Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 28 February 2012

Jikoni Leo -Bamia,Kwanini Wanaume wengi Hawali?Burudani- Nshomile!!!!!

Bamia za kukaanga na mafuta,Hapo naongeza na nyanya.

Mimi hupenda na Ugali.



Bamia za Kuchemsha[Mrenda]
Waungwana hivi ni kwanini mboga hii ya Bamia Wanaume wengi Hawali/Hawaipendi? Jee wewe Unapenda Bamia na Unapikaje?Wengine wanatia na nyanyachungu,Kwenye Samaki Wakavu na....Jee Unaweza kula Bamia na Ugali wa Muhogo? Karibuni sana!!!!

Monday 27 February 2012

Mtoto Wetu Leo-Sabrina!!!!!!

katika Poziii
Alikuwa MC
Mifugo ni adimu kwao,weee paka njoo hapa!!!
Kwanini jana ulikimbia?utahama humu oohh,haya niamkie..
                                          Kama hutaki ngoja nikuamkie wewe!!!
Waswahili wanasema vyakurithi Vinazidi jee ni kweli?
Jee Watoto wanaweza kurithi Vituko,Ucheshi,Upole na Ugomvi?
Na kwanini baadhi ya misemo ya watoto inafanana kama Maji,kuwa Mma,Nyonyo na.....?
Kunawakati unaweza cheka na Mtoto mdogo au Kulia kwa mambo yake!!!!
Wengine hawapendi kula,kulala Usiku na mambo mengi.Pia kuwa na Mtoto kuna Raha yake!!

Kama wewe huna Mtoto na Unahitaji,Mungu yu Mwema  Uskate Tamaa!!!!

Sunday 26 February 2012

Nawatakia J'pili Njema,Burudani-Unastahili Kuabudiwa !!!!

Naye alipowaona Makutano,alipanda mlimani;na alipokwisha kuketi,Wanafunzi wake walimjia;.Akafumbua kinywa chake,akawafundisha,akisema,Heri walio maskini wa Roho Maana ufalme wa mbinguni ni wao.Heri Wenye huzuni;Maana hao Watafarijika.Neno la  Leo;Mathayo Mtakatifu:5;1-16.Mbarikiwe sana!!!

Saturday 25 February 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Muzina yaTabu ley,Zaiko Langalanga na Bozi boziana!!!

Leo nimekurudisheni nyuma kidoogo,Vipi  kuhusu vibao hivi leo,kuna lolote unalokumbuka?Twende Sote na Burudani !!!!!Nawatakia week end Njema.

Wednesday 22 February 2012

Wanawake na Mitindo,Leo Uvaaji wa Miwani!!!!



Nimatumaini yangu woote wazima,Haya Waungwa vipi kuhusu Wanawake wavaapo Miwani,Nikuongeza Urembo,Kuvutia,Haiba,Kujikinga na jua au Wanaficha kitu,Wanaaibu,Wanajishaua? Na jee Wanaona vizuri kweli ?Wewe /Mkeo unapenda kuvaa/Avae Miwani na kwasababu ipi?


Karibu sana Waungwana.

Tuesday 21 February 2012

Nderemo na Vifijo Leo -Rwanda, Ni da'Rubango apata Mwenza!!!!!!




















Hayawi hayawi sasa Yamekuwa! dada Rubango na Mumeo Hongereni sana kwa kuwa MKE na MUME!!
Mungu asimamie maisha yenu yawe yenye Baraka na Amani.

UJumbe;dada Rubango na  nawatakia maisha mema yenye Furaha na Upendo wewe na Mumeo,Mungu awenanyi kila iitwapo Leo,Nawapenda sana.
   Wako Neema Nyanyile
      COVENTRY.

Sunday 19 February 2012

Nawatakia j'pili Njema,kibao kutoka Kijitonyama-Masiah wanyi!!!!!!!


Ni juma pili nyingine tena Mpendwa,Tunamshuru sana Mungu kwa kututunza siku zote,Mimi na Familia yangu tunawataki kila lililo jema na Baraka,Amani,Upendo,Umoja na Utuwema.Mungu awe nawe kila inapotwa Leo.Tusamahe na kuomba Msamaha pale tunapokosana/kukwazana.Mungu ni Pendo Apenda Watu.Mimi nakupenda wewe!!!.Twende Sote sasa,PAMOJA SANA!!!!!

Friday 17 February 2012

Waswahili na Maisha yao - Washington DC,Marekani na Mzee Yusuf,Nyumbani kwa Missy Temeke!!!

Haya wapendwa waswahili na  Maisha yao,Makhanjumati/Vyakula kwa wingi,Burudani, watu na furaha.ilikuwa siku ya Wapendanao,Wao waliamua kupendana kihivyo,Hayo yote ni Mapenzi,Umoja,Kufurahi ,Kushirikiana na Wengine!.Ukitakata kujua zaidi ingi. http://swahilivilla.blogspot.com

Tuesday 14 February 2012

Siku kama ya Leo dada Nadia Nyembo Alizaliwa!!!!

Siku kama ya leo familia ya Bibi na Bwana Nyembo Fundikira, walipata mtoto wa kike na wakamwita NADIA!!.Leo dada Nadia ametimiza miaka 2.''Chimami'' tunakutakia kila lililojema maishani mwako,Mungu awe nawe daima,Uwe baraka kwa Wazazi,Ndugu,Jamaa ,Marafiki na Watu wooote.


Familia ya Fundikira,Jumaa,Tuwa na Kiwinga,Tunaungana pamoja katika kukutakia kheri na kumuomba Mungu asimamie makuzi yako.


Hongera sana'' VALENTINE''NADIA.

Monday 13 February 2012

Wanawake Mpo?Balozi wa Tanzania Mh. Mwanaidi Maajar!!!!!

Hongera Mange/U-Turn Blog. Tunapo kula na kunywa,Tusisahau na Wenye Shida!!!!!




Hongera Mange/U-Turn Blog na Wooote mlioshiriki/Kufanikisha jambo hili,Mungu awabariki sana.
Nijambo jema tena lenye maana na Mfano mzuri.Watoto Yatima,Wasiojiweza,Wenye hali/Maisha magumu ni Jukumu letu sote,kuwasaidia na kuwanao pamoja na kuwapa Upendo.
Mungu ni Pendo Apenda Watu!!!!!!Pamoja.

Kuona/Kujua zaidi, Ingia. hptt://www.U-turn.co.tz.

Mablogger na Mahojiano na Prof. Ibrahim Lipumba (Pt I)!!!!!!

Saturday 11 February 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Gere,Warumba Mpoo?kutoka kwa Wana Njenje!!

OMARY MJENGA AKIWA NA FAMILIA YA BALOZI MDOGO WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA MH. CHABAKA KILUMANGA




Kutoka kulia ni Mtoto wa Balozi Mdogo nchini Uingereza anaitwa Maya, anaefuata ni Mwakilishi wa UNOPS Siera Leone Ndugu Omary Mjenga, anaefuata ni Mke wa Balozi Mdogo Uingereza, anaefuata ni Balozi mdogo wa Tanzania Nchini Uingereza Mh. Chabaka Kilumanga, na wa mwisho ni Aziz Msuya mtoto wa Balozi wetu Pretoria Afrika ya kusini.
Mjenga yuko Nchini Uingereza kuhudhuria moja Kikao ambacho kiko ndani ya majukumu yake ya kikazi.

Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog.
Ahsante sana.

Friday 10 February 2012

Harambee ya Msiba wa Mtanzania Mwenzetu,Washington DC.Kutoa ni Moyo!!!

Marehemu Christavina Kusaga Cryor
Familia ya Kusaga inawaomba watanzania wote walioko Marekani na hasa eneo la Washington DC na vitongoji vyake kushirikiana nao katika harambee (fundraising) ili kupata pesa ya mazishi ya mtanzania mwenzetu Christavina Kusaga Cryor aliyefariki February 7, 2012 kwa sarakani ya utumbo.

Marehemu alikuwa akiishi Landover, MD. Ameacha mume na watoto wawili- mvulana wa miaka 4 na msichana wa miaka 2. Alikuwa akisumbuliwa na cancer ya utumbo.

Tafadhali fika tushirikiane kusaidia mume wake na watoto na familia wamzike mpendwa wao. Jumla ya gharama za mazishi ni $11,000, na mpaka sasa tuna $3,000. Tunashukuru kwa waliokwisha saidia.

Harambee itakuwa Jumapili February 12, 2012, kuanzia saa 8.30 mchana (2.30pm).

Anuani ni: 3621 Campus Drive, College Park, MD 20740.

Kwa wale wa mbali au wasioweza kuhudhuria tafadhali tusaidie mchango wako kwa kutumia Capital One Bank, Account# 1351500235; Routing # 255071981. Jina la Account ni Lavorn Cryor. Tafadhali eneza habari hii kwa ndugu na marafiki wote. Asanteni sana kwa ushirikiano wenu katika wakati huu mgumu.

Kwa habari zaidi mpigie: Magoma (202.607.1976); Adelaida (240.602.3183); Matinyi (301.792.2832); Mkakile (240.938.3177); Teddy (301.254.4169); Makaya (202.460.1044); Latifah (240.603.7353); au Rebecca (202.580.4648).

M/Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amen

Thursday 9 February 2012

Wednesday 8 February 2012

Waswahili na Maisha yao -Nyimbo za Mipasho[Rusha Roho]!!!!!!!

Waungwana vipi kuhusu nyimbo hizi za MIPASHO,[RUSHA ROHO]Zinajenga au Zinabomoa?jee nahii michezaji vipi?kwani mpaka tukukatike na kugusana?jee hizi  ni Taarabu,Chakacha au ni Mitindo gani?Wenyewe wanaema meseji Send wewe unasemaje?Duuhh SWAHILI NA WASWAHILI AU VIPI? KARIBUNI SAAANA.

Tuesday 7 February 2012

Wanawake na Mitindo ni Mswahili-Maskat Designs!!!


Leo wanawake na Mitindo ni da'Maskat,yeye ni Desings,mimi nimevutiwa sana na kazi zake.
unaweza kuangalia zaidi kazi zake kupitia http://www.zib-fashion.blogspot.com.

Jikoni Leo ni Chai ya Waswahili!pata na Burudani; Ray C-Mama Ntilie!!!!!!!


Waungwana leo tuangalie chai za Waswahili.Unapenda kufumgua kinywa/Chai na nini Asubuhi?
Kuna wanaopenda Viporo,Vitu vya kuchemsha,Vyakukaanga,Kuungwa,Uji,Supu na vingine Vingii.
Jee upo kwenye lipi? na jee hapo ulipo unavipata kwa Urahisi kama kununua vilivyopikwa au unapika mwenyewe?na jee Kifungua kinywa chako kina Faida kiafya?.
Karibuni sana Waungwana katika Yote!!!!

Sunday 5 February 2012

Nawatakia J'Pili Njema na Burudani-YUMWEMA ANGEL CHOIR

Hali ya Hewa baadhi ya Sehemu iko hivi,Isiwe sababu ya kutokwenda  kwenye Nyumba za ibada Wapendwa,Mungu awabariki sana, na Muwe na J'Pili njema yenye Baraka,Amani na Upendo. Mungu yu Mwema Maishani mwetu,wenyekuamini hivyo na Tuseme AMINA!!

Friday 3 February 2012

Dada huyu Auwawa Kikatili na Rafiki yake wa Kiume!!!!

Da'Rudo Mawere Enzi ya Uhai wake.


Dada huyu ameuwawa na aliyekuwa Rafiki yake wa Kiume/Mpenzi wake, Jason Dube,Naye mwanaume huyo baada ya kufanya mauaji  hayo  huko Ireland,akarudi U.K. naye amekutwa amejiua.Kaka Jason alikuwa akiishi hapa Coventry,Poleni sana Familia ya Dube na Mawere.Habari kamili unaweza kuipata hapa;http://www.nyasatimes.com/malawi/2012/01 au htt://www.independent,pia ukiingia face book andika Rudo Mawere pia unaweza kupata maelezo vizuri.Habari hii imetuhuzunisha sana kwani huyu mwanaume tulikuwa tunamfahamu.