Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 13 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..13...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Ni siku nyingine tena Mungu ametuchagua na  ametupa Kibali cha kuendelea kuiona siku hii...
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako..

Asante kwa ulinzi wako usiku na wakati wote..
Asante kwakutuamsha salama na wenye Afya..

Tunashukuru na kukusifu Daima..
Tunashuka mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..

Utuepushe katika majaribu na utuokoe na yule mwovu na kazi zake..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo..yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote,Tupate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..

Ukatubariki na kubariki vyote tunavyoenda kufanya/kutenda...

kuingiakwetu/kutoka kwetu na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Mfalme wa Amani ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..

Tazama wenye shida/tabu,wanaopitia magumu/majaribu,waliokatika vifungo mbalimbali.. Baba wa mbinguni nyoosha mkono wako wenye nguvu ,ukawaokoe katika mapito yao na ukawaponye kimwili na kiroho pia,ukawajibu na kuwafuta machozi wote wanaokuomba na kukukimbilia..Mungu ukaonekane kwenye mahitaji yao..
Na ukawape sawasawa na mapenzi yako..

Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia..
tukatii na kufuata Neno lako..
Tukaishi kwa kukutegemea wewe zaidi..
ukatupe maarifa na ubunifu katika kazi zetu,Biashara zetu..
popote tupitapo ukaonekane Mungu wetu..
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu na ukatupe sawasawa na mapenzi yako...


Bwana Mungu amenipa ufasaha wa lugha, niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubuhi hunipa hamu ya kusikiliza anayotaka kunifunza. Bwana Mungu amenifanya msikivu, nami sikuwa mkaidi wala kugeuka mbali naye. Mgongo wangu niliwaachia walionipiga, mashavu yangu waliozingoa ndevu zangu; walioniaibisha na kunitemea mate, sikujificha mbali nao. Bwana Mungu hunisaidia, kwa hiyo siwezi kufadhaika. Uso wangu nimeukaza kama jiwe; najua kwamba sitaaibishwa. Mtetezi wangu yuko karibu. Ni nani atakayepingana nami? Na aje tusimame mahakamani. Adui yangu ni nani? Na ajitokeze mbele basi. Tazama Bwana Mungu hunisaidia. Ni nani awezaye kusema nina hatia? Maadui zangu wote watachakaa kama vazi, nondo watawatafuna. Nani kati yenu amchaye Mwenyezi-Mungu? Nani anayetii maneno ya mtumishi wake? Kama yupo atembeaye gizani bila taa, amtumainie Mwenyezi-Mungu, na kumtegemea Mungu wake. Lakini nyinyi mnaowasha moto, na kujifanyia silaha za mienge, tembeeni kwa mwanga wa moto huo, miali ya moto mliowasha nyinyi wenyewe. Mtakachopata kutoka kwa Mwenyezi-Mungu ni hiki: Nyinyi mtalala chini na mateso makali.


Tunakutumainia wewe siku zote na kukusifu Daima..
Tunakushukuru katika yote na kukutukuza Mungu wetu..
Tunayaweka haya yote mimkononi mwako Mungu wetu..
Tukiamini wewe ni Mungu wetu na hatuna Mungu mwingine..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!

Niwashukuru sana wote mnaondelea kupita hapa..
Mungu akaonekane kwenye maisha yenu..
msipungukiwe katika mahitaji yenu na akawape sawasawa na mapenzi yake..
Nawapenda.

Sheria kuhusu ukoma

1Mwenyezi-Mungu aliwaambia Mose na Aroni, 2“Iwapo mtu yeyote atakuwa na uvimbe au upele au kipaku mwilini mwake, ikadhihirika kwamba ni ukoma, basi, ataletwa kwa kuhani Aroni au mmoja wa wanawe aliye kuhani. 3Kuhani atapakagua mahali palipo na ugonjwa na ikiwa nywele za mahali hapo zimebadilika kuwa nyeupe na ugonjwa wenyewe ukionekana kuwa uko ndani zaidi ya ngozi ya mwili wake, basi, huo ni ukoma. Kuhani akimaliza kumkagua, hivyo atatangaza kuwa mtu huyo ni najisi. 4Lakini ikiwa kipele hicho, ingawa cheupe hakikuingia ndani sana ya ngozi na wala nywele za mahali hapo hazikubadilika kuwa nyeupe, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa muda wa siku saba. 5Siku ya saba, kuhani atamwangalia tena mtu huyo, na ikiwa, kulingana na uchunguzi wa kuhani, ugonjwa huo haujaenea kwenye ngozi yake, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku nyingine saba.
6“Kuhani atamkagua tena mtu huyo siku ya saba. Kama kulingana na uchunguzi wake, ile sehemu ya ugonjwa imefifia na ugonjwa haujaenea, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi; huo ni upele tu. Mtu huyo atafua mavazi yake, naye atakuwa safi. 7Lakini upele huo ukiwa umeenea kwenye ngozi, baada ya mtu huyo kujionesha kwa kuhani kwa ajili ya kutakaswa kwake, basi, atakuja tena kwa kuhani. 8Kuhani atamwangalia tena, na kama ule upele umeenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; huo ni ukoma.
9“Kama mtu ameshikwa na ukoma, ataletwa kwa kuhani. 10Kuhani atamwangalia na kama kuna uvimbe mweupe ambao umezifanya nywele zake ziwe nyeupe na uvimbe huo umegeuka kuwa kidonda kibichi, 11huo ni ukoma wa muda mrefu. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Hakuna haja ya kumweka mtu huyo kwa uchunguzi kwani yu najisi tayari. 12Kama ukoma umemshika na umeenea mwili mzima, toka utosini hadi nyayoni kama atakavyoona kuhani, 13hapo kuhani atamwangalia. Kuhani akiona kuwa ukoma umemwenea mwili mzima, basi, atamtangaza mtu huyo kuwa safi kwa sababu mwili umegeuka kuwa mweupe na hivyo mtu huyo yu safi. 14Lakini kukionekana mwilini mwa mtu huyo kidonda kibichi, basi, mtu huyo atakuwa najisi. 15Kuhani ataangalia hicho kidonda kibichi na kumtangaza kuwa ni najisi kwa sababu huo ni ukoma. 16Lakini hicho kidonda kikigeuka tena kuwa cheupe, mtu huyo atarudi kwa kuhani. 17Kuhani atamwangalia na akiona kuwa kimegeuka kuwa cheupe, basi, atamtangaza mtu huyo kuwa safi.
18“Kama mtu ameshikwa na jipu, nalo limepona, 19lakini mahali pale lilipokuwa jipu pamegeuka kuwa uvimbe mweupe au kuwa pekundu lakini peupe kiasi, ni lazima kumwonesha kuhani. 20Kuhani atamwangalia huyo mtu. Kuhani akiona pamegeuka kuwa na shimo na nywele za mahali hapo zimegeuka kuwa nyeupe, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; huo ni ugonjwa wa ukoma ambao umetokana na jipu. 21Lakini kama kuhani atamwangalia huyo mtu na kuona kuwa nywele za mahali hapo si nyeupe na wala hakuna shimo, ila pamefifia, basi, atamtenga huyo mtu kwa muda wa siku saba. 22Kama ugonjwa huo utaenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; sehemu hiyo ina ugonjwa. 23Lakini, kama ile sehemu haijaenea, basi, lile ni kovu la jipu tu. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi.
24“Au, Iwapo kuna mahali palipoungua na ile nyama mbichi imegeuka kuwa nyekundu-nyeupe au ni nyeupe, 25kuhani atapaangalia. Kama akiona kuwa nywele zimegeuka kuwa nyeupe na pana shimo, basi, huo ni ukoma. Ukoma huo umejitokeza kwa njia ya mahali hapo palipoungua. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; kwani anao ugonjwa wa ukoma. 26Lakini kama kuhani akiona kuwa nywele za mahali hapo si nyeupe na hakuna shimo ila pamefifia, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa muda wa siku saba. 27Siku ya saba kuhani atamwangalia. Kama umeenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; kwani anao ugonjwa wa ukoma. 28Lakini, kama ile alama haijaenea, ila imefifia, huo ni uvimbe uliotokana na kuungua; basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi; kwani hilo ni kovu la kuungua.
29“Kama mtu yeyote mwanamume au mwanamke, ana kidonda kichwani au kidevuni, 30kuhani atauangalia ugonjwa huo. Iwapo kuhani ataona kuwa kuna shimo na nywele ni manjano na nyembamba, basi, atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; kwani huo ni upele na ni ukoma wa kichwa au wa kidevu. 31Kama kuhani ataona kuwa hakuna shimo na nywele si nyeusi, basi kuhani atamtenga mtu huyo kwa muda wa siku saba. 32Siku ya saba kuhani atakiangalia kile kidonda. Kama kidonda hicho hakijaenea na hakuna nywele zenye rangi ya manjano wala hakuna vipele vyovyote mahali hapo, basi, 33mtu huyo atanyoa nywele au ndevu zake. Lakini mahali pale penye vipele hatapanyoa. Kisha kuhani atamtenga mtu huyo kwa muda mwingine wa siku saba. 34Siku ya saba, kuhani ataviangalia vile vipele. Iwapo kuhani ataona kuwa vipele hivyo havikuenea kwenye ngozi na wala havikwenda ndani ya ngozi, basi, atamtangaza mtu huyo kuwa safi. Mtu huyo atafua mavazi yake, naye atakuwa safi. 35Lakini iwapo vipele hivyo vimeenea baada ya kutakaswa, 36mtu huyo ataangaliwa na kuhani na ikiwa vimeenea kwenye ngozi, kuhani hatahitaji kutafuta nywele zenye rangi manjano; mtu huyo atakuwa najisi. 37Lakini iwapo kuhani ataona kuwa vile vipele vimepona na nywele nyeusi zimeota mahali hapo, basi, vidonda hivyo vimepona, basi, mtu huyo ni safi. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi.
38“Kama mtu yeyote, awe mwanamume au mwanamke, ana alama nyeupe mwilini mwake, 39kuhani atamwangalia mtu huyo. Iwapo kuhani ataona kuwa alama hizo ni nyeupe kiasi, huo ni upele wa kawaida; mtu huyo ni safi.
40“Kama mwanamume amepata upara, yeye ni safi kwani ana upara tu. 41Iwapo upara huo umetanda tangu nyuma mpaka mbele mtu huyo ana upara tu na yu safi. 42Lakini kama kwenye kichwa penye upara au kwenye paji la uso penye upara kuna alama nyekundu-nyeupe, huo ni ukoma unaotokea kwenye upara wake kichwani au kwenye paji lake. 43Kuhani atamwangalia. Iwapo kuhani ataona kuwa huo uvimbe ni mwekundu-mweupe kwenye upara au kwenye paji lake na unaonekana kama ukoma kwenye ngozi yake, 44basi, mtu huyo ana ukoma; yeye ni najisi. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Ugonjwa wake upo kwenye kichwa chake.
45“Mwenye ukoma yeyote atavaa nguo zilizochanika, nywele zake hatazichana, na mdomo wake wa juu ataufunika na atapaza sauti akisema, ‘Mimi ni najisi, mimi ni najisi.’ 46Ataendelea kuwa najisi kwa muda wote alio na ugonjwa huo. Yeye ni najisi; naye atakaa peke yake nje ya kambi.”

Sheria kuhusu upele katika nguo

47“Kama kuna namna ya upele wa ukoma kwenye vazi, liwe la sufu au kitani, 48vazi hilo liwe limefumwa au limesokotwa kwa kitani au sufu au ni vazi la ngozi ya aina yoyote ile, 49iwapo upele huo una rangi ya kijani au nyekundu katika vazi hilo, basi, vazi hilo lina upele. Kwa hiyo ni lazima kumwonesha kuhani. 50Kuhani atauangalia upele huo na kuliweka vazi hilo kando kwa muda wa siku saba. 51Siku ya saba atauangalia upele huo. Ikiwa upele huo umeenea katika vazi hilo, liwe ni la kufuma au kusokotwa au la ngozi au la ngozi ya aina yoyote ile, vazi hilo lina upele. Hivyo vazi hilo ni najisi. 52Kuhani atalichoma moto vazi hilo kwani lina namna ya upele wa ukoma.
53“Kama kuhani ataona kuwa upele haukuenea katika vazi, basi, 54ataamuru vazi hilo lifuliwe na kuwekwa kando kwa muda mwingine wa siku saba. 55Kuhani ataliangalia hilo vazi baada ya kuoshwa. Ikiwa ile alama haijabadilika rangi yake hata ingawa upele haukuenea, basi, vazi hilo ni najisi. Vazi hilo utalichoma moto, iwe alama ya upele ipo nyuma au mbele ya vazi hilo.
56“Kama kuhani ataona kuwa ile alama imefifia baada ya kufuliwa, basi atararua ile sehemu iliyo na namna ya upele wa ukoma. 57Kisha, ikiwa hiyo alama inaonekana tena baadaye katika vazi lililofumwa au lililosokotwa au katika kitu chochote cha ngozi, basi upele umeenea. Hapo vazi hilo utalichoma moto. 58Lakini vazi ambalo upele umetokea baada ya kulifua itabidi lifuliwe mara ya pili na hivyo lipate kuwa safi.” 59Hiyo ni sheria kuhusu namna ya upele wa ukoma unaotokea katika vazi la sufu au kitani au lililofumwa au lililosokotwa au la ngozi. Kwa njia hiyo mtaweza kupambanua kati ya vazi lisilo najisi na lile lililo najisi.

Mambo Ya Walawi 13;1-59

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 12 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..12...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote..

Asante Mungu wetu Baba yetu,Asante kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako usiku na siku zote umekuwa nasi Jehovah..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa Kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwa uwezo wetu wala nguvu zetu ni kwa Neema/Rehema yako tuu Mungu wetu sisi kuwepo leo hii na kuweza kufanya yote haya tufanyayo..

Tazama Jana imepita Baba wa Mbinguni Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..
Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Yahweh..

Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Roho mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Utuepushe na majaribu ya yule mwovu na kazi zake..Utuokoe na kutufunika na Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase  Miili yetu na Akili zetu kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Tukaanze nawe Bwana wetu katika wiki hii..yote tunayoenda kufanya/kutenda yakaendane na matakwa yako Jehovah..

ukaonekane kwenye maisha yetu Yahweh..!ukatupe hekima,Busara katika kuamua na kutenda,tukapate kutambua/kujitambua..
Tukaelewe na kulijua Neno lako,Tukafuate na  tukatii sheria zako na Amri zako

Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Kila kuhani mkuu ambaye huchaguliwa miongoni mwa watu hupewa jukumu la kushughulikia mambo ya Mungu kwa niaba ya watu, kutolea zawadi na tambiko kwa ajili ya dhambi. Maadamu yeye mwenyewe ni dhaifu, anaweza kuwatendea kwa huruma wale wasiojua kitu na wanaofanya makosa. Kwa sababu hiyo anapaswa kutoa tambiko si tu kwa ajili ya watu, bali pia kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe. Hakuna mtu awezaye kujifanya mwenyewe kuwa kuhani mkuu. Kila mmoja huteuliwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kama alivyokuwa Aroni. Hali kadhalika naye Kristo; yeye hakujitwalia mwenyewe heshima ya kuwa kuhani mkuu, bali Mungu alimteua na kumwambia: “Wewe ni Mwanangu; mimi leo nimekuwa baba yako.” Alisema pia mahali pengine: “Wewe ni kuhani milele, kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.” Yesu alipokuwa anaishi hapa duniani, kwa kilio kikuu na machozi, alisali na kumwomba Mungu ambaye alikuwa na uwezo wa kumwokoa kifoni; naye alisikilizwa kwa sababu ya kumcha Mungu. Lakini, ingawa alikuwa Mwana wa Mungu, alijifunza kutii kwa njia ya mateso. Na alipofanywa mkamilifu, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii, naye Mungu akamteua kuwa kuhani mkuu kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.
Ukatuongoze ee Mungu wetu na ukatubariki na kubariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo nasi utupe neema ya kuwabariki wenyekuhitaji..

 Neno lako likawe Mwanga kwenye maisha yetu likawe faida na likatufae sisi na wengine pia..
Wale walio asi wakapate kurudi kundini na kuwa pamoja katika kuamini na kujifunza zaidi..



Tunayo mengi ya kusema juu ya jambo hili, lakini ni vigumu kuwaelezeni, kwa sababu nyinyi si wepesi wa kuelewa. Kwa wakati huu nyinyi mngalipaswa kuwa waalimu tayari, lakini mnahitaji bado mtu wa kuwafundisheni mafundisho ya mwanzo juu ya neno la Mungu. Mnahitaji maziwa badala ya chakula kigumu. Kila anayepaswa kunywa maziwa ni mtoto bado, hajui uadilifu ni nini. Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu waliokomaa, waliofunzwa kwa vitendo kubainisha mema na mabaya.

.Baba wa Mbinguni ukaonekane kwenye Maisha yetu na tusipungukiwe na mahitaji yetu..

Tunayaweka haya yote mikononi mwako,Tukiamini wewe ni Mungu wetu hatuna Mungu mwingine..
Yote tuliyoyanena na kutonena Baba unayajua na unatujua kuliko tunavyojijua..
Mungu wetu ukatupe sawasawa na mapenzi yako..


Sifa na Utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..

Amina..!
Mungu aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake..
Niwashukuru sana kwakunisoma/kupita hapa..
Nawapenda.

Kuwatakasa wanawake baada ya kujifungua

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2“Waambie watu wa Israeli hivi: Mwanamke akipata mimba, akajifungua mtoto wa kiume, atakuwa najisi kwa muda wa siku saba kulingana na siku zake zihusikanazo na hali ya wanawake. 3#Taz Mwa 17:12; Luka 2:21 Mtoto huyo atatahiriwa katika siku yake ya nane. 4Kisha mama mtoto ataendelea kuwa najisi kwa muda wa siku thelathini na tatu. Wakati huo, kamwe asiguse chochote kilichowekwa wakfu wala kuingia mahali patakatifu mpaka siku za kutakasika kwake zitakapotimia. 5Lakini, kama amejifungua mtoto wa kike, basi, atakuwa najisi kwa muda wa majuma mawili kama ilivyo anapokuwa katika siku zake. Ataendelea katika kutakasika kwake kwa muda wa siku sitini na sita.
6“Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, iwe amepata mtoto wa kiume au wa kike, atamletea kuhani mlangoni mwa hema la mkutano mwanakondoo wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na kinda la njiwa au hua, kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi. 7Kuhani atamtolea mbele ya Mwenyezi-Mungu na kumfanyia huyo mama ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu. Hivyo huyo mwanamke atakuwa safi kutokana na damu yake. Huo ni mwongozo kuhusu mwanamke yeyote anayejifungua mtoto wa kiume au wa kike.
8 # Taz Luka 2:24 “Kama hawezi kutoa mwanakondoo, basi, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa; mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuondolea dhambi. Kuhani atamfanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.”

Mambo Ya Walawi12;1-8


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 9 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..11...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Ni siku nyingine tena Mungu ametuchagua na kutupa Kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwa uwezo wetu wala si kwa nguvu zetu,si kwamba sisi ni wema sana au wazuri mno kuliko wengine ambao leo hii wapo vitandani,wapo waliotangulia/kufa,wengine wapo hoi hata kuita Mungu au kutubu wameshindwa,wapo wanaotamani kuandika/kusoma kama si kuongea au kuacha wosia/usia kwa wapendwa wao..
Sisi tumempa nini Mungu wetu? ni kwa Neema/Rehema zake Mungu sisi kuwepo na kuwa hivi tulivyo..
Tumshukuru Mungu kwa wema na Fadhili zake na tukatumie nafasi hii aliyotupa vizuri  kwa kutenda yaliyo mema na tuzidi kumtafuta kwa maana anapatikana..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yake..
Asante Mungu wetu na Baba yetu uliye Mbinguni..
Asante kwa kulinzi wako wakati wote na kutuamsha salama..
Tazama Jana imepita Baba wa Mbinguni Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine..

Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mungu wetu, kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakuju/kutojua..Mfalme wa Amani..
Tunaomba nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe nasi waliotukosea..
utuepushe na Majaribu Mungu wetu na utuokoe na yule mwovu na kazi zake..ututakase na kutufunika kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu pia tupate kutambua/kujitambua..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi.
Tunaomba utubariki na kubariki vyote tunavyoenda kufanya/kutenda,na ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo vyote tunavyoenda kugusa/kutumia..
Maisha yetu yapo mikononi mwako Mungu wetu..
yote tuliyoyanena na tusiyo yanena Mungu wetu unayajua na kutujua kuliko tunavyojijua sisi..
Ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo nasi utupe neema ya kuwabariki wanaohitaji..
Baba wa Mbinguni  tusipungukiwe katika mahitaji yetu na ukatupe sawasawa na mapenzi yako..



Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo na ndugu yake Yakobo, nawaandikia nyinyi mlioitwa na Mungu na ambao mnapendwa naye Mungu Baba, na kuwekwa salama kwa ajili ya Yesu Kristo. Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.

Tunarudisha Sifa na utkufu ni wako,Tunakushukuru na kukusifu Daima..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu  hata Milele...
Amina..!!



Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta nyinyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake, kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina.


Asanteni sana wapendwa/waungwana kwa kutembelea hapa..
Mungu akawaongoze katika maisha yenu na msipungukiwe katika mahitaji yenu na akawape sawasawa na mapenzi yake..
Sina neno zuri kwenu zaidi ya kuwaombea na kuwaambia..
Nawapenda.

Wanyama najisi na wasio najisi
(Kumb 14:3-21)

1Mwenyezi-Mungu aliwaambia Mose na Aroni, 2“Wawaambie Waisraeli hivi: 3Kati ya wanyama wote duniani, mmeruhusiwa kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua. 4Lakini msile mnyama yeyote ambaye hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika sehemu mbili, au ambaye kwato zake zimegawanyika lakini hacheui. Msile ngamia, kwani hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika sehemu mbili. Kwenu huyo ni najisi. 5Pelele msimle; yeye hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika; kwenu huyo ni najisi. 6Sungura msimle; yeye hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika; kwenu huyo ni najisi. 7Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu huyo ni najisi. 8Kwa sababu wanyama hao ni najisi msile nyama yao wala msiguse mizoga yao.
9“Samaki yeyote wa baharini au mtoni mwenye mapezi na magamba, mnaweza kumla. 10Lakini chochote kinachoishi baharini au mitoni, ambacho hakina mapezi wala magamba, yaani viumbe vyote viendavyo majini na viumbe vingine vyote viishivyo majini ni najisi kwenu. 11Viumbe hivyo vitakuwa daima najisi kwenu. Msile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao kwani ni najisi. 12Chochote kinachoishi majini ambacho hakina mapezi na magamba ni najisi kwenu.
13“Ndege wote wafuatao ni najisi kwenu; hivyo msile: Tai, furukombe, kipungu, 14mwewe, aina zote za kozi, 15aina zote za kunguru, 16mbuni, kirukanjia, dudumizi, aina zote za kipanga, 17bundi, mnandi, bundi kubwa, 18mumbi, mwari, mderi, 19korongo, aina zote za koikoi, hudihudi na popo.
20“Wadudu wote wenye mabawa na waendao kwa miguu minne, hao ni najisi kwenu. 21Lakini, baadhi ya wadudu wenye mabawa na wanakwenda kwa miguu minne ya kurukia ardhini mnaweza kula. 22Hao ni: Kila aina ya nzige, kila aina ya senene, kila aina ya panzi na kila aina ya parare. 23Lakini wadudu wengine wote wenye mabawa na miguu minne ni najisi kwenu.
24“Kugusa wanyama fulanifulani humfanya mtu kuwa najisi; yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni. 25Mtu akichukua sehemu ya mizoga yake atakuwa najisi mpaka jioni, na mavazi yake ni lazima yafuliwe. 26Mtu yeyote akigusa mnyama mwenye kwato zilizogawanyika lakini hacheui, mtu huyo atakuwa najisi. 27Wanyama wote waendao kwa vitanga vyao ingawa wana miguu minne, ni najisi kwenu; na yeyote atakayegusa mzoga wa mnyama kama huyo atakuwa najisi mpaka jioni. 28Mtu yeyote anayebeba mzoga atakuwa najisi, naye atasafisha mavazi yake. Hao ni najisi kwenu.
29“Viumbe vifuatavyo ni najisi kwenu: Kicheche, panya, kila aina ya mjombakaka, 30guruguru, kenge, mijusi, goromwe, na kinyonga. 31Hao wote ni najisi kwenu na yeyote atakayegusa mizoga yao, atakuwa najisi mpaka jioni. 32Ikiwa mzoga wa viumbe hao unakiangukia kitu chochote, kiwe ni kifaa cha mbao au vazi au ngozi au gunia au chombo chochote kitumiwacho kwa kusudi lolote lile, chombo hicho kitakuwa najisi mpaka jioni. Ili kukifanya kiwe safi ni lazima kukiosha kwa maji. 33Ikiwa mzoga wake umeangukia chombo cha udongo, basi, chochote kilicho ndani ya chombo hicho ni najisi na lazima chombo hicho kivunjwe. 34Chakula au kinywaji chochote kilichokuwa ndani ya chombo hicho kitakuwa najisi. 35Kila kitu ambacho sehemu ya mzoga imekiangukia, kitakuwa najisi. Ikiwa ni tanuri au jiko, ni lazima kivunjwe. Vitakuwa najisi navyo ni najisi kwenu. 36Hata hivyo, kisima au chemchemi ya maji vitakuwa safi. Lakini chochote kinachogusa mzoga kitakuwa najisi. 37Iwapo sehemu ya mzoga inaziangukia mbegu za kupanda, mbegu hizo hazitakuwa najisi. 38Lakini ikiwa mbegu zimetiwa katika maji ili kuota na sehemu yoyote ya mzoga ikaziangukia, basi, mbegu hizo ni najisi kwenu.
39“Iwapo mnyama yeyote mnayeruhusiwa kula, anakufa mwenyewe, yeyote atakayegusa mzoga wake, atakuwa najisi mpaka jioni. 40Mtu yeyote akila nyama ya mzoga huo atafua mavazi yake na atakuwa najisi mpaka jioni. Na yeyote atakayebeba mzoga huo, atafua mavazi yake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
41“Kiumbe chochote kitambaacho duniani ni najisi kwenu, kamwe msikile. 42Chochote kiendacho kwa tumbo lake, chochote kiendacho kwa miguu yote minne au nyayo nyingi, naam, chochote kitambaacho, kamwe msikile kwa maana ni najisi kwenu. 43Hivyo msije mkawa najisi kwa kula viumbe vitambaavyo na hivyo mkawa najisi. 44#Taz Lawi 19:21; 1Pet 1:16 Kwa kuwa mimi Mwenyezi-Mungu ndimi Mungu wenu, jiwekeni wakfu na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mtakatifu. 45Kwa kuwa mimi Mwenyezi-Mungu ndimi niliyewatoa nchini Misri ili niwe Mungu wenu; kwa hiyo muwe watakatifu kwa maana mimi ni mtakatifu.”
46Hiyo basi, ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege na viumbe vyote hai ambavyo huishi majini na nchi kavu, 47ili kupambanua kati ya kisicho najisi na kilicho najisi; kinachoweza kuliwa na kisichoweza kuliwa.

Mambo Ya Walawi11;1-47


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 8 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..10...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu katika yote..
Asante Baba wa Mbinguni,Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo,Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Yahweh..!Jehovah..!Jehovah nissi..!Jehovah Shammah..!Jehovah Jireh..!Jehovah Rapha..! Jehovah Roi..!Jehovah Shalom..!!
Hakuna kama wewe Baba wa Mbinguni wewe ni Alfa na Omega,Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Unatosha Mungu wetu...!!

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako,
Asante kwa kutulinda usiku na wakati wote na umetuamsha salama..
Asante kwakutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..

Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachili mikononi mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwa kuwaza,kunena,kutenda,kujua/kutojua..Baba wa Mbinguni Tunaomba nasi utupe Neema ya kuiweza kuwasamehe waliotukosea..

Utuepushe na majaribu, utuokoe na yule mwovu na kazi zake..Mungu wetu ututakase na utufunike kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu tupate kutambua/kujitambua..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..

Mungu wetu tunaomba uwabariki na kuwatendea,Ukawaguse na mkono wako wenye nguvu Yatima na Wajane na ukawaponye kimwili na kiroho wote wanaotaabika kwa Shida/tabu,wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,waliokwenye vifungo mbalimbali Baba ukawafungue na wote waliokata tamaa,wenye hofu/mashaka wakapate tumaini na wakawe na Amani ya moyo na ukawatendee sawa sawa na mapenzi yako.


Wapendwa tumrudishie Sifa na Utukufu Mungu wetu,Tuwe na wakati wa kukumbuka na Kumshukuru Mungu kwa Mema meengi aliyotutendea/anayotutendea..Tusiwe watu wa kulalamika tuu kila siku na kusahau wema wa Mungu..Tunasahau mangapi ametenda kwenye maisha yetu,Tusiwe wepesi wa kukumbuka mapito/majaribu tuu na kumuasi Mungu wetu kwamba ametuacha..Tukumbuke wapi tulipotoka na wapi tunaenda,tukumbuke wema na fadhili zake,tukumbuke si kwamba mimi/wewe ni wema sana na tunaweza yote hayo kwa uwezo wetu..
Tukumbuke kwa Neema/Rehema zake ndiyo tunaishi,Tunapata mahitaji yetu wala si kwamba tuna nguvu ya kufanya kazi/biashara au kwa akili zetu wenyewe pasipo maarifa aliyotupa Mungu ndiyo tunafanikiwa..


Ee Mungu wetu Tunakushukuru katika yote,Tunakushukuru kwa uweza wako na kutupa sisi nafasi ya kufanya/kutenda yote haya..

Tusipo weza kumshukuru Mungu wetu kwa kidogo tulichonacho jee tutakumbuka kwa kikubwa..?Tusijilinganishe na maisha ya wengine na kulalamika Mungu mbona mimi hivi na huyu vile,Tumshukuru kwa hili kwanza na tumuombe na atupe maarifa,ubunifu na tukatumie vyema karama alizotupa...
Tumkabidhi maisha yetu na kuomba muongozo huku nasi tukijibidisha..


Ee Mwenyezi-Mungu, unifundishe kutii masharti yako; nami nitayashika mpaka mwisho. Unieleweshe nipate kuishika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote. Uniongoze katika njia ya amri zako, maana humo napata furaha yangu. Unipe ari ya kuzingatia maamuzi yako, na si kwa ajili ya kupata faida isiyofaa. Uniepushe, nisifuate mambo ya upuuzi; unioneshe njia yako, unipe uhai. Unitimizie mimi mtumishi wako ahadi yako; ahadi unayowapa wale wanaokuheshimu. Uniokoe na lawama ninazoogopa; maana maagizo yako ni mema. Natamani sana kuzitii kanuni zako; unijalie uhai maana wewe ni mwadilifu.
Mungu wetu yu Mwema sana...!
Ee Mungu wetu ukatuongoze na kutuepusha na mambo yote yasiyokupendeza..
Ee Mungu wetu ukatupe kujua na kulielewa vyema Neno lako..

Ee Mwenyezi-Mungu, upokee sala yangu ya shukrani; na kunifundisha maagizo yako.
Asante Mungu wetu Tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Tukiamini na kukusifu daima..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukukufu hata Milele..
Amina..!
Mungu aendelee kuwabariki..
Asanteni sana kwakunitembea/kunisoma..
Nawapenda sana.





Dhambi ya Nadabu na Abihu

1Nao Nadabu na Abihu, wanawe Aroni, walichukua kila mmoja chetezo chake, wakaweka moto na ubani, wakamtolea Mwenyezi-Mungu moto najisi, ambao haukulingana na agizo lake Mwenyezi-Mungu. 2Basi, moto ukatokea mbele ya Mwenyezi-Mungu, ukawateketeza hao vijana, wakafa mbele yake. 3Hapo, Mose akamwambia Aroni, “Kwa tukio hili Mwenyezi-Mungu amekuonesha maana ya kile alichosema: ‘Nitajionesha kuwa mtakatifu miongoni mwa wale walio karibu nami; nitatukuzwa mbele ya watu wote!’” Aroni akanyamaza kimya.
4Basi, Mose akawaita Mishaeli na Elsafani, wanawe Uzieli, baba mdogo wa Aroni, akawaambia waje kuondoa maiti za ndugu zao maskani na kuzipeleka nje ya kambi. 5Wakachukua maiti za ndugu zao na kuzipeleka nje ya kambi wakiwa wamevaa mavazi yao, kama Mose alivyoamuru. 6Kisha Mose akamwambia Aroni na wanawe, Eleazari na Ithamari, “Msivuruge nywele zenu na wala msirarue mavazi yenu kuomboleza, la sivyo mtakufa na kuiletea jumuiya yote ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu. Lakini ndugu zenu yaani jumuiya yote ya Israeli, wanaweza kuomboleza kwa sababu ya moto huo aliouleta Mwenyezi-Mungu. 7Msitoke nje ya mlango wa hema la mkutano, la sivyo mtakufa; kwani mafuta ya kupaka ya Mwenyezi-Mungu yangali juu yenu.” Aroni na wanawe wakafanya kama Mose alivyosema.
8Mwenyezi-Mungu aliongea na Aroni, akasema, 9“Mnapoingia ndani ya hema la mkutano, wewe na wanao msinywe divai wala kileo chochote, la sivyo mtakufa. Hii itakuwa sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote. 10Ni lazima mtofautishe kati ya mambo matakatifu na mambo yasiyo matakatifu, kati ya mambo najisi na yasiyo najisi. 11Mtawafundisha Waisraeli masharti yote ambayo nimewaambia kwa njia ya Mose.”
12 # Taz Lawi 6:14-18 Mose akamwambia Aroni na wanawe waliosalia: Eleazari na Ithamari, “Chukueni ile sehemu ya sadaka ya nafaka iliyosalia kutoka sadaka anazotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto; muile karibu na madhabahu bila kutiwa chachu kwa sababu ni takatifu kabisa. 13Mtaila katika mahali patakatifu kwa sababu hiyo ni haki yako na wazawa wako kutoka katika sadaka anazotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto. Hivyo ndivyo nilivyoamriwa. 14#Taz Lawi 7:30-34 Lakini kidari ambacho hufanywa nacho ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu na mguu unaotolewa sadaka kama ishara, mnaweza kula mahali popote pasipo najisi. Utakula wewe, na watoto wako wa kiume na wa kike. Vitu hivyo umepewa kama haki yako na ya wazawa wako kutoka sadaka za amani za watu wa Israeli. 15Ule mguu uliotolewa na kidari cha sadaka ya kufanyia ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu watavileta pamoja na sadaka za mafuta zitolewazo kwa moto, ili kufanya ishara ya kuvitolea mbele ya Mwenyezi-Mungu, viwe sadaka ya kutolewa kwa ishara. Hivyo vitakuwa vyako pamoja na wanao; ni haki yenu milele kama Mwenyezi-Mungu alivyoamuru.”
16Basi, Mose alichunguza kwa makini kuhusu mbuzi mmoja aliyetolewa sadaka ya kuondoa dhambi, kumbe akagundua kuwa alikwisha teketezwa. Hivyo akawakasirikia sana Eleazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia, akawauliza, 17#Taz Lawi 6:24-26 “Kwa nini hamkumla katika mahali patakatifu kwa vile huyo ni kitu kitakatifu kabisa na mlikuwa mmepewa huyo ili kuondoa hatia ya jumuiya na kuwafanyia ibada ya upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu? 18Tena, kwa vile damu yake haikuletwa ndani ya mahali patakatifu, ni dhahiri iliwapasa kumla ndani ya mahali patakatifu kama nilivyoamuru.” 19Aroni akamwambia Mose, “Tazama, leo wametolea sadaka yao ya kuondoa dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele ya Mwenyezi-Mungu; hata hivyo mambo haya yamenipata! Tena kama ningekula ile sadaka ya kuondoa dhambi hivi leo, je, ingekubalika mbele ya Mwenyezi-Mungu?” 20Mose aliposikia hayo, akaridhika.

Mambo Ya Walawi10;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 7 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..9...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...
Mtakatifu..!Mtakatifu..!Mtakatifu.! Baba wambinguni Tunakushukuru na kukusifu..
Asante kwa wema na fadhili zako,
Asante kwa ulinzi wako wakati wote na kutuamsha salama..

Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii.
Tunakuja mbele zako Mfamle wa Amani tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mokononi mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mungu wetu....kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Utuepushe katika majaribu,Utuokoe na yule mwovu na kazi zake Baba wa Mbinguni..
Ututakase na kutufunika kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Utupe moyo wenye Hekima,Busara,Amani ya moyo,Upendo wa kweli,kuchukuliana/kuvumiliana,kusameheana na Upole Kiasi..
Tupate kujitambua/kutambua..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Baba wa Mbinguni tunaiweka siku hii mikononi mwako,Ukatubariki,ukatamalaki maishani mwetu na ukatuatamie..
Ikawe siku njema na yenye kukupendeza wewe..
Ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo,vilaji/vinywaji,kuingia/kutoka kwetu,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..
Ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo nasi ukatupe neema ya kuwabariki wenye kuhitaji..
Tazama wenyeshida/tabu,wanaopitia magumu/majarubu mbalimbali,waliokatika vifungo mbalimbali,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao..Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu,ukawaponye na kuwaoko,ukaonekane kwenye mahitaji yao,wakapate kupona kimwili na kiroho pia..


Ee Mungu wetu tunaweka Nchi hii tunayoishi mikononi mwako Ukaibariki na kuwabariki watu wote tunaoshia humu,Ukatusamehe pale tulipokwenda kinyume,pale tulipokuasi na kufuata mambo yetu wenyewe..Ee Baba ukasikie kulia kwetu,ukasikie maombi yetu,ukasimame nasi katika yote,Ukatuepushe na Udini/ukabila,chuki na hasira,ukawabariki Viongozi wetu wa KIROHO Baba wa Mbinguni ukawape macho ya rohoni, ukabariki Familia zao pia,Ukawabariki na wanaotuongoza Baba wa Mbinguni wakatuongoze katika haki na kweli..
 Tuungane pamoja kuombea Amani kwenye Taifa hili,Mungu wetu ukaonekane na kutawala Milele...

Ee Mungu wetu tunaiweka Tanzania mikononi mwako,Amani ya kweli,Upendo wa Kweli,Ukaibariki na kuwabariki watu wake popote walipo,walio ndani ya Nchi na walio nje kwa sababu ya kusoma,kwa sababu ya kutafuta maisha,waliokatika matibabu na mengine yote Mfalme wa Amani ukatawale maisha yao, Ukatuongoze vyema na ukatupe mwanga katika maisha yetu,ukaonekane Mungu wetu,Kuna sababu ya kuwa Wa Tanzania haijalishi watu wanaishi wapi,wako wapi Mungu wetu yupo nasi..
Mungu wetu tunaiweka Afrika yote yote mikononi mwako waafrika popote walipo Baraka na Amani ziwafuate..
Mungu wetu tunaiweka Dunia hii mikononi mwako wewe ukawe mtawala mkuu na ukawabariki na kuwaongoza wote wanaotuongoza, Kiroho na kidunia wakatuongoze vyema kwa misingi yako Mungu wetu..

Wapendwa/waungwana tusikome kuombea Mtaifa yetu,watu wetu,Viongozi wetu wa KIROHO na wakimataifa/kidunia..
Tusichoke kuombeana mema hata kama tulikoseana tuombane msamaha na kuendela vyema katika maisha yetu,Muombee mwenzio mema,Ombea watoto wa wenzio,Tuombee Nchi tunazoishi na tulipotokea/zaliwa na watu wake Kwani Amani ikitawala hapo ulipo au ulipotokea/zaliwa nawe utakuwa na Amani ya moyo..
Ombea kazi,Karama za wengine walizobarikiwa na Mungu nawe una zako pia wengnine hawana hizo,Mungu wetu ni muweza wa yote..
Ombea adui yako,Samehe kama Mungu anavyotusamehe..
Tuachane na wivu,visasi na kukwamishana utachelewesha tuu kwani vinamwisho Mungu akimbariki mtu amembariki..

Mungu akatulinde na mabaya yote yaliyonenwa,yaliyotendwa kwa sababu yetu..Mungu akabariki vinywa vyetu na kutusamehe..tulipowanenea mabaya wengine,Tulipoadhibu,Tulipo hukumu na kusababisha makwazo kwa wengine..
Mungu akatubariki katika yote na tukajue kweli..

“Katika mwaka Dario mwana wa Ahasuero, Mmedi, alipoanza kutawala juu ya milki ya Wakaldayo, mimi Danieli nilikuwa nikivisoma kwa makini vitabu vitakatifu, na humo nikaelewa maana ya jambo lile Mwenyezi-Mungu alilomfahamisha nabii Yeremia kuhusu ile miaka sabini, muda ambao utahusika na kuharibiwa kwa Yerusalemu. Nilimwomba Mwenyezi-Mungu, kwa moyo, nikimtolea dua pamoja na kufunga, nikavaa vazi la gunia na kuketi kwenye majivu. Nilimwomba Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, na kuungama, nikisema: “Ee Bwana, wewe ni Mungu mkuu na wa kuogofya. Wewe ni mwaminifu kwa agano lako na unawafadhili wakupendao na kuzitii amri zako. Tumetenda dhambi, tumekosa, tumetenda maovu na kukuasi. Tumezikiuka amri zako na kanuni zako. Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako waliongea na wafalme wetu, wakuu wetu, wazee wetu na taifa letu lote. Kwako, ee Bwana, kuna uadilifu, lakini sisi daima tumejaa aibu. Jambo hili ni kweli kwetu sote tuishio Yudea, wakazi wa mji wa Yerusalemu na Waisraeli wote ambao umewatawanya katika nchi za mbali na za karibu kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako. Aibu, ee Bwana, ni juu yetu, wafalme wetu, wakuu wetu na wazee wetu, kwa sababu tumekukosea. Wewe, Bwana Mungu wetu, una huruma na msamaha, ingawa sisi tumekuasi. Tulikataa kukusikiliza, ee Bwana, Mungu wetu; hatukuishi kulingana na sheria zako ulizotupa kwa njia ya watumishi wako manabii. Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwagiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika sheria ya Mose, mtumishi wako. Umethibitisha yale uliyosema utatutenda sisi pamoja na watawala wetu kwa kuuadhibu mji wa Yerusalemu vikali zaidi ya mji mwingine wowote duniani. Umetuadhibu kama ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, lakini mpaka sasa, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, hatukuomba msamaha wako kwa kuziacha dhambi zetu na kutafakari uaminifu wako. Kwa hiyo, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ulikuwa tayari kutuadhibu, na ukafanya hivyo, kwa kuwa daima unafanya yaliyo ya haki, nasi hatukukusikiliza. “Na sasa ee Bwana, Mungu wetu, uliyewatoa watu wako nchini Misri kwa nguvu yako kuu na kulifanya jina lako litukuke mpaka sasa, tunasema kwamba tumetenda dhambi; tumefanya maovu. Ee Bwana, kwa kadiri ya matendo yako ya haki usiukasirikie wala kuughadhibikia mji wako wa Yerusalemu, mlima wako mtakatifu. Watu wote wa nchi za jirani wanaudharau mji wa Yerusalemu na watu wako, kwa sababu ya dhambi zetu na maovu waliyotenda wazee wetu. Kwa hiyo, ee Mungu, isikilize sala yangu na maombi yangu mimi mtumishi wako. Kwa hisani yako, uifadhili tena maskani yako iliyoharibiwa. Tega sikio, ee Mungu wangu; angalia uone taabu tulizo nazo na jinsi unavyotaabika huo mji uitwao kwa jina lako. Tunakutolea maombi yetu si kwa sababu tumetenda haki, bali kwa sababu wewe una huruma nyingi. Ee Mwenyezi-Mungu, utusikie; utusamehe ee Mwenyezi-Mungu. Ee Mwenyezi-Mungu, kwa hisani yako utusikie na kuchukua hatua, wala usikawie, ee Mungu wangu, kwa ajili ya mji huu na watu hawa wanaoitwa kwa jina lako!
Sifa na Utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Tunayaweka haya yote  mikononi mwako Mungu wetu..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!

Asanteni sana wote mnaotembelea hapa..
sina neno zuri lakusema..zaidi ya kuwaombea
Baraka na Amani zikamiminike katika maisha yenu..
Nawapenda.

Aroni anatoa sadaka

1Siku ya nane baada ya siku saba za kuwekwa wakfu, Mose akamwita Aroni na wanawe pamoja na wazee wa Israeli. 2Mose akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; wanyama wote wasiwe na dosari. Kisha watoe sadaka mbele ya Mwenyezi-Mungu. 3Waambie Waisraeli wachukue beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi, na ndama mmoja na mwanakondoo mmoja wote wa umri wa mwaka mmoja na wasio na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, 4fahali mmoja na kondoo dume mmoja kwa ajili ya sadaka za amani, wakamtolee Mwenyezi-Mungu pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta kwa maana leo Mwenyezi-Mungu atawatokea.”
5Waisraeli wakaleta vyote hivyo mbele ya hema la mkutano kama Mose alivyowaamuru na jumuiya yote ikaenda kusimama mbele ya Mwenyezi-Mungu. 6Mose akawaambia, “Hili ndilo jambo ambalo Mwenyezi-Mungu aliwaamuru mlifanye ili utukufu wake uonekane kwenu.” 7Hapo Mose akamwambia Aroni, “Nenda kwenye madhabahu, utolee hapo sadaka yako ya kuondoa dhambi na sadaka ya kuteketezwa na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yako na kwa ajili ya watu wa Israeli. Kisha tolea hapo sadaka za watu na kuwafanyia ibada ya upatanisho kama alivyoamuru Mwenyezi-Mungu.”
8Basi, Aroni akaikaribia madhabahu, akamchinja yule ndama aliyemtoa awe sadaka ya kuondoa dhambi yake mwenyewe. 9Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika damu hiyo na kuzipaka pembe za madhabahu. Damu iliyosalia akaimwaga kwenye tako la madhabahu. 10Lakini mafuta na figo akaviteketeza vyote juu ya madhabahu kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Mose. 11Lakini ile ngozi akaiteketeza kwa moto nje ya kambi.
12Kisha Aroni akamchinja mnyama wa sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyizia madhabahu pande zote. 13Kisha wakamletea sadaka ya kuteketezwa, kipande kimojakimoja, na kichwa; naye akaviteketeza juu ya madhabahu. 14Akaosha matumbo na miguu na kuiteketeza pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa kwenye madhabahu.
15Kisha, Aroni akaweka mbele sadaka ya watu. Alimchukua mbuzi wa sadaka ya watu ya kuondoa dhambi, akamchinja na kumtoa sadaka ya kuondoa dhambi, kama alivyofanya kwa yule wa kwanza. 16Kisha akaweka mbele ile sadaka ya kuteketezwa akatolea sadaka hiyo kulingana na agizo. 17Kisha akaweka mbele sadaka ya nafaka akijaza konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya kila asubuhi.
18 # Taz Lawi 3:1-11 Halafu Aroni akamchinja pia fahali na yule kondoo dume wa sadaka za amani kwa ajili ya watu. Wanawe wakamletea damu ambayo aliinyunyizia madhabahu pande zote. 19Mafuta ya fahali huyo na kondoo dume, mkia wa kondoo, mafuta yaliyofunika matumbo, figo na sehemu bora ya ini 20wakayaweka juu ya vidari, naye akaviteketeza kwenye madhabahu. 21Lakini vile vidari na ule mguu wa nyuma wa kulia, Aroni alifanya navyo ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu, kama Mose alivyoamuru.
22 # Taz Hes 6:22-26 Aroni alipomaliza kutolea sadaka zote: Sadaka za kuondoa dhambi, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, aliwainulia watu mikono, akawabariki, kisha akashuka chini. 23Ndipo Mose na Aroni wakaingia ndani ya hema la mkutano; walipotoka waliwabariki watu, nao utukufu wa Mwenyezi-Mungu ukaonekana kwa watu wote. 24Mwenyezi-Mungu akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipouona huo moto walipaza sauti na kusujudu.

Mambo Ya Walawi9;1-24


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 6 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..8...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Ni siku nyingine tena Mungu wetu ametuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona tena leo hii..
Tumshukuru Muumba wetu kwa wema na fadhili zake..
Asante Baba wa Mbinguni kwa ulinzi wako na kutuamsha salama..
Asante kwa siku hii na tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako..

Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kunena,kutenda,kwakujua/kutojua..
Baba wa mbinguni nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Mfalme wa Amani tunaomba utuepushe katika  majaribu utuokoe  na yule mwovu na kazi zake,Ututakase Miili yetu na Akili zetu na utufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,Yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena na kutenda tupate kutambua/kijtambua na tukawe na kiasi..
Tukawe barua njema na tukasomeke sawasawa na mapenzi yako..
Ukabariki ridhiki zetu ziingiazo /zitokazo nasi ukatupe Neema ya kuwabariki wengine..
Ukabariki tuingiapo/tutokapo,Vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..Vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba wa mbinguni ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..

Tazama wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,waliokwenye vifungo mbalimbali,waliokata tamaa,waliokataliwa,wenye hofu/mashaka,Wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao..Ukawaguse na mkono wako wenye nguvu,ukawaponye kiroho na kimwili..wakakuone kwenye shida zao Mungu wetu,wanaokutafuta wakuone,wanaokulilia ukawafute machozi,wanaokuomba ukawajibu Mungu wetu,Ukawainue wanyonge,waliodhulumiwa wakapate haki zao,ukawatendee sawasawa na mapenzi yako..



Kwa wimbo nitalisifu jina la Mungu, nitamtukuza kwa shukrani. Jambo hili litampendeza Mwenyezi-Mungu zaidi, kuliko kumtolea tambiko ya ng'ombe, kuliko kumtolea fahali mzimamzima. Wanyonge wataona hayo na kufurahi; wanaomheshimu Mungu watapata moyo. Mwenyezi-Mungu huwasikiliza fukara; hatawasahau kamwe watu wake wafungwa. Enyi mbingu na dunia msifuni Mungu; bahari na vyote vilivyomo, msifuni. Maana Mungu atauokoa mji Siyoni, na kuijenga tena miji ya Yuda. Watu wake wataishi humo na kuimiliki; wazawa wa watumishi wake watairithi, wale wanaopenda jina lake wataishi humo.

Mpendwa haijalishi unapitia nini Mungu wetu yu mwema na kamwe hawezi kukuacha,jipe moyo,Muombe, muite naye ataitika,Mungu wetu hakawii wala hachelewi,Yeye yupo,yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,Yeye anatujua zaidi tunavyojijua,yeye atosha..Usife moyo,simama,usikatishwe tamaa na wanadamu,Mungu wetu hashindwi yeye ni mwingi wa Rehema/Neema..Yeye ni muweza wa yote..yeye hawezi kukuacha,Mungu wetu si kiziwi anasikia,Mungu wetu si kipofu anaona,Mungu wetu si Bubu anajibu..
Inuka anza na Bwana yeye atakushindia..Bado hujachelewa,Haijalishi umeanguka kiasi gani,haijalishi umehasi kwa muda gani..Mungu wetu husamehe na kuokoa,Anaponya moyo wako na mwili wako..yeye ni Ndimi Mungu wetu..Hachoki,Halali wala hasinzii..
Mungu akubariki na kukuinua..

Asante Baba wa Mbinguni..

Tunayaweka haya yote mikoni mwako Mungu wetu..Tunaamini wewe ni Mungu wetu hakuna Mungu mwingine..
Wewe unatujua kulikotunavyojijua..

Tunakushukuru Mungu wetu,Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe..

Kwakua Ufalme ni Wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!

Asanteni sana kwakutumbelea hapa..
MUNGU akawabariki katika yote..
Nawapenda.


Kuwekwa wakfu kwa Aroni na wanawe

(Kut 29:1-37)

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2“Mwite Aroni na wanawe wakutane mbele ya mlango wa hema la mkutano; chukua mavazi matakatifu, mafuta ya kupaka, ng'ombe wa sadaka ya kuondolea dhambi, kondoo madume wawili, na kikapu cha mikate isiyotiwa chachu. 3Kisha, ikusanye jumuiya yote ya Waisraeli mbele ya mlango wa hema la mkutano.” 4Mose akafanya kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu, akaikusanya jumuiya yote mbele ya mlango wa hema la mkutano. 5Mose akaiambia jumuiya yote hivi: “Lifuatalo ni jambo ambalo Mwenyezi-Mungu ameamuru lifanywe.” 6Hapo Mose akawaleta Aroni na wanawe na kuwatawadha. 7Kisha akamvika Aroni joho na kuifunga kwa mkanda, akamvika kanzu, akamvalisha kizibao na kukifunga kiunoni mwake kwa mkanda uliofumwa kwa ustadi. 8#Taz Kut 28 Kisha akaweka kifuko kifuani pa Aroni na ndani ya kifuko hicho akatia mawe ya kauli. 9Halafu akamvika Aroni kilemba na upande wa mbele wa kilemba hicho akaweka pambo la dhahabu, taji takatifu, kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru.
10Kisha Mose akachukua mafuta ya kupaka, akaipaka ile maskani na vitu vyote vilivyokuwa ndani yake akaviweka wakfu. 11Alinyunyiza sehemu ya mafuta hayo juu ya madhabahu mara saba, akaipaka mafuta na vyombo vyake vyote, birika na tako lake, kuviweka wakfu. 12Vilevile Mose akampaka Aroni mafuta kichwani ili kumweka wakfu. 13Kisha Mose akawaleta wana wa Aroni akawavika joho na kuwafunga mikanda viunoni, na kuwavisha kofia kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.
14Kisha Mose akamleta ng'ombe wa sadaka ya kuondoa dhambi, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha ng'ombe huyo. 15Mose akamchinja huyo ng'ombe, akachukua damu akazipaka pembe za madhabahu pande zote kwa kidole chake kuitakasa. Kisha akachukua damu iliyobaki akaimwaga chini kwenye tako la madhabahu ambayo aliweka wakfu kwa kuifanyia ibada ya upatanisho. 16Kisha, akachukua mafuta yote yaliyokuwa kwenye matumbo yake, sehemu bora ya ini pamoja na figo zote mbili na mafuta yake na kuviteketeza juu ya madhabahu. 17Lakini nyama ya ng'ombe huyo, ngozi yake na mavi yake, akaviteketeza kwa moto nje ya kambi kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.
18Kisha, Mose akamleta kondoo dume wa sadaka ya kuteketezwa. Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo. 19Mose akamchinja na damu ya kondoo huyo akairashia madhabahu pande zake zote. 20Alimkata huyo kondoo vipandevipande, akaviteketeza pamoja na kichwa chake na mafuta yake. 21Baada ya matumbo na miguu kuoshwa kwa maji, Mose aliviteketeza vyote juu ya madhabahu pamoja na sehemu nyingine za huyo kondoo kama sadaka ya kuteketezwa. Hiyo ni sadaka itolewayo kwa moto, yenye harufu ya kumpendeza Mwenyezi-Mungu. Mose alifanya kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu. 22Kisha akamleta kondoo dume mwingine, kwa ajili ya kuweka wakfu. Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo. 23Mose akamchinja. Akachukua damu ya kondoo huyo na kumpaka Aroni kwenye ncha ya sikio lake la kulia, kidole gumba cha mkono wake wa kulia na cha mguu wake wa kulia. 24Wanawe Aroni nao wakaja, naye Mose akawapaka kiasi cha damu kwenye ncha za masikio yao ya kulia, vidole gumba vya mikono yao ya kulia na kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kulia. Damu nyingine akainyunyizia madhabahu pande zake zote. 25Kisha, akachukua mafuta yote, mkia pamoja na mafuta yake, mafuta yote yanayofunika matumbo, sehemu bora ya ini, pamoja na figo zote mbili, mafuta yake na paja la mguu wa kulia wa nyuma wa huyo kondoo dume. 26Kisha, kwenye kile kikapu cha mikate iliyowekwa mbele ya Mwenyezi-Mungu akatoa mkate mmoja usiotiwa chachu, mkate mmoja wenye mafuta na mkate mmoja mdogo, akaviweka vyote juu ya vipande vya mafuta na ule mguu. 27Mose akaviweka mikononi mwao Aroni na wanawe, nao wakafanya ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu. 28Kisha Mose akavichukua vitu hivyo vyote kutoka mikononi mwao na kuviteketeza juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa. Hii ni sadaka ya kuwekwa wakfu, yenye harufu ya kumpendeza Mwenyezi-Mungu; ni sadaka itolewayo kwa moto. 29Kisha Mose akachukua kile kidari na kufanya ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu. Sehemu hiyo ya yule kondoo dume wa kuweka wakfu ni mali yake Mose kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.
30Halafu Mose akachukua mafuta ya kupaka na damu kutoka madhabahu akamnyunyizia Aroni na wanawe hata na pia mavazi yao. Hivyo Mose akamweka wakfu Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao.
31Mose akamwambia Aroni na wanawe, “Chemsheni ile nyama mbele ya mlango wa hema la mkutano, muile hapo mlangoni pamoja na mkate kutoka katika kikapu chenye sadaka za kuwekea wakfu. Fanyeni kama nilivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu, kwamba sehemu hiyo italiwa na Aroni na wanawe. 32Nyama yoyote au mkate wowote utakaosalia ni lazima kuteketezwa. 33Hamtatoka nje ya mlango wa hema la mkutano kwa muda wote wa siku saba, yaani mpaka muda wenu wa kuwekwa wakfu umekwisha, muda ambao utachukua siku saba. 34Mwenyezi-Mungu ameamuru tufanye kama tulivyofanya leo ili tuwafanyieni ibada ya upatanisho. 35Mtabaki mlangoni mwa hema la mkutano usiku na mchana kwa muda wa siku saba, mkifanya mambo aliyoamuru Mwenyezi-Mungu, la sivyo mtakufa. Ndivyo nilivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.” 36Basi, Aroni na wanawe wakafanya mambo yote aliyoamuru Mwenyezi-Mungu kwa njia ya Mose.

Mambo Ya Walawi8;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 5 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..7...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu, Baba yetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo,Mfalme wa Amani, Muweza wa yote, Alfa na Omega, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.. Yahweh..!Jehovah..!
Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza, tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Mfalme wa Amani..

Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Baba..kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mungu wetu tunaomba nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..


Utuepushe na majaribu na utulinde na yule mwovu na kazi zake, Ututakase Miili yetu na Akili zetu utufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Asante kwa ulinzi wako usiku wote na siku zote Mfalme wa Amani umekuwa nasi..
Tazama Jana imepita Baba wa Mbinguni Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine...

Asante kwakutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Tunaomba ukatubariki na kubariki katika  yote tunayoenda kufanya/kutenda na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Tukaanze siku/wiki hii nawe Mungu wetu,ikawe yenye Baraka,Amani,Upendo,utuwema,fadhili na kuchukuliana..

ukatupe Hekima,Busara katika kila jambo, tupate kutambua/kujitambua na Utukufu tukurudishie wewe Muumba wetu..


Yesu aliendelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri. Mtu mmoja akamwuliza, “Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?” Yesu akawaambia, “Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza. Wakati utakuja ambapo mwenye nyumba atainuka na kufunga mlango. Nyinyi mtasimama nje na kuanza kubisha mlango mkisema: ‘Bwana, tufungulie mlango.’ Lakini yeye atawajibu: ‘Sijui mmetoka wapi.’ Nanyi mtaanza kumwambia: ‘Sisi ndio wale tuliokula na kunywa pamoja nawe; na wewe ulifundisha katika vijiji vyetu.’ Lakini yeye atasema: ‘Sijui nyinyi mmetoka wapi; ondokeni mbele yangu, enyi nyote watenda maovu.’ Ndipo kutakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo na manabii wote wapo katika ufalme wa Mungu, lakini nyinyi wenyewe mmetupwa nje! Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini na kukaa kwenye karamu katika ufalme wa Mungu. Naam, wale walio wa mwisho watakuwa wa kwanza; na wale walio wa kwanza watakuwa wa mwisho.”

Baba wa Mbinguni tunaiweka" Coventry "mikononi mwako ,
Tunaiweka "LONDON- UK "Nchi nzima mikononi mwako..
ukailinde na kutulinda wote tunaoishi hapa,ukatuokoe na wenye nia mbaya..ukatuepushe na Udini/Ukabila na tofauti zozote zinazoendelea na ukawafariji waliopatwa na  msiba na ukawaponye waliopatwa na maumivu/kuumizwa..Tunaomba Amani itokayo kwako,Tunaomba ukatawale ee Mungu wetu tunaomba ukatupe hekima na busara na uvumilivu kwenye  wakati huu mgumu...Mungu wetu ukaonekane na kututendea...

Tazama wenye shida/tabu na wote wanaopitia magumu/majaribu, wenye vifungo mbalimbali Mfalme wa Amani ukawaguse na mkono wako wenye nguvu  kuwaponye kimwili na kiroho pia..

Tunayaweka haya yote mikononi mwako Mungu wetu, Tuliyoyanena na tusiyoyanena Baba wa Mbinguni unayajua na kutujua zaidi ya tunavyojijua..
Kwa kuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..

Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea..
wote mnaopita hapa na akawape sawasaswa na mapenzi yake..
Asanteni sana kwakuwa nami/kunisoma..
Nawapenda.


Sadaka za fidia

1“Ufuatao ni mwongozo wa ibada kuhusu sadaka ya kuondoa hatia. Sadaka hiyo ni takatifu kabisa. 2Mnyama wa sadaka ya kuondoa hatia atachinjiwa mahali wanapochinjiwa wanyama wa sadaka za kuteketezwa, na damu yake itarashiwa madhabahu pande zake zote. 3Mafuta yake yote: Mafuta ya mkia na yale yanayofunika matumbo yatatolewa na kuteketezwa 4pamoja na zile figo mbili pamoja na mafuta yake na ile sehemu bora ya ini. 5Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama sadaka anayotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto. Hiyo ni sadaka ya kuondoa hatia. 6Wanaoruhusiwa kula sadaka hiyo ni wanaume wa ukoo wa makuhani peke yao; ni sadaka takatifu kabisa. Italiwa katika mahali patakatifu. 7Sheria ni moja kuhusu sadaka ya kuondoa hatia na sadaka ya kuondoa dhambi: Kuhani anayefanya ibada ya upatanisho ndiye atakayeichukua. 8Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa ya mtu yeyote, atachukua ngozi ya mnyama aliyetolewa. 9Sadaka yoyote ya nafaka iliyookwa jikoni au katika sufuria au katika kikaango itakuwa mali ya kuhani anayeitoa. 10Kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au kavu, itakuwa ya wazawa wa Aroni, na wote wagawiwe kwa sawa.

Sadaka za amani

11“Ufuatao ni mwongozo wa ibada kuhusu sadaka za amani ambazo mtu aweza kumtolea Mwenyezi-Mungu. 12Ikiwa mtu anatoa sadaka hiyo ya kumshukuru Mungu, basi, ataitoa pamoja na maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopakwa mafuta, mikate myembamba iliyopakwa mafuta na maandazi ya unga laini uliochanganywa na mafuta. 13Pamoja na sadaka hiyo yake ya amani ya kumshukuru Mungu, ataleta maandazi yaliyotiwa chachu. 14Kutokana na maandazi hayo, atamtolea Mwenyezi-Mungu andazi moja kutoka kila sadaka; maandazi hayo yatakuwa yake kuhani anayeirashia madhabahu damu ya sadaka za amani. 15Nyama ya sadaka hiyo ya amani ya kumshukuru Mungu italiwa siku hiyohiyo inapotolewa; hataacha hata sehemu yake hadi asubuhi. 16Lakini kama sadaka hiyo ya amani ni ya nadhiri au ya hiari, italiwa siku hiyohiyo inapotolewa na sehemu nyingine yaweza kuliwa kesho yake. 17Lakini nyama yoyote ya sadaka hiyo inayobaki hadi siku ya tatu itateketezwa. 18Tena nyama yoyote ya sadaka ya amani ikiliwa siku ya tatu, haitakubaliwa, wala haitapokelewa kwa faida yake mtu aliyeitoa. Nyama hiyo ni chukizo na mtu atakayeila atawajibika kwa uovu wake.
19“Nyama yoyote inayogusa kitu najisi isiliwe. Nyama hiyo itateketezwa kwa moto. Wote walio safi wanaweza kula nyama 20iliyotolewa sadaka ya amani kwa Mwenyezi-Mungu. Lakini mtu yeyote aliye najisi, akila nyama hiyo, atatengwa na watu wake. 21Mtu yeyote anayegusa kitu chochote kilicho najisi, au kitu najisi cha mtu, au mnyama aliye najisi, au kitu chochote najisi ambacho ni chukizo, akila nyama ya sadaka ya amani aliyotolewa Mwenyezi-Mungu, mtu huyo atatengwa na watu wake.”
22Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 23“Waambie Waisraeli hivi: Msile mafuta ya ng'ombe au ya kondoo au ya mbuzi. 24Mafuta ya mnyama yoyote aliyekufa mwenyewe au ya mnyama aliyeuawa na mnyama wa porini yaweza kuwekwa kwa matumizi mengine, lakini kamwe msiyale. 25Mtu yeyote akila mafuta ya mnyama aliyetolewa kwa Mwenyezi-Mungu kwa moto, atatengwa na watu wake. 26#Taz Mwa 9:4; Lawi 17:10-14; 19:26; Kumb 12:16,23; 15:23 Tena, kamwe msile damu yoyote ile, iwe ya ndege au ya mnyama mahali popote mnapoishi. 27Mtu yeyote akila damu yoyote, atatengwa na watu wake.”
28Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 29“Waambie watu wa Israeli hivi: Mtu yeyote akitoa sadaka ya amani, atampa Mwenyezi-Mungu sehemu ya sadaka hiyo. 30Atamletea kwa mikono yake mwenyewe kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Ataleta mafuta yake pamoja na kidari ambacho atafanya nacho ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu. 31Kuhani atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe makuhani. 32Mguu wa kulia wa nyuma wa mnyama wa sadaka zenu za amani mtampa kuhani. 33Mguu huo utakuwa mali ya kuhani aliye mzawa wa Aroni anayetoa damu ya sadaka za amani na mafuta yake. 34Mwenyezi-Mungu amewaagiza watu wa Israeli watenge kidari hicho na mguu huo wa mnyama wa sadaka zao za amani, wampe kuhani Aroni na wazawa wake, maana sehemu hiyo wamewekewa hao makuhani milele. 35Hiyo ndiyo sehemu iliyotengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe kutoka katika sadaka anazotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto, tangu siku walipotawazwa kuwa makuhani wa Mwenyezi-Mungu. 36Walipowekwa wakfu kwa kupakwa mafuta, Mwenyezi-Mungu aliamuru Waisraeli wawape sehemu hiyo ya sadaka; hiyo itakuwa daima haki yao.”
37Basi, hayo ndiyo maagizo kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya kuondoa dhambi, sadaka ya kuondoa hatia, kuhusu kuwekwa wakfu na kuhusu sadaka ya amani. 38Mwenyezi-Mungu alimpa Mose amri hizi mlimani Sinai siku ile alipowaamuru Waisraeli wamletee sadaka zao, kule jangwani Sinai.

Mambo Ya Walawi7;1-38


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.