Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 8 March 2013

Leo ni Siku Ya Wanawake Duniani;Wanawake Tusiogope!!Leo Tumuangalie da'Mwandale!!!!!!!





Waungwana; Leo ni Kilele cha Siku ya "WANAWAKE DUNIANI" Nami nichukue Nafasi hii kuwatakia Mafanikio,Ubunifu,Uwezo,Maarifa na Baraka katika Utendaji na Maisha  Mema...

WANAWAKE TUSIOGOPE,Kujaribu,Kutenda,Kuamua,Kuuliza/Kujiuliza,Kuchekwa na Kufanikisha Malengo/NdotoZetu.....

Hakuna aliyezaliwa anaweza..wote walijifunza na kulikuwa na Chanzo/Mwanzo mpaka Wale Waliofanikiwa kutimiza Ndoto zao zikawa kweli.....Na kwenye Safari ya Maendeleo kuna Mapito/Changamoto nyingi sana mpaka ufikie Malengo...
Kuna kukatishwa Tamaa,Kuchekwa na Kubezwa.....

Pia ni Vigumu kwa walio wengi kujitambua Yeye anakipaji,Mzuri kwa kufanya nini na Kujikubari au Kukubarika kwa Siku za Mwanzo..Lakini hakuna linaloshindikana mbele za MUNGU..Kama ni Safari uendayo ni yako au si yako Itajulikana Tuu...Hakuna cha Kazi hizi za KIUME au KIKE..
WANAWAKE wa LEO Wanajitahidi Sana Sana  Kujitoa/ Kujihusisha na Mambo mbalimbali ili kufanikisha NDOTO zao na Kuleta Mabadiliko,Katika Utendaji,Kujitafutia Kipato na Kusaidia Familia na Jamii Pia.Wengi wao Wamekuwa si WAOGA !!!!!!!!!!

Nisi watenge/Kuwasahau MAMA zetu, Hasa wa KIJIJINI, Pia nao kwa sasa Wanasonga Mbele..Japo bado wanapitia changamoto nyingi sana....Lakini Wengi wao WANAJITAMBUA.

Basi kwa Leo niishie hapa kwani Maneno yanakuwa Meeengi Sana..
Mimi huwa Navutiwa Sana na WANAWAKE Wanaojichanganya na Mambo Tofauti Kama DADA/MWANAMKE HUYU;MWANDALE MWANYEKWA!!!!!!!!!!!!!!

Vipi Mwenzangu dada Huyu anakuvutia? Karibuni kwa Maoni/Ushauri na Tuelimishane kwa Upendo!!!

AFRIKA BARA LETU,TANZANIA NCHI YETU,KISWAHILI LUGHA YETU!!!!!!

   "Swahili NA Waswahili "Wanawake Tusiogope!!!!!!

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

wanawake tunaweza na kweli tusiogope kufikisha ujumbe kwa uma
pamoja daima..