungumzwa na watu
wanaokadiriwa kufikia milioni 100 hivi sasa, Kiswahili ndio lugha pekee
ya kiAfrika iliyo miongoni mwa lugha rasmi za Umoja wa Afrika. Na
inaaminika kuwa lugha ya saba kwa watumiaji wengi duniani

Na matumizi
yake kama lugha inayozungumzwa na wengi wenye lugha tofauti katika
ukanda wa Afrika Mashariki na Kati unaifanya lugha hii kuwa muhimu zaidi
kwa watu wengi walio na mahusiano na / ama wanaotaka kujishughulisha na
biashara, kazi ama diplomasia katika ukanda huo.

Kiswahili sasa
kinafunzwa katika vyuo visivyopungua 50 hapa nchini Marekani, lakini pia
inafundishwa kwenye vyuo vikuu mbalimbali Ulaya na hata bara Asia.

Kiswahili
ni lugha muhimu katika habari, shule, kazi za kiofisi, kidiplomasia na
hata usalama miongoni mwa mataifa na naamini ndio sababu hata jumuiya ya
waTanzania hapa Washington DC wakaona ni jambo la busara kuanzisha
darasa la kufunza Kiswahili kwa watoto hapa DMV.

Na leo,
wawakilishi wa wahusika wa mpango huo, Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV
(Washington DC, Maryland na Virginia) Idd Sandaly pamoja na walimu Asha
Nyang'anyi na Bernadeta Kaiza wamekuwa wakarimu sana kujiunga nami
katika studio za JAMII PRODUCTION hapa Washington DC.

KARIBU UUNGANE NASI

Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV (Washington DC, Maryland na Virginia) Iddi Sandaly akishiriki kipindi ndani ya studio za Jamii Production
Mmoja wa walimu wa darasa la Kiswahili hapa Washington DC Bernadeta Kaiza ndani ya studio za Jamii Production
Mmoja wa walimu wa darasa la Kiswahili hapa Washington DC Asha Nyang'anyi akishiriki kipindi ndani ya studio za Jamii Production
Twawapenda....Tukutane juma lijalo kwa kipindi kingine cha HUYU NA YULE tutakapohojiana na wadau wengine juu ya jambo jingine MUHIMU kwa jamii yetu

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Mahojiano ya Jamii Production na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Dr Charles Kimei‏

Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei (kulia) akizungumza na Jamii Production  ndani ya ofisi ya Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nchi za Marekani na Mexico uliopo Jijini Washington DC

Jumatano ya Oktoba 9, 2013, Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRBD Dr Charles Kimei akiambatana na Mkurugenzi wa Masoko wa (CRDB) Tully Mwambapa, Bw. Mkurugenzi wa Hazina (CRDB) Alex Ngusaru na Msaidizi wa Dk.Kimei , Kenneth Kasigila walikuwa jijini Washington DC (pamoja na mambo mengine) kueleza mipango ambayo CRDB inayo katika kuboresha huduma za akaunti ya Tanzanite pamoja na kutambulisha huduma mpya ya JIJENGE.

Jamii Production ilipata fursa ya kuhojiana na Dr Kimei ambaye amefafanua mengi kuhusu huduma hizo.

KARIBU UUNGANE NASI





Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei na akipata picha na mpiga picha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry baada ya mahojiano.

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA@ CAPITAL RADIO. Kutekwa kwa Waziri Mkuu wa Libya na kukamatwa kwa Al-Libi‏



Kutoka Tripoli nchini Libya....Watu wenye silaha mapema Alhamis walimteka na baadae kumuachia huru Waziri Mkuu wa nchi hiyo Ali Zeidan juu ya kile ambacho waasi wamesema ni kuonyeshwa kukerwa na matatizo ya RUSHWA NA USALAMA katika nchi hiyo.

Hili linaonekana kutekelezwa kufuatia kukamatwa kwa mshukiwa wa kundi la kigaidi la AlQaeda Nazih Abdul-Hamed al-Ruqai, ambaye pia anafahamika kama Abu Anas al-Libi aliyekamatwa jumamosi iliyopita nchini Libya na makomandoo wa Marekani

Huu ni muendelezo wa taarifa tofauti na za kuchanganya tangu kukamatwa kwa Al-Libi

Ifuatayo ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es
Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ilikuwa ripoti ya Oktoba 12, 2013


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

www.jamiiproduction.blogspot.com
http://www.youtube.com/user/mutwiba/videos
https://soundcloud.com/jamii-production

Sunday 13 October 2013

Nawatakia J'Pili Njema;Bethany Children's choir from Tanzania sing 'Mambo sawa sawa' na Nyingine!!

Wapendwa Nawatakia J'Pili Njema yenye, Imani,Ulinzi,Tumaini,Furaha na Tusisahau kusaidia wenye Kuhitaji....
Hatimaye,ndugu,tuombeeni neno la BWANA liendelee,na kutukuzwa vile vile kama ilivyo kwenu;
Neno La Leo;2Wathesalonike:3:1-18;Neema ya BWANA wetu YESU Kristo na iwe pamoja nanyi nyote.

Burudani ya Leo Kutoka kwa Bethany Children's Choir Tanzania; Kujua Mengi au kwa Msaada zaidi ili uwafikie Watoto Hawa Ingia Hapa;http://www.bethanyfamily.net






"Swahili Na Waswahili" MUNGU awabariki Sana.

Saturday 12 October 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Sam Mangwana na Franco!!!!


Mmmmmhhh mambo ya kitambo kidogo...
Endelea kupata Burudani..
.



"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Thursday 10 October 2013

Mtu Kwao; kaka Tonny Samaka-Ana Haya ya Kusema!!!!


   Maneno ya  kaka;Tonny Samaka

Boom fc,ashanti,sharif star,forever fc,god lion,pentagon,barcelona,mkunguni fc,fildaus fc,dizonga fc,santa maria nk,popote ulipowahi kusikia kati ya hizo timu zinacheza iwe tmk,kino nk,ujue watoto wa ilala WANAWAKILISHA NA USHINDI NJE NA NDANI,i love ILALA bana!team#ILALA.

Wewe unasemaje?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja sana.


Wednesday 9 October 2013

Sunday 6 October 2013

Nimatumaini Yangu J'Pili inaendelea Vyema;Burudani-Ruach Team-Godwin Ombeni,Mwamba wenye Imara na...!!!!!

Wapendwa muendeele na J'Pili  hii Vjema,Muwe na Imani,Matumaini,Furaha na Ushindi.....

[31]Akawatolea mfano mwingine,akisema,Uflame wa Mbinguni umefanana na Punje  ya hadali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;
[32]Nayo ni ndogo kuliko mbegu zote;lakini ikiisha kumea,huwa  kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti,hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.
Neno La Leo;Mathayo Mtakatifu:13:24-35.






"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Tuesday 1 October 2013

Ya Kale Ni Dhahabu-Zilipendwa;Arusi!!!!!!

Binti P.. akienda kufunga Ndoa..
Bibi Na Bwana...
Watoto na Show..

Waungwana ya Kale ni Dhahabu..

Unaweza kutambua hii ni miaka gani?
Nini kimekuvutia/Bado Unakipenda na Nini umekumbuka kupitia Picha hizi?
Una Maoni/Ushauri gani kwa Arusi/Wanaofunga Ndoa sasa?

Kama una picha zako za zamani na unapenda kushiriki nasi,Tuma kupitia Email;rasca@hotmail.co.uk.

"Swahili NA Waswahili" Tunawatakia kila la kheri Wanandoa katika Maisha yenu Yoote.

Pamoja Daima.