Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 25 March 2016

Tanzania: Journalists on Gender equality in media



Pili, a journalist at a community radio station, and Saumu, newspaper journalist at Dar-es-Salaam, share their experiences as women working in the media. In an interesting and intimate discussion, the two journalists share their professional path and the obstacles they face every day as women working in the media and come up with potential solutions directly inspired by their own issues.

This interview takes part in the framework of the UNESCO project “Empowering Local Radios with ICTs”, supported by Sweden, aims to strengthen the capacities of local radio stations to improve the quality and variety of their programmes and broadcasts by increasing the use of information and communication technology (ICT) in order to provide poor populations and marginalized groups – in particular women and girls - with access to quality information on issues of local concern and foster their participation in the public debate by increasing the number of women working as journalist or interviewed as sources and experts.

Shukrani/Thanks;UNESCO 

WANAFUNZI WA FEZA BOYS HIGH SCHOOL WATEMBELEA VIRGINIA INTERNATIONAL UNIVERSITY


Wanafunzi wa Feza Boys High School kutoka jijini Dar es Salaam wakipata picha ya pamoja walipokua Virginia International University iliyopo jimbo la Virginia siku ya Alhamisi March 24, 2016, wanafunzi hao wapo kwa ziara maalum ya kuangalia uwezekano wa kujiunga na chuo hicho katika masomo ya juu.
 Makamu Rais wa Chuo hicho Dr. Suleyman Bahceci (kulia) akiwaeleza wanafunzi hao taratibu za kufuata kwa ajili ya kujiunga na VIU
Kushoto ni Alex Luketa Mtanzania anayefanyakazi chuoni hapo kwa ajili ya kusajili wanafunzi kutoka Afrika Mashariki akiwa pamoja na wanafunzi wa Feza Boys High School wakimsikiliza Makamu Rais wa chuo (hayupo pichani) alipokua akielezea wanafunzi hao utaratibu wa kujiunga na masomo VIU.
Wanafunzi wa Feza Boys wakipata mulo.
Mazungumuzo yakiendelea.
 Picha ya pamoja

Thursday 24 March 2016

Jikoni Leo; Mandazi ya kusokota ,Mapishi ya biscuit za karanga,na Sophie's Kitchen...

Wapendwa/Waungwana natumaini mnaendelea nyema na maandalizi ya Pasaka..
Ni Jikoni Leo na mapishi haya yatawasadia kuongezea kwenye maakuli ya Pasaka..
Mapishi haya kutoka kwa "da'Sophie"...

Basi nisiwachoshe na maneno meengi...

Twende sote sasa....






Shukrani;Sophie Kitchen...Zaidi;jitukumbuka63

"Swahili Na Waswahili"Muwe na wakati mwema.




Sunday 20 March 2016

MISA YA KUMBUKUMBU YA JAMES LUHANGA JR, BALTIMORE, MARYLAND NCHINI MAREKANI


Padri Honest Munishi akiongoza misa ya kumbukumbu ya marehemu James Luhanga Jr iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland nchini Marekani. Marehemu James Luhanga Jr alifariki Februari 3, 2016 mkoani Iringa. Picha na Vijimambo Blog/ kwanza Production.
Ndugu wa marehemu wakipeleka matoleo ya sadaka ya misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao James Luhanga Jr.
Wanafamilia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao marehemu James Luhanga Jr. iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 Baltimore, Maryland nchini Marekani.
Wanafamilia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao marehemu James Luhanga Jr. iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 Baltimore, Maryland nchini Marekani.
 
Pamela (kushoto) na Eliza Madada wa marehemu James Luhanga Jr. wakiwa katika picha ya pamoja kama kumbukumbu ya misa ya kumkumbuka mdogo wao aliyefariki Februari 3, 2016 mkoni Iringa. 
Wakati wa kupata chakula.
Katika picha toka kushoto ni Pamela Luhanga, James Luhanga Sr na Eliza Luhanga.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Thursday 17 March 2016

TANZANIA RED CARPET YAFANA SEATTLE, WASHINGTON STATE


Mama mitindo Asya Idarous Khamsini (kati) akiwa katika picha ya pamoja na mashabiki wake wa mitindo kwenye usiku wa Tanzania Red Carpet uliofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 mjini Seattle jimbo la Washington na kuhudhuriwa na Watanzania wanaoishi jimbo hilo na marafiki zao.
Mama mitindo Asya Idarous Khamsini akipata ukodak moment.
Wavaaji nguo za mitindo wakipata picha ya pamoja na mama mitindo Asya Idarous Khamsini.

Tuesday 15 March 2016

Ujumbe wa JWTZ watembelea Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Washington, DC (11 Machi, 2016)

Mhe. Wilson M. Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Washington, DC alikutana na Ujumbe wa JWTZ ulioongozwa na Mkuu wa Tiba Jeshini, Brigedia Jenerali (Dkt.) Denis Raphael Janga, aliyekuwa amefuatana na Mkuu wa Chuo cha Kikeshi cha Tiba - Lugalo, Brigedia Jenerali (Dkt) Robinson Mboni Mwanjela. Wengine ni Mkurugenzi wa Kinga Jeshini, Luteni Kanali Charles Emilio Mwanziva pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wauguzi, Luteni Kanali Lawrence Tia Banda. Ujumbe huo ulikwa na ziara ya Kikazi ya wiki moja hapa Marekani, katika kuendeleza mahusiano baina na JWTZ na majeshi ya Marekani.
 Pichani kutoka kushoto: Col. Adolph Mutta (DA), Brig. Gen. (Dkt) Denis R. Janga, Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi, Brig. Gen. (Dkt) Robinson M. Mwanjela, Lt. Col. (Dkt) Charles E. Mwanziva na Lt. Col. Lawerence T. Banda



HARAMBEE YA KUMCHANGIA MARIAM HUSSEIN YAFANYIKA DMV




Mariamu Hussein akihudhuria harambe ya kumchangia iliyofanyika siku ya Jumamosi Silver Spring, Maryland nchini Marekani na kuhudhuriwa na WanaDMV na marafiki zao. Mariam Hussein nasumbuliwa na ugonjwa wa saratani.


Vitu mbalimbali vilivyoletwa na WanaDMV kwa ajili ya kuvipiga mnada kwenye harambee iliyofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, Maryland nchini Marekani.

WanaDMV na marafiki zao waliohudhuria harambee ya Mariam Hussein (wanne toka kushoto) iliyofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, Maryland nchini Marekani.
Baadhi ya WanDMV wakiendelea kupata mapochopocho  kwenye harambee ya kumchangia Mariam Hussein (hayupo pichani) iliyofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, Maryland nchini Marekani.
Mariam Hussein (kati) akiwa na familia yake kwenye harambee ya kumchangia fedha za matibabu ya saratani iliyofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016
Mnada ukiendelea 
Vitu mbalimbali vilivyoletwa katika mnada wa harambee ya Mariam Hussein uliofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, maryland nchini Marekani.
Mariam Hussein (kati) akifuatilia Harambee ya mnada wa kuwezesha kupatikana kwa fedha za matibabu ya Saratani siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, maryland nchini Marekani.
Picha ya pamoja
Picha ya pamoja
Picha ya pamoja