Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 30 November 2012

Kisa Cha Leo; na Mswahili Emu-Three-Uchungu-wa-mwana-aujuaye-ni-mzazi-31!!!!



Waungwana; Si Mwingine ni Emu wa 3. "Kisa cha Leo" ni Uchungu wa Mwana.....Inaendelea,Si mimi ni yeye  na 

DiaryYangu [Yakeeeee!!!!]



Marejeo: Tukumbuke hiki kisa alikuwa akisimulia yule binti niliyekutana naye akiwa kajiinamia kashika shavu, ….akiwa kasimuliwa na mama yake. Huyu binti kwa hali aliyokuwa nayo, alifikia hadi kukusudia hata kujiua.

Binti aliona kabisa , kuwa maisha kwake hayana thamani tena. Na binadamu anapofikia hapo, ujue kweli kuna jambo…nani asiyependa kuishi, hata yule anayekusudia kujiua, muda roho ikitaka kutoka, huwa anajitahidi kuiondoa ile kamba shingoni, lakini anakuwa keshachelewa, siku yake imeshafika, inabidi aonje umauti…na jamani kutoka kwa roho sio kitu cha mchezo.

Katika kisa hiki utagundua kuwa kuna mwanamama hapo ambaye ana jina hilo hilo, …jina ambalo nilisikia akiitwa huyu binti na mama yake mdogo, wakati namuulizia kuhusu maisha yake, kwanini imetokea hivyo, sasa tuendelee na kisa chetu, ………….

*********

‘Mimi sikujua kabisa huyo baba mlevi ninayeishi naye sio baba yangu wa kunizaa, kumbe alikuwa ni baba wa kufikia, hayo niliyajua baadaye, wakati najiandaa na safari ya kuja kuishi huku Dar, mji ambao kila mmoja kule kijijini alitamani kuja kuishi.

Mama yangu aliniambia huyo baba ndiye aliyekuja kumuokoa pale alipoachwa pale porini…..ili wenzake wafike huko wanapohitajika kwa wakati muafaka, na baadaye watarejea kumchukua, au kumtafutia sehemu ya kumuhifadhi.

Wakati kaachwa pale, akiwa kachoka, kwani mwili ulikuwa hauna nguvu, baada ya safari ndefu, baada ya mapigano, na yeye kujitolea kumsaidia huyo jamaa aaliyeficha sura yake kwa kofia ya ngozi ….na haat kujeruhiwa tena…akawa anatamani kulala tu.

‘Wewe pumzika hapa, na utakula nyama hii…mimi nahitaji huko kwetu haraka, leo najua inawezekana ikawa siku ya mwisho, nimeota kuwa nahitaji haraka sana….na kama ulivyoona, hawa watu walikuja kuniua, lakini tumeweza kuokoka…..ngoja nifike huko nyumbani haraka, halafu nitarudi kuhakikisha kuwa upo mikono salama….’akasema.

‘Sawa wewe nenda tu, na nakutakia mafanikio mema, mungu yupo pamoja na wewe, ila ninachokuomba ni kuhusu mtoto wangu…..naomba siku ukija, uje na mtoto wangu, usije bila ya kuwa na mtoto wangu….’akasema huyo mwanamama.

‘Naahidi nitafanya hivyo…na wewe hakikisha unakuwa salama, usiondoke, hapa, …hapa ni salama zaidi’akasema na akambusu kichwani na kuondoka. Huyu mwanamama alikaa pale kwa muda, halafu akaona akatafute maji ya kuoga, maji yaliyokuwepo pale yalikuwa ni machache, ….........
Endelea kusoma Zaidi,Ingia;http://miram3.blogspot.co.uk/

                           "Swahili NA Waswahili" Pamoja Saaaana.

Wednesday 28 November 2012

Ngoma Africa Band growing stronger and stronger in Europe !!!



Ngoma Africa Band, a German based Tanzanian band is now one of the oldest and most successful Africans bands in Germany.

Many African bands in Europe hardly survive for more than a year. Yet Ngoma Africa Band, founded by Ebrahim Makunja aka Ras Makunja in 1993, is still growing stronger.
The band plays "Bongo Dance", which is a unique combination of traditional and modern Tanzanian rhythms with  Soukous and Rumba. All theirs songs are in Kiswahili.

Ngoma Africa Band has released several successful hits including "Mama Kimwaga" (Sugar Mummy), "Anti-Corruption Squad" and "Apache wacha Pombe" (Stop over drinking).

In 2010 Ngoma Africa Band released a single in praise of Tanzania's President Jakaya Kikwete. The song titled "Jakaya Kikwete 2010" praises Mr. Kikwete's good leadership skills and commitment to fight corruption.

On 12th August 2012, Ngoma Africa Band received the International Diaspora Award (IDA) at the International African Festival Tubingen 2012, Germany, for their hard work in promoting East African music throughout Europe.

Ms. Susan Muyang Tatah, CEO of the International African Festival Tubingen 2012 said Ngoma Africa Band was also chosen for the Award because of their creative performance on stage. It's difficult to resist dancing at their concerts, she said.

This year the band released a new CD titled "Bongo Tambarare" featuring "Supu ya Mawe" and "Uhuru wa Habari". The new release is already dominating air waves in Tanzania.

"Supu ya Mawe" advices the listeners to work hard and be patient while pursuing their objectives in life. It also appeals for generosity towards the needy.

"Uhuru wa Habari" praises African journalists who are bold enough to speak out the truth in environments where freedom of speech is quite limited.

Ngoma Africa Band is famous for staging thrilling shows in festivals in different parts of Europe. The band's joyful female dancers, wearing traditional costumes and dancing vigorously to their tunes, always leave fans asking for more.

Ngoma Africa Band is composed of talented young musicians including soloist Christian Bakotessa aka Chris-B, Said Vuai, Matondo Benda, Jonathan Sousa, Aj Nbongo, Richard Makutima, Bedi Beraca "Bella" and Jessy Ouyah.

For further information about Ngoma Africa Band and to listen to their music, please visitwww.ngoma-africa.com.
By Stephen Ogongo Ongong'a



Watanzania waishio Ujerumani kufanya hafla ya kumuaga Mhe,Balozi Bw.Ahmada Ngemera !!!








Watanzania waishio Ujerumani kufanya hafla ya kumuaga Mhe,Balozi Bw.Ahmada Ngemera !
Jumamosi 08-December 2012 mjini Berlin,Ujerumani



Umoja wa Tanzania Ujerumani (UTU) unaheshima kubwa kutarifu na kuwaomba watanzania wote
wanaoishi ujerumani na jirani ya Ujerumani kuwa umoja wetu tunatarajia kufanya afla ya kumuaga
Mheshimiwa balozi  Bw. Ahmada Ngemera ambaye anamaliza mda wake wa kufanya kazi,
Afla hiyo itafanyika mjini Berlin siku ya Jumamosi tarehe 8.12.2012 .
Mhe.Balozi bwana Ahmada Ngemera amekua balozi wa Tanzania nchini Ujerumani na watanzania
wanaoishi ujerumani watamkumbuka daima Mheshimiwa Balozi Bw.Ahmada Ngemera kwa kuwa
karibu sana na jamii ya watanzania,pia atakumbukwa kwa jitihada zake au kile ambacho watanzania
 wa ujerumani wanachokiita kuasisi Umoja na mshikamano wa watanzania nchi ujerumani,ambapo
 Mhe.Balozi Bw.Ngemera na msaidizi wake Mhe.Bw.Ali Siwa wahamua kuhamasisha watanzania 
waishio Ujerumani kuungana katika kila hali kuanzisha umoja wa mshikamano wa watanzania,kitu 
ambacho mabalozi wengi walishindwa kufanikiwa kufanya labda kwa sababu ya ukubwa wa nchi ya
 ujerumani wa watanzania wanaishi katika miji mbali mbali,lakini kazi hiyo ya kuwaungunganisha 
watanzania, Balozi Bw.Ahmada Ngemera na Msaidizi wake Bw.Ali Siwa walifanikiwa kuwafikia
 watanzania wote waishio Ujerumani na kuwashauri waanzishe umoja wa mshikimano,na matunda
ya juhudi zao ndipo kukazaliwa Umoja wa waTanzania Ujerumani.(UTU)  Umoja ambao ni chombo
 cha watanzania wote ! chombo ambacho watanzania waishio ujerumani wanajivunia !
UMOJA NA MSHIKAMANO NDIO MSINGI WETU IMARA!
OMBI:
TUNAWAOMBA WATANZANIA WOTE ! NA MARAFIKI WOTE WA TANZANIA
AMBAO WANATAKA KUSHIRIKI KATIKA AFLA HII,
TUNAOMBA MTOE MCHANGO WA EURO 20.00 NA KWA WANAFUNZI EURO 10.00 TU
 kwa kupitia Account : Union of Tanzania in German e.V.
VR Bank Rosenheim-Chiemsee AG
Konto-No.: 59641   BLZ: 71160161
Verwendungszweck: „Kumuaga Mhe. Balozi Ngemera


Pia unaweza kuwasiliana na kamati.utu@googlemail.com
simu namba +491734297997 au Katibu simu namba 01734744265 .




Tuesday 27 November 2012

Ya Kale Ni Dhahabu;Burudani-Kanda Bongo Man na Brandy - I Wanna Be Down na Nyingine!!!!!





Waungwana "Ya Kale Ni Dhahabu"  Duuhh Zilipendwa.........Haya unakumbuka nini ukiangalia picha hiyo na Miziki hii....hahahhaa Jamani jamani...

 Jee Ulivaa Loso/Rosooo,Robot/Utanikoma Saa Nane, T-shirt iliandikwa Yes/No, Bareeeet/Kofia,Mungu Usinione/Kofia,Raba Mtoni na sketi ya Jeans..... Mkanda wa Kipepeo,wa Plastiki....ulipaka Ayu/Yolanda....Kunyoa Panki,Push Back..... na..... Ongezea Mwenyeweeeee!!!!!!

Leo Nimewaletea Sister Duuuhhh wa Uhakika.........

Ngoja Niimbe kidogo...........Inde moniiiiiiii  Inde moniiii Inde Inde........eeehhh ukishakula umaaa tingisha umaaaa......

Hahahahaha "Swahili NA Waswahili" Mjumbe Hauawiiiiii.....

yeehhh mayebo yakuporaaaaaa dengu kuchanganya na dengueee dengu na piripiriiii.....

Tutumie Picha zako za Enziii  kupitia; rasca@hotmail.co.uk

  Pamoja Daima.

Sunday 25 November 2012

TAARIFA RASMI YA MSIBA WA MTOTO MARY SHABANI KACHUA KUTOKA CANADA.


Marehemu Mary Shabani Kachua (3 Yrs) enzi za uhai wake.
Familia ya Dr Shabani Kachua kutoka Canada inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Mary Kachua kilichotokea tarehe 19/11/2012 nchini Canada.
Mwili wake uliagwa jana York Funeral Home, Fredericton, NB. Canada na leo kutakuwa na misa maalum Symthe Cathedral Church, Fredericton, NB, Canada.
Familia ya Dr S. Kachua wataondoka leo Canada kuelekea Jijini Dar es salaam Tanzania kwa ajili ya kuupokea mwili na wanatarajiwa kufika kesho jumapili saa 7:30 Mchana kwa ndege ya Ethiopia Airlines.
Mwili wa marehemu Mary Kachua unatarajiwa kufika siku ya Jumatano tarehe 28/11/2012 kwa ndege ya KLM. Shughuli na taratibu za mazishi zinatarajiwa kufanyika nyumbani Tanga mjini.
Kwa mawasiliano zaidi ya taratibu zote za mazishi unaweza ukapiga namba:
+255 784 670866
+255 713 254553
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi.
Amen

Thursday 22 November 2012

jikoni Leo;Tupike Pamoja-Mapishi ya Puréed Vegetables - Recipe of (In Swahili)!!!!!



Waungwana; "Jikoni Leo" ni  Puréed vegetables (a special meal for children from 18 months to 4 years old)

 Mpishi si Wengine ni da'Sophi wa "Tupike Pamoja". Mmmhhh Tamu Saaaana!!!!! 

Kwa kujua zaidi ingia;Tupike Pamoja  au www.tupikepamoja.com

"Swahili NA Waswahi" Pamoja Daima.

East Africa Ultimate Frisbee Tournament Arusha, Tanzania


East Africa Ultimate Frisbee Tournament
Arusha, Tanzania
November 23-24,  

Arusha Ultimate Frisbee Association is pleased to announce the East Africa Ultimate Frisbee Tournament which will be held in Arusha, Tanzania on November 23-24, 2012, Four teams will be participating in game  played at Arusha Technical College:-

The teams that will be participating:
1)  MOSHI KILL KILLERS  -Captain: Frank Mushi
2)  MWANZA TOSSERS  -Captain: Andrew Bergman
3)  ARUSHA ULTIMATE FRISBEE  -Captain: Silau Ole Nyasi
4)   NAIROBI ULTIMATE  -Captain: Aaron Colverson

For any additional information and request, please call one of The Organizers Oli - 0684082908 or 0752216040

Tuesday 20 November 2012

DR SHABANI KACHUA APATA MSIBA: AFIWA NA MTOTO WAKE KIPENZI.!!!!!!!


Mke wa Dr Shabani Kachua, Jemima akiwa na mtoto wao kipenzi Mary wakati wa uhai wake.
Dr Shabani Kachua
Mama Shabani Kachua akiwa amembeba mtoto wake kipenzi marehemu Mary wakati wa uhai wake.
Mtandao wako unaungana pamoja na familia ya Dr Shaban Kachua katika kipindi hiki kigumu cha majonzi, kwa heshima kubwa tunampa pole sana kwa msiba huu mkubwa ambao wameupata.
Mtoto Mary amefariki Dunia Nchini Canada jana alipokuwa anaishi na wazazi wake, mazishi yatafanyika huko huko.
"BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

Monday 19 November 2012

Kisa Cha Leo na Mswahili Emu-3-Uchungu wa Mwana Aujuaye Mzazi;Sehemu ya 25!!!!!!



Kwa marejeo: Kais alipohisi kuwa huyo mwanaume, aliyemuona na yule mwanamke, ni askari wa mzee Hasim, alikimbia….., je alikimbilia wapi, na huko alipokwenda aliishia wapi, ukumbuke kuwa binti huyo alikuwa mja mzito, je ujauzito wake uliishia wapi….tuendelee sehemu hiyo ya Kaisi……..

Kais, alipozindukana alijikuta yupo kwenye kitanda, na wakati hupo tumbo lilikuwa likimuuma sana, na harufu aliyoisikia hakuwahi kusikia kabla, akageuza kichwa huku na kule, lakini hakuona mtu kwa upeo wa mcho yake. Akainua kichwa na , kwa mbali akaona watu wamevaa nguo nyeupe, moyoni akajua ni malaika, akakumbuka hadithi alizowahi kusimuliwa za malaika kuwa ni wao ni weupe, na kwasababu hawana dhambi, kila kitu chao ni cheupe.

‘Ina maana nimeshakufa nipo mbinguni,…nipo peponi na malaika’akawaza na kabla hajaweza kuinua kichwa vyema, mara akahisi kuna watu wameshikilia miguuni yake, na sauti zikawa zinaongea, mmoja akasema,;

‘Huyu tusipomfanyia upasuaji, tunaweza tusiwaokoe wote’

Kais akawaza hawa malaika wanataka kumfanya nini, kumfanyia upasuaji, haiwezekani, kwao hakuna kitu kama hicho, wanaamini kuzaa ni kwa njia ya kawaida tu, kuna dawa unakunywa, na haichukui muda kujifungua, na kabla hajajua nini kinachoendelea, akahisi tumbo likaanza kumuua, liliuma sana, maumivui ambayo hakuweza kuyavumilia akaanza kupiga ukulele.

Mmoja wa wale, watu ambao yeye aliwaona kama malaika, wakaja na kumshika vyema, na mmoja akawa kashika sindano,..Kais aliogopa sana, lakini hakuweza hata kujitetea, kwani mwili ulikuwa hauna nguvu hata ya kuinua mkono, kutokana nay ale maumivu, akapigwa sindano, ambayo ilimfanya atulie, na kuzama kwenye giza, …alipozindukana akasikia kitoto kikilia..

‘Mtoto wako mnzuri ana afya njema,..’ akaambiwa, na alipogeuza kichwa pembeni, akaona kitoto kimelazwa kwenye kitanda kidogo pembeni yake. Kilikuwa cheupe, kizuri, akatabasamu, na akainua mkono na kukishika. Baadaye aliwageukia wale watu ambao kipindi cha nyuma aliwaona kama malaika, lakini sasa akili ilikuwa imetulia, na ile hali ya mwanzo aliiona kama ndoto, akasema; kusoma zaidi ingiahttp://miram3.blogspot.co.uk/


"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima

Sunday 18 November 2012

Nawatakia J'Pili yenye Nuru;Burudani-Bahati Bukuku - Yehova na Nyingine Nyingiii!!!!!



Wapendwa;Nawatakia J'Pili yenye Nuru na Neema.

Ondoka,uangaze;kwa kuwa Nuru yako imekuja,Na utukufu wa BWANA umekuzukia.

Neno La Leo ISAYA:60:1-6;Maana tazama,giza litafunika Dunia,Na giza kuu litazifunika kabila za watu;Bali BWANA atakuzukia wewe,Na utukufu wake utaonekana juu yako.


"Swahili NA Waswahili" Mbarikiwe Woooote.

Friday 16 November 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-Mapishi ya Country salad - Recipe of (Swahili)!!!!!!

Waungwana;"Jikoni leo" si wengine ni "Tupike Pamoja," Walipotea kidogo lakini waswahili wanasema kinya kingi kina.............basi wamerudi tena kwa kishindo.

Nisiwachoshe kwa maneno meeengi.Fuatana nasi katika Pishi la Leo ni "Country Salad" ...

Haya mambo hayo...ukitaka kujua zaidi usisite ingiaTupike Pamoja au www.tupikepamoja.com            

"Swahili NA Waswahili"Karibuni Woote!!!
 

Thursday 15 November 2012

Wa-Afrika na Sherehe zao;Leo Ma-Arusi wa Leo wanavyo Jimwaga!!!!!

S n W
Waungwana; vipi Maarusi wa leo wanavyojimwaga/cheza,changamka? inapendeza au inachukiza? 

Ma-Arusi wa Leo wanafuraha sana na wanajimwaga vilivyo, yaani wanaonyesha furaha zao kabisa na ukichukulia siku kama hizi hazijirudii.
Unafikiri kwanini wanakuwa hivi jee, wamechaguana wenyewe,wanakwenda na wakati,hawana Aibu,wamengojea kwa muda mrefu kuwa MKE/MUME au............?

Vipi wa zamani ni kilio mtindo mmoja jee wengi wao wamelazishwa,Upweke wa kuwa mbali na familia,Furaha iliwazidi,Kutojuana/kuchaguliwa,wali-Olewa/Oa wakiwa wadogo  Au......?

"Swahili na Waswahili" Karibuni woooote!!!!!!

Monday 12 November 2012

Da'CHIKU ETUTU'S BABY SHOWER,Waalikwa[2]!!!!


                                          Da'Chiku MUNGU alikuingiza vyumba vyote....Mrembo mke wa Etutu!!

















Wapendwa mmetokelezea/Pendeza sana na MUNGU awape Moyo wa ushirikiano Daima na Mapenzi.
                                        Swahili na Waswahili Tunakutakia kila lililo Jema na Baraka.MUNGU azidi kuwabariki  katika Uzao wenu.
Bibi na Bwana ETUTU..Wanawashukuru Wooote.
         Picha na Mpiga wetu Bai mwana wa Mussa,Shukrani Mingi.

Mapenzi Na Wapenzi;Burudani-Ali Kiba-MAPENZI YANA RUN DUNIA - Diamond na KIZAIZAI!!!!

Waungwana;" Mapenzi na Wapenzi".Mapenzi ni Raha Karaha?  jee Unampenda uliye naye au Unajikaza tuu ili siku ziende?

 kwanini  baadhi ya Wanawake wengi wanalaumiwa na baadhi ya waume zao eti wakisha zaa/kupata mtoto Mapenzi yanapungua kwa MUME?

 Jee kuna ukweli au Wanaume wanawivu hata kwa Watoto wao?

Karibu sana kwa Maoni/Ushauri na kuelimishana kwa Upendo.

Diamond anasema.....Kizaizai oohh Mapenzi yanauma eee nyie Mapenzi karahaaa Kizaizai.........
Ali Kiba anatuambia
......aaa aEeehhh eeeooohh ....Unatema BIG kwa Karanga za Kuonjeshwaaaa..Mapenzi yana Run Duniaaaaaa..

Mhhhhhh wewe UNASEMAJEE........

 
"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima
.
S n W

Sunday 11 November 2012

Wanawake Waswahili Wa Coventry Wamtakia Kheri na Baraka;Mpendwa wao-Chiku Etutu's Baby Shower!!!!!![1]

           Mwenyewe da'Chiku katika pozi mwanana.



Pozi tofauti mama Kitumbo!

              Mikeki 
                  Kula baba kama si wewe nisingeitwa mama..
                        Kula mama kama si wewe nisingekuwa baba......






                      Zawadi na mkono wa kheri na baraka kutoka kwa Waungwana.....[Eeehh dada yangu unavisa wewee wapi Nana]hahahaaaa
k
Kamati ya Shughuli hii,Mnatishaaaa Cov Mamazzzzzzzz[WWWCUK]
              Picha na Mpiga Picha wetu BAI Mwana wa Mussa mamaaa ya Cov..

Usicheze mbali picha zitaendeleaa nani kavaa nini na nani alikuwepo nani katokelezeaaaaa?

       "Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.