Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 30 May 2016

MISS TANZANIA USA PAGEANT AEESHA KAMARA TEMBELEA, KUONGEA NA KUTOA MSAADA KENTON HIGH SCHOOL


Miss Tanzania USA 2015-2016 Aeesha Kamara akiongea na wanafunzi wa Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam siku alipotembelea shuleni hapo katika moja ya majukumu yake ya kuhudumia jumuiya. Miss Kamara anadhamini wanafunzi wawili shuleni hapo
Miss Tanzania USA Pageant Aeesha Kamara akimkabidhi msaada mwalimu mipira siku alipotembela shule ya Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania USA Aesha Kamara akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wawili anaowadhamini kwa kuwasomesha shuleni hapo.
Picha ya pamoja

TAARIFA YA MSIBA: JACQUELINE OSWALD KAPINGA WA SINZA AFARIKI


TAARIFA YA MSIBA: JACQUELINE OSWALD KAPINGA WA SINZA AFARIKI

MAREHEMU JACKLINE OSWALD KAPINGA

Familia ya Marehemu Mzee Oswald Kapinga ya Sinza - Dar e salaam (karibu na  white inn) inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Jacqueline kilichotokea jana tarehe 29/05/2016 katika hospitali ya muhimbili jijini Dar es salaam. 

Familia inapenda kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki ya kuwa, msiba utakuwa nyumbani kwa wazazi wake hapo sinza. 

Taratibu za mazishi zinaendelea kufanyika, taarifa ya awali kutoka kwa familia, Marehemu wanategemea kumuhifadhi kwenye nyumba yake ya milele siku ya kesho (Jumanne) ya Tarehe 31/05/2016 katika makaburi ya sinza karibu na Ukumbi wa mwika kuanzia saa 8.00 Mchana. 

Kwa taarifa zaidi na maelekezo mbali mbali unaweza kuwasiliana na makaka wa marehemu hapo chini: 

JOSEPH O. KAPINGA (Mwananchi communication)  - 0788617654

GOSBERT O. KAPINGA - 0754286301

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA, 
JINA LAKE LIHIMIDIWE
AMEN.



Sunday 29 May 2016

Natumaini Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema;Burudani-Ephraim Sekelet Uniongoze,Majaribu Ni Mtaji By Ambwene Mwasongwe,Yesu Ni Bwana by E R Mwansasu Chidumule

Wapendwa habari za Jumapili,Natumai ni njema/inaendelea vyema..
kwetu ni salama kabisa na tunaendelea vyema na leo kulikuw na jua
jumapili inaishia vizuri..

Basi tuendelee kuombeana katika yote,Uwepo wa Mungu utawale pale ulipo,
Watoto wanaondelea na shule Mungu akawaongoze vyema,wale walio kwenye mapumziko kama hapa
kwetu wakawe na wakati mzuri,
Mungu awabariki na kuwaongoza..

          

Neno La Leo;3 Yahane 1-15
Mimi mzee, nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni. 3Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakashuhudia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli. 4Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.

                       Uaminifu wa Gayo
5Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni. 6Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu. 7Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.8Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.



Diotrefe na Demetrio
9Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza. 10Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuza nje ya kanisa.
11Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.


 
                                 
 

Salamu za mwisho
13Ninayo bado mengi ya kukuambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino. 14Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana.
15Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.







"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 26 May 2016

Jikoni Leo na Bi Sheikha Agili-Achari ya Mraba





Ingredients:
2 cups sugar
1 and a half cups water
Salt
Chili powder
Red food colour 
Dried uncooked achari (slithered mangoes that have been dried in the sun)
Method:
In a pot, add everything except the achari.
Cook the mixture until it gets sticky enough and the liquid has reduced abit then add the achari and mix well while still on the stove.
You can leave the achari abit saucy(rojo) or let the liquid dry abit so they be somewhat sticky(mraba). If the syrup is done right you can even let liquid completely dry and let the achari get coated with sugar while the syrup is drying (kavu).
Once the desired stage of the achari is reached remove from the stove and let them cool.
Enjoy!!


Zaidi ingia;Sheikha Agil


"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 22 May 2016

Natumaini Jumapili ilikuwa njema/inaendelea vyema;Burudani-Natembea kidogo kidogo nikinyatanyata......Happy Birthday da'Tracey-Sarah

Wapendwa natumai Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema..
Mungu azidi kuwabariki katika yote..


Hapa kwetu Jumapili ni njema kabisaa
Leo tunaungana na binti yetu mpendwa kwa kumbukumbu yake ya siku ya kuzaliwa
Siku kama ya leo Mungu alitubariki na kutujaalia mtoto wa kike da'Trace-Sarah
Mungu anaendelea kumtunza vyema katika yote..
Mungu yu mwema sana tunamrudishia sifa na utukufu kwakwe
Tunamwachilia binti huyu mikononi mwake Baba wa Mbinguni katika yote
Aendelee kuwa Baraka kwetu kama wazazi,walezi, Ndugu,Jammaa,Marafiki na Jamii yote
Mungu yu Mwema mnoooo
Happy Birthday da'Tracey-Sarah.

 8Mungu asema: “Nitakufunza
na kukuonesha njia unayopaswa kufuata.
Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.

Neno La Leo;Zaburi:32:8-11

9Usiwe mpumbavu kama farasi au nyumbu,
ambao lazima wafungwe lijamu na hatamu,
la sivyo hawatakukaribia.”
10Watu waovu watapata mateso mengi,
bali wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu wazungukwa na fadhili zake.
11Furahini na kushangilia kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu;
pigeni vigelegele vya shangwe enyi wanyofu wa moyo.

Bible Society of Tanzania


"Swahili Na Waswahili"Muwe na wakati mwema.