Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 4 August 2011

Mswahili Wetu Leo ni Bi Zaituni wa Mrisho; Anaishi ILALA!!!!!!!

Bi Zaituni wa Mrisho katika Picha ndiyo Mswahili wetu wa Leo,Anaishi Ilala mtaa wa Mwanza.
Bibi huyu ana hadithi na habari nyingi sana za maisha na siasa,Leo  anaongelea kuhusu ULIMBUKENI!!
Anasema watu wanaharibikiwa sana kwa kukataa yote ya zamani na kuingia kwenye mitindio mipya tuu,kwamba si yote mapya mabaya la! bali na yazamani pia yakumbukwe hasa yale mazuri, Na tuwe tunawafundisha watoto wetu,Asema utakuta mtu kazaliwa na kukulia kwenye familia ya kiswahili lakini mwaka mmoja tuu akienda nje ya nchi,anajifanya kasahau kabisa Kiswahili, mara oohh yah oohh yes, pia hawapendi hata watoto wao wanaowazaa huko au kukulia huko kuwafundisha KISWAHILI, tena na kujisifia wakipiga simu huku nyumbani mwanangu hajui/kasahau kabisa Kiswahili,Kama baba na mama Waswahili iweje mtoto wako asiongee Kiswahili?
Mwisho anawatakia Waislam wote duniani Funga njema yenye baraka na amani.

Nami nasema Ahsante sana bi Zaituni  wa Mrisho na kaka Mtaruke[mjuukuu wa binti Mrisho] yeye ndiye aliyetuunganisha na BIBI huyu.
Haya wapendwa Waswahili neno hilo kutoka kwa bibi unalionaje? Karibuni sana kwa kuchangia,kuelimishana  na.....
Kama una lolote jema na kuelimishana , Unataka kuwaambia Waswahili wenzio karibu  sana unaweza kutumia email hii Rasca@hotmail.co.uk. katika kipengele hiki cha Waswahili na Maisha yao ndani ya Swahili na Waswahili.
Nawatakia Swaumu njema kwa Waliofunga!!

3 comments:

emu-three said...

Nashukuru ndugu yangu kwa maneno hayo ya hekima toka kwa bibi na familia kwa ujumla. Ni kweli mkataa mila ni mtumwa!

Simon Kitururu said...

BI Zaituni kamaliza!

Rachel Siwa said...

emu-tree ndugu yangu na kaka wa mimi Kitururu bi Zetty kiboko!